Enzi za utoto: Funny life experieces

Enzi za utoto: Funny life experieces

Nakumbuka enzi hizo watoto cku moja ucku baba alirud ucku akatuletea keki sasa kaka mkubwa nd akapewa kugawa,, yey ikabdi abuni utaratibu eti tufany kama wakristu wanavoend kupokea mwil wa kristu (mkate kanisani)

Sasa ikabd tujipang mstari tulkua km watatu na yy kaka wa nne,, alichokifany kaka akazima kibatari tukawa tunaenda kupokea gizani,, badala ya kutupa keki tulizonunuliw yeye akaanz kukata ugal uliobaki ucku nd anatugawia alafu yeye keki anakla, tulipokuj kustuka huo ugomvi mzee ndio alkuj kuuamua,, siwez kusaau ,utoto raha sanaa…!!
 
SAA kumi na mbili jioni.nipo video show.na sh 30=yangu.naenda kuangalia love story.nusu porno ile.
 
Nakumbuka enzi hizo watoto cku moja ucku baba alirud ucku akatuletea keki sasa kaka mkubwa nd akapewa kugawa,, yey ikabdi abuni utaratibu eti tufany kama wakristu wanavoend kupokea mwil wa kristu (mkate kanisani)

Sasa ikabd tujipang mstari tulkua km watatu na yy kaka wa nne,, alichokifany kaka akazima kibatari tukawa tunaenda kupokea gizani,, badala ya kutupa keki tulizonunuliw yeye akaanz kukata ugal uliobaki ucku nd anatugawia alafu yeye keki anakla, tulipokuj kustuka huo ugomvi mzee ndio alkuj kuuamua,, siwez kusaau ,utoto raha sanaa…!!
Nimecheka!
 
U
Habari wa kuu.

J3 ndio inaishia hivyo,hatuna budi kurelax kidogo wakati tukiisubiria j4.

Jioni ya leo nimejikuta nakumbuka maisha yangu ya utotoni na vituko vyote nilivyopitia kwa kadri nilivyoweza kukumbuka. Katika matukio mawili niliyoweza kuyakumbuka,ni mawili ndio yamenigusa na kunikumbusha mbali.

La kwanza nakumbuka tulikuwa tunacheza kwenye migomba kwa masaa mengi na watoto wenzangu,katika mkungu wa ndizi kuna kile kikonyo mwishoni kabisa,hicho ndio nilikuwa nakichezea,nakichanua kuangalia vindizi vidogo vilivyokuwa ndani. Sasa mida ya mchana nilipoitwa kula,nilinawa mikono ila ule utomvu haukuisha. Kila nikila chakula kwangu ladha ilikuwa chungu,mwanzoni nilivumilia ila badae ikabidi niulize "Hivi ladha ya chakula mnaionaje? Mbona upande wangu kichungu?"

Mama ndio alikuja kunifumbulia fumbo lile,hapo msosi ndio ukaanza kushuka vizuri.

Kisa cha pili kwenye kucheza kombolela na wenzangu,niliokota kichupa flani hivi cha rangi ya silva. Kutokana na udadisi,nilihangaika sana kukifungua. Nilikiponda sana na jiwe pamoja na chuma,hatimae kikafunguka. Nakumbuka kwenye kuta za ndani kilikuwa na unga unga mweusi,hakukuwa na kitu kingine zaidi. Nilikinusa ili kujua harufu yake. Ilo lilikuwa kosa,mwili ulianza kuishiwa nguvu taratibu. Nikakitupa na kurudi home. Hali ilizidi kuwa mbaya,ikabidi Baba akakitafute kile kichupa then nkapelekwa nacho hospitali kupata matibabu. Nilipona,ila sitosahau.


Wewe mwana JF mwenzangu unakumbuka nini??

Share your childhood experiences with us.
Utundu wa kucheza kwenye miti siku nikiwa na bro na marafiki wa jirani si tulivamia majani ya upupu, tuliwashwa htr hata ukioga muwasho hautoki, watoto wa sikuizi hawakumbani na hizo rabsha
 
Alikuja binamu yetu wakati huo akisoma Uyole basi mahindi ya kuchoma alikua anasema anatutafutia njia, ukushtuka ameshakula nusu ya hindi.
Anataftia vipi njia kwa kutumia mahindi?
 
Loohh kuna kituko kimoja wkt tupo kidato cha nne.
Paper ya historia ilifanyika mchana, basi binti mmoja ile anaingia viunga vya shule tuu anaambiwa kuna feki umelipata. Binti kapaniki sijalipata. Yule kijana akampa point za feki.
Binti akamwambia andika paja LA kushoto na Mimi na andika kwenye paja la kulia.
Binti bize anamaliza yule kijana hata point za swali moja bado.
Akamuuliza mbona hujaandika wewe vipi? Kijana mapaja yako laini sana nimeshindwa kuandika
Kuingia kwenye paper likawa feki kweli kweli.
 
Anataftia vipi njia kwa kutumia mahindi?
Hahaa,, unakuta hindi zima halijapukuchuliwa sasa yy anafany kupukuchua mstari m1 au miwili ili kumrahisishia anayekula kweny kupukuchua…!!
 
Loohh kuna kituko kimoja wkt tupo kidato cha nne.
Paper ya historia ilifanyika mchana, basi binti mmoja ile anaingia viunga vya shule tuu anaambiwa kuna feki umelipata. Binti kapaniki sijalipata. Yule kijana akampa point za feki.
Binti akamwambia andika paja LA kushoto na Mimi na andika kwenye paja la kulia.
Binti bize anamaliza yule kijana hata point za swali moja bado.
Akamuuliza mbona hujaandika wewe vipi? Kijana mapaja yako laini sana nimeshindwa kuandika
Kuingia kwenye paper likawa feki kweli kweli.
Hahahaaa,,, mimi pia iliwahi tokea hiyo kweny mock ya la saba ,kuna madada walkua na possible sas wakawa wanaziandika kwenye mapaja na sisi wavulan tulipojua,, bila ajizi ikabd tuwe tunawafunua mapaja kila siku ili tujue kama wana possibl but in real sense ilkua ni kuwachungulia tuu……!!
 
Skikua kabonge lakini nilikuwa sakala sana, uzuri wangu kwenye kuongea na nguvu sina, kila msuto ulinihusu.
duh!!!!huu Uzi umenifanya nikumbuke ya zamani Sana.Nilikuwa na tabia hiyo pia ndugu. Nilikuwa mbea balaa na lakini matukio ya kusutwa sio mengi na nilikuwa nikisutwa hata sisemi kitu nakuwa mdogo ukiniweka kwenye piriton miguu haifiki chini.

Sasa kuna siku buana nikawakimbia watu shuleni nikarudi zangu home, kumbe wameniona kwa mbali wakanifuatilia ile nimebakiza mita kadhaa nimalize barabara ya lami niingie ya vumbi home weeee!!!!nikawekwa mtu Kati,aisee nilikuwa natetemeka nikaanza kuita jina la dada angu mpaka akafungua geti hafalu wale wote wakageuka kucheck geti linakofunguliwa,nilipata Ka space kadogo tu nilivyopenya ile sehemu Hata sielewi nikazama ndani. Dada angu akawatimua pale getini walivonifuata. Nilichekwa sana nyumbani ile siku.
 
Duh!!! ninaKumbuka nilikuwa naogopa sana sindano enzi ya utoto wangu.
Nilikuwa na tabia ya kuweka maji kwenye kikombe then nina yaficha upande wa chini ndani ya freezer. Yanaganda na kuwa barafu kabisa,Nina ya gonga gonga na kuyala huku Nina yatafuna,Hata maziwa nikipewa nilikuwa nakunywa nusu na nusu nilikuwa nafanya upuuzi huo.

Baada ya muda,Nikaanza kusikia koo linaniuma nikimeza mate. Mama yangu alikuwa nesi,nikaawa najua kidoho kuhusi panadol inatuliza maumivu nikawa nakunywa dawa hizp kwa siri na kupata nafuu. After a week Kaanza kusikia natoa harufu mbaya nikiongea,nakumbuka Mara nyingi akawa ananiulza umepiga mswaki Leo?,najibu Ndio.

Baada ya muda akaanza kunikagua kinywa,akagundua Nina tatzo akaniuliza unakunywa maji ya baridi,nikakataa. Wakati Huo sijastop ile tabia ya kugandisha maji na panadol zangu. Mama akaanza kunichunguza,nikawa sometimes siyakuti maji yangu niliyoweka na kwasababu ya akili za utoto sikuwa najiuliza nikawa narudia kuyaweka nakuta yametolewa mpaka usiku Naenda kulala sipati barafu zangu.

Siku moja toka agundue Nina nini mdomo alanifuata shuleni tukaenda hospital,nikasikia neno injection,nikamuuliza mama mnanichoma sindano mama akasema NO, sio za kwako. Baadae akaniambia twende huku,nikisoma kibao cha mlangoni naona chumba cha sindani,nilikimbia kurudi nyumbani. Walinitafuta sana mlinzi aka confirm nilitoka nakimbia,mama akanigombeza sana. Alivyorudi nyumbani. Usiku nimelala alinichoma sindano nikaanza kulia usiku tena kwa nguvu sana. Sitokuja kusahau,na iliendelea kuchomana sindano usingizini mpaka zilipoisha. Nikawa asubuhi nagoma kwenda shule eti sindano zinauma it's my living memory jamani,sitasahau yaani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom