East Afrika Hotel-Arusha

East Afrika Hotel-Arusha

Wakati ninaondoka mwaka jana(November) niliacha hotel hii ikiwa inatambulika kwa jina hilo EAST AFRICA HOTEL ila baada ya kurudi juzi Arusha nimeshangaa tena Hotel hiyo imebadilishwa jina na sasa inaitwa GOLD CREAST.

Sasa sijajua huu uchumi uligonga hodi kwenye hiyo hotel na kuuzwa ila yote ya yote tuachane nayo,nimependa sana ukuaji wa mji wa arusha hasa miundombinu nimekuta imeongezwa ikiwa ni sambamba na ujenzi wa barabara ya kutokea Moshi kuingia Arusha ila ikiwa bado ipo kwenye ujenzi (ila inakuja kuwa barabara atakayokuwa na viwango vya kipekee katika miji mikubwa hapa nchini.

Pili,nimeona ujenzi wa hotel mpya ya Hyatt Regency,Kijenge ni moja ya majengo yatakayoiweka Arusha kuonekana jiji la kipekee sana,pia kukamilika kwa jengo la PPF PLAZA kumefanya jiji lizidi kunoga kwa majengo mazuri.

Kiukweli mji huu kama utaendelezwa hivi naona kama unakuja kuupiku Mwanza tena kwa kasi ya ajabu ,kwa mawazo yangu (Mwanza kwa sasa inaizidi Arusha idadi ya watu ila miundombinu na majengo Arusha iko juu)

EAST AFRICA-GOLD CREAST
Tumejipanga mwaka huu tutaisoma.

Umesahau jengo refu kuliko zote Arusha---Jakaya Kikwete Ngorongoro Tower
 
Kwa majina yaani kubwa nadhani zaidi ni New Arusha Hotel hizo nyingine zilizobaki sio mbaya mt. Meru ndio ilikuwa the best
 
We jamaaa wa ajabu sana uwezi ukalinganisha Arusha kwa kutumia Mwanza bana tafuta miji mingine
mwanza kuna nn ww? Jiji lmepanuka sana ila mitaa imechoka mno!
Ziwa tu ndo linaiweka kwenye dira!
 
Mbona nilisikia ni 18....
15 juu na 3 za chini kama Parking
Jk ngorongoro tower...!
1480771449387.jpg
 
Back
Top Bottom