Elimu na nadharia ya muziki

Melody ya Muziki- Melodic Contour and Melodic Motion

Mkong’osio au melody ndiyo sehemu kubwa ya muziki ambayo hukumbukwa sana na wasikilizaji kwani ndiyo inayoingia sana ubongoni mwa msikilazji; ni muungano wa sauti inayobadilika badilika kwa vipindi mbalimbali kadri muda unavyokwenda. Melody nzuri ni zile zinazofananana na mazungumzo yanayohusisha maswali na majibu; yaani zina vipindi vyenye msukumo au maswali (tension) sana na vipindi vyenye kuondoa msukumo huo au majibu ya maswali (tension release).

Post hii isome kwa makini sana kwa sababu ndiyo inajenga msingi wa kutunga nyimbo zinazoweza kuingia sana kwenye ubongo wa msikilizaji na hivyo zikawa za kukumbukwa kwa muda mrefu sana. Nadhani sehemu hii ndiyo ambayo wanamuziki wetu wengi sana hawaijui, kwani nimechambua nyimbo zao nyingi na kuona kama zinatungwa kwa uvumbuzi (intuition) tu na mara nyingi hazinagalii ukweli huu. Jikumbushe tena maana ya phrase na measure kwenye wimbo lama tulivyozijadili huko nyuma.

Kumbuka tena kuwa katika sauti zote 12 za kwenye Octave moja ni sauti saba tu zinashabihiana, ambazo mwanzoni tulizionyesha kwa namna za kirumi I-II-III-IV-V-VI-VII, tukimalizia na sauti ya nane VIII ambayo ni sauti ya kwanza kwenye kwenye Octave inayofuata. Zile sauti 12 za octave hujulikana pia kama chromatic scale, wakati sauti hizo saba zinazoshabihiana hujulikana kama diatonic scale. Sauti hizi za diatonic scale kuanzia ya chini hadi ya juu ndizo zina majina kama ifuatavyo kwenye jedwali hili:

SautiJinaMatumizi
ITonic
Sauti za kupumzikia; hutumika mwanzo na mwisho wa phrase moja
IISupertonic
IIIMeadiant
Sauti za kuhama kutoka na kuingia kwenye tonic
IVSubdominant
VDominant
Sauti za Kuchangamsha, yaani zenye msukumo sana
VISubmediant
VIILeading tone
VIIINext tonicSauti ya kupitia kuingia na kutoka kwenye octave inayofuata.


Kwenye utunzi wa melody sauti hizi zimegwawanya katika mafungu mawilii; yaaini stable tones na unstable tones. Sauti za Tonic, Mediant na Dominant ndiyo ndiyo stable tones, halafu zile Supertonic, Subdominant, Submediant, na Leading tones ni unstable tones. Tonic (I) ni stable zaid ya ikifuatiwa na Dominant (V) na kuishia na Mediant (III) kwa stability. Sauti ya Leading note (VII) ndiyo ambayo ni unstable zaidi ikifuatiwa na Sebmediant (IV) halafu Supertonic(II) na kushia na Subdominant (VI). Picha hii inaonyesha mlingano wa stability katika sauti hizo.

View attachment 1183739

Kwa waliofanya physics ya pendulum ukihusisha na potential energy, mnajua kuwa pendulum bob ikiwa inaning’ia freely chini ya kamba yake inakuwa stable kwa sababu potential energy ni ndogo sana; ukiiacha katika position hiyo, itabaki imepumzika pale pale, ila ukiihamisha kutoka hiyo stable position, basi itaanza kuswing kujaribu kurudi kwenye stable position yake. Ina maana unapoihamisha kutoka kwenye stable position yake basi unaiweka kwenye unstable position ambayo siyo comfort zone yake.
View attachment 1183740


Sauti za diatonic scale pia zina tabia hiyo hiyo, hizo unstable tones zinakuwa zinamfanya msikilizaji atake zirudi kwenye kweye stable tones. Siku zote Leading tone itapenda kuingia kwende Dominant siku zote, na Submediant nayo itapenda kuingia kwenye Dominant siku zote. Sauti za Subdominant nazo zitapendwa kwenye kwenye Dominat kwa vile ni stable zaidi ya Mediant; hata hivyo inaweza kwenda kwenye Mediant na kukubalika. Supertonic nazo zitapenda zaidi kwende kwenye tonic kwa vile hiyo ni stable zaidi ya median, lakini pia zinaweza kuingia kwenye mediant na kukubaliwa bila matatizo yoyote.

View attachment 1183741


Kama tulivyosema huko nyuma wimbo mzuri huanza kwa sauti za Tonic au Supertonic lakini pia unaweza kuanza na Dominant kwa vilanayo ni stable tonic, lakini ni lazima kushia na sauti za Tonic kwa vile hiyo ndiyo sauti stable kuliko zote. Kutoka kwenye sauti stable na kelekea kwenye sauti unstable kunaweka msukumo mkubwa yaani tension ambayo humfanya msikilizaji atake iondolewe kurudi kwenye stable tena ambayo ndiyo comfort zone ya ubongo; kipindi hicho cha sauti unstable kinajulikana kama Continuation, kwamba ukishaiingia kwenye unsatable tone, basi msikilizaji anategemea uendelee ili urudi kwenye stable tone tena. Continutiation hutokea sehemu yotote katikati ya phrase, kabla phrase haijaisha lazima tension iondolewe kwa kiasi fulani. Wakati tension inaondolewa, inaweza kurudi kwenye stable kabisa yaani Tonic au kwenye less stable za Dominant au Median. Mapumuziko katika stability tone ya tonic inaitwa Finality, yaani hali inayomuashiria msikilizaji kuwa mambo yamekwisha. Mapumizko katika satuti za Dominant au Submediant yanajulikana kam Temporary repose, yaani mapumziko mafupi yanayompa msikilizaji nafasi ya kupumua akijua kuwa safari bado inaendelea.

Kwa kawaida melody nzuri hairudi kwende Tonic kabla shairi lote halijaisha, kwa hiyo wakati wa kumaliza phrase ndani ya shairi unaweza kuingia kwenye Mediant au Dominant, yaani temprora repose lakini usiashiririe finality. Kuondoa tension kabisa, yaani finality, hutokea mwisho kabisa wa shairi ambapo ndipo unarudi kwenye Tonic. Melody inatakiwa iwe inamjaza msikilzaji tension yaani upepo, na kuuondoa kidogo na kujaza tena na kuondoa kidogo hadi kufikia mwisho ndipo unaaondoa upepo wote na kufanya ubongo upumzike tena. Mambo haya ya kumjaza msikilizaji upepo na kuuonda hufanyika pia kwenye Vibwagizo Tangulizi, Vibwagizo na Vivuko; Utangulizi ni sauti unstable tu, Tamatisho ni sautu stable tu lakini Mapumuziko piayanachanganya suti satble na unstable tu. Hata hivyo, kwa vile Vibwagizo tangulizi vinamtayarisha msikilizaji kuskia kibwagizo, huwa haviishii na Tonic, vinaweza kuishia na Mediant au Dominant.

Melodic Motion na Melodic Contour

Mtungaji wa wimbo, iIangalie melodi kama safari ya kupanda mlima wenye maumbile (contour) mbalimbali zenye vilima na mabonde yanayoruhusu mapumziko kidogo ndani na kisha mwishoni ni kushuka chini kabisa; safarihiyo hujulikana kama melodic contour. Upandaji, mapumziko na kushuka huo mlima hujulikana kama melodic motion. Kila utunzi una contour yake; safari inaweza kuanza kwa kuingia bondeni kabla ya kupanda tena, na vile vile inaweza kuanza kwa kurukia juu klabisa ya mlimna na baadaye kuanza kutua. Contours zenye tension (contiuation) nyingi na mapumziko ya kati (temporary repose) mengi kabla ya kufikia mwisho (finality) hufanya ubongo wa msikilizaji kuwa busy sana na iwapo unapanda kwa spidi sana, yaani kama BPM yake ni kubwa sana basi unaweza kumchosha kuzikiliza haraka sana. Kukiwa na uwiano mzuri kati ya BPM na wingi wa vilima na mabonde kwenye controur hiyo, basi msikilzaji ataburudika sana na ataupenda sana wimbo huo.

Melodic contour nzuri ni ile yenye mlingano mzuri kati kupanda na kushuka na ina kilele (peak au sauti ya juu kabisa) moja tu, ambacho kinatakiwa kwenye sehemu ya pigo moja kubwa kwenye rhythm yako. Tofauti kati ya sauti yza chini kabisa sauti ya juu kabisa hitwa range. Melodic contrours zenye range kubwa ndizo zenye tension sana na vile vile ndizo zinazosisimua sana kuliko zile zenye range ndogo. Mifano ya michache ya melodic Contours ni kama hizi zifiatayo; kila sehemu tambarare (palateau) ni sehemu ya kuondolea tension na kwenye slope ni sehemu yenye kujaza tension.
View attachment 1183750View attachment 1183751

Mahairi ya wimbo wa Kwangaru wa Harmonize yanatumia melodic contour rahisi kama hii lakini yana peak moja kwa kila shairi, na range ya wimbo ni kubwa sana, ndiyo maana wimbo huo umekubalika sana, hauchoshi kirahisi.
View attachment 1183753
Ingawa kibwagizo chake kina contour tofauti.

Kwenye mwendo huo wa melodic motion, kutoka point moja hadi nyingine, sauti zitakuwa zinabadilika kwa kutumia mojawapo ya style nne: (a) sauti zinazojirudia (repeats) kwa mfano kutoka sauti C hadi sauti C tena; (b) sauti zinazoruka kwa noti moja moja kwenda juu au chini (steps) kwa mfano kutoka sauti C mpaka sauti D kwenye C-major; (c) sauti zinazoruka noti mbili kwenda juu au chini (skips) kwa mfano kutoka sauti C mpaka sauti E kwenye C-major, na (d) sauti zinazoruka zaidi ya noti mbili kwenda juu au chini (leaps) kwa mfano kutoka sauti C mpaka sauti G kwenye C-major. Picha hii inaonyeshaa style hizo.

View attachment 1183756

Ili kupata uwiano mzuri kati kati ya kupanda na kushuka kwenye contror yako, ukianza na steps kadhaa za kwenda upande mmoja, basi jaribu kuweka skips au leaps za kurudi upande ulikotoka kidogo kabla ya kurudi kwenye upande wa kwanza tena kama bado unaendelea, ila bila kuingia kwenye sauti stable tones. katika kufanya hivyo, punguza sana matumizi ya repeats kadri iwezekanavyo, na vile vile usiwe na steps nying sana.

Kati ya mapungufu makuu ya wimbo wa Diamond wa My Number one original ni kuwa una steps na repeats nyingi sana na vile vile hauna peak inayojulikana wazi wazi kwenye kila phrase, yaani range yake ilikuwa ndogo sana; hivyo ilikuwa ni rahisi kwa wimbo huo kuchosha msikilizaji wake haraka sana. Remix waliyofanya Davido ilirekebisha sana makosa hayo wakabadilisha steps nyingine kuwa skips na hivyo kuweza kuwa na peak kubwa kidogo kuliko mwanzo. Kupendwa wa My Number One remix hakutokani na davido tu bali vile vile ile balance ya tension na tension release iliyokuwapo kwenye wimbo huo tofauti na ule original ambao haukuwa na tension kabisa.

Katika Makala ijayo, nitaongelea dhana tatu kubwa kabla ya kuanza kutunga melodies zetu wenyewe na kuchambua melodies za waimbaji wengine; dhana hizo zitakuwa ni articulation, melodic motiffs na melodic phrases.

Tuendelea kutumia sauti za diatonic major na minor scales tu japokuwa kuna scales nyingine nyingi ambazo siyo diatonic (non diatonics scales), na ambazo siyo diatonic ambazo siyo major au major au minor (zinaitwa diatonic scale modes), lakini kama nilivyotambulisha huko nyuma, mambo hayo tatawaachia maveterani tu. Sisis tutatumia diatonic major na diatonic minor tu.


Wasomaji wangu wakuu nkumbison, Madaga, Gyole, Extra miles, MzaramoTz , Frega Bao,MRI; nadhani mjadala huu hili kuhusu melodic motion na melodic contours za nyimbo umeeleweka. Nimegundua kuwa kabla ya kuanza mjdala juu ya utungaji wa mkong'osio wa wimbo bado kuna mambo ya msingi kujadilia.katika mada ijayo tutajadili articulation, melodic motiffs na melodic phrases
Bado nakusoma na nazidi kukuelewa na kuyaelewa mengi zaidi. Maswali na comment zangu zitafuata kila ninapomaliza somo moja maana nimejipa muda wakuzielewa hizi nadharia kabla yakupractice!
Tupo pamoja maan naupenda sana muziki kuanzia kuuimba mpaka kuuandaa ila natumia kipaji zaidi so hapa pananitamanisha ku deal na hii elimu kiundani zaidi.
 
Ninapoandika kwa mara ya kwanza huwa sisomi sana post hiyo hadi baadaye ndipo nairudia. Kila ninaporudia hukuta typing errors na mambo kama hayo, na hujitahidi kuyarekebisha. Ukisoma post yangu mara ya kwanza ukakuta ina maneo yasiyo-make sense, au kuna obvious typing error, ujue nitakuja kuyarekebisha baadaye kidogo kidogo. Chukua muda uisome tena baadaye unaweza kukuta makosa hayo yamekwisha haririwa
 
Pa1
Ninapoandika kwa mara ya kwanza huwa sisomi sana post hiyo hadi baadaye ndipo nairudia. Kila ninaporudia hukuta typing errors na mambo kama hayo, na hujitahidi kuyarekebisha. Ukisoma post yangu mara ya kwanza ukakuta ina maneo yasiyo-make sense, au kuna obvious typing error, ujue nitakuja kuyarekebisha baadaye kidogo kidogo. Chukua muda uisome tena baadaye unaweza kukuta makosa hayo yamekwisha haririwa
 
Ninapoandika kwa mara ya kwanza huwa sisomi sana post hiyo hadi baadaye ndipo nairudia. Kila ninaporudia hukuta typing errors na mambo kama hayo, na hujitahidi kuyarekebisha. Ukisoma post yangu mara ya kwanza ukakuta ina maneo yasiyo-make sense, au kuna obvious typing error, ujue nitakuja kuyarekebisha baadaye kidogo kidogo. Chukua muda uisome tena baadaye unaweza kukuta makosa hayo yamekwisha haririwa
Sawa mkuu
 
Melody ya Muziki- Articulation and Dynamics.
Tumeshaongea mengi kuhusu nadharia ya muziki. Zaidi ya kujua muda unavyotumika katika kujenga mdundo wa mziki kuanzia noti mbili (breve) hadi sehemu moja ya kumi na sitini na nne ya noti (hemidemisemiquaver) na muundo wa phrases na measures katika muziki, sasa hivi tunajua pia dhana kama octave, chromatic scales, major diatonic scales, minor diatonic scales, major chords, minor chords, tonal stability, tonal tendencies, melodic contours, melodic movements, sehemu kuu za wimbo, na miundo mbalimbali za nyimbo.

Kabla ya kuanza kujadili namna ya kutunga melody nzuri, inabidi tujabili vipande vikuu vinne vinavyotengeza melody ya muziki. Kama nilivyotambulisha huko nyuma kdiogo, tutahitaji dhana za melodic articulation, dynamics, motif, theme, na melodic phrases. Articulation na dynamics kwa pamoja hueleza jinsi sauti za muziki zinavyotoka, yaani muda unaotumika kutoa sauti zile na nguvu inayotumika (time and strength). Sauti ile ile inaweza kutoka kwa namna kadhaa ambazo zimepewa majina ya kitaliano; sijui kwa nini alama nyingi za muziki hutumia lugha ya kitaliano. Articulation inaonyesha muda unaotumika katika kutoa sauti fulani kwa namna tofauti tofauti na kwa nguvu nguvu ya ain fulani, wakati dynamics huonyesha jinsi ya kubadili nguvu ya sauti hiyo hiyo hiyo. Ingawaje msikilizaji wa muziki ambaye haweki attention kwenye details hawezi kuona impact ya hizi effects za articulation na dynamics, kwa jumla huwa zinasaidia sana katika kutofautisha tungo makini na tungo za harakaharaka. Majaji wa Music Awards kubwa kubwa kama Grammys (siyo za online voting kama AFRIMMA) huangalia kwa makini vitu kama hivi katika kila tungo. Kwa hiyo hizi ni dhana za kiwango cha juu kidogo (Advanced) kwenye muziki, lakini nimeona nizitangulize hapa kwanza kabla sijaingia kwenye tungo kwani kuna mahali zinaweza kuhitajika kwenye tungo tutakazojadili huko mbele. Katika Makala hii niazungumzia Articalutaion na Dynamics, ila nitaaza na kuelezea Dynamics halafu nitamalizia na Articulation, halafu Makala ijayo ndipo tutakapojadili motifs, melodic themens na melodic melodic phrases kwa pamoja.

Dynamics

Kama nilivyosema hapo juu, dynamics inaonyesha nguvu inayotumiwa kwenye kutoa suati Fulani; kuna aina mbili: guvu sana (loud) na nguvu kidogo (soft). Majina ya kitalaiano yanayotumiwa kuonyesha nguvu hizo ni piano inayoonyesha nguvu kidogo (soft), hii huonyeshwa kwa alama p na nyingine ni forte inayoonyesha nguvu kubwa (loud) ambayo huonyeshwa kwa alama f. Alama hizo zikitanguliwa na herufi m ambayo maana yake ni mezzo, basi huzipunguzia makalai yake, mp (mezzo-piano) ni soft lakini siyo sana, na mf (mezzo-forte) ni loud lakini siyo sana. Kwa kawaida mp na mf zina maana moja. Alama hizo za f na p zikitumika mbili kwa mpigo huwa zinazongeza msisisizto wake mara mbili, yaani pp (piannissimo) maana yake ni soft sana, na ff (fortissimo) maana yake ni loud sana. Iwapo zitatumika mara tatu, basi zinaongeza misistioza mara tatu, kwa mfano ppp (pianississimo) ni soft sana sana, fff ni loud sana sana.

1566499120265.png


Wale maveterani wa muziki huweza kuchanganya alama hizo kutoa dynamics nzuri zaidi, kwa mfano fp ambayo maana yake ni forte-piano, kwamba unaaza kwa sauti kubwa halafu unamalizia na sauti laini. Video hii imeongelea dhana hizo na kutoa mifano mizuri



Kipande hiki cha wimbo nadhani kitaelewa vizuri kwa wasomaji waliopitia Makala zetu za nyuma.
1566499153615.png


Time signature yake ni robo noti nne nne kwa kila measure, beat yake ni robot noti 110 kwa dakika; wimbo unatumia vyombo vinne: Classical guitar, Acousting Guitar mbili na Acoustinc Bass guitar moja. Classical guital linapigwa katika chords zinazochanganya sauti nne nne na sauti tatu tatu likitumia chords za C-major, A-Minor, F-Major, G-major na D-minor ya sauti nne; ukisoma vizuri utaona kuwa chord hizi zina inversions fulani fulani ambazo mtunzi hakuonyesha waziwazi, nadhani akitegemea msomaji atazielewa tu. Mistali (Phrases) yake inarudiwa mara mbilimbili. Neno ambalo halieleweki hapa ni “Swing” chini ya alama ya beat. Ingawa neni hilo lina maana nyingie (ambayo hatujajadili) kwenye rhythm ya muziki, lakini matumzi yake kwenye kipande hili ilikuwa ni kuonyesha kuwa wimbo huo ni kwa ajili ya mtindo wa swing ambayo ilikuwa ni Jazz ya zamani ya kimarekani iliyokuwa inapigwa katika scale ya C-major.

Accoustic Guitar ya kwanza inapigwa kwa pianissimo, halafu acoustic guitar ya pili inapigwa katika mezzo-forte, wakati ile acoustic bass guitar inapigwa katika piano kwanza ikifuatiwa na mezzo-piano. Kama kuna alama kwenye wimbo huu sijaiongelea, msomaji anaweza kuuliza swali kwa kuweka comment hapa chini. Nadhani labda alama ambayo sijaongelea ni ile ya upinde kuunganisha sauti mbili yaani
1566499448301.png
, ambayo nitaiongelea baada ya muda mfupi.


Katika kuelezea dynamics watunzi huonyesha pia jinsi sauti zinavoweza sauti zitakavyokuwa zinaongeza au kupungua, yaani badala ya kukurupuka na sauti ya juu au ya chini, kipande cha muziki kinaweza kuanza na sauti ya juu na kuishia na sauti ya chini, au kuanza na sauti ya chini kikiishia na sauti ya juu kwa ukuaji wa polepole (gradual). Alama itumiwayo kupandisha sauti pole pole ni
1566499641188.png
ikimaanisha Crescendo; halafu alama itumia kupunguza sauti pole pole ni
1566499696894.png
ikimaanisha Diminuendo au Decrescendo.

Angalia matumizi ya alama hizo kwenye wimbo huu wa kijapani
1566499765674.png


Video hii inaweza kusaidia kueleza dhana hizo mbili za Crescendo na Decrescendo



Wimbo huu wa Because I am your lady ulioimbwa na Celine Dion umetumia sana dynamics hizo za Piano, forte, Crescendo na Decrescendo



Articulation

Articulation hueleza namna sauti mbalimbali zitakavyotolewa. Ingawa kuna namna nyingi sana za articulation, aina kuu zimegwanyika katika makundi mawili, kundi la kuunganisha sauti mbili au zaidi kusikika kama kama sauti moja, na kundi kutoa sauti moja kwa urefu (wa muda) tofauti tofauti. Kuunganisha sauti mbili hufanywa kwa kutumia ama ties (mafundo ya sauti zinazofanana) au slurs (mafundo ya sauti tofauti). Sauti mbili zinaweza kuunganishwa kusikika kama sauti moja isiyobadilika kwa kutumia ties, na sauti zinazobadilika au huweza kuunganishwa kusikia kamka sauti moja inayobadilika kwa kutumia slurs. Zote ties na slurs huonyeshwa kwa alama ya upinde kwenye virungu vya noti kama ifuatavyo; upinde huo unaweza kuwa juu au chini kulingana na uelekeo wa mlingoti wa noti hizo. Iwapo mlingoti unakwenda juu, basi upinde utakuwa chini, na iwapo mlingoti unatazama chini basi upinde utakuwa juu.
1566500062666.png

Kwenye video hii, nadhani jamaa huyu amejitahidi kuonyesha maana ya slurs na ties kutumia violin kwa kiasi cha kutosha kuilewa dhana yenyewe. Kuna video nyingi unaweza kupata zinazoonyesha ties na slurs; sina video au mafaili yangu binafsi kuonyesha mifano yake.



Katika kutoa sauti kwa mida tofauti zipo aina tano kuu kama ionekanavyo kwenye picha hii hapa chini; noti iya sauti husika inawekewa alama ya ziada juu au chini ya kirungu chake (accent mark)
1566500158122.png

Aina hizo tano ni kama ifuatavyo:
(a) kutoa sauti katika muda wake wote (tenuto), yaani kama ni robo noti basi inatoka muda wote wa robo noti; sauti hizo huonyehswa kwa mastali mdogo juu yake kama hivi .
1566500814528.png
Kwa jumla, kama sauti haina alama yoyote juu yake basi hiyo pia ni tenuto, ingawa watunzi wengine hutaka tenuto iwe ndefu kidogo kuliko noti isiyokuwa na alama.
(b) kutoa sauti katika nusu ya muda wake tu (stacatto) yaani sauti ya robo noti inatoka kwa muda ambao ni nusu ya robo noti, karibu sana na sehemu moja ya nane ya noti kamili; sauti hizo huonyeswha kwa kuwa na doti juu ya noti zake kama hivi
1566500948310.png

(c) kutoa sauti katika robo ya muda wake tu (staccatissimo), yaani robo noti inatoka kwa muda ambao ni robo ya robo noti karibu na sehemu moja ya kumi na sita ya noti kamili; sauti hizo huonyeshwa na pembetatu juu yake kama hivi.
1566501012255.png

(d) kutoa sauti kamili lakini ikiwa na nguvu sana kwenye nusu ya muda wake tu, na baadaye kupungua nguvu katika muda wake unaobaki (marcatto); sauti hizo huonyeshwa kwa kona inayotazama kulia ambayo hujulikana pia kama accent (huchanganya wanamuziki wengine kwani accent mark ni alama zote za articulation, wakati accent pekee bila neno mark ni articulation hii). Alama ya marcatto au accent ni hii
1566501342647.png

(e) kutoa sauti muda wote ila kwa nguvu zaidi ya sauti nyingine zinazoizunguka (marcattissimo au martellato); alama yake ni hii
1566501429891.png
.

Michanganyiko ya hizo articulation tano za msingi zinapounganiswa kwa kutumia ties na slurs tunapata articulation nyingine kadhaa ambapo maarufu ni legato ambayo ni slur ya sauti kadhaa za tenuto, na portato, ambayo ni slur ya sauti kadhaa za staccato kama ionekanavyo hapa
1566501542676.png


Sikuweza kupata video nzuri sana ya kuelezea dhana hizi, ila hii niliyochagua hapa inajitahidi kuliko nyingine zote

 

Attachments

  • 1566500934778.png
    1566500934778.png
    1.3 KB · Views: 13
Articulation -Sound effects

Katika makala iliyopita tulionyesha articulation ambazo ni za kawaida sana; hata hivyo kama nilivyokuwa nimetanguliza, kuna aina nyingi sana za articulations. Kuna mbili nyingine ambazo nimeona nizitambulishe kwani pia hutokea mara kwa mara kutoa sound effects za madoido kwenye wimbo ingawa siyo articulation za msingi; hizi ni fermata na vibrato au tremolo

Ni kawaida kuwa kuelekea kwenye mapumziko ndani ya wimbo (tonic), ile sauti ya mwisho kabla ya mapumziko au sauti ya mapumziko yenyewe huweza kurefushwa sana kuliko kawaida. Kitendo cha kuirefusha huitwa fermata na huonyeshwa kwa alama ya jicho juu ya sauti husika kama hivi
1566568040549.png


Kuna aina tatu za fermata, hiyo ya kawaida kama tulivyoonyesha hapo juu, au ndefu kupita kiasi (long fermata) ambayo na vile vile inaweza kuwa fupi tu (short fermata); aina zote tatu zimeonyeswa katika picha hii.
1566568282471.png

Video hii inatoa maelezo mazuri ni mfano wa fermata



Mwishoni kabisa mwa muziki au hata sehemu yoyote katikati ya muziki, mtunzi anaweza kutumia sauti za kutetetemeka (vibrato au tremolo). Hii huonyeshwa kwa mistali mitatu kwenye sauti husika kama hivi
1566569924876.png

Nyimbo nyingi za Beyonce hutumia sauti hizi za vibrato sana

Video hii inaonyesha mfano wa sauti za tremolo.


 
Melody ya Muziki- Motifs

Kama ilivyo katika muundo wakitabu, kuwa kina sura kadhaa, na kila sura inaweza kuwa na aya kadhaa, melody pia ina melodic phrases kadhaa na kila melodic phrase ina motifs kadhaaa. Yaani motif (au motive) ni sehemu ndogo sana ya melody inayojitegemea. Ukiunganisha motifs kadhaa basi unapata melodic phrases ambayo pia inajitegemea, na ukishaunganisha hizo melodic phrases ndipo unapata melody kamili. Tofauti na kitabu ambamo aya zote zinatofautiana, kwenye melody hizo motifs huwa zina uhusiano fulani baina yake kiasi na mara nyingi sana motif kadhaa hurudiwa sana. Wimbo mzima unaweza kuwa na motifs tatu au nne tu lakini kwa kuzibadilisha badilisha kwa mitindo fulani fulani kama tukavayojadili hapa unafikia kuwa na melody ndefu inayovutia. Katika makala haya tutajadili dhana ya motifs na katika makala ijayo ndipo tutajadili dhana ya melodic phrases na kukamilisha utunzi wa melody yote.

Motifs

Motif ni vipande vya melody vinavyojengwa kwa kutumia measure moja au mbili; hivi ndivyo vinavoelezea wazo kuu la muziki wenyewe. Motif inaweza kuanza na sauti yoyote na kuisha na sauti yoyote, melodic contour ya motiff pia inaweza kuwa ya aina yoyote ile, inaweza kupanda juu tu, kutelemka chini tu, kupanda na kutelemka na vile vile kutelemka na kupanda. Wazo lolote lile linawezekana.

Kwanza nikumbushe kuwa kabla hujaanza kutunga melody ni lazima uwe umeshaamua muundo wa wimbo wako. Kwa vile melody katika sehemu mbalimbali za wimbo hutegemea sana rhythm yake, ni lazima rhythm pia iwe imeshaunda na kupangiliwa vizuri. Ingawa tulipojadili rhythm kwa mara ya kwanza tulisema ni mdundo unaojirudia rudia kwenye wimbo, kwa kawaida mdundo huwa lazima uwe pia unabadilika badilika kwenye wimbo ili usimchoshe msikilizaji. Kwa mfano badala ya kutumia meter ya aina moja wimbo wote, unaweza kuchanganya simple meter na simple duple meter au compound na compound duple meter. Vile vile rhythm ya kwenye mashairi inaweza kuwa tofauti na rhythm ya vibwagizo na kadhalika, mradi usibadilishe beat ya wimbo sana kiasi cha kumfanya msikizaji ashindwe kuendana na mabigo, kwa mfano ashindwe kucheza.

Ukishakuwa na rhythm nzuri ya wimbo wako, sasa ndiyo unatunga motif za sehemu mbalimbali. Unaweza kuwa na motif moja au mbili (zisiwe nyingi sana) kwenye mashahiri, na mofif moja au mbili kwenye vibwagizo na motif moja kwenye kiungo, na motif moja kwenye mapumziko. Utunzi wa motif hauna formula, hapo ndipo kipaji na ubunifu vinapotakiwa. Njia mojawapo ya kujenga kipaji ni kusikiliza nyimbo za aina mbalimbali nyingi sana, kusikiliza milio ya ndege na wanyama wa porini na vitu vyovyote vitoavyo sauti zinazojirudia rudia.

Watunzi wengi hutunga motif zao kwa kutumia sauti zisizozidi nne tu; unaweza kuwa na sauti mbili, tatu au nne ingawa motif ya sauti moja pia inawezekana. Kwenye mifano yetu katika makala hii tutatumia motif yenye sauti nne tu za D-F-E-B kwenye scale(key) ya C-major kama ionekanavyo hivi

1566781602971.png


Bila kujali kuwa sauti hizo ni Tonic, Mediant au vyovyote vile, ni kwamba imetupa melodic contour fupi ambayo sauti zake zinasikikika hivi zikiwa na skip moja, step moja, na leap moja ikiwa na sura ya namna hii
1566781687256.png



Motiff hiyo ndiyo hujulikana kama prime motif, yaani wazo kuu (mojawapo) la muziki wako; unaweza kuwa na motif mbili au tatu kwenye mziki mmoja, ila tutaumia motif moja tu ili kuelezea dhana nzima ya utungaji wa melody. Ukishaipenda motif hiyo, utaitumia kutoa sauti nyingine nyingi sana kwa njia mbalimbali kama ifuatavyo:
(1) Kuzichanganya (Permutations): Kwa kufanya permutations ya sauti hizo nne DFEB za prime motif, unaweza kupata sauti nyingine 4x3x2x1=24, za DFEB, DFBE, DEFB, DEBF, DBFE, DBEF, FDEB, FDBE, FEDB, FEBD, FBDE, FBED, EFDB, EFBD, EDFB, EDBF, EBFD, EBDF, DFEB, BFDE, BEFD, BEDF, BDFE,na BDEF. Kwa mfano sauti za FBED zitakuwa na motif ya
1566782238673.png
ambayo itasikika hivi. Kwa jumla hizo ni sauti nyingi sana, zijaribu uchague chache utakazopenda kulingana na ladha unayotaka kwenye muziki wako.

(2) Kuzihamisha juu au chini kwenye scale (real transposition). Kwa mfano sauti DFEB inaweza kuhamishwa kwa sauti moja kuwa EGFC kwa mfano
1566782368584.png
inayosikika hivi. Vile vile unaweza kuzihamisha kwa sauti mbili kuwa FAGD. Sauti hizi nazo ukizafanyia permutation kama tulivyoeleza hapo juu, utapata motifs nyingine 48. Unaweza kuzihamisha kwa sauti tatu au nne kupata motifs nyinge 24 kwa kila hamisho.

(3) Kuzihamisha juu au chini kufuata idadi ya steps(tonal transposition). Njia hiyo ya real transposition hapo juu, ilikuwa inahamisha sauti kwenye scale bila kujali sauti hizo zinaruka steps ngapi. Kumbuka kuwa scale ya major sauti zake zimepishana kwa steps za KKN-K-KKN. Kwa hiyo unapozihamisha kwa noti nzima chini ya real transposition, kuna sauti zitaruka nusu hatua na kuna zitakazoruka hatua kamili. Hii Tonal transposition hurusha sauti kwa idadi ya step zile zile, kwa mfano DFEB ikiwa transposed kwa steps tatu itakuwa FA♭GD (Angalia tena chromatic scales na major scales). Kwenye mjadala huu tutaziacha hizi tonal transpositions kwa vile zinahitaji uchambuzi zaidi. Lakini Transposition hii pia itakupa motiffs nyingine nyingi sana kulingana na namba ya steps unazoruka.

(4) Mabadiliko ya mtililiko (variations) hufanywa kwa kutumia sauti hizo hizo kwa mfumo ule ule lakini kwa kubadilisha mtililiko wake. Mabadiliko haya yapo ya aina tatu:
(a) Retrograde ambapo sauti ya kwanza inakuwa ya mwisho, na sauti ya mwisho inakuwa ya kwanza yaani sauti zinajipanga kinyumenyume,
(b )Inversion ambapo sauti ya kwanaza inabaki ile ile ile, lakini sauti za juu yake zinakwenda chini kwa step idai ile ile ya noti, na zile za chini yake zinakwenda juu kwa idadi ile ile ya noti,
(c) Retrograde-Inversion ambapo sauti zinabadilishwa kama retrograde hapo juu, halafu zinabidilishwa tena kwa Inversions.

Picha hii inaonyesha mifano hiyo ukilingansiha na ile prime motiff, na pia sauti zitokanzano na variations zote hizo ni hizi hapa
1566783144774.png



(5) Mabadiliko ya noti moja moja (embellishment). Kwenye stage hii mtungaji anaweza kufanya mabadiliko ya sauti moja moja moja au zote kweye hiyo prime motif yake kadri atakavyopenda mwenyewe. Kwenye mfano wetu hapo juu unaweza kubadili sauti hizo za prime na variations hizo tatu kwa kama ifuatavyo hapa chini, kwa mfano tu. Embelellishement yoyote inawezekana kama mfano huu unavyoonyesha na pia unaweza huhamisha kwenda juu au chini noti moja au zaid kwa hatua zozote utakazopenda.

1566783834154.png

sauti hizo sitasikika hivi

Kwa kutumia motif moja tu ya sauti nne, mabadiliko hayo tuliyajadili hapo juu yanaweza kutoa motifs takribani 500 ! Nadhani hapa mada imeanza kueleweka kuwa motif moja inaweza kufungua bahari nzima ya vipande vya melodies, ambavyo vikiunganishwa vitaweza kukamilisha sehemu kubwa ya wimbo wako.

Kama mafaili ya mp.3 ninayoweka haweza kuplay weka comment hapa chini kusudi nifikirie namna ya kuyabadilisha katika format nyingine

Wasomaji wangu wakuu nkumbison, Madaga, Gyole, Extra miles, MzaramoTz , Frega Bao,MRI; nadhani mjadala huu hili kuhusu motifs na zizotangulia kuhusu dynamics na articulation zimeelewa. Katika makala ijayo tuajadili namna ya kuungansha hizi motifs katika kukamilisha melodic phrases na kuzingnaisha kuwa wimbo kamili
 

Attachments

  • motif0.mp3
    43.7 KB · Views: 20
  • motif1.mp3
    42.9 KB · Views: 18
  • motif2.mp3
    42 KB · Views: 17
  • motif3.mp3
    156.3 KB · Views: 17
  • motif4.mp3
    154.7 KB · Views: 20
Melody ya Muziki- Melodic Phrases

Melodic phrase ni muungano wa motifs kadhaa kutengeneza kipande kikubwa kwa melody. Kama motif zako ni za measures mbilimbili, unaweza kuunganisha motif mbili au tatu kuwa na melodic phrases zenye measures nne au sita. Kila phrase inaweza kuwa na measure mbili au zaidi, nyimbo nyingi hutumia measures nne kwa kila phrase. Katika mashairi, melodic phrase ni sentensi moja ya shairi, na kulingana na urefu wa mistali ya shairi, siyo lazima melodic phrase ijaze measures zote kwenye phrase, inaweza kuishia katikati ya measure. Katika lugha ya muziki, melodic phrase siyo lazima iwe sawa na phrases za cleffs kama tulivyotanguliza huko nyuma. Ni kawaida na ni vizuri melodic phrase zikalingana na phrases za cleff lakini siyo lazima

Ingawa motifs zinaweza kujengwa kwa sauti zozote zile, sauti zinazotumika kwenye melodic phrases zina utaratibu fulani wa kufuatwa. Melodic phrases zinatakiwa ziwe katika mafungu ya phrases mbilimbili yanayojulikana kama period: melodic phrase ya kwanza kwenye period inatakiwa iweke tension fulani masikioni mwa msikilizaji (antecedent), na phrase pili inaondoa tension hiyo (consequent).

Mwisho wa kila melodic phrase lazima kuwe na sauti ama ya kusubiri (continuation), au ya kupumzika kidogo (temporal repose) au ya kupumzika kabisa (finality). Sehemu hiyo ya mwisho kwenye melodic phrase inaitwa cadence. Kuna aina nne za cadences:

(1) Cadence ya ukweli (Authentic Cadence) ambapo mapumziko ni kutoka sauti ya Dominant-V kwenda Tonic -I. Hizi cadence za ukweli zinaweza kuwa ni kamili (perfect authentic cadence au PAC) iwapo sauti ya mwisho ni Tonic ya kwenye Octave inayofuata, na ambazo siyo kamili (imperfect authentic cadences au IAC) ambapo mapumziko yanatoka kwente Leading tone –VII au Supertonic kwenda Tonic–I yoyote. Aina zote mbili ni za kuonyesha finality.
(2) Cadence nusu (Half Cadence) ni zile zinazoishia na Dominant –V kutoka kwenye sauti yoyote.
(3) Cadence isiyokuwa ya ukweli (Plagal Cadence) ni zile zinazkiwsha kwa kutoka Subdominant-IV kwenda Tonic-I; kwa wanaokwenda makanisani ya kikatoliki, hii ndiyo hutumika kusema Amen.
(4) Cadence zinazodanganya (Deceptive Cadence) zinakwesha na sauti za ama Submediant –VI au Leading Tone-VII kutoka kwenye sauti yoyote.

Authentic cadence na Plagal Cadence ndizo zinazoashiria finality ambapo msikilizaji anajua mambo yamekwisha. Half Cadence zinaashiria Temporal repose, humfanya msikilizajia apumzike lakini akiwa bado anategemea zaidi. Mwishoni, Deceptive cadence zinaashiria Continuation, yaani hizi humwacha msikilizaji akiwa tension na hivyo akiwa na hamu ya kusikiliza zaidi.

Melodic phrase ya kwanza kabisa ya shairi itaanza na ama na sauti za Tonic au Dominant, halafu melodic phrase ya mwisho kabisa wa shairi nayo itakwisha kwa sauti hizo hizo za za Tonic au Dominant (Authentic cadence na Plagal Cadence). Melodic phrase inayoweka tension lazima ianze na sauti stable (siyo lazima iwe tonic), na kuishia na sauti unstable (Deceptive Cadence) ili kumfanya msikilizaji asubiri melodic phrase inayofuata. Watunzi wengi huepuka kutumia sauti za Tonic kumaliza phrases za katikati ya shairi mpaka mwisho wa mwisho tu.

Wimbo huu wa Happy birthday uko katika scale ya G-major, na una phrases tatu ambapo kila phrase ina measure tatu tatu; hata hivyo melodic phrases zake hazijipangi sawa na phrases za za wimbo kwa sababu measure ya kwanza inaanza ikiwa imechelewa beat mbili (ambazo hazionyeswi hapa, kwa hivyo melodic phrase inaenda kushia katikati ya measure ya tatu. Kwa jumla kuna melodic phrases nne kwenye wimbo huo.

1566789756683.png


Hebu angalia melodic phrases na measures zake zilivyopangwa kwenye trebble cleff tu, usiangalia bass cleff. Measure ya kwanza imekosewa kidogo kwani kuna pumziko la beat mbili kabla mashairi kuanza ambalo halikuonnyeshwa mwanzoni, kwa hiyo measure inaonekana kama in robo noti tu badala ya kuwa na robo noti tatu. Kwenye scale ya G-major sauti zake ni hizi:

G (I), A(II), B(III), C(IV), D(V),E(VI), F# (VII), G(I)*

Kwa hiyo kwenye melodic phrase ya kwanza utaona kuwa measure ya kwanza kabisa inaanza na sauti D-ambayo ni Dominant (stable) na kuisha na Dominant (stable) hiyo hiyo- hii haikuweka tension yoyote. Measure ya pili pili inaanza na E-Submediant na kutelemka kwenye D-Dominant na kuisha kwa kupanda kwenye G-Tonic. Mwisho wa melodic phrase ya kwanza ni ile theluthi mbili ambayo ni sauti ya F#(Leading tone) ambayo ni deceptive cadence; kwa hiyo msikilzajia baada ya mstali huo anategemea kusikia zaidi. Phrase ya pili inarudia phrase ile ile ya kwanza. Phrase ya tatu inaanza kama phrase ya kwanza lakini inashia na E-Submediant ambayo bado ni deceptive cadence lakini ikiwa inasikika tofauti na ile iliyopita ili kutommchosha msikilizaji. Phrase ya mwisho inaaza na C-Subdominant, mwishoni kabisa inakwisha na sauti ya G-Tonic ambayo ni Authentic Cadence kwani inatokea kwenye suati A- Supertonic na kumaliza Shairi. Angalia ile legatto kwenye cadence ya tatu, na alama ya jicho kuonyesha fermata iliyotuma mwishoni kabisa mwa wimbo.

Ukiungalia tena kwa makini, wimbo huu una motif mbili tu. Motif ya kwanza ni hii hapa chini iliyotumika kwa kuimba maneno ya happy; ina sauti moja tu. Katika phrase tatu za kwanza imetumika hivyo hivyo, lakini katika phrase ya nne, ikahamishiwa juu (real trasposition) kwa sauti sita.
1566790331325.png


Motif ya pili ni ile inayomalizia sehemu ya pili ya msitali, ambayo ni hii hapa.
1566790403248.png



Kwenye melodic phrase ya kwanza, motif hii imetumia sauti hizi hizi za EDGF, halafu sauti hizo zikafanyiwa mabadiliko mbalimbali kama tulivyojadili huko nyuma kwenye makala ya motifs kupata motif nyingine nne kama ifuatavyo. Melodic phrase ya pili ilihamisha sauti mbili za mwisho kwenda juu kwa noti moja kuwa na sauti za EDAG, na baadaye kwenye phrase ya tatu imetelemsha sauti mbili za kwanza kwa noti moja, yaani E kuwa D, halafu sauti ya pili kwa noti mbili yaani D kenda B, halafu ikazirusha Octave moja na kuwa DBG(FE) wakati sauti za FE zinatoka kwa pamoja kama legatto, na mwishowe kwenye phrase ya nne inamaliza kwa sauti za BGAG. Ziangalie tena kwa makini


Kwa vile mjadala wa ukamilishaji wa melody utatumia mifano ya nyimbo zilizoko sokoni, itaweza kuwa ndefu kidogo, ngoja niupe makala yake maalum, hivyo kwe leo nitaishia hapa.



Wasomaji wangu wakuu nkumbison, Madaga, Gyole, Extra miles, MzaramoTz , Frega Bao,MRI; nadhani mjadala huu hili kuhusu melodic phrases na matumi za motifs kwenye kujenga melodic phrase motifs umeelewa kiasi cha kutosha. Katika makala ijayo tuajadili njia mbalimbali za kuungansha hizi melodic phrases katika kukamilisha melody ya wimbo kamili. Halafu tatajadili jinsi waimbaji maarafu walivyozitumia kwenye nyimbo zao. Baada ya hapo ndipo tutakaporudi tena kwenye wimbo wetu wa Kuku ambao mashari yake niliyachukua kutoka kwa Andanenga (Sauti ya Kiza) na kutumia mbinu hizi kuutunga wimbo kamili kwa kutumia Ableton Live. Sipendi kutumia FL Studio kwa sababu binafsi, ila kama kuna anayeipenda aniarifu. Mimi nina Version 12 tu, najua the latest nadhani ni Version 19.
 

Attachments

  • HappyBirthday.mp3
    266.9 KB · Views: 17
Baada ya kujua dhana ya motif, melodic phrases na periods, mada ninayojiandaa kujadili kwa kina ni aina za periods na namna ya kuziunganisha katika kutengeza melody ya wimbo wako. Nimechagua wimbo huu wa Rolling in the Deep ulitungwa na kuimbwa na Adele Adkins akisaidiwa na Paul Epworth. Ingawa ni wimbo wa kawaida sana, una watazamaji 1.5b youtube, hivyo ni wimbo ambao; Tungo hii ina changamoto kadhaa ambazo ndizo zinazonifanya niitumie katika mada hii.



Maneno (lyrics) ya wimbo huo ni haya hapa chini. Kuna sehemu ambapo wimbo hutumia sauti za background (BG); jizozeze na wimbo wenywe pamoja na muundo wake kabla hatujautumia katika mada yetu ifuatayo:

[Utangulizi]

There's a fire starting in my heart
Reaching a fever pitch, and it's bringing me out the dark
Finally, I can see you crystal clear
Go ahead and sell me out, and then I'll lay your ship [shit] bare

[Shairi 1]

See how I'll leave with every piece of you
Don't underestimate the things that I will do
There's a fire starting in my heart
Reaching a fever pitch, and it's bringing me out the dark

[Kibwagizo-Tangulizi]

The scars of your love remind me of us
They keep me thinkin' that we almost had it all
The scars of your love, they leave me breathless
I can't help feeling, …..

[Kibwagizo]

We could have had it all
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
Rolling in the deep
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
You had my heart inside of your hand
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
And you played it to the beat
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)


[Shairi 2]

Baby, I have no story to be told
But I've heard one on you
Now I'm gonna make your head burn
Think of me in the depths of your despair
Make a home down there
As mine sure won't be shared

[Kibwagizo-Tangulizi]

( BG: You're gonna wish you – never had met me)
The scars of your love remind me of us
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
They keep me thinkin' that we almost had it all
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
The scars of your love, they leave me breathless
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
I can't help feeling, ……


[Kibwagizo]

We could have had it all
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
Rolling in the deep
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
You had my heart inside of your hand
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
And you played it to the beat
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
Could have had it all
Rolling in the deep
You had my heart inside of your hand
But you played it with a beating


[Shairi 3]

Throw your soul through every open door
( BG: oh-oh)
Count your blessings to find what you look for
( BG: whoa-oh)
Turn my sorrow into treasured gold
( BG: oh-oh)
You'll pay me back in kind and reap just what you sow


[Kivuko]

( BG: You're gonna wish you – never had met me)
We could have had it all
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
We could have had it all
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
It all, it all, it all
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
We could have had it all


[Tamatisho]

( BG: You're gonna wish you – never had met me)
Rolling in the deep
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
You had my heart inside of your hand
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
And you played it to the beat
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
We could have had it all
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
Rolling in the deep
( BG: Tears are gonna fall, rolling in the deep)
You had my heart inside of your hand
( BG: You're gonna wish you – never had met me)
But you played it, you played it, you played it
You played it to the beat
 
Tungo za melody za Wimbo huo wa Rolling in the Deep ulitungwa na kuimbwa na Adele Adkins akisaidiwa na Paul Epworth ni hizi hapa
1567371613119.png


1567558856689.png


1567371700957.png



1567371769388.png


1567371828196.png


1567558803838.png

[Kibwagizo Tangulizi]

[Kibwagizo]

1567371985240.png


1567372056221.png


1567372109270.png


Mambo yasiokuwa ya kawaida katika tungo hii ni kuwa

(a) Measure ya mwisho ya Kibwagizo tangulizi haikamiliki, ila kipande cha measure hiyo kilichobaki hutumiwa kama mwanzo wa kibwagizo.

(2) Kwa vile Tamatisho limetumia sauti za kibwagizo pia, basi hata measure ya mwisho kwenye Kivuko kabla ya tamatisho nayo haikukamilika, ikiacha sehemu iliyobaki itumiwe kwenye Tamatisho.

Ninachotaka kuweka wazi hapa ni kuwa katika utunzi, wewe jali wimbo wote usijali sehemu za wimbo huo kwa kuzitenganisha, ziweke pamoja kama wimbo mmoja. Siyo lazima kuwa sehemu zote za wimbo zikamilishe measures zake. Baadhi ya measures zinaweza kutumiwa na sehemu mbili za wimbo kama Adele alivyofanya kwenye wimbo huu.
 
Melody ya Muziki- Periods

Utangulizi Kutoka Post zilizotangulia

kama tulivyokiwsha ona huko nyume, Melodic phrase ni muungano wa motifs kadhaa kutengeneza kipande kikubwa kwa melody inayojitegemea. Kila phrase inaweza kuwa na measure mbili au zaidi, nyimbo nyingi hutumia measures nne kwa kila phrase. Katika mashairi, melodic phrase ni sentensi moja ya shairi, na kulingana na urefu wa mistali ya shairi, siyo lazima melodic phrase ijaze measures zote kwenye phrase, inaweza kuishia katikati ya measure.

Ingawa motifs zinaweza kujengwa kwa sauti zozote zile, sauti zinazotumika kwenye melodic phrases zina utaratibu fulani wa kufuatwa. Mambo machache ya kuzingatia katika kujenga motifs ni kama ifuatavyo:
  • Weka balance nzuri kati ya kutumia steps, skips na leaps kwenye melodic contour yako. Kuwa na leaps chache sana lakini pia usizidise steps na skips sana. Kwa mfano, badala ya kutumia sauti zenye leaps kama I-VI-II-V-III-VI-VIII, ni afadhali kubadilisha motif itumie sauti hizo katika mpangilio wa I-II-III-II-III-IV-V ambao hauna leaps kabisa.
  • Kwa kawaida steps nyingi zinamchosha haraka sana msikilizaji wako. Iwapo melodic contour yako inataka steps za kupanda zaidi, basi changanya mwendo wa kupanda na kushuka kusudi uingize skips kidogo. Kwa mfano badala ya kupanda sauti kwa steps za I-II-III-V-II-IV-V ni afahadhali kuzipanga I-II-III-II-V-IV-V.
  • Kama contour yako inahitaji leaps, hasa zile kubwa za kuruka step nne au zaid, kwanza test sauti zako hizo kama zinasikika vizuri; kuna zile zinazosikika vizuri lakini leaps kubwa nyingi kwa mfano sausti za kuruka baina ya sauti za IV na zile za VII au baina ya sauti za Octave moja kwa step 7 huwa zinasikika vibaya sana. Iwapo leap yako inasikika vibaya, basi fanya utaratibu wakumuandaa msikilizaji wako. Kumuandaa msikilizaji, ni kuruka nusu ya leap hiyo kwanza na kurudi njuma step moja kabla ya kuruka zaidi kukamilisha leap uliyokusudia
Ukisha kuwa na motifs, hatua inyofuata ni uundaji wa Melodic phrases ambazo zinahitajika ziwe na sehemu (subphrases) mbili mbili; subphrase ya kwanza inajulikana Basic Idea (BI), hii ndiyo ambayo ama hujaza tension kwa masikilizaji au haifanyi chochote kwa msikilizaji badala yake inamwacha kwenye suspence. Subphrase ya pili hujulikana kama Contrasting Idea (CI) ndiyo huondoa tension iliyoletwa na BI kwa kiasi fulani, kwa hiyo mwisho was subphrase ya pili, lazima msikilizaji awe katika hali fulani ya kupumzika.


Miundo ya Periods

Katika kutengeza melody ya wimbo, hizi melodic phrases zinapangwa makundi ya phrases mbili mbili au tatu tatu yanayojulikana kama period. Kukiwa na phrase mbili kwenye period, ina maana kuwa melodic phrase ya kwanza (antecedent) kwenye period inatakiwa iache tension fulani masikioni mwa msikilizaji, na phrase pili (consequent) inaondoa tension kwa kiasi fulani kumpa msikilizajia nafasi ya kurelaz. Mara nyingi Consequent huwa inarudia vipande fulani vya Antecedent lakini kwa kuvilainisha na kuviondolea tension yote. Mwisho wa kila melodic phrase lazima kuwe na sauti ama ya kusubiri (continuation), au ya kupumzika kidogo (temporal repose) au ya kupumzika kabisa (finality). Sehemu hiyo ya mwisho kwenye melodic phrase inaitwa cadence. Kama tulivyotambulisha huko nyuma, kuna aina nne za cadences:
  • Cadence ya ukweli (Authentic Cadence-AC) ambapo mapumziko ni kutoka sauti ya Dominant-V kwenda Tonic -I. Hizi cadence za ukweli zinaweza kuwa ni kamili (Perfect authentic cadence au PAC) iwapo sauti ya mwisho ni Tonic ya kwenye Octave inayofuata (I*), na ambazo siyo kamili (Imperfect Authentic Cadences - IAC) ambapo mapumziko yanatoka kwente Leading tone –VII au Supertonic –II kwenda Tonic–I yoyote. Aina zote mbili ni za kuonyesha finality; hutokea mwishoni mwa Utangulizi, Shairi au Kibwagizo.
  • Cadence nusu (Half Cadence-HC) ni zile zinazoishia na Dominant –V kutoka kwenye sauti yoyote. Half Cadence zinaashiria temporal repose, humfanya msikilizaji apumzike lakini akiwa bado anategemea zaidi. Hizi hutumika Zaidi kwenye kumalizia Kibwagizo-Tangulizi na Kivuko.
  • Cadence isiyokuwa ya ukweli (Plagal Cadence-PC) ni zile zinazikwisha kwa kutoka Subdominant-IV kwenda Tonic-I; kwa wanaokwenda makanisani ya kikatoliki, hii ndiyo hutumika kusema Amen. Hii nayo inatumika kuonyesha finality, kwa hiyo inaweza kuwa mwisho wa Utangulizi, Shairi au Kibwagizo.
  • Cadence zinazodanganya (Deceptive Cadence-DC) zinakwisha na sauti za ama Submediant –VI au Leading Tone-VII kutoka kwenye sauti yoyote. Hizi humwacha msikilizaji akiwa na tension ambayo lazima iondolewe na sehemu ya wimbo inayofuata; zinaweza kutumika mwishoni mwa Antecedent au mwishoni mwa subphrase za kwanza kwenye kila melodic phrase.
Melodic phrase ya kwanza kabisa ya wimbo au shairi itaanza na ama na sauti za Tonic au Dominant, halafu melodic phrase ya mwisho kabisa wa shairi au wimbo nayo itakwisha kwa sauti hizo hizo za Tonic au Dominant (AC au PC. Melodic phrase inayoweka tension lazima ianze na sauti stable (siyo lazima iwe tonic), na kuishia na sauti unstable (DC) ili kumfanya msikilizaji asubiri melodic phrase inayofuata. Watunzi wengi huepuka kutumia sauti za Tonic kumaliza phrases za katikati ya shairi mpaka mwisho tu.

Ingawa kimsingi tunataka kila period iwe na melodic phrase ya antecedent inayoweka tension na melodic phrase ya consequent inayoondoa tension hiyo, siyo lazima periods zote za melodi lazima ziwe na tension kukifatiwa na tension relief namna hiyo. Inawezekana kabisa kuwa antecedent haiweki tension kabisa au inaweka na kuondoa tension kabla ya kufika mwisho, na hivyo hakuna haja ya kuwa na consequent inayoondoa tension. Antecedent inaanza na Basic Idea (BI)ambapo sauti zinaweka tension kiasi fulani, halafu inafuatiwa na contrasting idea (CI) inayoondoa tesion na kupizikia Half cadence (HC) au imperfect authentic cadences (IAC). Baada ya hapo Basic Idea (BI) ya Consequent inafuata, ambayo pia inaweka Tension mpaka kiasi Fulani ikufuatiwa na Contrasting idea (CI) kuondoa tension hiyo na kupumizikia kwenye perfect authentic cadence au (PAC) au Plagal Cadence (PC).

Kwenye period, siyo lazima antecedent phrase iwe na urefu sawa na consequent phrase; iwapo zinalingana basi period ile inajulikana kama symetrical period, na iwapo hazilingani basi zinajulikana kama assymmetrical period. Muundo wa symmetrical period yenye measures 8 (ambayo ndiyo maarufu zaid kwenye miziki mingi) ni kama ionekanavyo kwenye picha hii ya kushoto na muundo wa wa assymetrical period yenye measures 10 umeonyeshwa kwenye picha ya kulia.
1567727288068.png
1567727301464.png



Kuna aina tatu za Symmetric periods:

(a) Parallel Period ni ile ambayo Consequent phrase ni sawa kabisa na antecedent phrase, yaani marudio kamili (repetition); hii huonyeshwa kwa alama AA au BB.

(b) Contrasting period, ni ile ambayo Consequent phrase ni tofauti kabisa na Antecedent; hii huonyeshwa kwa alama AB;

(c) Double period
kama jina linavyosema, ni period mbili ambazo kwa pamoja zinasikika kama vile ni period moja ndefu. Phrases zote mbili zinazounda antecedent zinaishia na Half cadence (HC) au imperfect authentic cadences (IAC), halafu kwenye consequent, phrase ya kwanza nayo inaishia na Half cadence (HC) au imperfect authentic cadences (IAC) ambapo phrase ya pili ndio inaishia na perfect authentic cadence au (PAC). Periods zote mbili huanza na phrases zinazofanana, na huisha na phrases zinazokaribia kufanana ila cadences zake ndizo zinazotofautiana kidogo. Double periods huonyeshwa kwa alama ya ABAB’

Assymetrical periods
zote ni contrasting periods; mfano mmojawapo wa assymetrical measure ni kama ionekanavyo kwenye picha ya kulia hapo juu; antecedent yake ina measures 4, wakati consequent ina measures 6. Namba zozote za measures zinawezekana mradi tu pande zote mbili za period ziwe na urefu toauti; kwa mfano, Antecedenet inaweza kuwa ndefu kuliko Consequent.

Periods zenye phrases tatu pia zinakubalika; hizi zinajulikana kama three-phrase periods. Period za namna hiyo bado zina huo muundo wa Antecedent na Consequent kama tulivyoeleza hapo juu kila moja ikiwa na cadence yake. Hata hivyo mojawapo baina ya Antecedenet na Consequent hutokea mara mbili ikiwa na mabadiliko fulani kidogo. Kwa hiyo three-phrase period inaweza kuwa na ama Antecedent mbili au Consequent mbili kama picha hii invyooneyesha.
1567727117429.png

Melody za nyimbo nyingi nzuri huwa na periods mbili mbili tu, yaani melodic phrases nne, ingawa kuna nyimbo zenye period moja tu. Siyo kawaida kuwa na wimbo wenye periods zaidi ya tatu kwani utakuwa ni mrefu sana kwa msikilizaji kukumbuka.

Melodic phrases nne (yaani peridos mbili) zinaonekana kuwa ndiyo namba ambayo ubongo wa binadamu unaweza kupokea haraka sana- hata mashari ya Kiswahili yale ya akina Shaaban Robert yalitungwa kwa periods tatu, pamoja na kibwagizo chenye period moja. Kuna aina nyingi sana za melodies, ndiyo maana dunia ina watunzi wengi sana na nyimbo nyini sana zinazotofautiana. Inategemea wimbo una periods za aina gani na ngapi kuanzia period moja hadi tatu. Kwa vile Makala imeshakuwa ndefu, kwa leo nitaachia hapa ila nitendelea na kutazama mindo mbalimbali za mebolfies kwa kutumia nyimbo tulizo nazo hapa kwa sasa kabla sijaongeza nyimbo nyingine kusudi kujaribu kuchambua aina nyingi za melody.

Wasomaji wangu wakuu nkumbison, Madaga, Gyole, Extra miles, MzaramoTz , Frega Bao,MRI; mjadala huu na zile tatu zilizopita ni kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya mjadala wetu ujao unaohusu uundaji wa melodies. Mwanzoni nilidhani ningeweka yote katika makala haya lakini nimekuta andiko limekuwa refu sana, kwa hiyo nimekata vipande viwili.
 
Nakufatilia kwa ukaribu sana huku nikifanyia kazi mkuu. Heshima sana kwako aisee.
 
Katika siku za hivi karibuni nimekuwa na mambo mengi ya kutafutia ugali nimeshindwa kuhudumia thread hii vizuri, ila bado iko active. Kuna mambo ya ki-uhariri bado nayafanya kwenye post ijayo inayohusu utunzi wa melody ya wimbo mzima kama inavyoonekana hapa chini ambayo ni work in progress; kwa hiyo wasomaji wangu wakuu nkumbison, Madaga, Gyole, Extra miles, MzaramoTz , Frega Bao,MRI msikate tamaa au kudhani kuwa ngoma imezimikia njiani. Bado kuna mengi ya kujadili kwenye thread hii kabla hatujafika mwisho wa safari yetu.

1568685693516.png
 
Thread hii niliipumzisha kidogo kutokana na majukumu ya umma; nitaiendeleza tena kidogo wakati huu wa mapumziko ya krismasi.
 
Thread hii niliipumzisha kidogo kutokana na majukumu ya umma; nitaiendeleza tena kidogo wakati huu wa mapumziko ya krismasi.
Mkuu Ahsante kwa somo zuri..
Mimi nina shida moja. I'm a man na hua naimba kanisani lakini sauti yangu naona inafaa kuimba Alto..ila imebidi niimbe bass. Je hivi kwanini Soprano na alto waimbe wanawake tu.? Mimi napenda alto zaidi
 
Back
Top Bottom