Edward Lowassa huenda ndio mwanasiasa anayeonekana mchafu zaidi hapa Tanzania kutokana na kashfa za Ufisadi zilizomfanya kujiuzuru bafasi ya uwaziri mkuu 2008.
Mbali na hapo inaonekana ndio mtu mwenye nia, mipango na mikakati mingi zaidi kuhakikisha anakuwa rais wa Tanzania 2015 kwa gharama yoyote!!
Ukiondoa wafuasi wake, watu wengi wakisikia jina la Lowassa fikra na mawazo yao yote huhamia kwenye kashfa za Ufisadi alizonazo kuliko kitu kingine chochote kinachomuhusu Lowassa.
Lowassa ameonekana akifanya juhudi kadhaa kuhakikisha nyota yake ya kutaka urais inang'aa kupitia mikakati kadhaa;
1/Kuhakikisha wapambe wake wanapata nafasi muhimu za kisiasa ndani ya serikali, bungeni na ndani CCM.(Kwa sehemu kubwa sana amefanikiwa hususani ndani ya CCM)
2/Kufifisha nguvu ya kambi zingine pinzani za urais ndani ya CCM.
3/Kujitakasa kisiasa kwa kutumia taasisi za kidini hususani makanisa(Kila mara ameonekana makanisani kama mgeni wa heshima na kutakaswa kwa maneno ya mibaraka kama ''Lowassa ni mnyonge hodari aliyeonewa''!!)
4/Kumwaga pesa nyingi za kumsafisha kwenye taasisi, vyombo vya habari, jamii na baadhi ya watu hususani viongozi wa dini na wanasiasa.
*Ni vipi Lowassa anaweza kuvuka kisiasa katika hali hii ya kashfa za kifisadi zinazomwandama ambazo hazifutiki?
Mbali na hapo inaonekana ndio mtu mwenye nia, mipango na mikakati mingi zaidi kuhakikisha anakuwa rais wa Tanzania 2015 kwa gharama yoyote!!
Ukiondoa wafuasi wake, watu wengi wakisikia jina la Lowassa fikra na mawazo yao yote huhamia kwenye kashfa za Ufisadi alizonazo kuliko kitu kingine chochote kinachomuhusu Lowassa.
Lowassa ameonekana akifanya juhudi kadhaa kuhakikisha nyota yake ya kutaka urais inang'aa kupitia mikakati kadhaa;
1/Kuhakikisha wapambe wake wanapata nafasi muhimu za kisiasa ndani ya serikali, bungeni na ndani CCM.(Kwa sehemu kubwa sana amefanikiwa hususani ndani ya CCM)
2/Kufifisha nguvu ya kambi zingine pinzani za urais ndani ya CCM.
3/Kujitakasa kisiasa kwa kutumia taasisi za kidini hususani makanisa(Kila mara ameonekana makanisani kama mgeni wa heshima na kutakaswa kwa maneno ya mibaraka kama ''Lowassa ni mnyonge hodari aliyeonewa''!!)
4/Kumwaga pesa nyingi za kumsafisha kwenye taasisi, vyombo vya habari, jamii na baadhi ya watu hususani viongozi wa dini na wanasiasa.
*Ni vipi Lowassa anaweza kuvuka kisiasa katika hali hii ya kashfa za kifisadi zinazomwandama ambazo hazifutiki?