Nimemfahamu Lowasa kama kiongozi mwenye msimamo na Kiongozi anayesimamia mambo bila kuyumbishwa.
Kinachonipa wasiwasi kwake ni Watu waliomzunguka ambao ndio wanaoisapoti safari yake ya matumaini.
Watu hao ni Rostam Aziz, Ibrahim Msabaha, Nazir Karamagi na wengine wengi ambao wamewahi kutuhumiwa kwa ufisadi.
Mashaka yangu kwa Watu hawa. Ni je baada ya ushindi wa El kama Rais hawa watu si watagawana Nchi vipande vipande kwa manufaa yao na ili kurudisha gharama zao walizotumia kwenye safari ya Matumaini?.
Watanzania tutafakarini sana kwa maslahi ya wote na sio kwa ajili ya wachache.