Angel Msoffe
JF-Expert Member
- Jun 21, 2011
- 6,781
- 1,639
hivi uongozi ni kipawa toka kwa Mungu au Elimu?
Kwenye misiba utani ni kitu cha kawaida sana,huwezi jua kama anautani na ukoo huo au anautani na kabila hilo.
Kwenye misiba utani ni kitu cha kawaida sana,huwezi jua kama anautani na ukoo huo au anautani na kabila hilo.
wenye Elimu kubwa mbona ndiyo wezi wakubwa. Hata kama hajasoma watamchagua tena tu na safari hii ccm itajuuuuuta kurudia uchaguzi Arusha mjini maanake wanazidi kuongeza chuki ndani ya jamii dhidi yao. Mimi nakaa pembeni natazama huo mpambano maanake Arusha huwezezi mwambia mtu kuhusu CCM akakuelewa. Sijui watakuja na mbinu gani? Elimu nini bana sisi tunataka maendeleo tu na siyo vinginevyo
:rockon:[/QUOT
tatizo sio kuangalia yupi ataiba na yupi hawezi,tatizo kubwa ni je tukiibiwa tutajua kama tumeibiwa??tuna elimu ya kutosha juu ya nchi yetu....usifkiri viongozi wa nchi zilio endelea hawapendi kuiba,wanataka ila haiwekani kwakua wanamchii wana elimu ya kutosha juu ya nchi yao,wana wabana kila sekta!!!
Lema, wakili wapigana vijembe mahakamani Send to a friend
Wednesday, 14 March 2012 19:14 Peter Saramba, Arusha
VIJEMBE na malumbano kati ya shahidi wa kwanza wa upande wa utete, Godbless Lema na wakili , Alute Mughwai anayewawakilisha wadai katika kesi kupinga matokeo ya ubunge katika Jimbo la Arusha Mjini, ni miongoni mwa mambo yaliyotawala ukumbi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha jana.
Hali hiyo ilimlazimisha Jaji Gabriel Rwakibarila, kuingilia kati mara kwa mara na kutoa muongozo ili kuokoa muda wa mahakama.
Malumbano hayo yalisababishwa na aina ya maswali kutoka kwa wakili Mughwai na majibu ya Lema ambaye ni Mbunge wa Arusha Mjini na ambaye ni mdaiwa wa kwanza katika shauri hilo lililofunguliwa na wapiga kura watatu.
Walalamikaji hao ni, Mussa Mkanga, Agnes Mollel na Happy Kivuyo wanaoimba mahakama, kutengua ushindi wa Lema kwa madai kuwa alitumia maneno ya kashfa na udhalilishaji dhidi ya aliyekuwa mgombea wa kiti hicho kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Batilda Burian.
Baadhi ya hoja zilizozua malumbano kati ya wakili na shahidi huyo ni pamoja na hatua ya Mughwai kuhoji kama shahidi anajua mila na desturi za kabila la Waarusha (Wamaasai) na Wachagga zinazowabagua wanawake katika nafasi za uongozi wa kimila na zile za kupigiwa kura
Mimi siyo kiongozi wa kimila, bali ni kiongozi wa kisiasa na kiserikali, hivyo sijui mila na desturi za uongozi wa kimila za jamii ya Waarusha, Wamaasai na Wachagga. Kwa nafasi yangu ya ubunge mimi ni kiongozi wa makabila yote yaliyoko katika Jimbo la Arusha Mjini wakiwemo Wanyaturu na wewe (wakili Mughwai),
Akijibu swali kuhusu sababu za kutokuwapo kwa mwanamke aliyewahi kuchaguliwa kushika nafasi ya ubunge katika wilaya za jamii ya Waarusha, Lema alidai wengi wamejitokeza kugombea akiwamo mgombea wa Chadema aliyegombea katika Jimbo la Longido lakini hawakuchaguliwa.
Alisema wanawake hao hakuchaguliwa katika kura za jumla au kura za maoni ndani ya vyama kama ilivyotokea kwa wakili huyo aliyeshindwa kwenye katika kura za maoni ndani ya CCM katika Jimbo la Singida Mashariki.
Baadhi walishindwa kwenye kura za maoni kama wewe ulivyoshindwa kule Singida Mashariki. Wengine walishinda kura za maoni lakini hawakuchaguliwa na wananchi kwenye uchaguzi mkuu kama ilivyokuwa kwa Dk Burian hapa Arusha, alidai Leman na kufanya wasikilizaji kuangua kicheko.
Shahidi huyo aliendelea kumrushia maneno wakili Mughwai baada ya kudai kuwa amedanganywa na wateja wake kwa kumweleza kuwa aliomba Dk Burian asichaguliwe kwa sababu siyo mkazi wa Arusha.
Alidai kuwa kisheria, Mtanzania yeyote ana haki ya kugombea ubunge katika jimbo lolote bila kujali ukazi wala asili yake ya kuzaliwa.
Kwamba nilisema Dk Burian asichaguliwe kwa sababu ni mkazi wa Zanzibar ni hoja ya uwongo na mufilisi, wateja wako wamekudanganya sana kuhusu hilo kwa sababu hoja hiyo isingefanya asichaguliwe ndiyo maana mimi ni mchaga wa Hai, Kilimanjaro lakini nimegombea Arusha na kushinda na leo ni mbunge wako, alidai Lema.
Kauli ya kudanganywa na wateja wake, ilionekana kumkera wakili Mughwai na kuamua kumuonya kwa mara nyingine sahidi huyo kuacha tabia ya kumpiga misumari kwa kumrushia maneno, badala yake ajibu maswali anayomuuliza.
Kwa mara nyingine nakuonya usinipige misumari kwa kunirushia maneno. Wewe jibu maswali yangu, alisema wakili Mughwai.
Wakili Mughwai anayesaidiana na Modest Akida kuwakilisha wadai katika shauri hilo, aliingia kwenye malumbano mengine na Lema alipomzuia kumalizia kukariri maneno yake kuhusu mikopo kwa wanawake, aliyoyatamka katika mikutano yake ya kampeni kitendo kilichomfanya shahidi kukataa kujibu swali lake hadi atakapomaliza kukariri maneno yote.
Kitendo hicho kilichomfanya Jaji Rwakibarila kuingilia kati na kumruhusu amalizie.
Lakini alipoanza kukariri maneno hayo, kuhusu taratibu ngumu za mikopo kwa wanawake, wakili Mughwai aliingilia kati na kumtaka ajirejeshe nyuma na kuzungumza kama vile anahutubia mkutano wa hadhara mwaka 2010, kitendo kilichomfanya mbunge huyo kuanza kwa kauli mbiu na salama ya Chadema ya Peoples huku wasikilizaji wakiitikia power .
Hapana, hapana, hiyo ya peoples power acha kwa sababu muda hautoshi, rudia tu maneno yako kuhusu mikopo kwa akina mama kwa kukariri maneno halisi uliyoyatamka kwenye mikutano yako ya kampeni kuhusu hoja hiyo, alisema wakili Mughwai akimkatisha Lema.
Awali hoja kuhusu utata juu ya elimu ya mbunge huyo iliibuka baada ya wakili Mughwai kuhoji taarifa zake za elimu zilizopo katika kumbukumbu za nyaraka za bunge, hoja iliyojibiwa na shahidi huyo kuwa imetokana na makosa ya uchapaji uliosababishwa na Bunge lenyewe akidai tayari aliiandikia ofisi ya Bunge kuelezea hilo na kutaka marekebisho.
Elimu ya Mbunge wa Jimbo la Arusha mjini, GODBLESS LEMA aliyoieleza Mahakamani wakati ya kesi inayomkabili kufuatia ushindi wake wa Ubunge jimboni humo ni tofauti kabisa na ile iliyoko kwenye profile yake iliyooneshwa kwenye tovuti ya Bunge. Aidha hakuna ukweli wa moja kwa moja wa CHUO ambacho Mh. huyo mwenye Mbwembwe sana alichosomea.
Hebu tuangalie hii ya bunge ilivyo na utata yenyewe kwanza:
- Kamaliza darasa la saba 1989 na kuanza kidato cha kwanza kwaka huohuo wa 1989. Je hii inawezekana?
- Ameanza kidato cha kwanza mwaka 1989 na kumaliza 1991. Je miaka hiyo elimu ya kidato cha nne ilikuwa ni miaka 3 badala ya minne?
- Amemaliza kidato cha nne mwaka 1991 na mwaka huohuo akaanza kidato cha tano. Je hili liiikuwa linawezekana?
- Hii Diploma aliyosoma Cambridge College ni ya nini? siasa? uchumi? fundi mchundo? au nini?
Iko haja sasa Sheria ifuate mkondo kwa TCU kukagua CV za Wabunge wetu ili kuepusha Nchi yetu kuingia katika majanga yatakayosababishwa na Wanasiasa wa aina hii.
GENERAL Salutation Honourable Member picture
First Name: Godbless Middle Name: Jonathan Last Name: Lema Member Type: Constituency Member Constituent: Arusha Mjini Political Party: CHADEMA Office Location: Box 16531, Arusha Office Phone: +255 764 150747 Ext.: Office Fax: Office E-mail: Member Status: Date of Birth
EDUCATIONS School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level Kalangala Primary School Primary Education 1983 1989 PRIMARY Geita Secondary School O-Level Education 1989 1991 SECONDARY Kolila Secondary School A-Level Education 1991 1993 SECONDARY Cambridge International College Diploma 2008 2010 DIPLOMA Cambridge International College Degree 2010 Todate NOT COMPLETED
CERTIFICATIONS Certification Name or Type Certification No. Issued Expires
EMPLOYMENT HISTORY Company Name Position From Date To Date The Parliament of Tanzania Member - Arusha Urban Constituency 2010 2015 PTN Chief Executive Officer (CEO) 2007 2008 Tanzania Labour Party, TLP District Secretary General 2005 2008 DENETRIA Director 2005 2008
POLITICAL EXPERIENCE Ministry/Political Party/Location Position From To Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Member of Parliament 2010 Date Tanzania Labour Party, TLP District Secretary General 2005 2008 Tanzania Labour Party, TLP Candidate, Member of Parliament 2005
PUBLICATIONS Description Published Date Lema Godbless: Msaada wa haraka kutoka katika Biblia, Arusha 2008 Godbless Lema: Wisdom Time, Arusha 2008
SPECIAL SKILLS Skill Name or Description Years Experience Acquired Through Skill Level
RECOGNITIONS Recognition Type Recognition Date Reason Action Taken Issued by
Wakati huu hapakuwa na sheria ya kuandikwa wala mikataba ya kimataifa.bila elimu wanakuwa hawajiamini,wakiona karatasi na kingereza ni kutetemeka tu.hivi mkuu bila wabunge kuwa na elimu nani? Atabadilisha sera ya madini,na nyingine kibao ambazo ni mbovu ajabu.ebu tafuta tu gvt public yeyote,then tafakari mtu kama lusinde atachangia nn?.tunaangalia uwezo wa mtu katika uongozi na si elimu ya mtu katika uongozi, babu zetu hawajui hata kusoma lakini wametuongoza kwa busara
Nimefuatilia hoja zako zote na nimegundua huna lolote zaidi ya chuki binafsi,kote ulikochangia kuusu lema point yako ya msingi imekua ni personality na ulipoona haueleweki umetafuta jingine la msibatatizo sio elimu hapa..tatizo ni kua godbless lema hana personality ya kuongoza jimbo lenye hadhi kama hili la arusha...unaweza kusoma mbaka nywele zika nyonyoka ila ukakosa lhekima..hana hekima kabisa.....mie nimemuona kwa macho yangu nilipo kwenda kwenye kilio cha dada mmoja hapa arusha,wakati ndugu wa marehemu wakilia kwa uchungu kwa kupotelewa na msichana mdogo huyu lema akaingia kwenye nyumba yenye msiba.....alipo ingia unaweza sema petrol station inatembea,alikua ananukia breweries ya kutosha..huku watu wakiwa na huzuni kubwa,akasema "jamani msilie sana,ni swala la kuomba tu ili arudi tena dunia,haya jamani tumuombee afufuke"hiyo kauli iliwafanya ndugu wengine marehemu kutoka nje......sasa hii ni kutokua na hadhi ya uongozi!!!