eFootball Special Thread

Nikatoa boko bhana jamaa akaweka chuma wavuni mapema sana, kabla hajamaliza kushangilia vizuri nikamnyamazisha na ubao ukawa unasoma 1-1 πŸ˜‚.

Dakika chache kabla ya kipindi cha kwanza hakijaisha nikaweka chuma ya pili na ubao ukawa unasomeka 2-1, nikasema sasa hapa naweka ultra defensive ili nimalize kipindi nikiwa naongoza πŸ˜‚.

Kurudi kipindi cha pili sasa jamaa akaja na moto mwingi sana ikabidi niweke ultra defensive mapema πŸ˜‚, haikupita muda mrefu akajichanganya bhana nikaweka chuma ya 3, ubao ukasomeka 3-1.

Huko dvn nikiwa naongoza tu basi ujue kinachofata hapo ni kukuwekea ultra defensive πŸ˜‚, jamaa aliniwashia moto lakini katikati ya mechi nikapata ujasiri wa kuscreenshot sababu ya ultra defensive.
πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡


Namna vile ambavyo mpinzani alikuwa moto golini kwangu ila shukrani ziende kwa ultra defensive πŸ˜‚.
πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡
 
Wakati naanza kucheza Pvp ilikuwa mechi ikianza tuu nawasha defensive zote mbili πŸ˜ƒsasa nikikutana na mtu ambaye anawasha attacking zote mbili nilikuwa napenda mno maana nikipiga tu through na strikers wangu walikuwa na counter target unakuta yupo peke ake kinachofata ni kushinda tu goli 🀣 kuna mshkaji wangu aliniambia acha usizoee hvyo ndo nikaacha isingekuwa hvyo ningeendelea na umafaia wangu
 
Leo nimekutana na mtu kafanyiwa script alikuwa na Gnabry ana pinpoint crossing na Nunez wa booster mbili anaruka huyo balaa kila cross anpiga kichwa jamaa kapiga cross kama 14 hivi tano zimegonga post Nunez anruka kichwa kinagonga post tuuπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Alafu mbaya zaid dakika za jioni napata goli nadhan imemuuma sana hii mechi

Kuja kumchek jamaa yupo division one rank ya 79,000 na kikosi chake cha kawaida tuu
 
Huyo Ben white anapiga cross ajabu
 
Mimi hii huwa nawasha baada ya kuongoza kuanzia goli 2 au wakati mwingine ikiwa mpaka kipindi cha pili naongoza goli 1, huko dvn nitaitumia sana tu.
 
Nilikutana na jamaa DMF ni edgar davids aisee nilimtesa sana hapo kati nahisi baada ya mechi hakuvua viatu πŸ˜‚.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…