Epuka Mtego huu Jakaya

Epuka Mtego huu Jakaya

The Hunter

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2010
Posts
1,049
Reaction score
307
Naamini u mzima, na najua huwa unapita hapa kama baadhi ya watendaji wako wanavyopita kwa majina bandia.

Mgomo wa madraktari ndo ushatangazwa naamini mkuu utaweka siasa na kiburi chako pembeni katika kutatua swala hili, japo ulijaribu kuwatuliza kwa maneno yaliyojaa siasa kwenye hotuba yako ya mwisho wa mwezi amini mkuu haijasaidia kitu, kwani makubaliano ilikuwa ni within a month baadhi ya matatizo yawe yameshatatuliwa, swala la kutangaza kwamba waziri mkuu ndo kapokea faili dakika za mwisho za mwezi huo mliokubaliana ni uthibitisho wa kwamba mliwadanganya madaktari, mlitumia siasa kukubaliana nao huku mkisahau mwezi mmoja ni siku thelathini tuu.

Chief najua wewe ni mbishi na utaacha madaktari wagome kwani wewe huumii kwa lolote, najua utataka kuweka muscle kidogo kwa kutishia kuwafuta kazi, mkuu Stuka maamuzi ya hovyo katika swala hili yatagharimu maisha ya wengi, yataibua migomo toka kada nyingine na amini nalokuhasa itakugharimu mkuu.

Enzi za bora liende zimekwisha, fanya kazi kama ulivyoomba wananchi wakuamini na kukupa madaraka.

Ikulu si mahali pa kupatia visa za kwenda kuzurura nje ya nchi kila kukicha, Ikulu ni nyumba inayokutanisha Pure cream and Think Tanks ya taifa.
 
Swala la kuwaondoa mawaziri wako Mponda na Nkya yalikuwa juu yako kwani hao ni wateule wako, ulifahamu na unafahamu wewe ndo ulitakiwa uanze utekelezaji, kumtaja waziri mkuu wakati wewe ndo boss wake ni ishara tosha hufahamu hata hayo waliyokubaliana ama hujaona umuhimu wake
Peleka pesa ya walipa kodi kwenye uchaguzi wa Arumeru kitakapo waka utakosa pa kutokea
 
Rais hawezi kuwaondoa watendaji wake only kwa sababu madokta wanataka, akishamuondoa Nkya na Mponda watataka amuache na mama Salma Kikwete.
 
Mtoa maada, la kuvunda halina ubani. Umeona maoni ya mmoja wa "washauri" wake (anajiita maundumula) hapo juu?
 
Ujumbe umefika. Naunga mkono maoni yako. Huu sio wakati wa siasa kwenye maswala yanayolihusu Taifa letu. Asikilize ushauri!
 
....Chief najua wewe ni mbishi na utaacha madaktari wagome kwani wewe huumii kwa lolote, najua utataka kuweka muscle kidogo kwa kutishia kuwafuta kazi, mkuu Stuka maamuzi ya hovyo katika swala hili yatagharimu maisha ya wengi, yataibua migomo toka kada nyingine na amini nalokuhasa itakugharimu mkuu..
Sijakusoma Mkuu, unashauri? unatukana? au unasikitika? Wewe ni Daktari au basi tu leo mama kakuudhi home? Pole.
 
....Chief najua wewe ni mbishi na utaacha madaktari wagome kwani wewe huumii kwa lolote, najua utataka kuweka muscle kidogo kwa kutishia kuwafuta kazi, mkuu Stuka maamuzi ya hovyo katika swala hili yatagharimu maisha ya wengi, yataibua migomo toka kada nyingine na amini nalokuhasa itakugharimu mkuu..
inaonekana umeandika ukiwa uelewa pombe kali ee
 
Ujumbe umefika. Naunga mkono maoni yako. Huu sio wakati wa siasa kwenye maswala yanayolihusu Taifa letu. Asikilize ushauri!
Mbona mnatanguliza siasa au mnajua suala hili lina wanasiasa nyuma? manake kiongozi hawezi kufanya siasa kama hajachokzwa na wanasiasa wenzake. Tumabizane wakuu akina nanihii wako na Madaktari, jambo linalomkera Mkuu? Najua ndo zao kutafuta umaarufu.
 
madai ya madaktari yanafanyiwa kazi na serikali.nyie mnaotaka majibu baada ya siku tatu mjue kuwa utendaji na maamuzi ya nchi sio sawa na maamuzi ya familia ambayo wewe na mkeo mnaamka na kuamua jambo.hili ni suala la kitaifa linahitaji mambo mengi.subira inahitajika
 
Swala la kuwaondoa mawaziri wako Mponda na Nkya yalikuwa juu yako kwani hao ni wateule wako, ulifahamu na unafahamu wewe ndo ulitakiwa uanze utekelezaji, kumtaja waziri mkuu wakati wewe ndo boss wake ni ishara tosha hufahamu hata hayo waliyokubaliana ama hujaona umuhimu wake
Peleka pesa ya walipa kodi kwenye uchaguzi wa Arumeru kitakapo waka utakosa pa kutokea
Kwa hiyo ulitaka aseme amepokea faili wakati suala zima linashughulikiwa na PM. Ni umbumbumbu au nini?
 
mtu mwenye akili timamu hawezi kushabikia mgomo wa madaktari.mleta mada we ni mchochezi na wala huishi hapa tanzania huathiriki na matokeo ya mgomo wa madaktari.
 
Kama miaka 45 iliyopita hamkukumbuka kweli leo mwezi mmoja mmtaweza kufanya kitu?
Subra mnapolipana posho kubwa kubwa huwapo pia?
 
mleta mada ni msaliti wa damu ya watanzania maskini ambao hawawezi kwenda kutibiwa india
 
mleta mada ni msaliti wa damu ya watanzania maskini ambao hawawezi kwenda kutibiwa india

Ndugu Tamuchungu, kwanza umenihukumu nimelewa pombe, pili unaniita msaliti, kwako msaliti ni yule anaesema ukweli? ulitaka nikae kimya wakati namshuhudia mtalii wako akizurura nchi za wenzake kila uchwao? ameleta tija gani kama si kuwa hovyo toka alipoanza safari za kwenda kuomba omba kila leo?
Mimi na wewe nani msaliti sasa?!
 
Hivi ni nini hasa kinachomfanya Kikwete ashindwe kuwaondoa Nkya na Mponda? Kama ni wazuri sana kwenye utendaji si awahamishie wizara nyingine?
 
mtu mwenye akili timamu hawezi kushabikia mgomo wa madaktari.mleta mada we ni mchochezi na wala huishi hapa tanzania huathiriki na matokeo ya mgomo wa madaktari.

Mtu mwenye akili na ufahamu hawezi kutetea tumbo lake huku akiwa amezungukwa na ndugu jamaa na marafiki wenye shida na wasiojua kesho yao.
Tanzania ni yetu wote, maamuzi ya hovyo na dhulma zenu zinaiathiri jamii yote. Wezi wakubwa!!
 
Back
Top Bottom