Sami Omary Khamis
Member
- Sep 8, 2020
- 67
- 133
Jopo la waangalizi 89 waliobobea kwenye masuala ya demokrasia kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) likiongozwa na Mhe. Silvestre Ntibantunganya limesema uchaguzi wa Tanzania umefuata utaratibu, hivyo watanzania wanatakiwa kuendelea kuimarisha amani iliyopo.
Wabobezi hao, wenye weledi na uzoefu wa hali ya juu wa kusimamia chaguzi mbalimbali ulimwenguni, wamesema mzunguko wote wa uchaguzi umeenda kwa njia huru iliyogubikwa na haki.
Wataalamu hao wamesema vyama vyote vimefanya kampeni kwa uhuru, wasimamizi wa uchaguzi wamelinda haki za wapiga kura, na wapiga kura wamepata haki yao bila kubughudhiwa.
Aidha, manguli hao wamevitaka vyama vya siasa kufuata Sheria iwapo havitaridhishwa, sio kuhamasisha uvunjifu wa amani.
Pamoja na hayo, waangalizi wamesema kwamba uchaguzi wa mwaka huu umekua na amani ya hali ya juu.
Chanzo: BBC
Wabobezi hao, wenye weledi na uzoefu wa hali ya juu wa kusimamia chaguzi mbalimbali ulimwenguni, wamesema mzunguko wote wa uchaguzi umeenda kwa njia huru iliyogubikwa na haki.
Wataalamu hao wamesema vyama vyote vimefanya kampeni kwa uhuru, wasimamizi wa uchaguzi wamelinda haki za wapiga kura, na wapiga kura wamepata haki yao bila kubughudhiwa.
Aidha, manguli hao wamevitaka vyama vya siasa kufuata Sheria iwapo havitaridhishwa, sio kuhamasisha uvunjifu wa amani.
Pamoja na hayo, waangalizi wamesema kwamba uchaguzi wa mwaka huu umekua na amani ya hali ya juu.
Chanzo: BBC