ElPuto Jefe
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 5,286
- 19,463
Naona umeachiwa, karibu tena...
HahahahahaGodwin fanya hivo kwa JIWE basi atoke pale 'nyumba nyeupe' maana tunapata taabu sana..





ERIC SHIGONGO
DUNIA HAINA USAWA
Waandishi wa habari walipewa taarifa kuhusu Bilionea Olotu aliyekuwa njiani kutoka Mombasa kuelekea Nairobi. Waandishi hao kutoka katika mitandao ya kijamii, magazeti, redio na televisheni wakakusanyika kituoni hapo kwa ajili ya kuchukua habari na kupiga picha kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.
Kila mtu alitaka kuwa na picha ya bilionea huyo aliyekuwa gumzo kubwa nchini Kenya, kila mtu alitaka kuona kile ambacho kingetokea kwamba ilikuwaje mpaka bilionea huyo apange mipango ya kuweza kuiteka ndege ya rais kwa lengo la kwenda kuiuza? Kila mmoja alikuwa akijiuliza maswali mengi ambayo walikosa majibu kabisa.
Ilipofika majira ya saa tisa alasiri, gari la polisi kutoka Mombasa likaanza kuingia katika Kituo Kikuu cha Polisi. Waandishi wa habari ambao waliambiwa wasimame mbali kabisa wakaanza kupiga picha kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.
Bilionea Olotu akateremka huku akiwa na pingu mikononi mwake, alitia huruma, alionekana kuwa mnyonge sana kiasi kwamba kila mtu akaamini kwamba kweli mwanaume huyo alikuwa amefanya kile kitu kilichokuwa kimetangazwa sana katika mitandao ya kijamii.
Akaingizwa ndani, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kutaka kuonana na wakili wake, alijua kwamba alikuwa na kesi nzito iliyokuwa ikimkabili ambayo kwa namna moja au nyingine asingeweza kuchomoka salama, alihitaji kuzungumza na wakili huyo kwa lengo la kumwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea na kwamba ujumbe uliokuwa ukionekana katika simu yake, haukuwa wake na hakuwahi kuandika ujumbe wa namna ile.
“Sikuwahi kufanya kitu kama hiki,” alisema Olotu wakati wakili wake alipofika mbele yake. Alizungumza naye huku akilia, hakuamini kama mwisho wa siku ungekuwa namna hiyo, mipango yote ambayo ilielezewa katika simu yake haikuwa sawa kabisa.
“Lakini wanasema kwamba meseji zilionekana kwenye simu yako, ni kweli?’ aliuliza wakili, alitaka kujua ni kwa namna gani angeweza kumalizana naye katika kesi ile.
“Ni kweli?”
“Sasa inakuwaje unaposema kwamba si meseji zako?”
“Hata mimi nashangaa, sikuwahi kuandika meseji za namna hiyo! Inakuwaje sasa mpaka zipatikane katika simu yangu?” alihoji huku akionekana kuchanganyikiwa.
Wakili mwenye alishangaa alipoambiwa kwamba hizo meseji zilikutwa katika simu ya mteja wake. Hakuamini kama kungekuwa na mtu ambaye angetuma meseji za namna hiyo na kuziacha katika simu yake. Akahisi kwamba kulikuwa na kitu nyuma ya pazia na jambo kubwa kabisa alilokuwa amelifikiria ni kwamba inawezekana mwanaume huyo alimuachia mtu mwingine simu yake ambaye aliitumia kutuma meseji hizo.
“Sikumwachia mtu!”
“Sasa inakuwaje meseji hizo kukamatwa katika simu yako?” aliuliza wakili.
“Hata mimi nashangaa!”
Wakati hayo yote yakiendelea Rais Onyango alikuwa ikulu, alipewa taarifa kwamba bilionea yule alikuwa mikononi mwa polisi, moyo wake ukaingiwa na hasira, hakuamini kama kweli kungekuwa na mtu ambaye angejitolea kumsaidia kwa asilimia mia moja na mwisho wa siku kutaka kumgeuka kama alivyokuwa amefanya.
Akataka kumpoteza, akataka kummaliza kwa kila kitu alichokuwa nacho. Akawaambia polisi kwamba ilikuwa ni lazima mwanaume huyo afungwe gerezani kwa kile alichokuwa amekifanya, maelekezo yakatolea na siku iliyofuata kufikishwa mahakamani kusikiliza kesi yake.
Hakukuwa na kesi ambayo ilifautilia sana nchini Kenya kama ilivyokuwa kwa kesi hiyo. Kila mtu alitaka kufahamu kwa kile kilichokuwa kikiendelea. Wengi walilaani, wanasiasa walimwandama Olotu kwamba hakuwa ametenda haki kwa kuwa alihitaji msaada, akasaidiwa lakini kumbe nyuma ya pazia kulikuwa na jambo lake alilotaka kulifanya.
Kesi hiyo iliunguruma kwa wiki kadhaa na hatimaye akaonekana kuwa na kesi ya kujibu na hivyo kuhukumiwa miaka kumi na tano gerezani. Hapo, Wakenya wakaridhika, ni ghafla sana wakatokea kumchukia mwanaume huyo kwa kuwa alitaka kuwaingiza katika uhasama mkubwa na Watanzania ambao walionekana kama ndiyo waliokuwa wameiteka ndege hiyo na kuipoteza.
Japokuwa Olotu alihukumiwa lakini ndege haikuonekana. Wakenya walijaribu kuitafuta kila siku lakini hakukuwa na mafanikio yoyote yale, hawakujua kama ndege ilisafirishwa nchini Japan, ikauzwa huko na fedha kwenda kuingizwa katika akaunti ya Godwin ambayo hata watu wa benki wenyewe hawakujua akaunti hiyo ilikuwa na kiasi gani kwani ilionekana kama imefungwa na wakati kila siku kulikuwa na fedha zilizokuwa zikiingia na kutoka.
***
Ojuku aliamua kuwaita waandishi wa habari kwa lengo la kuzungumza nao, aliwaambia kwamba hatimaye Bokasa alikuwa amepatikana na hivyo ilikuwa ni lazima kushitakiwa kwa kila kitu alichokuwa amekifanya. Hakukuwa na mawakili wenye nguvu wa kumtetea kwani kila mmoja alikuwa akimchukia.
Aliua wanajeshi kadhaa kwa kuwapulizia sumu ikulu, hilo lilimfanya kuchukiwa na kila mtu kutamani kuona mwanaume huyo akihukumiwa kifo huko gerezani.
“Bora akahukumiwe kifo,” alisikika mwanaume mmoja akiwaambia wenzake.
“Kweli kabisa! Yule hafai! Yaani ni bora aondoke katika dunia hii,” alisema jamaa mwingine huku akimwangalia mwenzake.
Kesi hiyo iliunguruma kila siku na baada ya miezi miwili, akahukumiwa kufungwa kifungo cha maisha baada ya kupona ugonjwa aliokuwa akiumwa. Familia yake ambayo aliipanga kutoroka, ikakamatwa na kurudishwa nchini Tanzania, hawakutakiwa kuondoka, walitakiwa kuendelea kubaki nchini kwani bado walihisiwa kupanga njama mbaya za kuweza kufanya matukio ya kutisha Tanzania.
“Naomba nisamehewe kwa kila kitu kilichotokea,” alisema Bokasa huku akilengwa na machozi.
Waandishi wa habari wakamsogelea, japokuwa haikuwa ruhusa kwa mtu aliyehukumiwa kuzungumza na waandishi wa habari lakini yeye akapewa nafasi hiyo ya dakika tano kwa kuzungumza mara ya mwisho na Watanzania, kuwaomba msamaha kwa kila kitu alichokuwa amekifanya.
Alizungumza huku akilia, alijuta katika maisha yake kufanya mambo machafu, alijiona kuwa mjanja, mwerevu lakini mwisho wa siku akagundua kwamba alikuwa mjinga ambaye alitaka kuwaangamiza zaidi Watanzania.
Kila mtu aliyesikia jinsi alivyokuwa akiongea, alimuonea huruma, alisinyaa, hakuonekana kama alikuwa rais aliyepita nchini humo, alionekana kuwa dhoofu kiasi kwamba watu wengine walihisi kuwa kama angefika gerezani basi angeweza kufa kutokana na mawazo aliyokuwa nayo.
Alichukua dakika nne kuzungumza na waandishi wa habari, akachukuliwa na kisha kupelekwa gerezani huku akiwapungia mikono watu waliokuwa mahakamani hapo.
“Godwin! Umefanya kazi kubwa sana! Hebu tuonane kwanza tusherehekee,” alisema Ojuku wakati akizungumza na Godwin kwenye simu.
“Haina shida. Nafikiri nimemaliza kila kitu!” alisema Godwin.
“Ndiyo! Hebu kwanza tukutane kwanza tusherehekee, bila wewe basi Tanzania ingepotea,” alisema Ojuku.
Hilo halikuwa tatizo, baada ya saa kadhaa wawili hao wakakutana katika Mgahawa wa Manjumat uliokuwa Masaki. Ojuku alipomwangalia Godwin, hakuamini, alikuwa kijana mdogo mno, sawa na mtoto wake lakini kwa kitu alichokifanya kwa ajili ya Tanzania, yeye mwenyewe alishangaa.
Hata kabla ya kuzungumza kitu, akasimama na kumkumbatia kijana huyo, akamshukuru kwa kazi kubwa aliyokuwa ameifanya ambayo mwisho wa siku iliifanya nchi ya Tanzania kuwa huru kama ilivyokuwa kipindi hicho.
“Na wale marubani mmewafanya nini?” aliuliza Godwin.
“Tuliwarudisha kwao hukuu tukiwapa mikwara mizito kwamba kama kuna siku wangesema ukweli, basi tutawaua,” alisema Ojuku.
“Na wale vijana?”
“Tumewamaliza na kuwatupa baharini huku miili yao ikiwa imefungwa kwa vyumba vizito vya matairi ya gari kwani hatukutaka maiti zao zionekane, acha zikawe chakula cha samaki,” alisema Ojuku huku akimwangalia mwanaume huyo.
“Safi sana!”
“Wewe ni mtoto wa Bwana Mapoto?” aliuliza Ojuku.
“Ndiyo!”
“Aisee! Pole sana kwa kila kitu kilichotokea, hakika umepitia maisha ya shida sana mpaka muda huu kuwa hapa. Ila kwa ulichokifanya, hakika ni kisasi ambacho hakitoweza kusahaulika katika maisha yote ya watu waliowahi kukuumiza!” alisema Ojuku huku akimwangalia Godwin.
“Nashukuru sana!”
Walikaa hapo na kuzungumza kwa kipindi kirefu, watu wengine waliokuwa pembeni walishindwa kugundua kwamba mtu aliyekuwa akizungumza na Jenerali Ojuku alikuwa Godwin ambaye kila siku walitamani kumfahamu. Baada ya dakika arobaini, Godwin akasimama, akamuaga na kumwambia kwamba siku chache mbeleni angemualika kwa ajili ya kuhudhuria harusi ambayo angekwenda kufunga na msichana Winfrida.
“Kweli?” aliuliza.
“Hakika! Karibu sana!”
Godwin akatoka nje, akalifuata gari alilokuwa amekuja nalo lakini hata kabla hajaufikia mlango na kuufungua, akasikia akianza kuitwa kwa sauti kubwa kutoka nyuma yake. Hakujua mtu aliyekuwa akimuita lakini kwa jinsi alivyokuwa akiisikia sauti hiyo, ilionyesha kwamba ni ya mtu aliyekuwa akimfahamu kabisa.
“Godwin! Godwin!” aliendelea kuita mtu huyo.
Watu wote waliokuwa mahali hapo wakageuka na kumwangalia mtu aliyekuwa akimuita Godwin. Hapohapo akasimama na kuyapeleka macho yake kwa mtu aliyekuwa akimuita, alipomwangalia tu, hakuwa mgeni, alimfahamu mtu huyo, uso wake ukajawa na tabasamu, mtu yule akamsogelea.
“Godwin! Ni wewe kweli? Mungu wangu! Za masiku? Mbona ulipotea? Ni wewe kweli au naota?” aliuliza mtu huyo huku akihema kwa nguvu, Godwin akabaki akishangaa tu japokuwa alimfahamu vilivyo mtu huyo.
***
Godwin alibaki akimwangalia mwanamke aliyesimama mbele yake, sura yake haikuwa ngeni machoni mwake, alikumbuka kwamba aliwahi kumuona sehemu fulani japokuwa hakukumbuka ilikuwa wapi.
Alimkazia macho, mwanamke yule alikuwa akimwangalia huku akionekana kuwa na furaha mno. Wakati akizungumza naye, mwanaume mmoja naye akatokea na kumsabahi Godwin ambaye bado alionekana kushangaa tu.
“Unanikumbuka?” aliuliza mwanamke huyo huku tabasamu likiwa usoni mwake.
“Sura inakuja na kupotea,” alijibu Godwin.
Akamkumbusha jina lake kwamba aliitwa Rachel. Alivyolitaja jina hilo tu, Godwin akakumbuka kila kitu kwamba mwanamke huyo alikuwa yule wa Coco ambaye alimpenda, alimthamini na kumpa kila kitu alichokihitaji lakini mwisho wa kumuona ilikuwa ni katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
“Kumbe ni wewe!” alisema Godwin na kumkumbatia.
Alipomwangalia mwanaume yule aliyesimama karibu na Bi Rachel alimkumbuka, alikuwa mumewe, mwanaume ambaye alimtetea alipokwenda kumtembelea Bi Rachel katika hospitali hiyo.
Akamsalimia na kumshukuru kwamba kama si yeye basi polisi kipindi kile wasingeweza kulifuatilia gari lililokuwa limemteka na kutoweka katika mazingira ya hospitali.
“Ulikuwa wapi?” aliuliza Bi Rachel huku akionekana kuwa na furaha, japokuwa alikuwa na umri mkubwa zaidi ya kipindi cha nyuma lakini bado moyo wake haukumwambia kitu kwa Godwin.
“Niliondoka! Nashukuru sana kwa msaada wako, nashukuru kwa kila kitu,” alisema Godwin huku akiachia tabasamu pana.
Hawakuzungumza sana, akaondoka huku akiendelea kushangaa kwamba mwanamke huyo alimgunduaje na wakati kilipita kipindi kirefu pasipo kuonana.
Hakutaka kujali sana, akaondoka na kurudi nyumbani. Alipofika huko, akamwambia Winfrida kila kitu kilichotokea, kwamba alikutana na mwanamke yule ambaye alimsaidia sana kipindi cha nyuma ila mbali na hilo, akamsisitizia kwamba ni lazima waoane baada ya rais mpya kuapishwa.
Je, nini kitaendelea?
Asante MeyyadahShukrani nyingi ziwe kwako
KaribuRaha sana
Asante MoneytalkSantee jackal
Jackal santee
Karibu iron2012Ahsante sana Jackal naona mambo yanaelekea ukingoni kweli dunia haina usawa