jana 7/04/2016 wanazuoni wa ndani na nje yanchi wanaofanya utafiti kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi, utawala bora na ushindani wa kisiasa kwa kuzungumza na watu kutoka vyama mbalimbali na Viongozi wa Serikali wakiongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) walimtembelea nyumbani kwake Masaki jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu wa zamani aliyeshinikizwa kujiuzulu kwa kashfa ya RICHMOND na aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) baada ya kukatwa na CCM kutokana na taswira yake ya UADILIFU kwa Wananchi kuwa mbaya, EDWARD LOWASSA na kufanya naye mahojiano.
Katika Mahojiano hayo, LOWASSA aliyataja mambo matano yanayomfanya autilie shaka mustakabali wa Taifa chini ya Uongozi wa Rais wa Awamu ya Tano, Dr. John Pombe Magufuli. Ameyataja mambo hayo kuwa ni pamoja na Rais kugawa fedha wakati chombo cha kufanya hivyo kipo, watumishi kuachishwa kazi, upitishaji mizigo Bandari ya Dar es Salaam kushuka, nchi kunyimwa misaada, na ugumu wa maisha unaowakabili wanachi kwa sasa.
HAYA NI MANENO YA MFA MAJI. Mawazo kugawa pesa hayawezi kuisha kichwani mwa LOWASSA, alizoea kufanya hivyo ili kujipatia makundi ya kumuunga mkono kwenye harakati zake za klsiasa. ALIGAWA PESA sana kwenye taasisis za dini, baadhi ya watumishi wa Umma n,k. Anafikiri na Rais naye anafanya aliyoyafanya yeye. LOWASSA atambue kuwa fedha kwa ajili ya sherehe za Bunge, Uhuru, Muungano zipo kisheria, zilipitishwa na Bunge. Rais alichokifanya ni kubadilisha matumizi ya pesa hizo kutoka matumizi yasiyo na tija kwenda kwenye matumizi yenye tija. Lowassa anataka kutuambia hizo sherere ni muhimu kuliko vitanda mahospitalini na ujenzi wa barabara?
Lowassa hakuwahi kufanya biashara yoyote zaidi ya kuwa mtumishi ndani ya CCM na Serikalini. utajiri wake alionao na anaojivunia unatokana na UFISADI wake ndani ya chama na SERIKALI(KWA MANENO MENGINE , HAKUWA MWADILIFU KATIKA UTUMISHI WAKE). Ingeshangaza sana kuona anafurahia watumishi wazembe, Mafisadi na wala Rushwa kama alivyokuwa yeye wakiwajibishwa na Serikali yoyote ile acha hii ya JOHN POMBE MAGUFULI. Mafisadi wenzake watamuunga mkono kwa kauli yake kuhusu watumishi wabadhilifu kuchukuliwa hatua lakini Watanzania tulio wengi tunamuona kama anadhihirisha kuwa HAKIKA ALIKUWA FISADI.
Lipi bora? Upitisahaji mizigo Bandari ya Dar es Salaam kuongezeka mara dufu lakini tukakosa kodi au ukapungua mara dufu lakini kodi itokanayo na mizigo hiyo michache ikazidi ile mizigo mingi? Huku kote ni kutapatapa tu, ni kudhihirisha kuwa NI MUUMINI WA UFISADI.
Namna ya uzuiaji wa misaada uliofanywa na Marekani umejadiliwa sana. LOWASSA anataka kutudhihirishia yale yaliyosemwa na wengi sana kuwa YEYE ni KIBARAKA katika sakata hili.
Rais Magufuli Mungu akimuweka hai ataiongoza Tanzania kwa zaidi ya siku 1825. Ndiyo kwanza ameshaongoza siku 155 tu. maisha gani magumu wanayo wananchi kwa kipindi hicho cha siku 155 ukilinganisha na siku zilizotangulia? Hapana shaka thamani ya sarafu yetu imeimarika, kwa kipindi hicho, bei ya vyakula imeendelea kuwa pale pale na mahali pengine kushuka, Umeme na mafuta vimeshuka bei , n.k. LOWASSA anaishi wapi asiyaone haya?
KWA KASI YA MAGUFULI, MIAKA 5 NI MICHACHE SANA. LOWASSA NI LAZIMA AONGEE ANGALAU AONEKANE YUPO LA SIVYO ANAWEZA KUPOTEA GHAFLA ILA KWA KAULI ZAKE NI DHAHIRI NI MFA MAJI, ANATAPATAPA TU.