Elimu bure hakuna, Serikali imekurupuka

Elimu bure hakuna, Serikali imekurupuka

Hizo laki mbili zimetoka hazitatolewa tena mpaka mwakani 2017
hii ndio hoja. Serikali imekuwa bigwa Wa kuanzisha mwendo na si kuumaliza. Waamini Wa biblia wanajua kuwa heri mwisho mzuri kwenye ushuhuda. Matangazo yote mikwala n.k kumbe ni laki na nusu. Gharama za matangazo yanayofanyika nadhani yanazidi pesa zilizotolewa. Ni hvi unit cost ya mtoto mmoja wa private ya kawaida wanaolipa ada ya million 1.8 ni sawa na shule yangu yenye watoto 400 ya serikali. Kiuchumi bora umfundishe watoto kumi wanaolipa vizuri kulikon watoto 400 wasiolipa maana kuwabeba ni Mzigo. Tunashauri serikali isitumie neno la elimu bure waseme tunachanga nikuchangie ili hata wazazi na wanafunzi waone thaman ya elimu wanayoipata
 
Fafanua hizo bil.18 na point kwa shule ngapi za Tanzania ukatae hiyo laki 2 kwa kila shule?
anayetakiwa afafanue ni aliyeleta hoja kuwa haitoshi, sio mimi, ukileta hoja ni lazima uweze kuwa na strong arguments kutetea hoja yako sio kuniuliza tena mimi maswali wakati nategemea maelezo
 
Mbona mnakuwa wakali sana kila anayehoji haya mambo!!?

Lengo ni kujadiliana na pengine kuishauri serikali namna bora ya kutekeleza hii sera ambayo kwa vyovyote vile ni nzuri na hakuna anayeipinga.

Na tukunbuke pia kuwa utekelezaji wake ndo tu umeanza na ni kitu kilichokuwa nje ya utaratibu wa kibajeti. Kwa hiyo ni lazima tu kutakuwa na mapungufu ya hapa na pale ktk utekelezaji wake!!

Binafsi nimemuelewa mleta hoja na
wewe pia nimekuelewa.
Ni kwamba hizi 18.6bn ni kwa ajili ya
shule zote za msingi na sekondari kwa
mwezi desemba, 2015.
Kwa mujibu wa magawanyo wa fedha
hizo ni kwamba;

Kwa sekondari kidato cha I -IV kila mwanafunzi atalipiwa na serikali
Tshs. 45,000 kama fidia ya ada ambayo ilipaswa kulipwa na mzazi wa mwanafunzi.

Kwa shule za msingi kila mwanafunzi atalipiwa na serikali Tshs. 10,000= kwa mwaka.

Kwa utaratibu wa serikali ni kwamba hizo fedha zitakuwa zinatolewa kila mwezi kwa kutumwa moja kwa moja ktk shule husika, hazitalipwa kwa mkupuo mmoja!!

Sasa kwa mfano kama shule ya sekondari X ina wanafunzi 145 kidato cha I - IV (nyingi ya shule za vijijini zina idadi ya wanafunzi inayo range kati ya 90 - 350) maana yake shule hii shule ktk mgawa wa mwezi desemba imepata;

45,000 ÷ 12 × 145 = Tshs. 543,750/=

Maana yake haya ndiyo matumizi ya shule hii kwa mwezi January, 2016 mara shule zitakapofunguliwa!!

Hii ndiyo hoja nadhani nilivyomuelewa mleta mada. Swali lake ni kwamba, hizi pesa zinatosha kuendesha shule kwa mwezi??

Mimi binafsi sina jibu ktk swali hili kwa sababu kila shule ina mahitaji na bajeti yake ya mwezi, muhula na kwa mwaka mzima. Ninachoweza kusema ni kuwa inategemea na shule.

Kwa sababu kuna shule zina wafanyakazi (casual labours) ambao hawako ktk payroll la serikali na hulipwa na shule kama walinzi, wahudumu wa ofisi nk kulingana na vyanzo vya mapato ya shule husika iwe ni kutoka EK au michango ya wazazi kwa wakati ule kabla ya sera ya elimu bure kuanza. Pia kuna shule zingine vijijini hazina walimu wa kutosha especially wa sayansi na shule huajiri parttime teachers ambao hulipwa posho ya kati ya Tshs. 150,000 hadi 250,000 ili wanafunzi hawa wafundishwe

Hii kitu ni halisi wala si kuandika tu hapa. Mimi hapa naandika nikiwa Shinyanga na natembea sana vijijini. Kuna shule za sekondari ziko kwenye very remote areas na mazingira ni magumu sana to the extent kwamba walimu hupakimbia huko kila wanapopangiwa. Kuna shule moja iko wilaya ya Kishapu inaitwa Paji ina wanafunzi 123 wa kidato cha 1 - 4 na walimu 5 wote wa masomo ya Arts na language hasa Kiswahili ns History, Geography na Civics. Hakuna mwalimu wa Mathematics, physics, Biology na Chemistry.

Anachofanya mwalimu mkuu alikuwa anatafuta vijana wa walionaliza kidato cha sita na kusaidia kufundisha. Na huwezi amini kuwa kila mwaka mwalimu huyu hupeleka vijana wawili au watatu kidato cha tano (A'level). Sasa serikali ime consider hii kitu??

Na kuna shule zingine wala hazina watu wa namna hii kwa sababu kama ni walinzi au muhudumu wa ofisi ama mtunza bustani wote wanalipwa na serikali. Kwa hiyo ni wazi, shule kama hii pesa kama hii inaweza kutosha tu kwa mwezi japo kwa kubanana sana!

Kwa hiyo hii 18.6bn ni nyingi kwa kutamkwa kwa pamoja lakini zikishagawanywa mashuleni, picha halisi ya kitakachokwenda ktk kila shule ni kama nilivyoonesha hapo juu na kwa hakika kuna shule zinaweza kupata hata Tshs. 150,000 tu kwa mwezi!!!
kaka umeeleweka pesa kiukweli haitoshi ndiyo maana hata ukiangalia kwenye michango ya chakula na pesa za wapishi, kununa mafuta, kuni, majia, chumvi na vingine shule nyingi zimweongoze sana gharama hiyo ukilinganisha na miaka mingine hivy lengo wanataka kufidia kwakua pesa hyo haitoshi
 
Dah! Kuna watu wanakurupuka sana. Sijui huyu mleta mada kaandika wakati amepakatwa au ameinama! Yaani nawaza tu wadau.
Umezidi kwa umbeya. Kama una uhakika na unachokisema kwa nini haureveal hiyo shule ili tujue?
Magufuli kawafunga midomo UKAWA. Wamebaki kuandika umbea tu humu mitandaoni. Unamaikia John Mnyika siku hizi? Wapi amefia Salum Mwalimu? Wapi Tundu Lissu? Wapi Freeman Mbowe? Wote wameufyata kwa kasi ya Magufuli. Wakijaribu kusema wanabaki kuwa kituko. Yule mzee wa kujinyea nyea eti alilalamika kuwa wafanyabiashara waliomsaidia kwenye kampeni wanasakamwa na serikali. Alipotakiwa kuwataja ameufyata. Wengine wanasema eti Magufuli anatekeleza ilani ya UKAWA. kwikwikwikwiiiii
Siku zote wachawi ni adui wa maendeleo. Wachawi kama huyu mleta mada hawastahili hata kuishi. Ni wale ambao kwa mikoa ya wenzetu wanaangamizwa huku wanajiona
Kakuambia wewe kama nani? Pole sana
Unataka nije kwenye field gani ilhali kila siku nashinda field?
 
Serikali hapa inazid kupigilia msumar kwenye jeneza la elimu la Tz,achilia miundo mbinu kutotosheleza kupokea wanafunz wengi,kuna suala la madeni ya nyuma.Kuna shule ina wanafunz 810,inapatiwa sh.milion 2.5,wastan wa sh.3200 kwa mwanafunz kwa mwez,huku shule inadaiwa sh.million 18.Serikal haijatoa muongozo wa kulipa hayo maden ya nyuma hili ni tatizo.
 
mkuu hiyo hesabu yako umeipigaje, maana zimetolewa bilioni 18 na point, wewe hiyo laki mbili umegawanyaje hadi kuipata?
Bilion 18 sio kwa kila shule ni kwa shule zote jumla hiyo,katika hiyo bil 18 toa bil 3 za.ada za mitihani like NECTA
 
Hilo halituhusu tulishampa kura, akishindwa kukusanya kodi is up to yy
 
hii ndio hoja. Serikali imekuwa bigwa Wa kuanzisha mwendo na si kuumaliza. Waamini Wa biblia wanajua kuwa heri mwisho mzuri kwenye ushuhuda. Matangazo yote mikwala n.k kumbe ni laki na nusu. Gharama za matangazo yanayofanyika nadhani yanazidi pesa zilizotolewa. Ni hvi unit cost ya mtoto mmoja wa private ya kawaida wanaolipa ada ya million 1.8 ni sawa na shule yangu yenye watoto 400 ya serikali. Kiuchumi bora umfundishe watoto kumi wanaolipa vizuri kulikon watoto 400 wasiolipa maana kuwabeba ni Mzigo. Tunashauri serikali isitumie neno la elimu bure waseme tunachanga nikuchangie ili hata wazazi na wanafunzi waone thaman ya elimu wanayoipata
Changa nikuchangie mbona ilikua programu nzuri tu,ilianza enzi za Mwinyi ndo mdau huo hata michango ya madawat ilianza nami nikaamua kwenda na meza yangu shule
 
Bilion 18 sio kwa kila shule ni kwa shule zote jumla hiyo,katika hiyo bil 18 toa bil 3 za.ada za mitihani like NECTA
bilion 18 sio kila shule nafahamu hilo, ila inatolewa bilioni 18.6 kila mwezi na hakuna necta kila mwezi, mimi siungi mkono kama inatosha au haitoshi na serikali inapochemsha ni vizuri kuikosoa kwa nguvu, point yangu ni kuwa unapokuja kupost mada jamiiforums post kitu ulichokifafanua vizuri kwa facts& figures, ili uonekane una point, sio kusema vitu nusunusu, au vitu ulivyovifanyia utafiti nusu alafu unajifanya unajua full
 
Hvi kweli shule inapewa laki mbili hata kama ni kwa mwezi hapo hapo toa hela ya mlinzi,maji,umeme hapo bado Hela za chaki shule zitaendeshwa vp hizi!!!
Taja jina la hiyo shule na mahali ilipo ,kama ni kweli itafanyiwa kazi hatupo kwenye zama za Jk za usanii sanii unaotuletea ww
 
Idadi ya shule za Primary ni 15,816 na idadi ya wanafunzi ni 8,419,305
Idadi ya shule za Secondary ni 4,266 na idadi ya wanafunzi ni 1,638,695., ukichukua hizo takwimu utagundua kitu kingine cha kusikitisha kuwa watoto wengi wanaishia katika Elimu ya msingi kitu ambacho si afya kwa taifa..
Hapo kwenye mil 1 ya sekondari,zaid ya nusu huishia form IV hawaendeleo,nao wanaachwa hakuna.mwongozo wao
 
Watu wengne sijui mkoje. Mpo kwaajili ya kuchafua tu huo ni uchawi kabisa
 
Nimekuta na mkuu wa shule analalama kupewa mil.1.2,anauliza kama mock ya kanda alitumia mil.2 kununulia vifaa na chemicals za maabara kwa ajili ya mock ya form ya EZEB,atabalance vip mahesabu ili aweze kununua vifaa ya kufundishia?wazo la elimu bure ni zuri ila serikali imekurupuka kwa bila kuwashirikisha walioko kwenye field,elimu bure ni zaidi ya kulipia ada,bili za maji,umeme,mshahara wa mlinz,chak,kulipia ada ya mitihani wa form four n.k,kuna maandaliz ya mitihan ya mock ambayo nowdays iko kwenye continous assessment Necta,kwa shule za vijijin wasimamiz wa mitihan huhitaji kuhudumiwa na shule,vifaa vya maabara ni gharama hiv vyote havijapigiwa gharama na serikali hiyo tisa,kumi mlundikano wa wanafunz na walimu kutotimiziwa maslah yao,hii inaweza kuwa changa la macho kama BRN ILIVYOPIGWA CHINI NA WALIMU NASHAANGA WANAOANDAA RIPOTI WANAWADANGANYA WAFADHILI WA HUO MPANGA ILA KIUKWEL KATIKA ELIMU UMEFELI.
 
Hiyo ya laki mbili ni kweli.

Niliiona mahali ngoja ni attach
 
Soma hapo kuna shule moja inaitwa Koroma iko Arusha wamepewa 2k
 

Attachments

  • 1452349584117.jpg
    1452349584117.jpg
    109.6 KB · Views: 43
Na suggest elimu bora sio bora elimu....tz tunapenda free sana inatucost wadau....
 
Elimu bure makazi hakuna
Nchi ya maruhani one of the basic human neccessity is shelter (housing)not education
 
Back
Top Bottom