eFootball Special Thread

Mama kumbe Nunez ana Bullet Header ndo maana nashangaa mbona vichwa ananigonga sana😃😃😃


Gilberto_ ukimpanga Nunez natoka Room 🤣🤣🤣sichezi na wewe
Kuna kipindi nilimpa training za vichwa tu Jumping 100, heading 100 alikuwa anaua 🤣.. na ukijumlisha ana mashuti huyo, sema yupo mapumzikoni ye na BatiGoal kwa saivi
 
Kuna kipindi hapo kati hii card ilikuwa ya moto sana, kama mwezi uliopita tu. Nunez kila nikimtumia lazima atoke na mpira wake uwanjani. Sijui KONAMI hawajaamua kuiua hii card kama ya Edrick na phenomenal finishing yake lakini kibonde tu.
Wameipunguza makali dah sema kwenye heading bado yupo vizuri akikutana na mabeki wafupi.
 
Wakuu Mimi ndo naanza bhana..

Kuna hii shida nakutana nayo....yani pass hazitoki hata niguse mara 3 wala kick, wala through ball....hii shida inaishaje...

Kuna daraja la 9 na 8 nmecheza vyema sana bila shida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…