Thecoder
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 2,443
- 6,327
Dunia kwa ujumla wake ni sehemu ya matokeo yaliyo na sababu fulani.
Hakuna jambo lolote duniani ambalo linaweza kumkuta mtu au kutokea kwa bahati mbaya, bali kila jambo ambalo linamkuta mtu au linatokea jua ni matokea ya sababu au vyanzo vya kale.
Kwa maana hiyo basi, dunia haijawahi mtendea mtu jambo lolote ambalo hastahili bila kujali ya kwamba jambo hilo ni baya au zuri ila maadam limekutokea au kukupata basi kuwa na hakika hilo ni jambo ambalo limesababishwa na chanzo fulani katika kale yako.
Twende taratibu hapa, iko hivi, matokeo yoyote huandaliwa ingawa watu wengi wamezoea kufanya maandalizi kwenye matokeo ya mazuri ya kimwili ila yale matokeo mabaya ambayo huja tu kwa surprise hasa ya kiroho hawajui kama na yenyewe yaliandaliwa iwe kwa kujua au kutokujua iwe kwenye maisha haya au yaliyopita.
Kwasababu dunia haijawahi kuwa na kitu kipya, vitu ni vile vile ambavyo hujirudia kulingana na nyakati kwa kuzingatia vyanzo vyake ndani ya mbegu zilizomea katika nyakati au zama husika.
Na kimsingi wote tunajua ya kwamba, ukuaji na maendeleo yote hutegemea watu na mtu si mwili tu unaoonekana bali mtu ni roho iishiyo ndani ya mwili.
Sasa, roho ni mfano wa mbegu ambayo haiwezi potea duniani, na kama ilivyombegu nyingine huota pale ilipozikiwa.
Huwezi ukaizika mbegu Dar halafu utarajie iende ikaote Arusha, bali pale ilipozikiwa ndipo itakapochipukia.
Kwahiyo, ukuaji na maendeleo yanayotokea maeneo mbalimbali duniani kwakua huletwa na watu basi kuwa na hakika sehemu ambazo zimezika mbegu nyingi bora ndizo zitakazo otesha miche bora sana itakayopelekea uvunaji wa matunda mazuri.
Sawa, najua bado hujanipata vizuri ila wacha nijaribu kujenga hoja itakayonifanya nielekee kwenye mfano ambao utakupa mwanga kidogo, ni hivi….
Zipo mbegu ambazo husafirishwa kutoka katika nchi moja hadi nyingine au eneo moja hadi jingine na kwenda kuzikwa huko, kwahiyo utaona hapo ya kwamba kiasili si mbegu za maeneo hayo ila zimesafirishwa na kwenda kuzikwa kwenye maeneo mengine na yale ya asili yake ya kwanza, kisha zikaota na kumea huko.
Na nilikwambia mbegu ni mfano wa roho, kwahiyo pale ambapo utazikiwa ndipo ambapo utachipukia, inawezekana umeishi maisha yako yote Tanzania ila ikatokea ukaumwa ukaenda India kutibiwa ukafa na wakaamua kukuzika huko basi kwenye mzunguko ujao roho yako itachipukia India sio Tanzania tena.
Na hii ndio ambayo hupelekea kuna baadhi ya watu kiasili ni wanatokea kwenye mataifa fulani kwa namna ya kimwili na kule ambako walikozaliwa ila ndani yao hujikuta wanauhusudu sana utamaduni wa nchi au jamii tofauti na ile ambayo yeye anatokea.
Hili sio jambo la makusudi wala bahati mbaya ila ni jambo ambalo hutokea kwasababu wewe halisi yaani roho anakua na kumbukumbu fichi na ile asili yake ya kwanza kwasababu unakuta aliishi kwenye hiyo asili kwa takribani nusu na robo ya maisha yake yote yaliyopita kwahiyo hiko unachojiskia ni matokeo ya yale maisha ya nyumba ambayo roho yako iliwahi kuyaishi.
Kwahiyo kifo ni mwanzo wa maisha mapya, ingawa mwanzo huo hautokei kwa haraka kwa maana process nzima ni ile ya mtindo wa FIFO yaani first in first out.
So, utakufa mwili utapata uharibifu ila roho kama mbegu itarudi kwenye foleni kusubiri kurudishwa kwenye mzunguko mwingine wa duniani, ni kama vile ambavyo utazika mbegu ya muhindi kisha itaota na kumea na itapata mwili wa kuiunganisha moja kwa moja na Dunia kisha ule mwili utafika ukomo na kufa ila mbegu itahifadhiwa na kusubiri msimu wake ufike ipandwe tena.
Kwahiyo mchakato mzima wa maisha ya duniani upo katika mtindo wa infinity loop, kwa maana ni kitendo ambacho kinakwenda na kujirudia tena na tena.
Angalia bara la Africa ambavyo limekua na maendeleo makubwa kwenye upande wa imani, utaona makanisa misikiti imeenea maeneo mengi kiasi cha watu kuhoji kwanini kwetu Imani imekua kubwa while kule kwa wale waliotuletea huo utamaduni ni ndogo sana, ukitafakari hapo utapata jibu ya kwamba kuna mabadilishano ya mbegu yalitokea, zipo mbegu imara ambazo zilibebwa kutoka Africa na kupelekwa maeneo mengine ya dunia na kwenda kupandwa huko na pia zipo mbegu zilizotoka maeneo ya huko zilikua Africa na zikapandwa huku, na kama unavyojua mbegu huota pale ilipozikiwa au kupandwa so haya matokeo yote yalisababishwa na hiko chanzo.
Ila kitu kizuri ni kwamba, kwakua maisha ni mzunguko na mabadiliko hutegemeana na aina ya mbegu ambazo zilipandwa katika msimu husika basi tarajia uendelevu wa mabadiliko kulingana na msimu uliopo na aina za mbegu zilizopo kwenye foleni yaani kwenye queue.
Ndio maana utaona kuna baadhi ya watu wameanza kuhoji juu ya uwezo wa kutafakari na ubunifu wa mambo mbalimbali uliopo kwenye kizazi hiki na kile kilichopita, sasa haya yote ni matokeo yaliyoletwa na chanzo cha namna hiyo.
Huwezi kupanda mbegu za hovyo na ukategemea uvune mazao mazuri, mazao mazuri hutegemea aina ya mbegu ambazo zimepandwa.
Kwahiyo Dunia au ulimwengu ni sehemu ya matokeo yenye chanzo, Kila ambacho hufanyika sasa huenda kudefine future ya mtu binafsi au eneo husika, na hapa ndipo ambapo ile dhana ya karma huingia, hasa kwa mtu binafsi.
Kwa maana ulimwengu haumtambui mtu kwa mwili ama sura ila unamtambua mtu kwa mitetemo.
Kwahiyo mitetemo ndio kitu ambacho huenda kuathiri roho ya mtu moja kwa moja, kwahiyo kadri unavyoiathiri roho yako kwa mitetemo hasi basi ndivyo unavyoitengenezea mazingira ya kuanzia hapo kwenye hasi pindi itakaporudi tena kwenye mzunguko.
Lakini ukiiathiri roho yako kinamna chanya pindi itakapopandwa na kurudi tena kwenye mzunguko kuwa na hakika itaanzia hapo hapo kwenye chanya.
Kwahiyo Dunia humtendea mtu halisi kwa namna ile ambayo anastahili, kwasababu Dunia au ulimwengu kwa ujumla ni sehemu ya matokeo yaliyo na chanzo fulani.
Kwa maana hiyo basi, hayo maisha ambayo unayaishi sasa na namna watu wanavyokuchukulia bila kujali muonekano wako wa kimwili au jinsia yako, kuwa na uhakika hayo ni matokeo yaliyoletwa na hiyo mbegu ambayo ipo ndani ya mwili wako.
Najua kunamtu anaweza akasema sasa Mimi nnamakosa gani yaani makosa afanye mtu mwingine halafu tabu nije nizipate Mimi? Jibu ni kwamba, wewe ni yule yule tofauti hapo ni nyakati na mwili ila mbegu ni ile ile tu.
Kwahiyo hakuna mtu mwingine ambae alifanya hayo makosa bali ni wewe mwenyewe ila ni vile tu hauwezi kumbuka na pia hakuna mtu mwingine ambae alifanya wema ni wewe ila hauwezi kukumbuka.
Na ili uelewe vizuri hapa ni kwamba duniani wapo watu ambao wanaishi maisha mazuri yaani luxury life ila hayo maisha mazuri wanayoishi hawajawahi yagharamia wao wenyewe, unakuta mtu tangu anazaliwa hajawahi nunua nguo kwa pesa yake, hajawahi nunua simu, hajawahi jilipia Kodi ya nyumba wala hajawahi jinunulia gari kwa pesa yake, wala hajawahi jilipia nauli kwa pesa yake kwenda nchi tofauti tofauti ila vyote hivyo anavyo na anaishi maisha mazuri kupitia watu.
Yaani unakuta hata kazi ya maana hana ila anapewa gari, anapewa nyumba, anapewa OFA ya safari ya hapa na pale, tena wala sio kwamba analazimisha ila ni vitu ambavyo huja kwake venyewe. (Hapa sizungumzii wale wadangaji na wenye mambo ya hovyo nazungumzia wale ambao wako na akili timamu na ni watu wa maana sana ila wamejikuta tu maisha yao yanaenda kimtindo huo kiasi cha kufanya hata wao wasielewe ni kwanini mambo huwa hivyo ila kimsingi hayo yote ni matokeo ambayo yamesababishwa na maisha yaliyopita na ndio hapa sasa ambapo tunasema karma)
Pia kuna watu ambao utakuta wao ni wapole sana na wako na mionekano ya upole hata kwa sura zao ila ni watu ambao huogoza kuteswa na watu au kuonewa na watu wengine bila sababu za msingi, yaani unakuta Kila sehemu ambayo anaenda hatendewi vizuri na watu wa eneo hilo kiasi cha kufanya ajihisi labda ako na mikosi ila wala sio mikosi bali ni matokeo yaliyosababishwa na mbegu iliyopo ndani mwako kwa kuzingatia yale maisha ya nyuma na hiyo ndio karma.
Pia wapo watu ambao wao kazi yao ni kusaidia wengine tu, na kuna wakati mwingine si kwamba wako na kipato kikubwa kifedha ila hicho hicho kidogo unakuta wanagawana na wengine, na unakuta kutokana na tabia zao hizi wanapokua kwenye ndoa wanapata wakati mgumu kwa wenza wao kwa maana wanajikuta hadi wanachukiwa au kuachwa kabisa kwa maana maendeleo hakuna ila mtu kila akipata pesa lazima apatane na kipengele cha kutoa msaada na hii huendelea hadi mwisho wa maisha yake.
Haya yote ni matokeo yaliyosababishwa na maisha yaliyopita na hiyo ndio karma yenyewe, kiufupi matokeo yanayofuata taratibu za kilimwengu huwa ni ya kimsimu, kwahiyo hutokea zama hadi zama.
Ndio maana kila jambo ambalo utalifanya kiroho matokeo yake huwa ni ya kiroho na si yote unaweza yashuhudia kwa zama hizi ulizopo na kila jambo ambalo hufanyika kimwili matokeo yake huonekana kimwili na haya lazima utayaona kwa haraka sana, ingawa pia yapo mambo ambayo huathiri maeneo yote mawili kwa maana kiroho na kimwili katika wakati mmoja.
Na hupaswi kusahau ya kwamba ili upate mbegu bora lazima ujitahidi kuutunza mche uliobeba mbegu hiyo.
Hakuna jambo lolote duniani ambalo linaweza kumkuta mtu au kutokea kwa bahati mbaya, bali kila jambo ambalo linamkuta mtu au linatokea jua ni matokea ya sababu au vyanzo vya kale.
Kwa maana hiyo basi, dunia haijawahi mtendea mtu jambo lolote ambalo hastahili bila kujali ya kwamba jambo hilo ni baya au zuri ila maadam limekutokea au kukupata basi kuwa na hakika hilo ni jambo ambalo limesababishwa na chanzo fulani katika kale yako.
Twende taratibu hapa, iko hivi, matokeo yoyote huandaliwa ingawa watu wengi wamezoea kufanya maandalizi kwenye matokeo ya mazuri ya kimwili ila yale matokeo mabaya ambayo huja tu kwa surprise hasa ya kiroho hawajui kama na yenyewe yaliandaliwa iwe kwa kujua au kutokujua iwe kwenye maisha haya au yaliyopita.
Kwasababu dunia haijawahi kuwa na kitu kipya, vitu ni vile vile ambavyo hujirudia kulingana na nyakati kwa kuzingatia vyanzo vyake ndani ya mbegu zilizomea katika nyakati au zama husika.
Na kimsingi wote tunajua ya kwamba, ukuaji na maendeleo yote hutegemea watu na mtu si mwili tu unaoonekana bali mtu ni roho iishiyo ndani ya mwili.
Sasa, roho ni mfano wa mbegu ambayo haiwezi potea duniani, na kama ilivyombegu nyingine huota pale ilipozikiwa.
Huwezi ukaizika mbegu Dar halafu utarajie iende ikaote Arusha, bali pale ilipozikiwa ndipo itakapochipukia.
Kwahiyo, ukuaji na maendeleo yanayotokea maeneo mbalimbali duniani kwakua huletwa na watu basi kuwa na hakika sehemu ambazo zimezika mbegu nyingi bora ndizo zitakazo otesha miche bora sana itakayopelekea uvunaji wa matunda mazuri.
Sawa, najua bado hujanipata vizuri ila wacha nijaribu kujenga hoja itakayonifanya nielekee kwenye mfano ambao utakupa mwanga kidogo, ni hivi….
Zipo mbegu ambazo husafirishwa kutoka katika nchi moja hadi nyingine au eneo moja hadi jingine na kwenda kuzikwa huko, kwahiyo utaona hapo ya kwamba kiasili si mbegu za maeneo hayo ila zimesafirishwa na kwenda kuzikwa kwenye maeneo mengine na yale ya asili yake ya kwanza, kisha zikaota na kumea huko.
Na nilikwambia mbegu ni mfano wa roho, kwahiyo pale ambapo utazikiwa ndipo ambapo utachipukia, inawezekana umeishi maisha yako yote Tanzania ila ikatokea ukaumwa ukaenda India kutibiwa ukafa na wakaamua kukuzika huko basi kwenye mzunguko ujao roho yako itachipukia India sio Tanzania tena.
Na hii ndio ambayo hupelekea kuna baadhi ya watu kiasili ni wanatokea kwenye mataifa fulani kwa namna ya kimwili na kule ambako walikozaliwa ila ndani yao hujikuta wanauhusudu sana utamaduni wa nchi au jamii tofauti na ile ambayo yeye anatokea.
Hili sio jambo la makusudi wala bahati mbaya ila ni jambo ambalo hutokea kwasababu wewe halisi yaani roho anakua na kumbukumbu fichi na ile asili yake ya kwanza kwasababu unakuta aliishi kwenye hiyo asili kwa takribani nusu na robo ya maisha yake yote yaliyopita kwahiyo hiko unachojiskia ni matokeo ya yale maisha ya nyumba ambayo roho yako iliwahi kuyaishi.
Kwahiyo kifo ni mwanzo wa maisha mapya, ingawa mwanzo huo hautokei kwa haraka kwa maana process nzima ni ile ya mtindo wa FIFO yaani first in first out.
So, utakufa mwili utapata uharibifu ila roho kama mbegu itarudi kwenye foleni kusubiri kurudishwa kwenye mzunguko mwingine wa duniani, ni kama vile ambavyo utazika mbegu ya muhindi kisha itaota na kumea na itapata mwili wa kuiunganisha moja kwa moja na Dunia kisha ule mwili utafika ukomo na kufa ila mbegu itahifadhiwa na kusubiri msimu wake ufike ipandwe tena.
Kwahiyo mchakato mzima wa maisha ya duniani upo katika mtindo wa infinity loop, kwa maana ni kitendo ambacho kinakwenda na kujirudia tena na tena.
Angalia bara la Africa ambavyo limekua na maendeleo makubwa kwenye upande wa imani, utaona makanisa misikiti imeenea maeneo mengi kiasi cha watu kuhoji kwanini kwetu Imani imekua kubwa while kule kwa wale waliotuletea huo utamaduni ni ndogo sana, ukitafakari hapo utapata jibu ya kwamba kuna mabadilishano ya mbegu yalitokea, zipo mbegu imara ambazo zilibebwa kutoka Africa na kupelekwa maeneo mengine ya dunia na kwenda kupandwa huko na pia zipo mbegu zilizotoka maeneo ya huko zilikua Africa na zikapandwa huku, na kama unavyojua mbegu huota pale ilipozikiwa au kupandwa so haya matokeo yote yalisababishwa na hiko chanzo.
Ila kitu kizuri ni kwamba, kwakua maisha ni mzunguko na mabadiliko hutegemeana na aina ya mbegu ambazo zilipandwa katika msimu husika basi tarajia uendelevu wa mabadiliko kulingana na msimu uliopo na aina za mbegu zilizopo kwenye foleni yaani kwenye queue.
Ndio maana utaona kuna baadhi ya watu wameanza kuhoji juu ya uwezo wa kutafakari na ubunifu wa mambo mbalimbali uliopo kwenye kizazi hiki na kile kilichopita, sasa haya yote ni matokeo yaliyoletwa na chanzo cha namna hiyo.
Huwezi kupanda mbegu za hovyo na ukategemea uvune mazao mazuri, mazao mazuri hutegemea aina ya mbegu ambazo zimepandwa.
Kwahiyo Dunia au ulimwengu ni sehemu ya matokeo yenye chanzo, Kila ambacho hufanyika sasa huenda kudefine future ya mtu binafsi au eneo husika, na hapa ndipo ambapo ile dhana ya karma huingia, hasa kwa mtu binafsi.
Kwa maana ulimwengu haumtambui mtu kwa mwili ama sura ila unamtambua mtu kwa mitetemo.
Kwahiyo mitetemo ndio kitu ambacho huenda kuathiri roho ya mtu moja kwa moja, kwahiyo kadri unavyoiathiri roho yako kwa mitetemo hasi basi ndivyo unavyoitengenezea mazingira ya kuanzia hapo kwenye hasi pindi itakaporudi tena kwenye mzunguko.
Lakini ukiiathiri roho yako kinamna chanya pindi itakapopandwa na kurudi tena kwenye mzunguko kuwa na hakika itaanzia hapo hapo kwenye chanya.
Kwahiyo Dunia humtendea mtu halisi kwa namna ile ambayo anastahili, kwasababu Dunia au ulimwengu kwa ujumla ni sehemu ya matokeo yaliyo na chanzo fulani.
Kwa maana hiyo basi, hayo maisha ambayo unayaishi sasa na namna watu wanavyokuchukulia bila kujali muonekano wako wa kimwili au jinsia yako, kuwa na uhakika hayo ni matokeo yaliyoletwa na hiyo mbegu ambayo ipo ndani ya mwili wako.
Najua kunamtu anaweza akasema sasa Mimi nnamakosa gani yaani makosa afanye mtu mwingine halafu tabu nije nizipate Mimi? Jibu ni kwamba, wewe ni yule yule tofauti hapo ni nyakati na mwili ila mbegu ni ile ile tu.
Kwahiyo hakuna mtu mwingine ambae alifanya hayo makosa bali ni wewe mwenyewe ila ni vile tu hauwezi kumbuka na pia hakuna mtu mwingine ambae alifanya wema ni wewe ila hauwezi kukumbuka.
Na ili uelewe vizuri hapa ni kwamba duniani wapo watu ambao wanaishi maisha mazuri yaani luxury life ila hayo maisha mazuri wanayoishi hawajawahi yagharamia wao wenyewe, unakuta mtu tangu anazaliwa hajawahi nunua nguo kwa pesa yake, hajawahi nunua simu, hajawahi jilipia Kodi ya nyumba wala hajawahi jinunulia gari kwa pesa yake, wala hajawahi jilipia nauli kwa pesa yake kwenda nchi tofauti tofauti ila vyote hivyo anavyo na anaishi maisha mazuri kupitia watu.
Yaani unakuta hata kazi ya maana hana ila anapewa gari, anapewa nyumba, anapewa OFA ya safari ya hapa na pale, tena wala sio kwamba analazimisha ila ni vitu ambavyo huja kwake venyewe. (Hapa sizungumzii wale wadangaji na wenye mambo ya hovyo nazungumzia wale ambao wako na akili timamu na ni watu wa maana sana ila wamejikuta tu maisha yao yanaenda kimtindo huo kiasi cha kufanya hata wao wasielewe ni kwanini mambo huwa hivyo ila kimsingi hayo yote ni matokeo ambayo yamesababishwa na maisha yaliyopita na ndio hapa sasa ambapo tunasema karma)
Pia kuna watu ambao utakuta wao ni wapole sana na wako na mionekano ya upole hata kwa sura zao ila ni watu ambao huogoza kuteswa na watu au kuonewa na watu wengine bila sababu za msingi, yaani unakuta Kila sehemu ambayo anaenda hatendewi vizuri na watu wa eneo hilo kiasi cha kufanya ajihisi labda ako na mikosi ila wala sio mikosi bali ni matokeo yaliyosababishwa na mbegu iliyopo ndani mwako kwa kuzingatia yale maisha ya nyuma na hiyo ndio karma.
Pia wapo watu ambao wao kazi yao ni kusaidia wengine tu, na kuna wakati mwingine si kwamba wako na kipato kikubwa kifedha ila hicho hicho kidogo unakuta wanagawana na wengine, na unakuta kutokana na tabia zao hizi wanapokua kwenye ndoa wanapata wakati mgumu kwa wenza wao kwa maana wanajikuta hadi wanachukiwa au kuachwa kabisa kwa maana maendeleo hakuna ila mtu kila akipata pesa lazima apatane na kipengele cha kutoa msaada na hii huendelea hadi mwisho wa maisha yake.
Haya yote ni matokeo yaliyosababishwa na maisha yaliyopita na hiyo ndio karma yenyewe, kiufupi matokeo yanayofuata taratibu za kilimwengu huwa ni ya kimsimu, kwahiyo hutokea zama hadi zama.
Ndio maana kila jambo ambalo utalifanya kiroho matokeo yake huwa ni ya kiroho na si yote unaweza yashuhudia kwa zama hizi ulizopo na kila jambo ambalo hufanyika kimwili matokeo yake huonekana kimwili na haya lazima utayaona kwa haraka sana, ingawa pia yapo mambo ambayo huathiri maeneo yote mawili kwa maana kiroho na kimwili katika wakati mmoja.
Na hupaswi kusahau ya kwamba ili upate mbegu bora lazima ujitahidi kuutunza mche uliobeba mbegu hiyo.