KERO Elimu bure lakini Shule ya Nyampulukano – Sengerema kuna upigaji mkubwa. TAKUKURU walifanya kazi yao, 'wakapozwa' wakaingia 'mitini'

KERO Elimu bure lakini Shule ya Nyampulukano – Sengerema kuna upigaji mkubwa. TAKUKURU walifanya kazi yao, 'wakapozwa' wakaingia 'mitini'

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Nyampulukano .jpg
Shule ya Secondary Nyampulukano iliyopo Wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza ili kupata nafasi ya kuhamia pale au kwa Wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza wanatozwa Tsh. 320,000 au unapeleka mifuko 10 ya saruji pamoja na Nondo nne, kitu ambacho ni kinyume kabisa na utaratibu wa elimu bila malipo.

Ofisi ya Mkuu wa Shule hiyi imekuwa kikwazo kwa kuongeza michango ya shule pasipo utaratibu. Ukishatoa michango hiyo kama kiingilio unapaswa tena kuchangia gharama za kuishi hosteli hiyo kwa Mwaka 860,000 michango ambayo haina uhalisia.

Uchanganuzi wa michango hiyo upo hivi:
1. Tsh 250,000 kitanda
2. Tsh 65,000 Dawati
3. Tsh 50,000 ukarabati
4. Tsh 25,000 walimu wa muda
5. Tsh 645,000 chakula
BARUA 2 (1)_page-0001.jpg

BARUA 2 (1)_page-0002.jpg
Kwa hali hiyo shule inajikuta inatoza fedha nyingi kwa kila Mwanafunzi pasipo uhalisia kwa Wanafunzi hawa huletewa fedha kwa ajili ya Elimu bila malipo.

Tunaomba JF itusaidie kufichua uovu huu ni kero iliyoshindikana.

Tumechukua hatua kadhaa kutoa taarifa kwa viongozi ngazi mbalimbali lakini hakuna hatua sitahiki zilizochukuliwa.

Wazazi na Walezi wa Wanafunzi wanatozwa fedha ambazo hawakustahili kutozwa, ndio maana Walimu wengi wakiwemo wanaoshirikiana na Mkuu wa Shule na Idara ya Uhasibu wanatamani kubaki hapo kwa kuwa kuna maslahi mengi.

Taratibu za kuongeza malipo hazizingatiwi kwa kuwa Shule ya Serikali Mwalimu Mkuu au Uongozi hauwezi kujiamulia bila kushirikisha Wazazi na Walezi kisha kwenda hatua nyingine ngazi ya Wilaya na Mkoa, yote hayo hayafanyiki.
Screenshot 2026-01-14 160150.jpg
Unaweza kupiga picha tu kama kila Mwanafunzi analipia zaidi ya Shilingi Laki Nane, ukizidisha na idadi ya Wanafunzi utapata picha wanaingiza kiasi gani.

Serikali ya sasa mifumo yake mingi malipo yanafanyika kwa Control Number lakini huku Wazazi na Walezi wao wanalipia kupitia Akaunti ya Shule ambayo wanajua wanaimudu kutoa fedha.

WAKAGUZI WALIANDIKA RIPOTI IMEPOTEZEWA
Wakaguzi wa Kanda walikuja na kufanya ukaguzi kuhusu mambo mbalimbali, wakaandika ripoti lakini waliyoandika hayakutekelezwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Sengerema kwa sababu ambazo wanazijua wao wenyewe.

TAKUKURU SENGEREMA NAO WALIINGIA MITINI
Taarifa ya kinachoendelea ilifikishwa hadi TAKUKURU Taifa, wao wakaishusha ngazi ya Mkoa kisha ikashushwa TAKUKURU Sengerema, ikaanza kufanyiwa kazi vizuri hadi ikafikia hatua Mkuu wa Shule na Mhasibu Mkuu wakatakiwa kutotoka nje ya Mkoa.

Muda mfupi baadaye kimya kikatawala, TAKUKURU waliokuwa wakisimamia jambo hilo hawakutoa ushirikiano tena, tukajua tu KAZI TAYARI.

Wahusika wakaanza kutamba mtaani kuwa hawawezi kufanywa chochote na TAKUKURU kwa kuwa tayari wameshamalizana nao.

Tunakoelekea itafika hatua watu tutaacha kuripoti changamoto kama hizi kwa kuwa hakuna uwajibikaji, kama mamlaka tunazozitegemea na Viongozi tunaowategemea ambao ni wasaidizi wa Rais wananunulika kirahisi hivyo, basi ni ngumu kutoboa.

Video inayoonesha Shule ya Sekondari Nyampulukano.
Pia soma ~ Mwenyekiti wa Bodi: Shule ya Sekondari Nyampulukano idadi ya Wanafunzi waliohitaji kujiunga kwetu ni wengi kuliko uwezo wa shule
 
Du hapo ndo watz tunapo fail aisee. Kwamba hilo ndilo suluhisho?
Hakuna shule inayojiamulia michango hayo yote ni makubaliano ya kamati ya shule na wazazi , na kimsingi hiyo siyo shule ya bweni maana yake hizo hostel zinendeshwa kwa gharama binafsi … HAKUNA ELIMU BURE NI ELIMU BILA ADA
 
Na katika hizo gharama hapo ungependai ipi ipunguzwe?
 
Shule ya Secondary Nyampulukano iliyopo Wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza ili kupata nafasi ya kuhamia pale unatozwa hela Tsh. 320,000 au unapeleka mifuko 10 ya saruji pamoja na Nondo nne, kitu ambacho ni kinyume kabisa na utaratibu wa elimu bila malipo.

Ofisi ya Mkuu wa Shule imekuwa kikwazo kwa kuongeza michango ya shule pasipo utaratibu.

Ukishatoa michango hiyo kama kiingilio unapaswa tena kuchangia gharama za kuishi hosteli hiyo kwa Mwaka 860,000 michango ambayo haina uhalisia.

Uchanganuzi wa michango

1. Tsh 250,000 kitanda
2. Tsh 65,000 Dawati
3. Tsh 50,000 ukarabati
4. Tsh 25,000 walimu wa muda
5. Tsh 645,000 chakula
Hivyo, kujikuta shule inatoza fedha kubwa pasipo uhalisia kwa Wanafunzi hawa huletewa fedha kwa ajili ya Elimu bila malipo.

Tunaomba JF itusaidie kufichua uovu huu ni kero iliyoshindikana.

Tumechukua hatua kadhaa kutoa taarifa kwa viongozi ngazi mbalimbali lakini hakuna hatua sitahiki zilizochukuliwa.

Wazazi na Walezi wa Wanafunzi wanatozwa fedha ambazo hawakustahili kutozwa, ndio maana Walimu wengi wakiwemo wanaoshirikiana na Mkuu wa Shule na Idara ya Uhasibu wanatamani kubaki hapo kwa kuwa kuna maslahi mengi.

Taratibu za kuongeza malipo hazizingatiwi kwa kuwa Shule ya Serikali Mwalimu Mkuu au Uongozi hauwezi kujiamulia bila kushirikisha Wazazi na Walezi kisha kwenda hatua nyingine ngazi ya Wilaya na Mkoa, yote hayo hayafanyiki.
Unaweza kupiga picha tu kama kila Mwanafunzi analipia zaidi ya Shilingi Laki Nane, ukizidisha na idadi ya Wanafunzi utapata picha wanaingiza kiasi gani.

Serikali ya sasa mifumo yake mingi malipo yanafanyika kwa Control Number lakini huku Wazazi na Walezi wao wanalipia kupitia Akaunti ya Shule ambayo wanajua wanaimudu kutoa fedha.

WAKAGUZI WALIANDIKA RIPOTI IMEPOTEZEWA
Wakaguzi wa Kanda walikuja na kufanya ukaguzi kuhusu mambo mbalimbali, wakaandika ripoti lakini waliyoandika hayakutekelezwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Sengerema kwa sababu ambazo wanazijua wao wenyewe.

TAKUKURU SENGEREMA NAO WALIINGIA MITINI
Taarifa ya kinachoendelea ilifikishwa hadi TAKUKURU Taifa, wao wakaishusha ngazi ya Mkoa kisha ikashushwa TAKUKURU Sengerema, ikaanza kufanyiwa kazi vizuri hadi ikafikia hatua Mkuu wa Shule na Mhasibu Mkuu wakatakiwa kutotoka nje ya Mkoa.

Muda mfupi baadaye kimya kikatawala, TAKUKURU waliokuwa wakisimamia jambo hilo hawakutoa ushirikiano tena, tukajua tu KAZI TAYARI.

Wahusika wakaanza kutamba mtaani kuwa hawawezi kufanywa chochote na TAKUKURU kwa kuwa tayari wameshamalizana nao.

Tunakoelekea itafika hatua watu tutaacha kuripoti changamoto kama hizi kwa kuwa hakuna uwajibikaji, kama mamlaka tunazozitegemea na Viongozi tunaowategemea ambao ni wasaidizi wa Rais wananunulika kirahisi hivyo, basi ni ngumu kutoboa.

View attachment 3529774

Video inayoonesha Shule ya Sekondari Nyampulukano.
Hi shule ni ya kutwa hiyo michango ni makubaliano binafsi ya wazazi na uongozi wa shule kwa wanafunzi wanaotaka kukaa hostel

Kwa kuzingatia gharama za uendeshaji ya hostel, hizo gharama ni sahihi kabisa mkuu

NB
Shule hii ina advance pia inayoendesha kwa mfumo wa bweni na serikali na hakuna hizi gharama
 
Hyo shule wanafundisha haswa ipo vzur sana kitaaluma hvyo inawanafunz weng sana na wanaotaman kuhamia ni weng,kwahyo ili wapunguze usumbufu wa waomba nafas hvyo wameamua kutumia hyo kama fursa

Hvyo ni chaguo lako,hutak peleka mtoto kwingine
 
Hyo shule wanafundisha haswa ipo vzur sana kitaaluma hvyo inawanafunz weng sana na wanaotaman kuhamia ni weng,kwahyo ili wapunguze usumbufu wa waomba nafas hvyo wameamua kutumia hyo kama fursa

Hvyo ni chaguo lako,hutak peleka mtoto kwingine
 
Hyo shule wanafundisha haswa ipo vzur sana kitaaluma hvyo inawanafunz weng sana na wanaotaman kuhamia ni weng,kwahyo ili wapunguze usumbufu wa waomba nafas hvyo wameamua kutumia hyo kama fursa

Hvyo ni chaguo lako,hutak peleka mtoto kwingine
 
Back
Top Bottom