Tungekuwa mbali sana kimaendeleo, wanasayansi wetu wa zamani walidumazwa na wakoloni na wanasayansi wetu wa sasa wanadumazwa na sayansi za wazungu. Sayansi na tamaduni zetu ziliitwa za kishenzi . walikamatwa na na kufungwa jela watu wetu waliotengeneza bunduki, simu, ndege, redio, tomato sauce, mafuta ya break kwenye karakana zao badala ya kuwaendeleza na kuwaelekeza mapungufu yao kwenye bidhaa wanazozizalisha ili ziwe bora. Serikali zetu nazo zinaiga dhambi ileile iliyofanywa na wakoloni kwa kuzisigina tamaduni na bidhaa zinazozalishwa na wazawa.