buzitata
JF-Expert Member
- Apr 11, 2017
- 2,281
- 7,735
Habarini wakuu
Leo nimeona nikumbuke matukio niliyoyashuhudia ambayo yananiweka mdomo wazi na sijui nilikuwa nawaza nini(nitabase zaid upande wa kiroho)
Kwanza kabisa mimi ni aina ile ya watu ambao tunataka kujua kila kitu hata kama ni vya hatari ila nitajilazimisha nijue tu.
MImi ni mkatoriki ila sikua nyuma sana kuna kipindi niliamua kulivalia njuga swala la dini na kuchimba kidogo juu ya imani kwa ujumla na kupata mwanga fulani kuhusu imani niliyopo hasa swala la kuitwa wakatorik tunaabudu sanamu, ukweli ni kwamba hatuabudu sanamu ila kuna gap dogo sana ukiteleza kidogo utaangukia kwenye kuabudu sanamu
Maisha yakaenda mm kama binadamu nilipitia mapito fulani kimaisha nikayumba kiuchumi..nilijaribu kutatua changamoto zangu mwisho wa siku nikaangukia kwenye mambo ya waganga..uganga kweli upo na somehow unafanya kazi na matokeo yanaonekana japo fix zipo nyingi sana (kila mganga atakuambia hii dawa ninayokupa mtu akikugusa tu anakwenda na maji)
Nafsi yangu ilikuwa inagoma sana kuamini mambo ya kiganga na uchawi ila ndo hivyo tena maji yalikua yanaifika shingoni nikawa najikuta tu naenda kupata msaada
SIku moja nilikaa nikajiuliza kwanini naenda kwa mganga na huko kwa mganga natajiwa jina la mungu, nikaona ngoja niuchimbe kwanza huo uganga na uchawi unafanyaje kazi na kwanini upo
Nilifanikiwa kusoma vitabu vinne vya uchawi na uganga (jina kapuni kwasababu ni vya hatari kidogo)
Ndani yake nilifunguka kiakili sana nikaja kugundua uganga ama uchawi kwanza kabisa unaanza na wewe kuwa na imani ya hicho unachokifanya
Pili ni lazima kuwe na roho ambayo inakupa muongozo wa nini cha kufanya ili kufanikisha jambo lako
mtu ili kuwa mchawi kwa level wa chini kabisa inaweza kumchukua wiki tatu mpaka miezi 18 mpaka kuweza kufanya mambo ambayo yapo kinyume na mungu japo hivyo vitabu vinaita hiyo ni elimu safi na tuitumie kwa wema
TAtu. Uchawi ama uganga ni lazima uende kinyume na muumba hata kama majina yanayotamkwa ni ya muumba ila pale yanatamkwa kama dhihaka tu na hilo ndio lengo kuu ili uchawi uweze kufanya kazi
Uchawi unahusisha zaidi matumizi ya alama hasa nyota,duara na pembe, ukimaliziwa na maneno maalumu ili kuipa nguvu pamoja na imani ya kwamba unachokitamka kinakwenda kutokea
Matumizi ya vitu kama chumvi, hirizi,talasin ni mabaya sana kwasababu yanakufa uhisi nguvu inatoka kwenye hivyo vitu na sio muumba(mnaoshauriana kutumia chumvi ili kujikinga ama kusafisha nyota naomba mnisamehe bure)
NIliyoyashuhudia kwenye hiyo elimu ni makubwa sana na yalinifanya niujue ulimwengu na kujikita zaidi kwa muumba wangu na kuachana kabisa na hizo imani
Nguvu za giza zipo ila zile ni njia za mkato tu ambazo zinampumbaza mwanadamu na kumpeleka shimoni, ukiingia huko lazma upotee tu iwe kwa kujua ama kutokujua
Dunia ina mengi sana na mimi sio mwandishi mzuri wa magazeti hivyo naishia hapa kukiwa na swali lolote nitajitahidi kulijibu ama nikishindwa nitasaidiwa na mliopo humu
Leo nimeona nikumbuke matukio niliyoyashuhudia ambayo yananiweka mdomo wazi na sijui nilikuwa nawaza nini(nitabase zaid upande wa kiroho)
Kwanza kabisa mimi ni aina ile ya watu ambao tunataka kujua kila kitu hata kama ni vya hatari ila nitajilazimisha nijue tu.
MImi ni mkatoriki ila sikua nyuma sana kuna kipindi niliamua kulivalia njuga swala la dini na kuchimba kidogo juu ya imani kwa ujumla na kupata mwanga fulani kuhusu imani niliyopo hasa swala la kuitwa wakatorik tunaabudu sanamu, ukweli ni kwamba hatuabudu sanamu ila kuna gap dogo sana ukiteleza kidogo utaangukia kwenye kuabudu sanamu
Maisha yakaenda mm kama binadamu nilipitia mapito fulani kimaisha nikayumba kiuchumi..nilijaribu kutatua changamoto zangu mwisho wa siku nikaangukia kwenye mambo ya waganga..uganga kweli upo na somehow unafanya kazi na matokeo yanaonekana japo fix zipo nyingi sana (kila mganga atakuambia hii dawa ninayokupa mtu akikugusa tu anakwenda na maji)
Nafsi yangu ilikuwa inagoma sana kuamini mambo ya kiganga na uchawi ila ndo hivyo tena maji yalikua yanaifika shingoni nikawa najikuta tu naenda kupata msaada
SIku moja nilikaa nikajiuliza kwanini naenda kwa mganga na huko kwa mganga natajiwa jina la mungu, nikaona ngoja niuchimbe kwanza huo uganga na uchawi unafanyaje kazi na kwanini upo
Nilifanikiwa kusoma vitabu vinne vya uchawi na uganga (jina kapuni kwasababu ni vya hatari kidogo)
Ndani yake nilifunguka kiakili sana nikaja kugundua uganga ama uchawi kwanza kabisa unaanza na wewe kuwa na imani ya hicho unachokifanya
Pili ni lazima kuwe na roho ambayo inakupa muongozo wa nini cha kufanya ili kufanikisha jambo lako
mtu ili kuwa mchawi kwa level wa chini kabisa inaweza kumchukua wiki tatu mpaka miezi 18 mpaka kuweza kufanya mambo ambayo yapo kinyume na mungu japo hivyo vitabu vinaita hiyo ni elimu safi na tuitumie kwa wema
TAtu. Uchawi ama uganga ni lazima uende kinyume na muumba hata kama majina yanayotamkwa ni ya muumba ila pale yanatamkwa kama dhihaka tu na hilo ndio lengo kuu ili uchawi uweze kufanya kazi
Uchawi unahusisha zaidi matumizi ya alama hasa nyota,duara na pembe, ukimaliziwa na maneno maalumu ili kuipa nguvu pamoja na imani ya kwamba unachokitamka kinakwenda kutokea
Matumizi ya vitu kama chumvi, hirizi,talasin ni mabaya sana kwasababu yanakufa uhisi nguvu inatoka kwenye hivyo vitu na sio muumba(mnaoshauriana kutumia chumvi ili kujikinga ama kusafisha nyota naomba mnisamehe bure)
NIliyoyashuhudia kwenye hiyo elimu ni makubwa sana na yalinifanya niujue ulimwengu na kujikita zaidi kwa muumba wangu na kuachana kabisa na hizo imani
Nguvu za giza zipo ila zile ni njia za mkato tu ambazo zinampumbaza mwanadamu na kumpeleka shimoni, ukiingia huko lazma upotee tu iwe kwa kujua ama kutokujua
Dunia ina mengi sana na mimi sio mwandishi mzuri wa magazeti hivyo naishia hapa kukiwa na swali lolote nitajitahidi kulijibu ama nikishindwa nitasaidiwa na mliopo humu