Ebu tujikumbumbushe, enzi hizo ulikuwa wapi?

Ebu tujikumbumbushe, enzi hizo ulikuwa wapi?

primary tulikuwa hatununi bali ni kusemelea live.....!!! yaan utasikia mbona fulan hachapwi...

hahaha kama ulikuwepo vile
Kuna siku walimind wakasema mwalimu huyu hajawai, kapewa namba Yu, mmoja akakazia kabisa tena nimekuja nae mimi huyu,
Bhas ticha ikabidi aniambie nitoke mbele anochape, nikagoma nkamwambia mwalimu me nimewahi bhana, muulize kiranja' weee kutaja neno kiranja ilikua kosa maana darasa Zima wakapayuka 'tena huyo kiranja ndo amempa namba kisa rafki yake' ticha akamuuliza kiranja eti huyu amewahi?
Kiranja: amewahi mwalimu, huyo si mchelewaji
Darasa: muongo mwalimu anamtetea

Bhas ticha ikabidi aniambie twende ofisini, njian nikampiga sound mpk akanielewa......."

Na hadithi yangu ikaishia hapo
 
Chemchem pr.school....licha ya kuwahi namba ole wako kiunga chako cha maua uwe hujamwagia.
 
Namchukia sana teacher wangu wa primary. Alinitesa sana na mikamilwa na mizizi ya michungwa, sintamsahau!! Da tunatoka mbali!!
 
Kumbukumbu p/s, si unajua mambo ya kuwahi namba. Njia ya kufika shule kutoka home lazima upite kiwanja cha biafra, watu walikuwa wanasema uwanjani kuna majini ile asubuhi asubuhi na kweli tukipita tunaona nazi zimevunjwa na lugha iliyoandikwa ni kiarabu na shillingi shillingi. Msela wangu mmoja alikuwa anaokota nazi anaila na shillingi anazichukua tunaenda kuzitumia kwenye mihogo na kachori.
 
Daaa hiyo ilikuwa inaboa sana....namba wanahesabu watu 30 kiranja anaandika 45 af anawagawia rafiki zake
teh...tet.. kama nakuona vile wewe haumo kati ya wanogawiwa hizo namba nikifikiria na umbali wa zaidi ya km 3 toka home
 
Butimba Mazoez Pr...tulikuwa tunawah namba saa 11 asubui..tunaweka mawe na mlinzi af tunapanda milimani kwenda kutafuta sungwi na upuru wa kuuza....tumeanza ujasilia kitambo..wacha tujiajili tu dah
 
Mwananyamala "B" Primary School. Enzi zangu kiatu chachacha, kyupi ni costi, kidumu cha maji kwa ajili ya kumwagia maua yakiwemo maua saa 6, chelewa mkononi. Unawahi namba saa 12 asubuhi na kukimbia mchaka mchaka huku tukiimba " CCM namba one, CCM namba one" kuzunguka shule na kuna wakati tulikuwa tunafika hadi hospitali ya Mwananyamala na Jiji na masoko ya Mwananyamala.
 
Jamani tunakumbuka mambo ya namba tu na uvaaji wa viatu,Vipi orodha ya kuzidisha table ya 1-12,hii kitu ilitutesa sana enzi hizo,unashukuru kama zamu yako itaangukia orodha ya 2,5 na 10.
 
Hahahaa yan acha tu ukifka shule saa moja na dak tano mboko zake ni balaA

Kumbe ndio wewe ulijikwaa kidole gumba, damu ikatoka na Mwalimu akakupa ruhusa urudi kwenu. Si unalikumbuka lile jiwe la pale Gentle hills Hotel sasa hivi !!!!! Kwa hiyo siku hizi huvai raba mbofu mbofu tena !!!!!! Karibu Gangilonga, japo uchangie rim moja ya karatasi.
 
Kumbe ndio wewe ulijikwaa kidole gumba, damu ikatoka na Mwalimu akakupa ruhusa urudi kwenu. Si unalikumbuka lile jiwe la pale Gentle hills Hotel sasa hivi !!!!! Kwa hiyo siku hizi huvai raba mbofu mbofu tena !!!!!! Karibu Gangilonga, japo uchangie rim moja ya karatasi.

Hahaaa jiwe gangi tulienda tukapanda juu mji wote wa iringa ukawa unaonekana....tulikua tunatoroka tunaenda kuiba mapera ya watu
 
Kwandele primary kuchoma mahindi ya shamba la shule kwenye dampo la kutupia taka na kujifanya kama tuaota moto endapo mwalimu atakatiza eneo hilo
 
teh...tet.. kama nakuona vile wewe haumo kati ya wanogawiwa hizo namba nikifikiria na umbali wa zaidi ya km 3 toka home

We acha tu mkuu na hiv sikuwa ma rafiki kiranja ndo bas tena
 
Mimi nakumbuka enzi hizo wanafunzi wengi walikuwa hawavai viatu...mm nikivalishwa viatu nyumbani nikifika shule navivua nakuwa kama wenzangu, pia kukimbia mchakamchaka na kupiga bendi ya shule, nakumbuka ngoma zilivyokuwa zinapigwa mfano ngoma ndogo utasikia ddrrrrrrrrrrrrrrrrrrriiiii! ngoma kubwa inaitikia duuu! yaani mpaka raha. Shule moja ilikuwa inaitwa nganyeni
 
Asee.....kuna zile askrimu za maziwa,kwa wale wa shule ya msingi Mlimani(UDASA) wapi mzee Mombasa!!!!Mambo ya chimbo beach kidimbwi na mabwawa saba......enzi za “KIIIIIDEEEEEAAA-kideee kideeee,kide-kideeee"haahhhhaaaaa.......swahili media bwana,huko ni swahili speaking tu!!!
 
Nakumbuka kuna siku tulikuwa tunashangilia drsn sasa ikawa ni kelele tukaambiwa kila mtu afuate kiboko mlimani tukalala line moja ananyanyuka wa kwanza anachapa wote akifika mwishoni na yeye analala tulijichapa viboko idadi yetu piga picha drs moja lilivyokuwa linabeba wanafunzi wengi
 
Kuna siku monitor alipokabidhi majina ya wapiga kelele akapewa fimbo na ticha atembeze kibano nne nne kila mmoja. Si akaanza kuremba kwa kupiga kishkaji sababu alijua watu watamshika koo baadaye. Ticha akashtukia kama monitor anaremba. Akamwambia lete nikuonyeshe inavyotakiwa. Monitor akaambiwa ashike vidole. Akapewa demonstration ya mboko moja kali. Monitor alizunguka kwa maumivu hakuamini macho yake:wacko: ukizingatia tulikuwa hatumuoni huyo ticha akichapa watu. Basi akakabidhiwa aendelee na zoezi. Alianza kuweka mboko utadhani anauwa nyoka. Hakuangalia usoni:cool2:. Ilikuwa ni vita.
 
Back
Top Bottom