Edward Lowassa ashiriki kampeni za Uhuru Kenyatta

Edward Lowassa ashiriki kampeni za Uhuru Kenyatta

Anajitesa bure tu naye! Angetulia tuu.

Kuna mambo anapaswa kupunguza kuyafanya kwa Nia njema kabisa.
 
hili ni kosa la kimataifa, hivi haoni mgogoro uliopo usa , juu ya tuhuma kwamba russia waliingilia mambo ya uchaguzi wao?
hata labour party ya uk ni pro democrats ya usa, lakini ukija uchaguzi wa usa labour party hawamuungi mkono mgombea wa democrats hata kama wangependa ashinde mtu wa democrats, na vivyo hivyo kwa conservative party ya uk ni pro republicans lakini hawafiki ktk level ya kuingilia uchaguzi wa nchi zingine.
huyu atatuletea matatizo na nchi jirani kwa kiu chake cha madaraka
Mkuu unapigia gitaa mbuzi wa chadema hayo unayoshauri mazuri lakini chadema hii umepoteza muda kumejaa wanywa viroba
 
Wala hajakosea, Odinga nae anaungwa mkono na Magu.
 
Wakuu,
Hili suala silo la kushangiliwa wala kupongezwa... Ni suala la hatari kimahusiano kati ya nchi zetu mbili.

Lilipaswa kufanywa na wao wenywew bila kuingiliwa wala kusaidiwa na nguvu kutoka nje. Kitendo hiki kitazua hasira miongoni mwa wananchi wanaomuunga mkono Odinga na kama Uhuru atashinda basi kuna chuki itajengeka dhidi ya Lowassa na chama chake. Naye atalipwa hayahaya come 2020.

Ikumbukwe pia usalama miongoni mwa wananchi wa Kenya ni mdogo na ni watu wa "Liwalo na Liwee",lolote litakalo tokea juu ya uchaguzi huu litahusishwa na Watz.


Sioni Afya katika hili..... Isipokuwa bado litazidi kumharibia EL kama atagombea tena Uchaguzi ujao.
 
Kenyatta akichukua tena nchi sijui hizi nchi mbili zitakuwa na uhusiano wa namna gani maana naona Kenyatta kaamua kuonesha wazi kuwa yupo na mpinzani wa Magu
Mbona uhusiano wa Odinga na mkulu hujauona?
 
Lakini cdm wakiikosa network ndio sahihi. Maana tumelalamika sana juu ya kufadhiliwa na mabeberu.
Labda nikwambie kitu chadema kuunga mkono Kenyatta Wafadhili WA marekani hawatawaona tena. Urafiki wao na Raila ambaye ni binamu yake Obama ulimfanya Obama awashawishi wamarekani wawasaidie chadema kipindi cha slaa. Ndio maana chadema ilipata misaada mingi ya wazungu kwa ajili ya Obama. Sasa maadamu wamehamia kwa Kenyatta sio kesi wasubiri Kenyatta auze maziwa yake awachangie chadema. Chadema have lost a very important network. Na ieleweke kuwa chadema hakijawahi kaa mkutano mkkuu kupitisha azimio la kubadili sera za nje na kujadili hilo la chadema kuhama kutoka kumuunga mkono raila odinga na kuvunja urafiki naye na kuanzisha urafiki na Kenyatta na chama chake. Wanachama wa chadema wanaburuzwa na lowasa. Maamuzi hayo yalitakiwa yaamuliwe na mkutano mkuu wa chadema. Lowasa anaburuza wanachama ni dikiteta analotaka analazimisha liwe bila hata vikao na baraka za mkutano mkuu. Hilo la kumuunga mkono Kenyatta halina baraka za mkutano mkuu na vibaraka wake akina tundu lisu wanaojitia wanasheria nguli kwa hili wameufyata wakati liko wazi na ni uvunjifu wa katiba Ya chadema
 
itamgharimu vipi? Kwani Tanzania si Lowasa alishinda lakini CCM mkafanya uchakachuaji mkubwa huko kenya si kama Tanzania watu wapo makini uchakachuaji ni vigumu kupenya kama Tanzania
Another poor reasoning!
Eti CCM mkafanya uchakachuaji..
Si kila anayepinga baadhi ya hatua za Lowassa awe CCM
 
Sipendi kabisa haya mambo ya wanasiasa wetu kujiingiza kwenye siasa za nchi zingine hususan hizi za jirani.

Hata Magufuli naye aliwahi kushiriki kwenye kampeni za Odinga.

Disgraceful!!
 

Attachments

  • ODM 20.JPG
    ODM 20.JPG
    148.2 KB · Views: 39
Its long movie, ujue tupo high sana.
When you see such kind of move, think twice, there is a high possibilities Uhuru is in danger zone. My friend, don't just jump into conclusion, there is something wrong there with Kenyatta's chance of success, that is why he wanted political reinforcement at the final stage.
 
Sio mbaya kujifariji, anaumia sana kupigwa kumbo na Magu, so Uhuru akishinda basi atapata relief ya kupoteza bilions huku Tz labda!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cha msingi achunge kichwa chake siasa za Kenya zimejaa ukabila kule kudungua mtu au kuua wakati wa kampeni za uchaguzi ni kitu kidogo mno

si kweli, mbona hawakumdungua magufuli alipoenda kumpigia kampeni raila?
 
Back
Top Bottom