Edward Lowassa ashiriki kampeni za Uhuru Kenyatta

Edward Lowassa ashiriki kampeni za Uhuru Kenyatta

Moja ya kete wanayoitumia muungano wa NASA ni mgomo wa madaktari.
Kenyatta alipoomba madaktari kutoka tz, magufuli alikubali kumpatia. Lakini Mbowe alipinga na kuwashauri madaktari wasijaribu kuripoti kenya.

Mbowe alisema kama serikali ya Kenya imeshindwa kuwapa madaktari haki zao na imeshindwa kuwaajiri wakenya iweje ihitaji madaktari kutoka tz.

Leo CDM inamuunga mkono Kenyatta, wakati ule ilijaribu kuwashawishi madaktari wasikubali kuajiliwa Kenya.

Hii imekaaje?
 
Uchaguzi wa Kenya una taswira sawa Na uchaguzi utakao kuwa wa Tanzania mwaka 2020, Na kwa watu makini mtajaribu kuwaza yaliyoandikwa hapa,

Kwanza
Sababu KUU za kwanini Kenyatta ataendelea kuwa rais wa Kenya ,

1. Ni vigumu mno kwa nchi za Africa kwa rais kuongoza term Moja ya uongozi wakati ndo ana mamlaka yote Na kila kitu,

2. Tume ya uchaguzi Mara nyingi kwa Africa iko upande wa watawala, mtawala asiposhinda anashindishwa kwa lazima, hivyo hata LOWASA kuwa makini kajipange mwaka 2025 ugombee Na kina NCHEMBA,

3. Pamoja Na kwamba Kenya kuna changamoto ya rushwa, lakin Kenyatta kajitahidi sana kuleta maendeleo Na yanaonekana,

4. UPINZANI Mara nyingi ukishashindwa Mara ya kwanza watu hupoteza imani Nao, pili hata Ile desire ya mgombea kwenda ikulu Na kushawishika watu hupungua, maana agenda zake nyingi zinakuwa zimeshatekelezwa Na alomshinda ,pili wapiga kura hukata tamaa, hivyo raila odinga kamwe hatakuwa rais wa Kenya, ni kama ambavyo IPO hapa kwetu LOWASA ataishia kuwa rais wa mioyo ya watu,

Kila la heri JEMBE LA KENYA UHURU KENYATTA,

Tukutane tarehe 10.8.2017

By Samwel mathayo .
 
tume zao za uchaguzi zikoje?

wapinzani wao walitokea wapi?

mtoa maada yuko sahihi
Pili ajiulize kuwa ni mesema ni VIGUMU sijasema haiwezekan, pili hata mifano yenyewe ana miwili tu wakati chaguzi Africa zimefanyika zaid ya 50 Times
 
Well said brother., ila hata tukiweka ushabiki pembeni Kenyatta is the best candidate for Kenyans.
Huyu mwingine akishinda watajuta kama wale wengine wanaojuta kila kukicha
 
Well said brother., ila hata tukiweka ushabiki pembeni Kenyatta is the best candidate for Kenyans.
Huyu mwingine akishinda watajuta kama wale wengine wanaojuta kila kukicha
Maoni yako yanatokana na sababu zipi za kisayansi na kisiasa kwamba akishinda Raila wakenya watajuta? Au ni ramli tu kama sangoma?
 
Maoni yako yanatokana na sababu zipi za kisayansi na kisiasa kwamba akishinda Raila wakenya watajuta? Au ni ramli tu kama sangoma?
Hiyo siyo ramli ni kutokana na uwezo wangu mkubwa wa kupambanua mambo
 
Huyu mpinzani wa huku kaenda kule kwa KIKI ya kusema wamasai wanamuunga mkono kenyyat asa najiuliza kwa huyu wa huku wa madarakani sijui ataenda kwa odinga kwa KIKI gani?!

Au naye watasema wakatoliki wameamua kumuunga mkono
Nawaza tuu kwa sauti!!!
 
Hii ya Wamasai wa East Africa ni mdudu gani? Ni nchi in A katibu na sheria zake au ni ukabila tu? In Kenya it is more serious kwa vile sana matatizo ya ukabila tangiapo. Kuna Wajaluo nao wako huku na huku, je wakisema wanamuunga Raila itakuwaje? Mimi bombs Serkali itoe tamko kwamba Tanzania ahatuko hivyo; hatuendeshi mambo yetu kwaukabila. Lowassa kapewa na nani madaraka kuwasemea Watanzania watampigia nani, eti to aakwa misingi ya ukabila? Huku ni kuingilia mambo ya ndanu YA TANZANIA.
Kwani Lowasa alikuwa kwenye ardhi ya Tanzania. Wamasai Kenya wamemuunga Uhuru, yeye kama kiongozi wao mkuu kaenda kuongea. Kama wajaluo wa Kenya na Tanzania wana umoja na kiongozi wao yupo ruksa, sababu uchaguzibwa kenya always ni makabila kwahiyo hakuna kipya.
 
Huyu mpinzani wa huku kaenda kule kwa KIKI ya kusema wamasai wanamuunga mkono kenyyat asa najiuliza kwa huyu wa huku wa madarakani sijui ataenda kwa odinga kwa KIKI gani?!

Au naye watasema wakatoliki wameamua kumuunga mkono
Nawaza tuu kwa sauti!!!
Kwa huyu wa huku wa madarakani - hawezi kwenda kule kwa sababu huyu urafiki kwake huwa hauhusishi na madaraka aliyopewa. Ndiyo maana hata rafiki zake wengine amewatumbua kiurahisi.
 
Back
Top Bottom