jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,381
- 25,476
Nani amesema atapinga matokeo kama hatashinda? Uhuru? Please make sure hauamini hearsays.Sidhani kama katiba yao inaruhusu wasio Wakenya washiriki kwenye kampeni za chaguzi zao. Nilikuwa nataka Uhuru ashinde pamoja na mapungufu yake kama binadamu au kiongozi. Hili limeshampa Raila sababu za kupinga matokeo kama hatashinda na sababu chungu nzima za yaliyojiri kwenye hizi kampeni na yatakayojiri siku ya uchaguzi.
Nahisi damu kumwagika tena kwa wingi, na imeshaanza kumwagika. Chaguzi zetu nyingi za Africa ni lazima damu zimwagike. Hongera sana kwa Ghana.
Kwa upande mwingine, ni kweli kuna mambo tata yametokea during campaign, mojawapo kubwa ni mauwaji ya Christopher Chenge Musando. Definitely a dent on the current regime. Sijui nani atanufaika na kifo hicho, but wengi wanapeleka lawama kwa Kenyatta.
Pia hapo kwenye katiba yao kutoruhusu mtu asiye mkenya kushiriki kampeni, sina uhakika nalo.
Ila nilicho na uhakika nacho, ni kwamba jamii ya wamasai wa east Africa haina mipaka. Wamasai wa Kenya na Watz ni hao hao, hiyo mipaka iliwaathiri toka wakoloni walipoigawa Afrika, ila bado ni jamii moja. Ndo maana unaskia Lowassa aliposema kuhusu kutozuia wamasai kwenye mpaka wa Namanga.
Kiuhalisia, jamii ya wamasai haina mipaka east Africa. Pia imetokea kwamba Lowassa ndiye Laigwanan wa wa wamasai wa east Africa. Sijui alichaguliwa lini, lakini hata mimi leo ndo nimejuwa ni laigwanani wao.
Kwa jinsi ninavyowafahamu wamasai, wanamsikiliza sana kiongozi wao mkuu ambaye ndo Laigwanani. Atakachosema wanafuata bila shurti, ndivyo navyowafahamu wamasai.
Kwa jinsi ninavyowafahamu wakenya, huwezi kwenda sehemu kuomba kura bila kumtafuta kiongozi wa eneo hilo. Na mara zote kiongozi wa eneo husika hutokana na kabila lililopo eneo hilo.
Imetokea kuwa kiongozi wa kabila hilo la wamasai ambalo ni maarufu maeneo ya mipakani ni mtanzania.
Lakini pia Uhuru Kenyatta akitaka kuongea na hao wamasai, lazima atumie kiongozi wao, na kiongozi wao ndo Lowasssa. Sidhani kama "alitumia siasa tu", ndo maana hakuenda naye kwa wajaluo ama Wakisii kuomba kura.