The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,950
- 12,548
Hatupaswi kufurahia kushindwa utekelezaji wa mikakati yenye tija kwa taifa leo na siku zijazo..twapaswa kushiriki kwa karibu ktk kuisaidia serikari kutatua changamoto zilizopo kwa kila mmoja wetu hasa wenye uwezo kuchangia kwa namna moja uboreshaji wa baadhi ya miundombinu,vifaa ktk mashule yanayotuzunguka huku tunakoishi,tunakofanyia kazi,fanyia starehe n.k
Haya ndiyo mawazo yanayotakiwa ili kuwasaidia watunga sera na watekelezaji wa sera hizo.
Basically, hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kuupinga mpango huu kwa sababu lengo na dhamira yake ni njema, kuifanya elimu kuwa huduma ambayo accessible kwa kila mtu mwenye uwezo na asiye na uwezo.
Problem ina raise ktk utekelezaji wake, kuwa hakukuwa na maandalizi ya kutosha.
Mfano, serikali ya awamu ya nne ilikuja na sera ya ujenzi wa shule za sekondari ktk kila kata
Walifanikiwa kwa kiasi kikubwa japo ni sera ambayo iliibua changamoto nyingi ambazo mpaka leo hazijatatuliwa ikiwemo;
1. Upungufu wa walimu hasa wa masomo ya sayansi
2. Uhaba au kutokuwepo kabisa kwa nyumba za walimu hasa maeneo ya vijijini
3. Nyingi ya shule hizi za sekondari za Lowassa (about 95%) kutokuwa maabara kwa ajili ya kufundishia masomo ya sayansi kwa vitendo.
4. Shule hizi kutokuwa na vifaa vya kujifunzia na kufundishia vinavyokidhi mahitaji ya wanafunzi k.v vitabu, vifaa vya maabara nk
5. Mengi ya majengo ya shule hizi yalijengwa chini ya viwango kiasi ambacho lifespan yake si zaidi ya miaka 20 ijayo yatakuwa yamechakaa kwa kubomoka kabisa!
6. Malalamiko ya walimu hawa hawa wachache waliopo kutopatiwa ufumbuzi wa kudumu. Mfano; uboreshwaji wa maslahi yao, kutolipwa kwa madeni na stahiki zao mbalimbali za miaka mingi, walimu kutokuwa na nyumba za kuishi ktk maeneo ya kazi nk
Sasa leo kabla serikali haijayapatia suluhisho la kudumu haya imekuja na sera nyingine inayotumia mabilioni ya shilingi ktk utekelezaji wake na wakati huohuo matatizo hayohayo yaliyopo miaka mingi nayo yanahitaji uwekezaji wa mabilioni ya fedha huku eti wazazi/walezi woote bila kujali uwezo wao wakivuliwa jukumu lao la kuchangia elimu ya watoto wao. Yaani tumesahau kabisa sera ya "cost sharing!!"
Sina hakika kama hii kitu itakuwa sustainable. Naamini kabisa, mzigo huu in the end serikali itashindwa kuubeba na ni kwa sababu ya hali ya uchumi wetu kutokuwa na uwezo huu.
Na kwa maana hiyo, kama ambavyo wazo au sera hii chanzo chake ikiwa ni mihemko ya kisiasa "ili tushinde uchaguzi", vivyo hivyo mzigo huu in the end utakavyorejeshwa kwa wazazi/walezi kwa njia ileile ya kisiasa!!
Tusubiri bajeti ya kwanza ya JPM 2016/2017 utapata uhalisia wa hili!!