Duble Chris
JF-Expert Member
- May 28, 2011
- 3,481
- 564
Dah!aliona aibu.Thread hii imenikumbusha enzi nasoma Ifunda Tech. School: tulikuwa na secondmaster wa kijaluo aliyeitwa Saka, mzee alikuwa mpole sana ila alikuwa ni mbaya sana kama atakukamata na hatia kwa vile anaweza akakupa adhabu hata ya mwezi mzima. Alfajili moja alikwenda mabwenini kushtukiza zoezi la kukimbia mchakamchaka. Alipofika katika block no.3 la bweni la Seuta akagundua kwamba kuna wanafunzi ndani kama wa5 bado wamelala, akawaamsha na kuwaamuru watoke na wenyewe wajitaje majina yao akiamini kwamba watatii. Wale majamaa walishajua kuwa kwa giza lile si rahisi awakariri sura zao hivyo badala ya kutaja majina yao halisi wakajitaja kwa majina ya wachezaji wa Simba wa wakati ule: Hussein Masha, Mohamed Mwameja, Alfred Kategile, George Masatu na Edward Chumila. Alipomaliza kuandika majina yao akawaambia waungane haraka na wenzao ktk mchakamchaka. Kituko cha mwaka ni pale muda wa assembly ulipowadia na S/master huyo kuwasoma watuhumiwa wake ili awape adhabu, kila mtu aliangua kicheko na alipoambiwa kuwa hayo ni majina ya wachezaji wa timu ya simba na yy aliangua kicheko na kuondoka zake.
aisee hiyo ya headmaster kiboko. Duh!Issue ilikuwa ni Iyunga Sec,
- Nakumbuka nikiwa F1 jamaa yetu mmoja alipigwa na F2 hadi kuzimia kesi ikamfikia H/master, next day akaja assemble na huyu jamaa alikuwa adimu sana assemble siku akitokea tu wanafunzi wote wanakuja kumsikiliza wanajua kuna issue ya maana. Basi kauli aliyo itoa sitasahau alisema " Nyie F2 msiwapige hawa F1 tumboni mtawaletea matatizo " akaondoka zake na kuwaacha F2 wakishangilia
- Siku ya graduation yetu hakuna F4 aliye kula wali kwa nyama maana vyoote vilimwagwa na wahitimu wenyewe kwa scramble kubwa kutokea mesini.
Ulikuwa mwaka gani hapo Kanta?umenikumbusha Kanta,ilikuwa balaa,mpaka leo nikiangalia uso wangu nakumbuka sekeseke!, unapewa tsh 5, uende chanji kuleta sukar 1kg, na maandiz mfuko! We acha tu. Niliwapelekea mchanga kama 2kg hv, jamaa walishuka ka mvua kutoka kwenye vitanda juu, nilipokea kichwa cha mgosi mmoja,mpaka leo ni wanted kwangu!
umenikumbusha Kanta,ilikuwa balaa,mpaka leo nikiangalia uso wangu nakumbuka sekeseke!, unapewa tsh 5, uende chanji kuleta sukar 1kg, na maandiz mfuko! We acha tu. Niliwapelekea mchanga kama 2kg hv, jamaa walishuka ka mvua kutoka kwenye vitanda juu, nilipokea kichwa cha mgosi mmoja,mpaka leo ni wanted kwangu!
Hizo zote stori tu,mwisho wa maelezo ni UMBWE BOYS,siku tunaingia shule tulikuta raia kibao wamevaa vyuti,wanapokea wazazi,kumbe ni madenti,ukiwapa tranka lako tu,imekula kwako,,,ukiingia domitory unakuta vitanda vyote havina chagga,inabidi uende dorm 6,kwa ma 4m six ukanunue chaga,chaga moja ni buku,kama hutakilala chini.....
Mambo ya toilet tulikuta choo kimoja tu kizima,,,kama atm ya crdb saa 12 jioni...mtu nyomiiiii, ukiwa f5 au f1 ukiingia tu lazima "ukatwe mkia", yaani hiyo siku ni fimbo kwa kwenda mbelee, mtarushiwa mawe chumbani, immagine mtu anakuja kunoa panga dirishani kwako usiku wa manane,,,,,,,,,
uji tulikua tunauita fongo, watoto wanaojiweza ndo waliweza kununua sugar, sisi tulikuwa tunapiga fongo chuma-yaani bila sukari au tunachanganya super-deep(jussi kola) tunapata mafleva, uji wenyewe umechanganywa na pumba yaani full kutematema,.
Siku ya nyama au wali ni vita balaa,yaani ukuifanya utafiti,watu wengi sana wanarudi kwao na ngeu za wali....mwisho kabisa ni kwenye vita kati ya sisi na lyamungo boys,,,tulikuwa tunapigania uwanja flani mkuuuubwa tulikua tunapaita desert,tulikua na division of labour ya kutosha,form six walikuwa wapiganaji wakuu,form five kuvunja stoo na kuchukua zana kama majembe, shoka,panga etc....
Form four walikua warusha mawe na kuleta noma,form three walibeba viti,kuni,kuwavunjia wenzetu vioo,kama tungeshinda viti,,form two na one ni waokota mawe na kuwapa wakubwa ili wawarushie maadui na wasindikizaji cz hamna mtu kubaki nyuma.
UMBWE was something else,,,,,siku ya graduation wababe wanabeba mabench na wanaweka kambi kwenye familia yoyote waliokuja kumpongeza mwanao,wanagonga diko then wanahamia familia nyingine.....siku za kwenda shule za girls ni full kuanua nguo za watu na kupiga "butterfly" matranka ya watu ili kupata pamba,,,,,,,
Migomo ya ndani ,watu wanaenda kukata umeme kwenye transformer,,,,,,,,,wezi walikuwa ni wakali mithili ya carlos,watu wanaiba hadi bendera na bunduki ya mlinzi,kuiba ndizi kijijini,,,kuvamia soko la pale kijijini,,,,duuuh,,,,,,embu mwanaUMBWE mmoja aendeleze zile swagg zetu,maana nadhani hamna kambi kama lile
Ulikuwa mwaka gani hapo Kanta?
ha ha ha! Hii thread si mchezo, nakumbuka jitegemee enzi hizo h/master sasa alikua anataka watu waongee english muda wote wakati maafande wake hawajui kuna siku nilikamatwa mara wakati napelekwa ofisi ya nidham tukakutana na mkuu ghafla akauliza what is wrong with student? Afande akatoa macho, mzee nikadakia huku nikijitetea kwa lugha ya malikia na kumkandamiza afande kwamba ananikosesha vipindi. Kanali masawe akauliza kijeshi ''is it true?'' yule afande akauka na kujibu kwa sauti kubwa ''yes sir. Mzee nikaambiwa go to the class. Mbio nilizotoka hapo!
Yaap mkuu!ulitumia udhaifu wake,kosa moja>goli nyingi.ha ha ha! Hii thread si mchezo, nakumbuka jitegemee enzi hizo h/master sasa alikua anataka watu waongee english muda wote wakati maafande wake hawajui kuna siku nilikamatwa mara wakati napelekwa ofisi ya nidham tukakutana na mkuu ghafla akauliza what is wrong with student? Afande akatoa macho, mzee nikadakia huku nikijitetea kwa lugha ya malikia na kumkandamiza afande kwamba ananikosesha vipindi. Kanali masawe akauliza kijeshi ''is it true?'' yule afande akauka na kujibu kwa sauti kubwa ''yes sir. Mzee nikaambiwa go to the class. Mbio nilizotoka hapo!