Edward Lowassa ashiriki kampeni za Uhuru Kenyatta

Edward Lowassa ashiriki kampeni za Uhuru Kenyatta

hii inaitwa nipe nikupe[emoji56][emoji56][emoji56][emoji56]
 
Tumekua tukiona Rais JPM akionyesha urafiki na ukaribu wa dhati kabisa na Mgombea urais wa upinzani Kenya ambaye ni Raila Odinga. Imeonekana wazi kuwa Rais JPM anampa sapoti kabisa Ndg Raila Odinga ili ashinde uchaguzi wa Kenya mwaka huu.

Vivyo hivyo tumemuona aliyekuwa Mgombea urais wachama cha upinzani Tanzania mwaka 2015 Edward Lowassa, akimsapoti kwa hali na mali Rais wa Kenya Uhuru Kenyata ili aweze kushinda uchaguzi kwa mara ya pili nchini Kenya.

Edward Lowassa ashiriki kampeni za Uhuru Kenyatta

Hii Imeonekana kama ni mchezo wa kukomoana baina ya wawili wa Kenya na wawili wa Tanzania.

Yaani Mpinzani mkuu Tanzania, anamsapoti mtawala wa Kenya na mpinzani mkuu Kenya, anapewa sapoti na mtawala wa Tanzania.. Is it a coincidence?

Binafsi mimi sipendelei kwa wanasiasa wa nchi yetu kuingilia chaguzi za wengine in order to get something in return. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, marais nao ni binadamu, huwa wanakasirika na huweza pia kulipa kisasi.

Sidhani kama JPM anafurahia Lowassa kumuunga mkono uhuru, na sidhani pia kuwa Uhuru anafurahia Odinga kusapotiwa na Tanzania.

Hivyo, kuna harufu flani ya kuja kulipizana visasi na kukomoana in the future baina ya nchi hizi mbili kisa tu fulani alimsapoti fulani.

Yaani uhusiano wa hawa watu wanne, maana yake chanya yenye manufaa kwa wananchi wa nchi hizi mbili ni yapi? Naona ni kila mtu anamsapoti mwenzake kwa ajili ya faida yake mwenyewe ya kuja kusapotiwa pia ili ashinde.

Inaleta picha mbaya kwa Rais wetu kumsapoti mpinzani wa Rais wa nchi jirani badala ya kuwa neutral kwa kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia bila kufungamana na upande wowote.

Pia inaleta picha mbaya kwa mpinzani mkuu wa nchi yetu kujihusisha moja kwa moja na kampeni za Rais wa nchi jirani. Hii itamletea uhasama na mpinzani wa nchi hiyo endapo mpinzani huyo akishinda.


Ngoja nipate asali na mdalasini narudi..

kwa kua sisi wa afrika ni watu wa visasi ,kauli yako bila kusimama upande wowote naunga mkono hoja,ikisha narudi kusema hivii-wanao jua ualisia na ukweli ni wakenya wenyewe unapo jitokeza kwa nguvu kumpa sapoti mtu ambae ametenda yalio kasirisha nyoyo za watu leo ukamsapot je watu wakufikiriaje kuusu kusto kua na maslai binafsi kwa kutete uovu ulio fanywa na mgombea-mwilika nyoka uanzia miguuni kwake, je yalio fanywa barani afrika maovu mbona hatuoni wanao pazaa sauti kwa kuwakemea !!!! tujue kukosoana na kukemeana ,kukanyanaa si kupongezana tuu hii ina maana mauvu aya tusumbui bali ulaji ndo jadi yetu----
 
Mkuu nijuavyo ni kweli kuwa mh rais wa Tanzania ana urafiki na Odinga, ila ungetukumbusha namna ambavyo magufuli kama rais wa Tanzania ameshiriki kampeni hizo moja kwa moja au hata kwa kificho kumuunga mkono rafiki yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Magu ni mwoga hajiamini anaijua siri ya idadi ya kura alizopata 2015 ndo màana anahaha kupata sapoti zaidi kutoka kwa jirani na EL nae alipoona rais mwenye kila kitu bado anatafuta sapoti kutoka nje nae akaona amsapoti atakaemfaa tena hili goma limekaa poa
 
Maghu ndiyo kaanza kwa kupiga ban bidhaa za Kenya ikiwa maziwa kutoka Kenya Ili kutengeneza mazingira ya uhuru kukosa pesa za kampeni na Kenya wamejibu kwa kupiga ban gas ya tz
 
Hebu tupe ushahidi wa jinsi gani Magufuli kamsupport Odinga katika uchaguzi huu.
 
Uhuroto watashindwa vibaya mno, wameingia chaka kumtumia mtu mwenye nuksi na siasa. Huyu mzee hana ushawishi wowote, anajulikana ni fisadi hata kila mkenya anajua hilo, sasa akina uhuruto nao ni mafisadi?
 
Uhuroto watashindwa vibaya mno, wameingia chaka kumtumia mtu mwenye nuksi na siasa. Huyu mzee hana ushawishi wowote, anajulikana ni fisadi hata kila mkenya anajua hilo, sasa akina uhuruto nao ni mafisadi?
Nakubaliana na wewe
 
Uhuroto watashindwa vibaya mno, wameingia chaka kumtumia mtu mwenye nuksi na siasa. Huyu mzee hana ushawishi wowote, anajulikana ni fisadi hata kila mkenya anajua hilo, sasa akina uhuruto nao ni mafisadi?

wewe umepanic baada ya kumuona Lowasa.
 
Back
Top Bottom