Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 45,122
- 111,818
Wafanye tu iwe kesho tuunge wikendiBakwata watataka tule Jumanne 🥴
Wafanye tu iwe kesho tuunge wikendiBakwata watataka tule Jumanne 🥴
Tunakubaliana kuwa EID inategemea muandamo wa mwezi, ila ikishindikana kuonekana na ikiwa siku ya 30, bas siku ya 31 watu wanakula Eid?Muandamo wa mwezi ila ikitokea hujauona unafunga siku 30 kisha siku inayofuata unakula Idd, sawa kipenzi cocastic? Karibu Eid kesho Kigamboni.
Amina insha'AllahKesho jumapili ya tarehe 30 march 2025 ni sikukuu ya Eid Al fitri kwa waislamu wote duniani.
Eid hii inakuja baada ya kuonekana mwezi wa shawwaal (mfungo Moshi ) ambao ni alama ya kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Taarifa za kuonekana mwezi wa shawwaali zimepatikana toka mataifa mbalimbali ya kiislamu ikiwa pamoja na Saudi Arabia, Qatar na Umoja wa Falme za kiarabu UAE.
Mtume Muhammad صلى الله عليه وسلم amesema: "fungeni kwa kuonekana mwezi, na fungueni kwa kuonekana mwezi, na mwezi ukifunikwa juu yenu(msiuone) kamilisheni siku thelathini)
Kunako majaliwa mimi nataraji kuswali swala ya Eid kesho asubuhi saa Moja na nusu katika uwanja wa Mandela mtaa wa Pasua manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro..
Namuomba Allaah azikubali ibada zetu za mwezi wa Ramadhani, na kwa rehema zake atupe uwezo na umri wa kuifikia Ramadhani ya mwaka ujao. Aammiyn.
Upo sahihi.Tunakubaliana kuwa EID inategemea muandamo wa mwezi, ila ikishindikana kuonekana na ikiwa siku ya 30, bas siku ya 31 watu wanakula Eid?
Ahsante nitakaribia, unipokee pale Ferry.
Ahsante, 🙏🙏Karibu sana. 🤝
Tuwe makini katika elimu ya mustwalahul hadithi..الحديث صحيح غير صريح.
SABABU YA IBNU ABBAAS KUUKATAA MWEZI WA SHAMU HAIKO WAZI.
Na kama unaijua sababu hiyo itaje halafu ujiandae kujibu maswali.
Hadithi hii ya Kuraibu ni maarufu sana lakini maana yake haiko wazi na kwahiyo siyo hoja juu ya jambo lolote katika masuala ya mwezi!
Katika hadithi hii hakuna hata sentensi moja inayosema kwamba KILA NCHI NA MWEZI WAKE!.
Ukisema hadithi hii ni ushahidi kuwa kila nchi ina mwezi wake tutakuuliza NINI MAANA YA NCHI?!
Ukisema nchi ni kama vile Tanzania na Kenya kwa maana ya eneo linalotawaliwa na serikali moja chini ya mtawala mmoja tunakuuliza Mbona Abdullaahi Ibni Abbaas aliukataa mwezi wa Shamu wakati Madina alipokuwa anaishi Ibnu Abbaas na Shamu alipokuwa anaishi Muawiya ibn Abii Sufyaan ilikuwa nchi moja , dola moja, chini ya mtawala mmoja ambaye alikuwa Muawiya ibn Abii Sufyaan mwenyewe na Mji wa Madina ulikuwa ni mkoa ( jimbo ) katika serikali ya Muawiya?!
Mji wa Madina alipokuwa akiishi Ibnu Abbaas na mji wa Damascas (Dimashqi ) aliokuwa akiishi Muawiya ni kama vile Ibnu Abbaas kuishi Daar es salaam na Muawiya akawa Dodoma makao makuu ya nchi, je inafaa kusema kuwa watu wa DSM wawe na mwezi wao na watu wa Dodoma wawe na mwezi wao?!
Hadithi ya Kuraibu ni sahihi kabisa haina utata juu ya usahihi wake lakini utata upo kwenye maana yake, INATUFUNDISHA NINI?!
Sheikh ibn Baaz alisema ni "uwendawazimu dunia yote kufunga siku moja" kwa sababu maumbile ya dunia yenyewe yanakataa (yaani geography).Ndugu yetu @Chifu mkuu , anafunga msimamo wake na kuupambania kana kwamba ambao Wana msimamo wa pili wamepotoka wote kwa msimamo huo , wakati jambo hili ni lenye hitilafu kubwa hata Wanazuoni wakubwa wa zama zetu wakina Sheikh Ibn Uthaymeen, Ibn Baaz na Albani (Allaah awarehemu wote) wao wametolea ufafanuzi pia suala hili vizuri na kati ya hao hakuna hata mmoja aliyesoma ni makosa kusikia mwezi mahala Fulani (nchi nyingine) Kisha usifunge au kufungua , na wengine wameweka wazi kuwa msimamo wao kuwa kila watu wafuate mamlaka katika nchi Yao mahali walipo.
Naam uko sahihiKufunga siku ya eid ni dhambi na kula mchana wakati wa Ramadhan ni dhambi.
Mwezi kuonekana kwa mzunguko wake ni siku 29 au 30.Para ya 3 huyo mwenzako jana aliikataa, alisema ni funga ni siku 30, hakuna 28, au 29, ni 30 tyuh, na sio hiyo 31.
Ndo maana niliendelea na mjadala, nilicho kigundua, nyie wenyewe wahusika hamjui nini kinatakiwa kifuatwe, aidha siku timilifu za mfungo, au muandamo wa mwezi.
Naomba unijibu hili, EID inategemea siku timilifu za mfungo, au muandamo wa mwezi?
Hoja zenu zote zinajibika kirahisi ila kwa Sasa ni muda wa chai na naona mvua inapungua ngoja nikanywe chai kisha narudi kizijibu hoja zenu zote.Sheikh ibn Baaz alisema ni "uwendawazimu dunia yote kufunga siku moja" kwa sababu maumbile ya dunia yenyewe yanakataa (yaani geography).
Msimamo wake ni kuwa kila eneo kufuata mwandamo wake.
Sheikh Al-Uthaymeen alikuwa na msimamo kama Ibn Baaz, kwamba kila nchi inapaswa kufuata mwandamo wake, mradi wanazingatia ushahidi wa kisharia. Alisema kwamba kutokana na tofauti za maeneo na vipindi vya kuonekana kwa mwezi, si lazima nchi zote zifuate mwandamo mmoja.
Dalili alizozitumia ni pamoja na kauli ya Ibn Abbas (Radhiya Allahu Anhu) alipokataa kufuata mwandamo wa Muawiyah (Radhiya Allahu Anhu) kwa sababu mwezi haukuwa umeonekana katika mji wake. Hadithi hii inapatikana katika Sahih Muslim.
Hadithi ambayo huyu ndugu yetu Chifu mkuu anasema haipo wazi!
Ukifika Makka kwenye vibanda vya fatawa unaruhusiwa kuuliza swali tena ni bure bila gharama yoyote. Chifu mkuu aende akaulize hilo swali kule aangalie atapatiwa jawabu gani!
Hii ndiyo inaitwa kushibishwa itikadi. Yaani anashibishwa itikadi bila ya elimu, ni hatari hii.
Na ikiwa mhusika ana itakidi hivi, tumuulize; kama mwezi ni mmoja, Korea ya Kusini maghribi ikiingia yeye aliyepo huku Tz anaweza akafuturu? Kwamba Alhamdulillah mwezi ni mmoja duniani Korea ya kusini sasa hivi magharibi imeingia ngoja nifungulie!
Halikadhalika na kwako pia ujibu maswali yetu, tena kwa ufahamu wa kielimu na wala si kwa rai yako.Hoja zenu zote zinajibika kirahisi ila kwa Sasa ni muda wa chai na naona mvua inapungua ngoja nikanywe chai kisha narudi kizijibu hoja zenu zote.
Lakini nina maswali ambayo nitakuulizeni na nitahitaji majibu ya kielimu na sio ubabaishaji!.
Kheri mkuu , utaendelea na Hammaz kwa upande wangu Elimu yangu ndogo bado najitafuta na sijafikia uwezo wa kufanya mijadala ya kielimu na Wasomi.Hoja zenu zote zinajibika kirahisi ila kwa Sasa ni muda wa chai na naona mvua inapungua ngoja nikanywe chai kisha narudi kizijibu hoja zenu zote.
Lakini nina maswali ambayo nitakuulizeni na nitahitaji majibu ya kielimu na sio ubabaishaji!.
Ewaaa!Kheri mkuu , utaendelea na Hammaz kwa upande wangu Elimu yangu ndogo bado najitafuta na sijafikia uwezo wa kufanya mijadala ya kielimu na Wasomi.
Mimi kwenye hilo sijachagua upande Fulani upo sawa wala kusema upande fulani wana msimamo batili , ila niliposimamia ni kwamba jambo ambalo lina hitilafu kubwa na pande zote zina hoja na makundi ya Maulamaa wanaojulikana tena wakubwa wakispoti si vyema mtu ambaye kachagua upande mmoja kuwaona wenzake wapo kwenye batili tena bora awaone wapo kwenye batili maana inaweza litakotekea kwenye nafsi ya mtu naturally baada ya kupata Elimu ila kuwatangazia hadharani kwamba mko kwenye batili na wangu ndio sahihi wakati na unaodai wapo kwenye batili wana waliowatangulia wanavyuoni wakubwa katika msimamo wao.
Kwa hiyo najitoa kwenye majadiliano na sababu nyingine ni kwamba sijaweka wazi Mimi nipo upande upi .
Naaam! Naam! Naam!Binafsi nilishtushwa sana na kauli ya ndugu yetu kwamba dunia nzima tunapaswa kufuata mwezi mmoja na akasema yeye ni msomi
Sasa wakati mwezi unaandama sehemu fulani ya dunia,sehemu nyingine watu ni usiku wamelaa,sasa wakipambazukiwa na siku ya funga na wao hawajatia nia usiku kwa kuwa hawakuwa na taarifa za mwandamo kabla hawajalala,je watafunga kwa nia ipi ?
Maana ili funga ijuzu basi yampasa mtu alale na nia usiku wa kuamkia mfungo
Tusifuate itikadi bali tufuate dalili za kielimu
Ntabakia kuwa msomaji kwa yatakayo endelea
Kabla hatujaenda kwenye hoja zingine tuanzie kwanza hapaSasa palikuwa na mwezi wa Tanganyika na mwezi wa Zanzibar, Baada ya muungano tukabaki na mwezi mmoja! Sasa wewe uliyeenda darasani na madrassa unaweza kunisaidia kujua mwezi mmoja ulienda wapi baada ya muungano?!
Na je huu mwezi unaotangazwa na bakwata kwa Sasa ni ule wa Zanzibar au ni wa Tanganyika?!
Baarakallaahu fiykum.Ewaaa!
Wasomi ndiyo wanakuwa hivyo ndugu yangu kama wewe ulivyofanya.
Wanawazuoni wametofautiana uelewa, maswahaba wenyewe wametofautiana uelewa. Hii, inampaasa aelewe kwa namna hiyo.
Tunajaribu kumuonyesha kuwa upande mwengine wa ufahamu upo hivi, hivyo akimuona mwenzake anafuata mwandamo wa eneo lake basi asimuone ya kuwa ni mjinga au yumo kwenye makosa makubwa mnoo!
Maadamu kwa wengine leo ni Eid basi tunawatakia Eid mubaraka. Na wengineo wanaweza wakawa kesho ama kesho kutwa, basi nao tutawatakia Eid mubaraka.