- Amlalamikia Rais Magufuli kugawa fedha kwa shughuli mbalimbali wakati chombo chenye mamlaka kugawa fedha kipo ambacho ni bunge.(Pesa za uhuru na Pesa za Muungano)
- Asikitishwa na uachishwaji wa kazi kwa wafanyakazi, asema hali ngumu ya uendeshaji wa mashirika hayo ndio usababisha utendaji hafifu.
- Asononeshwa na hali ngumu ya maisha mtaani.
- Asikitishwa na ushukaji wa huduma ya Bandari kushuka kwa asilimia 50 na kusababisha vijana wengi kusota mtaani.
- Kitendo cha wahisani kujitoa kuisaidia nchi asema n i pigo kubwa kwetu kwa mustakabali wa uchumi wa nchi.
- Asema si kweli kwamba uongozi wa Rais mstaafu Kikwete kila mtu alikuwa mla rushwa, ni kweli mfumo ule ulikuwa mbovu na wa kifisadi.
Bila kutetea, tukumbuke kitabu kimoja kitakatifu kuna mfano ambapo uponyaji ulifanywa siku rasmi ya kuabudu, pia, msamaria mmoja alimsaidia mtu bila kujali kwamba atakuwa najisi kwa kutokwa damu nyingi.
Hebu tufananishe, maamuzi ya haraka ambayo yanafaida, kwa mfanmo kupeleka vitanda vya kutosha hospitali ya taifa, kupunguza tatizo la vitanda kwa mama wazazi; na kuamua barabara sumbufu za muda mrefu kule Mwanza na pale Morocco-Mwenge zitengenezwe na kupunguza kama siyo kupunguza kero kwa wananchi; mtoa mfano kwenye kitabu kitakatifu aluliza, lipi muhimu, kuokoa maisha au kusubiri utaratibu ambapo maisha yanakuwa yamepotea.
Kero za hospitali, mabarabara, na utaratibu mbovu, mfano sheria dhaifu ya manunuzi, vimelalamikiwa kwa muda mwingi sana. Na mara nyingi, kufuata utaratibu, mfano, wa manunuzi ya vifaa tiba, kungechukua muda mrefu, tena na kuumiza wengi. Mheshimiwa anauwezo wa kutangaza hali ya dharura na akafanya maamuzi yenye maslahi mapana, tena kwa afueni na faraja kwa walio wengi. Kama ilivyo kawaida, walio wengi wanafurahia hatua zinazoendelea kuchukuliwa, wachache, ambao kwa namna fulani walifaidika na udhaifu wa taratibu, wanalalama kwani hawaamini kwamba mabadiliko yamefika.
Kwenye aina za leadership, kuna moja inaitwa contingency leadership, ambapo kiongozi anawezajitokeza, na kukidhi haja ya kimazingira ya uongozi. Mh ameibuka kipindi ambapo nchi inahitaji kwa udi na uvumba aina ya uongozi anaoendelea nao.
Waliohaki watulie na maendeleo sasa yanakuja. Kumbukeni, viongozi kipindi kilichopita waliwekeza katika kuaminisha taifa kwamba nchi hii ni masikini na hatuna namna ya kutoka, lakini mkuu amewaonesha kinyume chake. Ni matumaini makubwa yenye sababu za msingi kabisa. TUUNGANE KWA PAMOJA KWENDA MBELE, TUSIRUDI MISRI.