Elimu kwa Ally Kamwe na Ahmed Ally juu ya hamasa viwanjani siku za mechi

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,319
12,622
Inasemekana kuwa Shabiki ni mchezaji 12 wa timu wakati wa mechi, hivyo Ally Kamwe na Ahmed Ally wasemaji wa Yanga na Simba wanafanya kila jitihada ya kuwataka wanachama na mashabiki wa timu hizo washangilie mwanzo mwisho wa mechi zao muhimu. Hata hivyo sayansi ya akili na tabia ya mtu inamtaka mtu mwenye afya timamu ya mwili na akili afurahi, kushangilia, kucheka, kupiga makofi na vigelegele na kutabasamu pale tu anapokutana, sikia au kuona tukio zuri linalompendeza.

Nipunguani tu anaeweza kucheka na kushangilia wakati wa huzuni. Kwa maana hiyo hakuna mwanachama wala shabiki wa Simba au yanga anaeweza kushangilia, kucheka na kupiga vigelegele mfululizo hata kama timu yake iko nyuma kwa magoli 3 dhidi ya mpinzani wake. Watu wanaoweza kushangilia timu muda wote hata kama timu imefungwa ni ama punguani au mtu mwenye maslahi na mechi husika zaidi ya furaha tu ya kushinda mechi.

Hivyo, basi ili watu ambao wanaweza kushangilia timu mwanzo mwisho bila kujali chenga za wachezaji wala matokeo ni watu wenye maslahi ya moja kwa moja (palpable) na mechi zaidi ya timu kushinda. Hawa watu wenye masilahi ya moja kwa moja (wanaolipwa) ndio wanaowatia hamasa ya kushangilia muda wote mashabiki ambao malipo yao ni furaha tu kwa timu kushinda mechi, Kifupi Yanga na simba lazima wawe na kikundi ambacho kitalipwa kwa kazi ya kushangilia bila kujali mwenendo na matokeo ya mechi. Timu zote kubwa kwenye nchi zote wanafanya hivyo.

Nitoe mfano kule US ambako basket ball inachezwa sana kwa hamasa. Vikundi vya hamasa vya kulipwa vina uwezo mkubwa mpaka wa kupita angani kwa ndege ndogo siku na muda mchache kabla ya mechi kuhamasisha watu kwenda uwanjani kwa kupeperusha mabango (banners) na moshi wenye rangi za timu husika. Ndege zinapita mitaa yote ya mji kualika watu waende kushangalia timu husika.

Kule kiwanjani kuna kuna kundi linashangilia sana na kuanzisha nyimbo ambazo zinafahamika na washabiki wote wa timu hiyo, hivyo uwanja wote wanaimba wimbo mmoja kutoka kona zote waliko mashabiki wao, na kama ni kelele ni za aina moja tu uwanja mzima. Hawa wanawaambukiza wengine kushangilia hata wale wenye njaa na kuwa kitu kimoja pale uwanjani. Hiki kikundi kitaimba na kushangilia kwa nguvu sana hata kama timu iko nyuma, maana wao wana maslahi mengine kabisa ambayo yana vigezo vyake vya ufanisi na ulipaji.

Huwezi kutegemea mtu mwenye njaa, asiekuwa na usafiri wa kurudia kwake na asiyelipwa chochote ashangilie timu yake hata kama imefungwa, huo utakuwa upunguani kama watafanya hivyo.
 
1. Position ya ukaaji wa wahamasishaji izingatiwe. Wanatakiwa wakae nyuma ya magoli. Wale wanaokuwa kwenye goli la timu pinzani ndiyo muhimu sana wawe active muda wote.

2. Watafutwe hata wahuni wavuta bangi wawape bendera za kubeba. Ukiangalia matamasha ya reggae kuna mchizi huwa anapepea bendera muda wote bila kuchoka. Watafute watu kama hao. Panya Road wapo tu hawana kazi, waajirini wale walete hamshahamsha viwanjani.

3. Waachane na matarumbeta maana hayapigwi kwa ustadi wala coordination matokeo yake yanageuka kelele tu. Nyimbo zenye vibwagizo sahihi na kupiga makofi kwa pamoja vinatosha. Achaneni na nyimbo ndefu zenye maubeti.
 
1. Position ya ukaaji wa wahamasishaji izingatiwe. Wanatakiwa wakae nyuma ya magoli. Wale wanaokuwa kwenye goli la timu pinzani ndiyo muhimu sana wawe active muda wote.

2. Watafutwe hata wahuni wavuta bangi wawape bendera za kubeba. Ukiangalia matamasha ya reggae kuna mchizi huwa anapepea bendera muda wote bila kuchoka. Watafute watu kama hao. Panya Road wapo tu hawana kazi, waajirini wale walete hamshahamsha viwanjani.

3. Waachane na matarumbeta maana hayapigwi kwa ustadi wala coordination matokeo yake yanageuka kelele tu. Nyimbo zenye vibwagizo sahihi na kupiga makofi kwa pamoja vinatosha. Achaneni na nyimbo ndefu zenye maubeti.
Yani timu lazima ziwe na nyimbo zao zinazofahamika na zinazoweza kuimbwa wa wadau wote wa timu husika pale uwanjani. Wanachohitaji ni mtu mmoja anzishe ubeti wa kwanza tu. Nyimbo ziwe fupifupi zinazoamsha hamasa, tuachane na vigoma binafsi vya wanaonengua, havisaidii. Wale wa Raja Casablanca walikuwa wachache lakini wakulipwa, umeliona balaa lao?
 
huwezi kuniambia mimi niimbe wakati wachezaji wetu wanakosa penalti wakati timu iko nyuma kwa bao 3-1, walah nitakuwa mwehu!!
 
Yani timu lazima ziwe na nyimbo zao zinazofahamika na zinazoweza kuimbwa wa wadau wote wa timu husika pale uwanjani. Wanachohitaji ni mtu mmoja anzishe ubeti wa kwanza tu. Nyimbo ziwe fupifupi zinazoamsha hamasa, tuachane na vigoma binafsi vya wanaonengua, havisaidii. Wale wa Raja Casablanca walikuwa wachache lakini wakulipwa, umeliona balaa lao?
Ni kweli nyimbo ziwe fupi fupi. Ila pia uwanja ungekuwa na speakers ingesaidia sana.
 
Inasemekana kuwa Shabiki ni mchezaji 12 wa timu wakati wa mechi, hivyo Ally Kamwe na Ahmed Ally wasemaji wa Yanga na Simba wanafanya kila jitihada ya kuwataka wanachama na mashabiki wa timu hizo washangilie mwanzo mwisho wa mechi zao muhimu. Hata hivyo sayansi ya akili na tabia ya mtu inamtaka mtu mwenye afya timamu ya mwili na akili afurahi, kushangilia, kucheka, kupiga makofi na vigelegele na kutabasamu pale tu anapokutana, sikia au kuona tukio zuri linalompendeza.

Nipunguani tu anaeweza kucheka na kushangilia wakati wa huzuni. Kwa maana hiyo hakuna mwanachama wala shabiki wa Simba au yanga anaeweza kushangilia, kucheka na kupiga vigelegele mfululizo hata kama timu yake iko nyuma kwa magoli 3 dhidi ya mpinzani wake. Watu wanaoweza kushangilia timu muda wote hata kama timu imefungwa ni ama punguani au mtu mwenye maslahi na mechi husika zaidi ya furaha tu ya kushinda mechi.

Hivyo, basi ili watu ambao wanaweza kushangilia timu mwanzo mwisho bila kujali chenga za wachezaji wala matokeo ni watu wenye maslahi ya moja kwa moja (palpable) na mechi zaidi ya timu kushinda. Hawa watu wenye masilahi ya moja kwa moja (wanaolipwa) ndio wanaowatia hamasa ya kushangilia muda wote mashabiki ambao malipo yao ni furaha tu kwa timu kushinda mechi, Kifupi Yanga na simba lazima wawe na kikundi ambacho kitalipwa kwa kazi ya kushangilia bila kujali mwenendo na matokeo ya mechi. Timu zote kubwa kwenye nchi zote wanafanya hivyo.

Nitoe mfano kule US ambako basket ball inachezwa sana kwa hamasa. Vikundi vya hamasa vya kulipwa vina uwezo mkubwa mpaka wa kupita angani kwa ndege ndogo siku na muda mchache kabla ya mechi kuhamasisha watu kwenda uwanjani kwa kupeperusha mabango (banners) na moshi wenye rangi za timu husika. Ndege zinapita mitaa yote ya mji kualika watu waende kushangalia timu husika.

Kule kiwanjani kuna kuna kundi linashangilia sana na kuanzisha nyimbo ambazo zinafahamika na washabiki wote wa timu hiyo, hivyo uwanja wote wanaimba wimbo mmoja kutoka kona zote waliko mashabiki wao, na kama ni kelele ni za aina moja tu uwanja mzima. Hawa wanawaambukiza wengine kushangilia hata wale wenye njaa na kuwa kitu kimoja pale uwanjani. Hiki kikundi kitaimba na kushangilia kwa nguvu sana hata kama timu iko nyuma, maana wao wana maslahi mengine kabisa ambayo yana vigezo vyake vya ufanisi na ulipaji.

Huwezi kutegemea mtu mwenye njaa, asiekuwa na usafiri wa kurudia kwake na asiyelipwa chochote ashangilie timu yake hata kama imefungwa, huo utakuwa upunguani kama watafanya hivyo.
Sio kweli
 
Sio kweli
kaka mtu ambae faida yake pekee kwenye timu ni kushinda na kuchukua kombe atashangilia tu kama wachezaji wakipiga chenga, udambwiudambwi, wakipiga pasi sahihi, wakifunga goli na wakichukua kombe (trophy), nothing more nothing less. Timu ikifungwa watu wao wataondoka uwanjani mapema kabisa. Timu imefungwa 5-0 mimi nipige vigelegele na kushangilia kwa nguvu nimerogwa? ni msukule?. Sisi wanachama na mashabiki tunashangilia pira safi na ushindi baaaaaasi, hivyo ili tununue jezz, twende viwanjani kwa wingi na kushangilia kwanguvu tunahitaji wachezaji wazuri, benchi la ufundi zuri, uongozi bora na makombe, baaaaaaasi!!! hayo mengine ni majungu tu maana sisi hatuna financial gains wala hisa kwenye timu, raha yetu ni ushindi na kandanda safi
 
Sio kweli
Kule kwetu Tobago tunasema wewe Una tatizo la ukosefu wa exposure, unataka watu washangilie kama wale kama vile lakini hutaki kujua ni kwanini wanashangilia wale kama vile. Unakopi tukio bila supporting background yake.

Kikundi Cha hamasa viwanjani inatakiwa kiwe ni sehemu ya muundo (organogram) wa timu. Kina bajeti yake kabisa ya kununua kama ni vigoma, matarumbeta, vibwaya, makayamba, chakula, nauli na posho.

Kila mtu pale uwanjani siku za mechi anatakiwa ajue nini kinakwenda kutokea uwanjani na sio kama Sasa utakutana na watu binafsi wanajipigia na kujicchea kwa hiari Yao TU. Wanarukaruka kama vile wanawashwa na viwavi.
 
Kuna time mechi ikitulia ushangiliaji wa mashabiki wa ulaya unavutia sana.

Mara wasimame kwa zamu jukwaa hadi jukwaa, waimbe nyimbo ya pamoja, wamuimbie mchezaji anaefanya poa kwa wakati huo. Wajipange kwa rangi ya timu yao/ picha fulan.
Inavutia kwakweli..

Njoo huku sasa ni mavuvuzela kwa kwenda mbele, ni pweeee pweeee mpaka boli linaisha.
 
Kuna time mechi ikitulia ushangiliaji wa mashabiki wa ulaya unavutia sana.

Mara wasimame kwa zamu jukwaa hadi jukwaa, waimbe nyimbo ya pamoja, wamuimbie mchezaji anaefanya poa kwa wakati huo. Wajipange kwa rangi ya timu yao/ picha fulan.
Inavutia kwakweli..

Njoo huku sasa ni mavuvuzela kwa kwenda mbele, ni pweeee pweeee mpaka boli linaisha.
Ushangiliaji wetu unaongozwa na hisia zaidi kuliko mpango mkakati wa timu. Wale wenzetu usione vile wanasangia muda wote, Wana watu ambao wanacoordinate ushangiliaji. Hawa watu ni kundi la watu ambao hawaadhiliwi sana na matokeo ya mechi kiwanjani, walipwa kwaajili ya kuratibu ushangiliaji bila kujali timu imefungwa au laa! Kazi Yao ni kuwarudisha mchezozi watazamaji hata kwenye nyakati mbaya za timu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom