Dunia ingekuwaje bila wazungu?

Dunia ingekuwaje bila wazungu?

Civilization has a mixed blessing to human happiness. Maendeleo pia yanabeba hasara.
 
Pia michepuko isingekuwepo,kashfa kwa wanaume wa dar kucheza mechi moja ingekuwa ajabu kuisikia
YANGETOKEA YAFUATAYO
1.Jamiiforums isingekuwepo

2.Tusingekuwa na Bombardier

3.Laptop na Smartphone, visingekuwepo

4.Biashara ya kubeti isingekuwepo

5.Tungekuwa na dini pamoja na tamaduni zetu wenyewe.

6.Pale posta pangekuwepo na vichaka vya kuogofya na tusingekuwa na barabara za lami.

7.Tusingekuwa na TANESCO, TCRA, NEC, TBC, n.k

8.Pasingekuwepo na UKIMWI wala CONDOM.

9.Mapenzi yangetegemea hisia za dhati na sii pesa.

10.Nisingekuwa naisubiri game ya Liverpool na Manchester United 17 ya October.
 
Utakuwa umesoma history na hivi ndivyo mlivyokuwa mnadanganywa na Pan Africanists!! Nijibu swali moja: Industrial revolution iliyotokea Europe zaidi ya miaka 500 iliyopita, hadi hivi sasa Afrika hatujaifikia pamoja na kwamba tuna kwa kujifunza... NDIYO AU HAPANA? Kama HAPANA, fafanua!


Nimejaribu kumjibu mleta Mada alivyouliza kwamba bila ya Wazungu hii Dunia ingekuwaje, nikasema kwamba kila kilichopo ni maendelezo ya kile kilichokuwepo na kila jamii ya watu wana mchango wao, siyo kwamba Wazungu ndiyo walioanzisha kila kitu HAPANA hata nao walijifunza kutoka jamii nyingine ambazo wkt wao Wazungu wanaanza zilikuwa mbele zaidi yao!

Kwa mfano Wazungu wamejifunza mengi sana ktk kwa Wachina na wamechukuwa mengi tu, Wazungu wamejifunza mengi sna ktk Ustaarabu wa Kiislamu, wamejifunza na kuchukuwa mengi ktk kwenye Uislamu sasa huwezi kuongelea Ustaarabu wa Kiislamu bila kugusia Timbuktu, Mali ambayo ndiyo Maktaba Kuu ya kwanza Duniani na Dola ya Timbuktu imechangia kwa kiasi kikubwa sana kwenye maendeleo ya Binadamu rekodi zipo kila mahali!
Hata Persia pia Wazungu wamechukuwa na kujifunza mengi tu, hata kuanzia maendneleo ya Wanubi Sudani mpaka kwa Farao wa Misri kote huko ni bara la Afrika!

Hivyo hakuna Binadamu anayeweza kusema bila ya mimi msingekuwa hapa kwani maendeleo ni hatua na jamii/civilization hupanda na hushuka ...
 
bila elimu hakuna kitu, afisa ana degree natumikia taifa miaka 35 anapata milioni 120, mtoto wa mwana siasa anaingia bungeni na miaka 22 baada ya miaka 5 anapata milioni 245 bado marupurupu, mshahara mkubwa, mkopo milioni 90 analipa nusu tu, usitegemee ubunifu kutoka kwa wataalamu.
 
MUNGU HANA UPENDELEO HATA CHEMBE, SIKU NCHI ZETU ZIKIWA NA MFUMO BORA WA KUENDELEZA VIPAJI, NA KUTOA ELIMU BORA BASI AFRICA TUTAKUWA ZAIDI YA ULAYA. TUMEZIDI KUWA WABINAFSI SANA, KUANZIA KWENYE NGAZI ZA FAMILIA HADI UONGOZI WA NCHI.
Nani alileta/sababisha huo ubinafsi kwanini wao sio wabinafsi
 
Hivi wachina walishawahi gundua chochote au wanadandia technology za wazungu
 
Tafiti kuhusu dunia ya kale (ancient egypt) watu wa mwanzo kbs kustaarabika, mwanzo wa elimu, maandishi, sanaa ya hali ya juu, chuo kikuu cha kwanza duniani, maajabu ya dunia na mambo lukuki, "The history of the world"..................
 
Tafiti kuhusu dunia ya kale (ancient egypt) watu wa mwanzo kbs kustaarabika, mwanzo wa elimu, maandishi, sanaa ya hali ya juu, chuo kikuu cha kwanza duniani, maajabu ya dunia na mambo lukuki, "The history of the world"..................

Nonsense history, hakuna chuo kikuu in the modern sense of a university kilikuwepo that time. Labda vyuo vya jando na unyago
 
Nonsense history, hakuna chuo kikuu in the modern sense of a university kilikuwepo that time. Labda vyuo vya jando na unyago
Mkuu Retired, hesabu walianzisha Waarabu, Wagiriki walileta demokrasia, Roman empire ndiyo iliwafundisha wazungu ustaarabu, tuliwafundisha wazungu kufua chuma.
 
Wakuu hili swali huwa najiuliza sana, kwamba hii dunia ingekuwaje bila hawa watu. Mambo mengi katika hii dunia wao ndo wagunduzi kuanzia mambo ya teknolojia, kieletroniki, sayansi na mengine mengi wakati Africa hakuna kitu cha maana chochote tulichofanya wakati white people ndo walioifikisha dunia hapa ilipo.

Hivi bila hawa jamaa ingekuwaje?
Tungekuwa tunafua chuma tu kutengeneza mishale.
 
Back
Top Bottom