Nakumbuka ticha mmoja alikuwa anamtokea demu wangu sasa Kwa kiburi cha yule ticha alikuwa anamsimamisha mtoto hata msitarini muda wa kutawanyika pale msitarini kulikuwa na miti ya michungwa ticha si akaanza kumwaga ubuyu huku anashika shika ile miti aaah aliipata Kwa kweli nyigu walimshukia na ilikuwa mchana jua limewaka noma sana jamaa alitoka nduki nikamchukua demu wangu tuka sepa zetu home
Jamaa kesho yake hakuja shule kama siku3 hivi
Siku aliyokuja vibaraka wakampa full story kwamba nilikuwepo maaneo Yale na washikaji zangu na nyigu zilipo muuma tuulikuwa tunacheka na kutangaza Kwa wanafunzi
Anyway ndyo hivo shule yenyewe ya private jamaa akaufyata
Tokea hapo somo lake kupata 21-32 mm na demu wangu ilikuwa ni kawaida sana hata kama tungepiga chabo Kwa darasa zima
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.