Embu tutafakari kidogo

Embu tutafakari kidogo

Hata huo utumwa wa Time + Space + Matter unaonekana kufanya kazi kwa msingi wa kumbukumbu tu.

Kwa maana muda wenyewe hauwezi kueleweka bila kumithirisha kilichopita na kilichopo sasa, vile vile space huwezi kuitambua bila reference ya sehemu nyingine ulizowahi kuziona na matter nayo hupata maana kutokana na patterns ambazo tayari zilishawahi kuonekana hapo kabla.

Kwahiyo hoja yangu kuu ni kwanini consciousness ya mwanadamu imefungwa ndani ya mfumo unaolazimisha kila kitu kiwe interpreted kupitia past?.

Kwa maana hata physics yenyewe haiwezi kufanya prediction bila kutumia previous observations.

Hakuna formula inayotabiri future kutoka kwenye utupu so lazima ichukue data za kale then ndio ijenge sheria fulani.

Ndio maana nikaja hapa tusaidiane kutafakari kwenye hili eneo, ila pia tujiulize kwa pamoja...

Je, sisi tunajua ukweli wa mambo,
au tunajua tu repetition ya mambo?

Kwasababu hata ukisema universe ni matokeo ya Time + Space + Matter, bado understanding yako ya hivyo vitu vitatu umetengenezewa na historical observation... Au nadanganya mkuu?

Hujawahi kushika future,
umeshika mabaki ya jana kisha ukayatumia kukisia kesho, hivi ndivyo always tunafanya.

So kutokana na Hilo ndio maana nikasema huenda hapo ndio limitation ya akili ya mwanadamu ilipo, ya kwamba haiishi nje ya mfumo wa kumbukumbu, ya kwamba asipokua na kumbukumbu yoyote ya kale kichwani mwake hawezi kuwa kama alivyo sasa.

Ila pia nikasema, sayansi yenyewe ni historia iliyokataa kufa.

Kwa sababu sheria zote za kisayansi ni matukio yaliyotokea mara nyingi sana hadi tukayapa hadhi ya ukweli wa kudumu ila in reality bado msingi wake ni past.

So andiko lote limekaa kutafakari zaidi pasipo kudemand au kutaka kubadili chochote kwenye universe especially dunia ila kwa jinsi mambo yalivyo naona tunaishi past na sasa sio sasa na future.
Mkuu naelewa unacho maananisha lakini napata tabu kuelewa unatakaiweje kwenye muktadha wako……. Kwamba tuwe hatukumbuki ya nyuma bali tunaona ya mbeleni(future) tu…………. Hebu tafakari ni future gani utaiona bila past?. Vitu huwa havitokei tu within a second, ni Mchakato, leo ukiwaza kutengeneza gari kesho unaamka umesahau kila kitu sasa utaionaje hiyo future ya kutengenezwa kwa gari?. Na hata “ukiona” future kwa muktadha wako ikija kutokea bado itakua past sababu uliiona kabla lakini ubongo wako utakuja kurea litakapo tokea mbeleni. Nafikiri maisha yako PERFECTLY the way yalivyo
 
Imani yangu inaniambia sisi ni bora ya zaidi ya hivi tulivyo, ila ni vile tumefungwa kwenye eneo ambalo halitupi mwanya wa kuona zaidi ya vile ambavyo tunalazimishwa tuvione.

Ndio maana nasema, ukifutiwa kila ulilowahi kujifunza, kila uso uliowahi kuuona, kila neno ulilowahi kusikia… usingebaki na akili bali ungebaki na utupu unaohitaji kufundishwa historia upya ili uweze kuruhusiwa kuishi tena ndani ya mfumo wa dunia kwasababu akili unayohisi uko nayo huna bali imetengenezwa na kuwa shaped kinamna ile dunia inataka iwe.
Hakika, umenena vyema...


Cc: Mahondaw
 
Mkuu naelewa unacho maananisha lakini napata tabu kuelewa unatakaiweje kwenye muktadha wako……. Kwamba tuwe hatukumbuki ya nyuma bali tunaona ya mbeleni(future) tu…………. Hebu tafakari ni future gani utaiona bila past?. Vitu huwa havitokei tu within a second, ni Mchakato, leo ukiwaza kutengeneza gari kesho unaamka umesahau kila kitu sasa utaionaje hiyo future ya kutengenezwa kwa gari?. Na hata “ukiona” future kwa muktadha wako ikija kutokea bado itakua past sababu uliiona kabla lakini ubongo wako utakuja kurea litakapo tokea mbeleni. Nafikiri maisha yako PERFECTLY the way yalivyo
Ukisoma andiko vizuri utaona hoja ambayo Mimi nimejikita nayo sana ni kwanamna maisha yetu yalivyokuwa ya reference, yaani Kila kitu kinategemea past, inamaana ukiiondoka past hamna maisha au nini?

Kwanini kila kitu kiwe kwa mtindo huo wa reference?

Kwanini past iwe ndio maisha yetu while future inabaki kuwa surprise?

Na kwanini hoja zozote za future zinapanguliwa hadi watoaji wanajikuta wanarudi kwenye eneo pendwa la kufanya akili ipumue?
 
Ukisoma andiko vizuri utaona hoja ambayo Mimi nimejikita nayo sana ni kwanamna maisha yetu yalivyokuwa ya reference, yaani Kila kitu kinategemea past, inamaana ukiiondoka past hamna maisha au nini?

Kwanini kila kitu kiwe kwa mtindo huo wa reference?

Kwanini past iwe ndio maisha yetu while future inabaki kuwa surprise?

Na kwanini hoja zozote za future zinapanguliwa hadi watoaji wanajikuta wanarudi kwenye eneo pendwa la kufanya akili ipumue?
Mkuu hizo fikra zako HAZIWEZEKANIKI kwasababu hata ukiiona future ya kesho ikifika hiyo kesho si bado utakua uliiona hiyo future jana yake ambayo ni past?. Hebu nifafanulie unatakaje kuishi kwenye future bila past?…………..Hakuna Future bila past na ndio maana nikakwambia uwepo wa ulimwengu ni matokeo ya utumwa wa Space Time na Matter, na hoja yako inaangukia kwenye time ambayo inajumuisha wakati uliopita, uliopo na ujao, …….. ukiondoa wakati mmoja wapo maana yake hakuna existence ya Time wala Ulimwengu
 
Hatari sana kila kitu ni marudio tu na kuna hile ya kwenda sehem uijui lakin unapata isia kma ulishawahi kufika iv
 
Back
Top Bottom