Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

DUNIA HAINA USAWA

Godwin alikuwa akiendelea kusoma kama kawaida, kichwa chake kilikuwa na mawazo mengi, alikuwa akifikiria namna ambavyo angeweza kuwawekea chuki kubwa wananchi juu ya viongozi wao waliokuwa wakiwaibia fedha wananchi wao na hata kuwakandamiza masikini.
Hakuacha kudukua mawasiliano yao, kila wakati alikuwa akicheza na kompyuta yake, alijua fika kwamba watu hao walikuwa wakiwasiliana, katika kila meseji walizokuwa wakitumiana wabunge wote nchini Tanzania, alizipata kwani alikuwa ameingiakatika namba zao bila kujua.
Ukiachana na hao, pia kulikuwa na watu wa usalama wa taifa ambao aliamini kwamba kama angefanikiwa kuwa na mawasiliano yao na kufuatilia kila kitu basi angefanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Bado aliendelea kukusanya namba za watu mbalimbali, wale waliokuwa na sauti nchini Tanzania. Alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana na ndiyo maana hata kikao kidogo cha watu sita ambacho kiliitishwa ikulu, naye alipata taarifa kwani kila walipopigiana au kutumiana meseji, alikuwa akipata taarifa hizo.
Alishangaa kuona watu hao walikusanyika kwa kuwa walitakiwa kuandika majina ya watu hamsini. Hakujua katika karatasi hizo waliandikwa wakina nani lakini baada ya mkurugenzi wa usalama wa taifa kupigiwa simu na kuambiwa kwamba walitakiwa kufanya mauaji ya watu waliokuwa nao mule ndani, tena kwa kuwataja majina ndiyo akagundua kwamba tatizo kubwa ni kwa sababu aliweka kila kitu kilichozungumziwa katika kikao kile hasa baada ya kudukua mawasiliano ya simu yaliyofanyika baada ya kikao.
Alijua kwamba kulikuwa na mtu mmoja miongoni mwa watu waliokuwa katika kikao kile alikuwa akienda kuuawa, hakujua ni nani na hivyo macho na masikio yake yalikuwa kwenye simu yake ambayo muda wote kazi kubwa ilikuwa ni kudukua mawasiliano ya viongozi hao.
Hapo ndipo akagundua kwamba mtu aliyekuwa akitakiwa kuuawa alikuwa Mzee Filipo, hakuamini macho yake kwani miongoni mwa watu waliokuwa wakiheshimika katika chama tawala alikuwa mtu huyo.
Hakutaka kuzungumza kitu, alitaka kuona kama mauaji hayo yangefanyika au la. Kile alichokuwa akikitegemea ndicho kilichofanyika kwani mzee huyo alikufa katika ajali ambayo mara baada ya kuifuatilia, akapata maswali kadhaa ambayo aliyaandika kwenye akaunti yake Instagram.
Alishangaa, hakuamini kwamba yeye ndiye alikuwa sababu kubwa iliyomfanya mzee huyo kuuawa, hakutaka kuona mauaji yakiendelea, alichokifanya ni kuposti kuhusu mauaji hayo, Watanzania wajue kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Wakati yeye akitafakari hayo yote upande wa pili Kimwinyi alionekana kuchanganyikiwa, pombe zote alizokuwa amekunywa ziliyeyuka kichwani mwake, ulevi wote ukamuondoka, akaegemea usukani na kuanza kuyafikiria maisha yake.
Alishirikiana na rais kwa kila kitu, walicheza michezo mingi ya mauaji lakini kipindi hicho mambo yalionekana kuwabadilikia, walidili na mtu ambaye hawakujua alikuwa wapi ingawa aliamini kwamba alikuwa na nguvu kubwa.
Mara baada ya kujifikiria kwa muda huku akiwa ndani ya gari, akampigia simu Rais Bokasa na kumwambia kilichokuwa kikiendelea, kwamba alipigiwa simu na mtu asiyemfahamu na kumwambia kwamba alikuwa akijua mchezo mzima na lazima afanye juu chini kuhakikisha majina yao anayaweka katika akaunti ile.
Hilo ndilo lililomchanganya zaidi, pamoja na uovu wake mkubwa lakini hakutaka kugundulika na mtu yeyote yule, kila siku alijifanya mtu mwema, aliwasaidia watu, kitendo cha mtu huyo kusema kwamba angeweka kila kitu hadharani kilimchanganya mno.
“Kwa hiyo tufanye nini Kimwinyi?” aliuliza rais.
“Sijajua! Hii hali inanichanganya sana. Nani anamwambia huyu mtu mambo haya?” aliuliza Kimwinyi.
“Hilo ndilo la msingi kujiuliza. Ila aliponipigia simu, kulikuwa na namba aliyotumia, nadhani tukiitumia hii, tutafanikiwa kumpata,” alisema mwanaume huyo.
“Unayo?”
“Ndiyo!”
“Hebu tuanze kuifuatilia.”
Hilo ndilo lililofanyika, siku iliyofuata Kimwinyi akaondoka kwenda makao makuu ya Mtandao wa Simu wa Tritel ambapo baada ya kufika huko akawapa namba ile iliyotumika kumpigia huku dhumuni lake likiwa ni kujua mahali namba hiyo ilipokuwa mara ya mwisho ilipokuwa ikitumika.
“Hii ndiyo namba yenyewe?” aliuliza dada aliyekaa kwenye meza iliyokuwa na kompyuta.
“Ndiyo!”
Akaanza kuifanyia kazi, akaiangalia kwenye kompyuta yake, muda wote alikuwa kimya, aliikodolea macho kompyuta yake huku Kimwinyi akiwa mbele yake akimwangalia tu.
Msichana yule alihangaika kwa dakika kumi nzima, hakufanikiwa, akaichukua laini ile na kumpatia Kimwinyi ambaye alikuwa na hamu ya kusikia mahali ilipokuwa.
“Hiyo namba bado haijaanza kutumika,” alisema msichana huyo.
“Haijaanza kutumika?”
“Ndiyo! Yaani kwa kifupi bado hatujatengeneza namba ya namna hiyo,” alisema msichana huyo huku akimwangalia Kimwinyi.
“Yaani sijakuelewa. Umesemaje?”
“Tuna namba ambazo tunazitengeneza. Namba zinazoanzia 8 bado hazijaanza kutengenezwa, zipo zinazoanzia na 6 ambazo ndizo tulizofikia,” alisema msichana huyo.
“Kwa hiyo hii namba haipo?”
“Ndiyo!”
“Sasa aliyenipigia mbona ndiyo kaitumia hii?” aliuliza.
“Hebu niione!”
Kimwinyi akampatia simu yake msichana yule ambaye aliiangalia ile namba, kweli ilitumika. Yeye mwenyewe hakujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, kwa nini namba ile itumike na wakati haikuwa imetengenezwa kwa matumizi.
Kila mtu aliyeulizwa humo, hakujua, vijana wa IT nao walishangaa. Mpaka Kimwinyi akaondoka baada ya kutumia saa mbili makao makuu hapo hakuwa amepata jibu la maswali yake juu ya namba ile.
“Kwa hiyo haipo?”
“Ndiyo mkuu!”
Wakati wao wakijiuliza kuhusu namba, upande wa pili Watanzania walikuwa wakijiuliza kuhusu mauaji ya Mzee Filipo, hawakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mpaka muda huo. Walitaka kusikia taarifa kutoka ikulu juu ya kile kilichokuwa kikiendelea nchini.
“Kumbe Mzee Filipo aliuawa?” aliuliza jamaa mmoja.
“Mmh! Wewe umepata wapi taarifa?”
“Ingia Instagram uone kwenye akaunti ya Mabadiliko ya Kweli ilivyoadikwa,” alijibu jamaa aliyeulizwa swali.
Jamaa huyo alipoingia, kila alichoambiwa ndicho alichokiona, hakuamini macho yake, si yeye tu bali kila mtu aliyeingia na kusoma katika akaunti ile hakuamini kama Mzee Filipo alikuwa ameuawa.
Kulikuwa na maswali ambayo yaliambatana na picha ile iliyowekwa, maswali hayo ndiyo yaliyozua gumzo kubwa hasa la jamaa ambaye alisema kwamba alikuwa mwanakijiji wa kijiji kilichotokea ajali na wakati hakuwa akijulikana na mtu yeyote hapo.
Jinsi maswali yale yaliyoulizwa yalivyokuwa, kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba Mzee Filipo alikuwa ameuawa na kisha ajali ile kutengenezwa ili ionekane kwamba alipata ajali mbaya na kufa.
Vichwani mwa watu wengi walikuwa na hamu ya kujua ni mtu gani alikuwa amehusika katika mauaji hayo. Waliambiwa kwenye akaunti ile kwamba hatimaye mtu aliyehusika angewekwa hadharani lakini pia waliambiwa kwamba kulikuwa na kikao cha watu sita kilichowekwa, kilikuwa kikao muhimu cha kummaliza mtu aliyekuwa na akaunti hiyo, hawakumfahamu, walikuwa wakicheza mchazo wa kubahatisha tu.
“Mimi ninataka kuwajua hao watu waliokuwa kwenye hicho kikao. Ni nani na nani sasa?” aliuliza msichana mmoja aliyekuwa akisoma posti katika akaunti hiyo.
Hilo ndilo lilikuwa hitaji la watu wengi, kila mmoja alitaka kuona majina ya watu waliokuwa kwenye kikao hicho na pia walitaka kujua watu wawili waliokuwa wamepanga mpango wa kumuua Mzee Filipo, tatizo lilikuwa nini na wakati kila mtu ndani ya chama alikuwa akimpenda mzee huyo?
Wakati watu wakihitaji majibu ya maswali yote waliyokuwa wakijiuliza, Rais Bokasa alikuwa na hofu tele, kwa kile kilichokuwa kikiendelea kilimchanganya kichwa chake.
Alitaka kuwaua watu wanne ambao aliamini kwamba kwa namna moja au nyingine mmoja kati ya ndiye aliyekuwa akihusika katika kumiliki akaunti hiyo lakini kitu cha ajabu kabisa, hata alipokaa na Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Bwana Kimwinyi watu walijua kile kilichokuwa kimezungumziwa, mipango yao mpaka jinsi mauaji hayo yalivyotakiwa kufanyika.
“Sasa huyu atakuwa nani? Au Kimwinyi mwenyewe? Kama tulipanga mipango wawili tu, mimi na yeye halafu kesho huyu mtu wa mtandao anajua, nani kamwambia kama si yeye? Nina wasiwasi naye, atakuwa anahusika huyu,” alijiuliza Rais Kimwinyi huku akionekana kuchanganyikiwa.
Kama walikuwa wawili tu, wakapanga dili na baadaye kubumbulika, akawa na uhakika kwamba Kimwinyi alikuwa akihusika na akaunti ile na kama si yeye basi alikuwa akimpa mtu huyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea, ili aendelee kuwa salama ilikuwa ni lazima amuue huyo Kimwinyi kwani tayari alikuwa na wasiwasi naye kupita kawaida.
Katika harakati za kumuua Kimwinyi hakutaka kumshirikisha mtu yeyote yule, alitaka kila kitu kiwe siri kubwa na kusiwe na mtu yeyote ambaye alitakiwa kufahamu kilichokuwa kikiendelea.
“Ni lazima nimtume aende Nigeria, akifika huko niwasiliane na Boko Haram wamuue,” aliwaza Rais Bokasa, mbinu hiyo ndiyo aliyotaka kuitumia, ilikuwa ni lazima amuue mwanaume huyo ambaye aliamini ndiye aliyemsaidia mtu mwenye akaunti ile Instagram kupata taarifa ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
***
Rais Bokasa hakutaka kukubali, alihisi kabisa kwamba Kimwinyi ndiye alikuwa adui yake namba moja, hakutaka kuona mwanaume huyo akiendelea kuvuta pumzi ya dunia hii, kile alichokitaka ni kumuua kisiri kwa kuamini kwamba baada ya kufanya mauaji hayo basi angekuwa salama kabisa.
Usiku mzima alikuwa na mawazo tele, aliwasiliana na mkuu wa kundi la Boko Haram lililokuwa Afrika Magharibi hasa nchini Nigeria, akamwambia kwamba alikuwa na kazi ambayo ilitakiwa kufanyika haraka sana, kulikuwa na mtu ambaye alitakiwa kuuawa.
Hilo hakukuwa na tatizo kwa Boko Haram, kwa kuwa kundi hilo lilihitaji sana pesa kwa ajili ya kujiendeleza, kazi ambayo waliambiwa kwamba waifanye haikuwa na tatizo lolote lile, wakapanga tarehe, akawatumia picha na kuwapa ratiba kamili ambayo Kimwinyi alikuwa akiondoka Tanzania na kufika nchini Nigeria.
Rais Bokasa akampigia simu Kimwinyi na kumpa taarifa kwamba alitakiwa kuelekea nchini humo kwa ajili ya kuzungumza na baadhi ya viongozi wa huko kuhusu kuidhibiti akaunti mtandaoni ambayo ilikuwa ikisumbua, alimwambia kwamba hakukuwa na mtu aliyekuwa akimwamini katika serikali yake zaidi ya huyo Kimwinyi maneno ambayo yalimfurahisha pasipo kujua kulikuwa na mpango kabambe wa kummaliza hata kabla hajafika hotelini.
“Nashukuru sana kwa kuniamini!” alisema Kimwinyi.
“Haina shida. Wewe nenda Nigeria kisiri na kila kitu tutazungumza ukifika huko,” alisema rais.
“Sawa.”
Wakati wakizungumza hayo mchana siku ya Ijumaa, kwa nchini Japan tayari ilikuwa ni asubuhi ya Siku ya Jumamosi asubuhi. Godwin alikuwa darasani akijisomea, mara akaona kompyuta yake ikimwambia kwamba kulikuwa na mawasiliano yalikuwa yakifanyika kutoka katika namba ya Rais Bokasa aliyokuwa ameidukua.
Haraka sana akachukua ‘hearphone’ zake, akazichomeka na kuanza kusikiliza mawasiliano yao. Simu ilikuwa imetoka kwa rais huyo na kwenda kwa Mkurugenzi wa Usalama wa taifa, Kimwinyi, aliyasikiliza mazungumzo yote na kitu kilichomjia kwa haraka mno kichwani mwake kilikuwa ni mauaji tu.
Alijua kwamba rais huyo alikuwa akijitahidi kufanya kila kitu kuona akaunti ya Mabadiliko ya Kweli inafutika, na kwa sababu alikuwa amemtuma Kimwinyi kumuua Mzee Filipo, basi alitaka kuificha siri hiyo hivyo kumuua Kimwinyi.
Saa moja baada ya kuyasikia mazungumzo hayo, Godwin akaingia kwenye akaunti yake na kuweka picha ya Tanzania kisha kuandika R.I.P na chini kuweka maneno machache yaliyosomeka ‘Kuna mtu anakwenda kufa, hatokufa Tanzania, atakufa mbali kabisa ila ni mchezo ambao umechezwa na mtu fulani. Unataka kujua ni nani? Endelea kusubiri tu!’.
Alipomaliza, akaiposti. Kila mtu aliyeiona posti hiyo alishtuka, walimwamini mtu aliyekuwa akiitumia akaunti hiyo, waliamini kwamba kulikuwa na mtu alikuwa akienda kufa na watu wengi wakauliza alikuwa nani lakini hakukuwa na aliyekuwa na majibu ya maswali yao.
Kimwinyi hakuwa akijua lolote lile, alipoambiwa hivyo, ndani ya saa moja akapanda ndege na kuanza kuondoka nchini Tanzania huku akiambiwa kwamba hapo uwanja wa ndege angepokelewa na mkurugenzi wa Usalama wa Taifa wa huko, The National Intelligence Agency (NIA), Bwana Andrew Okafor.
Njia nzima alikuwa na mawazo tele, kama alivyokuwa amechanganyikiwa rais naye alichanganyikiwa hivyohivyo. Muda mwingi alikuwa akiongea peke yake, kichwa chake hakikuwa sawa hata kidogo.
Safari hiyo ilichukua saa kadhaa ndipo ndege ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Murtala Muhammed uliokuwa jijini Lagos. Haraka sana baada ya ndege kusimama, abiria wakaanza kuteremka akiwemo yeye mwenyewe.
Mzigo wake ulipochunguzwa na kuuchukua akaanza kutoka ndani ya jengo hilo ambapo nje akakutana na mwanaume mmoja ambaye alikuwa akimwangalia sana, kwa muonekano wake tu ulionyesha ni ofisa wa usalama wa taifa kitu kilichomfanya kumsogelea.
“My name is Jonas Ogwadugu! I was told to come and pick you up,” (naitwa Jonas Ogwadugu! Niliambiwa nije kukuchukua) alisema mwanaume huyo huku akiwa na tabasamu pana.
“Ooh! Thank you! My name is Kimwinyi! How do you find me?” (Ooh! Asante! Naitwa Kimwinyi! Umenipataje?) aliuliza huku naye akitoa tabasamu.
“I got your picture,” (nina picha yako)
Akamchukua na kuelekea naye katika gari moja la kifahari. Kwa jinsi mapokezi yalivyokuwa, muonekano wa gari ulionyesha kabisa mtu huyo alikuwa ni kutoka katika usalama wa taifa wa Nigeria. Gari likawashwa na dereva wa gari hilo na kuondoka mahali hapo.
Njiani walikuwa wakizungumza mambo mengi, Jonas alionekana kuwa mchangamfu kupita kawaida. Kila wakati uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana na alipokuwa akiongea alionekana kama mtu aliyekuwa na akili kubwa mno.
Alimwambia Kimwinyi jinsi walivyokuwa wakifanya kazi, walikuwa na kikosi hatari sana ambacho kilipambana juu chini kuhakikisha nchi inalindwa kwa ngumu kubwa kuliko kitu chochote kile.
Hakumficha, alimwambia jinsi walivyoguswa kwa kuambiwa kwamba kulikuwa na akaunti ambayo ilikuwa ikiwasumbua. Wao, Nigeria walipita huko zamani, kulikuwa na wataalamu wa kompyuta mitaani, wote baadaye wakaajiliwa serikalini, hakukuwa na mtu aliyekuwa na uwezo mkubwa ambaye alikuwa nje ya serikali ila pamoja na hayo, wangemwambia ni jinsi gani wataweza kuizuia akaunti hiyo.
“Nitafurahi sana! Hakika imetusumbua sana,” alisema Kimwinyi huku akijisikia amani kabisa kana kwamba alipokelewa kupelekwa harusini.
Safari iliendelea, kile alichokitarajia kwamba hotelini alipotakiwa kwenda palikuwa karibuni kilikuwa tofauti na mategemeo yake, gari liliendeshwa kwa mwendo wa kawaida, wakaanza kutoka katika Jiji la Lagos na kuanza kwenda katika Jiji la Ibadan.
Alishangaa, alitamani kuuliza lakini akahisi kama kuingilia jukumu la watu hao hivyo kukaa kimya. Gari lilikwenda mpaka likaacha barabara ya lami na kuanza kuingia kwenye barabara ya vumbi, walikwenda kwa dakika zaidi ya ishirini, gari likasimama nje ya jumba moja kuukuu na kuambiwa kuteremka.
“Tumefika?” aliuliza lakini Okafor hakujibu chochote kile, akateremka kutoka garini.
Hata kabla Kimwinyi hajajua nini kilikuwa kikiendelea mahali hapo, wanaume sita waliokuwa na bunduki aina ya AK47 wakatokea mahali hapo, alishtuka, hakujua kitu chochote kile, akaamliwa kuteremka kutoka garini huku mikono yake ikiwa kichwani, akafanya hivyo huku akitetemeka mno.
“Nimefanya nini jamani?” aliuliza huku akitetemeka.
“Utamuuliza rais wako!”
“Rais wangu? Bokasa ndiye aliyewat...” aliuliza lakini hata kabla hajamalizia swali lake, akapigwa na kitako cha bunduki, akapoteza fahamu, wakamchukua na kuondoka naye.
****
Godwin alikuwa akiandaa ripoti yake ndefu, alitaka kuwaambia Watanzania kila kitu kilichokuwa kikiendelea, tangu mwanzo wa kikao chao mpaka hapo walipofikia, hakutaka kuficha kitu chochote kile, katika ripoti ile aliweka bayana hata ile mipango ambayo ilitakiwa kufanywa baada ya Kimwinyi kuuawa.
Ilikuwa ripoti ndefu na yenye kusisimua sana, aliamini kila Mtanzania ambaye angekwenda kuisoma ilikuwa ni lazima kumchukua rais huyo ambaye alijitahidi kuwaangamiza watu ili mambo yake machafu yasiendelee kutolewa.
Alimini kwamba kwa watu milioni ishirini ambao waliifolo akaunti yake wangeweza kubadilisha kila kitu, aliamini kwamba wengi waliokuwa wamemfolo walikuwa watu wake, waliunga kile alichokuwa akikifanya.
“Ila kweli rais ana mpango wa kumuua Kimwinyi au? Nisije kuonekana muongo!” alijiuliza Godwin, kila wakati macho yake yalikuwa kwenye mitandao mbalimbali nchini Nigeria kuona kama kweli Kimwinyi alikuwa ameuawa kama alivyohisi au la.
Saa ziliendelea kukatika, bado macho na masikio yake yalikuwa yakisikilizia kile kilichokuwa kikiendelea nchini Nigeria. Ilipofika majira ya saa kumi jioni siku ya Jumapili, taarifa aliyokuwa akiisubiri kwa hamu kubwa ikatangazwa.
Mtanzania mmoja alikutwa akiwa ameuawa na mwili wake kutupwa msituni. Japokuwa ilionekana kuwa habari mbaya lakini kwa Godwin ilimfanya kutabasamu sana. Hapohapo akaichukua na kuiweka katika mtandao wake na kuwakumbusha watu kwamba jana yake usiku kwa majira ya Afrika aliandika kwamba kungekuwa na mauaji ambayo yangekwenda kutokea nje ya Tanzania na hatimaye yalikuwa yametokea.
Kila mtu alishangaa, hawakujua ni kwa namna gani mtu huyo aliweza kupata mambo yote hayo. Ni kweli mkurugenzi wa usalama wa taifa alikuwa ameuawa nchini Nigeria ambapo taarifa zilisema kwamba alitekwa na Boko Haram kimakosa kwa kufikiri kwamba alikuwa Mganda, Oseah Mambo waliyekuwa wakimtafuta kwa kipindi kirefu.
“Huu ni mpango na si kwamba walimchanganya! Walijua kwamba walikuwa wakienda kumuua mkurugenzi wa usalama wa taifa, hivyo mnaposikia kwamba walimteka na kumuua kimakosa ni uongo, nitakuwekeeni ripoti kamili ya mambo yote haya” aliandika Godwin katika akaunti yake.
Watanzania wengi wakahisi kama akaunti hiyo ilikuwa ikiendeshwa na malaika kwani mtu huyo alikuwa alikuwa akijua mambo mengi sana, hata kama kulikuwa na mpango mliokuwa mkiufanya chumbani, kesho yake alikuwa akijua kila kitu.
Wengi wakamsifu lakini pia wakatamani kuiona ripoti hiyo ambayo ingezungumzia mambo mengi mno. Mitaani, kila mtu alikuwa akizungumza lake lakini wengi wakabaki na ukweli kwamba Kimwinyi aliyeuawa na Boko Haram ulikuwa ni mpango na si kutekwa kimakosa.
“Nitarudi Tanzania wiki hiihii ndani ya siku tatu! Nikija, nitahakikisha nawapeni mambo mengi zaidi,” aliandika Godwin ambapo watu wengi wakakomenti kwa kumkaribisha kwani hawakuona kama kungekuwa na mtu mwingine wa kuikomboa Tanzania zaidi yake.
“Karibu sana mkombozi wetu,” alikomenti jamaa mmoja. Godwin akajiandaa kurudi nchini Tanzania.
***
Mara baada ya taarifa za kifo cha Kimwinyi kusambazwa katika mitandao mbalimbali, Rais Bokasa akapigiwa simu na rais wa Nigeria na kuambiwa kilichokuwa kimetokea. kwanza akajifanya kushtuka kwa kutokuamini kile kilichokuwa kimetokea. Aliulizwa kama alimruhusu mtu huyo kuelekea nchini Nigeria lakini akakataa katakataka.
Alitaka kujisafisha, alijua fika kwamba kungekuwa na taarifa nyingi ambazo zingeandikwa kuhusu mauaji hayo, alitaka kuyazima mapema hata kabla mitandao ya kijamii haijaweka wazi hisia zao kwa kuhisi kwamba mtu huyo alikuwa ameuawa kimakusudi.
Hakutaka kuchelewa, hapohapo akachukua simu yake na kumpigia mkurugenzi wa televisheni ya taifa ambaye alimwambia kwamba alihitaji waandishi wa habari kwani kulikuwa na mambo aliyotaka kuzungumza.
Hilo halikuwa tatizo, baada ya dakika kadhaa, waandishi hao wakawa ikulu ambapo wakaanza kurusha matangazo moja kwa moja. Hakutaka kujificha, aliwaambia watu hao namna Kimwinyi alivyoondoka, alijifanya kuwasiliana na mawaziri wengine kutaka kujua sababu ya Kimwinyi kuelekea nchini Nigeria lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa na majibu.
“Nilishangaa kupigiwa simu na rais wa Nigeria na kuambiwa kuwa Kimwinyi alitekwa. Alikwenda Nigeria kufanya nini? Nani alimruhusu? Haya ni maswali ambayo nimekosa maj...” alisema lakini hata kabla hajamaliza sentensi yake, akaanza kulia.
Huo ndiyo ulikuwa ujanja wa kwanza kabisa alioufanya. Hakutaka kugundulika, alihisi kitendo cha kutoa machozi mbele ya waandishi wa habari kingemfanya kila mtu kuamini kile alichokisema, hilo ndilo lilivyokuwa kwani baadhi ya wananchi waliokuwa wakimwangalia katika televisheni hiyo waliamini kwamba hakuwa amefanya jambo hilo.
“Mpaka rais analia! Ameguswa sana jamani halafu kuna mpuuzi mmoja kwenye mtandao kajiunga na kibando chake cha wiki anamchafua rais wetu kwamba kahusika na mauaji hayo. Hivi kweli aliyehusika anaweza kulia?” alihoji jamaa mmoja aliyekuwa akiuza duka.
“Kwani kulia tatizo bwana?” aliuliza jamaa mwingine.
“Unadhani chozi la mwanaume linatoka hivihivi!”
“Mbona wengi wanalia bwana! Tena si kulia, wengine wamefiwa na bado wanacheka msibani,” alisema jamaa mwingine.
Ili kuonyesha kwamba alikuwa ameguswa na msiba huo, Rais Bokasa alikuwa bega kwa bega na familia ya Kimwinyi, alikuwa akijitolea kwa kila hali ili isionekane kama yeye ndiye aliyehusika katika mauaji hayo.
Kulikuwa na misiba mingi iliyokuwa imetokea lakini kwa msiba huo, rais huyo alijitoa kwa nguvu zote kiasi kwamba akaanza kuwalaghai Watanzania kwamba hakuwa amehusika katika mauaji hayo. Wakati akiwa msibani, akasikia simu yake ikiita, haraka sana akaichukua kutoka mfukoni na kuipeleka sikioni.
“Kuna nini?” aliuliza.
“Kumbe yule mtu wa ile akaunti hayupo Tanzania! Nimeona posti yake, amesema kwamba atakuja Tanzania ndani ya siku mbili tatu,” alisema mwanaume huyo.
“Hakikisheni mnaweka usalama wa kutosha katika uwanja wa ndege na mipakani, hakikisheni mnampata huyu mtu,” alisema Rais.
“Sawa.”
Akakata simu. Kichwa chake kilichanganyikiwa zaidi, alitamani kuondoka msibani hapo, hakukuwa na kitu alichokitaka kama kumfahamu mtu aliyekuwa nyuma ya akaunti ile iliyokuwa ikimuumiza kichwa chake. Hakutaka kukaa sana msibani, akaondoka na kuelekea ikulu.
Njiani, alikuwa na mawazo tele, aliongea peke yake, hakuonekana kuwa na raha hata mara moja na mpaka anafika ikulu alihisi kabisa kichwa chake kuwa kziito mno, hivyo akajilaza.
Aliamka majira ya saa tatu usiku, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuchukua simu yake na kumpigia mwanaume aliyempigia kabla na kumpa taarifa kwamba mtu aliyekuwa akitumia akaunti ile angefika nchini Tanzania ndani ya siku mbili tatu, alitaka kujua waliishia wap, alitaka kufahamu kila kitu.
“Mmefikia wapi?”
“Ulinzi umewekwa kila kona mkuu! Kila Mtanzania anayefika ni lazima kuchunguzwa sana!” alijibu mwanaume wa upande wa pili.
“Basi sawa. Ngoja niwaambie kitu kimoja. Mkiwakagua hakikisheni mnawaambia waingie kwenye akaunti zao za Instagram, wasijitoe, hakikisheni mnaangalia akaunti inayotumika ni ipi. Sawa?” alisema na kuuliza.
“Sawa mkuu!”
Hicho ndicho walichokifanya. Polisi na wanausalama wa taifa wakaambiwa kile kilichotakiwa kufanywa. Kila mtu aliyekuwa akiingia nchini Tanzania kupitia mipakani au uwanja wa ndege ilikuwa ni lazima kuchunguzwa yeye kama yeye na pia kuambiwa kufungua akaunti yake ya Instagram kwa ajili ya kuangalia kama wangekuwa watumiaji wa akaunti ya Mabadiliko ya Kweli.
Ilikuwa kazi kubwa lakini ilikuwa ni lazima kufanyika. Kila mtu alikuwa akishangaa, hawakujua sababu ya polisi na wanausalama kufanya kitu kama hicho.
Wakati hali hiyo ikiendelea, Godwin hakuwa akijua lolote lile. Alipanga kurudi nchini Tanzania kwani alisoma na kupata PhD yake katika masuala ya kompyuta. Hakutaka kubaki nchini Japana, akashukuru kwa Mzee Takesh na kurudi nchini Tanzania.
Njiani alikuwa akifikiria kile alichotakiwa kufanya, hakukubali kuona Tanzania ikiendeshwa na rais mmoja kwa miaka mingi, alitaka kubadilisha kila kitu, kama Bokasa aliiongoza Tanzania kwa miaka mingi kwa kuwa tu alibadilisha baadhi ya vipengele kwenye katiba, sasa ulikuwa muda wake kung’oka.
“Habari yako!” alisikia sauti ya msichana mmoja ikimsalimia.
“Salama! Za kwako!”
“Njema tu! Na wewe umetoka Dubai?” aliuliza msichana huyo kwa sauti nyembamba, alionekana kuwa mchangamfu mno.
“Hapana! Nimetoka Uholanzi!”
“Ulikuwa masomoni?”
“Yeah! Jiji Amsterdam!”
“Ooh! Naitwa Manka Msuya!” alisema msichana huo huku akimpa mkono.
“Naitwa Godwin Jr!”
Japokuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana lakini kila mmoja alionekana kuwa mchangamfu sana. Walikuwa katika kiti kimoja huku ndege ikiendelea kukata mawingu kuelekea nchini Tanzania. Walizungumza mengi, msichana huyo alionekana kuwa mkweli kwa kila kitu alichokuwa akikizungumza lakini kwa Godwin, hakukuwa hata na kitu kimoja cha kweli alichomwambia Manka.
Baada ya saa kadhaa, ndege ikatua katika Uwanja wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi nchini Kenya. Hawakuteremka, walibaki ndani ya ndege ambapo baada ya muda fulani ikapaa tena na kuelekea nchini Tanzania.
Wote walichoka lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa ladhi kulala kwani kwa jinsi stori zilivyonoga, hakukuwa na yeyote aliyekuwa tayari kumuacha mwenzake na yeye kulala.
Baada ya saa chache wakaingia jijini Dar es Salaam ambapo ndege ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Huku wakiwa pamoja kama mke na mume, wakateremka na kuelekea nje ya ndege ambapo wao na abiria wengine wakaunganisha mpaka katika jengo la uwanja huo.
“Mnatakiwa muende kule,” alisema dada mmoja huku akiwaangalia wawili hao.
“Kufanya nini?”
“Ni maagizo ambayo tumeachiwa! Hatujui kufanya nini!” alijibu dada huyo.
“Ni sisi tu?”
“Hapana! Hata wengine pia!”
“Sasa mbona Wazungu wanasepa zao?”
“Ni kwa ajili ya Watanzania tu,” alijibu msichana.
Si Godwin wala Manka aliyejua kilichokuwa kikiendelea kule, walishangaa lakini hawakuwa na jinsi kwani wenzao ambao walikwenda upande ule hawakuwa wakilalamika kwa lolote lile.
Kule, kulikuwa na watu wa usalama wa taifa waliovalia suti zao, walikuwa na wajibu wa kumchukua mtu yeyote na kumpeleka katika vyumba ambavyo walivitenga kwa ajili ya kufanyia kazi yao.
“Kuna nini?” aliuliza Manka.
“Hata mimi sijui! Hebu twende tukawasikilizie. “
“Ila naogopa mwenzio!”
“Hahaha! Kwani umeua Manka! Twende tukawasikilize,” alisema Godwin.
Walipowafikia usalama wa taifa, wakawachukua na kuwaambia kuingia ndani ya chumba kimoja. Godwin akaambiwa asubiri, Manka akachukuliwa na kuingizwa humo. Alikuwa akitetemeka, hakuwa amefanya kosa lolote lile lakini alijiona kama mhalifu.
Alipoingia, akaanza kuhojiwa baadhi ya maswali na kuambiwa kutoa simu yake. Hakubisha, akaitoa na kuambiwa aingie katika akaunti zake za Facebook na Instagram, hilo halikuwa tatizo, akafanya kama alivyoambiwa.
Ofisa mmoja wa usalama wa taifa akachukua simu ile na kuanza kuangalia alichotaka kuangalia. Alichukua dakika tano, alipomaliza, akamrudishia na kumtaka mtu mwingine aingie.
Godwin akaingia, akaambiwa akae kwenye kiti, akakaa na kuanza kuangalia na wanaume hao walioonekana kuwa makini kwa kila kilichokuwa kikitokea ndani ya chumba hicho.
Wakamuuliza maswali kadhaa, Godwin hakuonekana kutetemeka, alijibu kwa usahihi kila swali aliloulizwa, baada ya kila kitu akaambiwa atoe simu yake na kuwakabidhi.
“Ya kazi gani?” aliuliza Godwin.
“Kuna kitu tunataka kuangalia!”
“Kitu gani?”
“Wewe tupe simu yako,” alisema ofisa usalama.
“Hapana! Siwezi kuwapa kirahisi namna hiyo!” alisema Godwin huku akiachia tabasamu kana kwamba kile alichokuwa akikizungumza kilikuwa na utani.
Huo ndiyo ulikuwa msimamo wake, alikataa katakata kuwapa simu yake. Kila mmoja aliyekuwa ndani ya chumba kile akahisi kwamba inawezekana Godwin alikuwa mtu waliyekuwa wakimtafuta.
Walimlazimisha, walipoona amekataa, wakaichukua kinguvu. Wala hakubisha. Walipoichukua, kazi kubwa ilikuwa ni kuifungua simu hiyo. Ilikuwa imefungwa, hakukuwa na mtu aliyejua namba za siri zaidi yake.
“Tupe namba zako za siri!”
“Nitawapa vipi na wakati mmeichukua kinguvu! Itumieni basi,” alisema Godwin, hapohapo akakunja nne, kuonyesha kwamba hakuwa na hofu yoyote ile.
Wakaanza kumpa vitisho ndani ya chumba kile ili aogope. Alihisi kabisa kulikuwa na kitu wanausalama hao walitaka kuangalia na kama akili yake ilikuwa imemwambia kwani akaunti ya Mabadiliko ya Kweli iliyokuwa Instagram haikuwa imetolewa hivyo kama watu wale wangeingia katika mtandao huo, wangekutana na akaunti hiyo.
“Toa namba za siri!” alisema mwanaume mmoja.
“Kutoa siwezi! Kama mna uwezo, futeni kila kitu,” alisema Godwin huku akionekana kumaanisha, mwanausalama yule aliyekuwa akimuhoji na mwenzake wakajiangalia viunoni mwao kuona kama kulikuwa na bastola, zilikuwepo, na pingu nazo, zilikuwepo.
“Tunakupa nafasi ya mwisho! Fungua simu yako!”
“Simu ni yangu, nilinunua kwa pesa yangu, hamkunichangia kwa chochote, iweje niwafungulie? Kufungua siwezi! Mkikasirika, vimbeni mpasuke,” alisema Godwin maneno yaliyowafanya maofisa wale kuvimba kwa hasira.

Je, nini kitaendelea?
 
Hongera sana mkuu, ikiwa ndefu ivyo ndo poa sana asee shukrani, ongezea basi mkuu
 
daah sasa godwin karudi kwanini jaman bora angebaki huko huko tu
 
  • Thanks
Reactions: ram
DUNIA HAINA USAWA

Godwin alikuwa akiendelea kusoma kama kawaida, kichwa chake kilikuwa na mawazo mengi, alikuwa akifikiria namna ambavyo angeweza kuwawekea chuki kubwa wananchi juu ya viongozi wao waliokuwa wakiwaibia fedha wananchi wao na hata kuwakandamiza masikini.
Hakuacha kudukua mawasiliano yao, kila wakati alikuwa akicheza na kompyuta yake, alijua fika kwamba watu hao walikuwa wakiwasiliana, katika kila meseji walizokuwa wakitumiana wabunge wote nchini Tanzania, alizipata kwani alikuwa ameingiakatika namba zao bila kujua.
Ukiachana na hao, pia kulikuwa na watu wa usalama wa taifa ambao aliamini kwamba kama angefanikiwa kuwa na mawasiliano yao na kufuatilia kila kitu basi angefanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Bado aliendelea kukusanya namba za watu mbalimbali, wale waliokuwa na sauti nchini Tanzania. Alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana na ndiyo maana hata kikao kidogo cha watu sita ambacho kiliitishwa ikulu, naye alipata taarifa kwani kila walipopigiana au kutumiana meseji, alikuwa akipata taarifa hizo.
Alishangaa kuona watu hao walikusanyika kwa kuwa walitakiwa kuandika majina ya watu hamsini. Hakujua katika karatasi hizo waliandikwa wakina nani lakini baada ya mkurugenzi wa usalama wa taifa kupigiwa simu na kuambiwa kwamba walitakiwa kufanya mauaji ya watu waliokuwa nao mule ndani, tena kwa kuwataja majina ndiyo akagundua kwamba tatizo kubwa ni kwa sababu aliweka kila kitu kilichozungumziwa katika kikao kile hasa baada ya kudukua mawasiliano ya simu yaliyofanyika baada ya kikao.
Alijua kwamba kulikuwa na mtu mmoja miongoni mwa watu waliokuwa katika kikao kile alikuwa akienda kuuawa, hakujua ni nani na hivyo macho na masikio yake yalikuwa kwenye simu yake ambayo muda wote kazi kubwa ilikuwa ni kudukua mawasiliano ya viongozi hao.
Hapo ndipo akagundua kwamba mtu aliyekuwa akitakiwa kuuawa alikuwa Mzee Filipo, hakuamini macho yake kwani miongoni mwa watu waliokuwa wakiheshimika katika chama tawala alikuwa mtu huyo.
Hakutaka kuzungumza kitu, alitaka kuona kama mauaji hayo yangefanyika au la. Kile alichokuwa akikitegemea ndicho kilichofanyika kwani mzee huyo alikufa katika ajali ambayo mara baada ya kuifuatilia, akapata maswali kadhaa ambayo aliyaandika kwenye akaunti yake Instagram.
Alishangaa, hakuamini kwamba yeye ndiye alikuwa sababu kubwa iliyomfanya mzee huyo kuuawa, hakutaka kuona mauaji yakiendelea, alichokifanya ni kuposti kuhusu mauaji hayo, Watanzania wajue kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Wakati yeye akitafakari hayo yote upande wa pili Kimwinyi alionekana kuchanganyikiwa, pombe zote alizokuwa amekunywa ziliyeyuka kichwani mwake, ulevi wote ukamuondoka, akaegemea usukani na kuanza kuyafikiria maisha yake.
Alishirikiana na rais kwa kila kitu, walicheza michezo mingi ya mauaji lakini kipindi hicho mambo yalionekana kuwabadilikia, walidili na mtu ambaye hawakujua alikuwa wapi ingawa aliamini kwamba alikuwa na nguvu kubwa.
Mara baada ya kujifikiria kwa muda huku akiwa ndani ya gari, akampigia simu Rais Bokasa na kumwambia kilichokuwa kikiendelea, kwamba alipigiwa simu na mtu asiyemfahamu na kumwambia kwamba alikuwa akijua mchezo mzima na lazima afanye juu chini kuhakikisha majina yao anayaweka katika akaunti ile.
Hilo ndilo lililomchanganya zaidi, pamoja na uovu wake mkubwa lakini hakutaka kugundulika na mtu yeyote yule, kila siku alijifanya mtu mwema, aliwasaidia watu, kitendo cha mtu huyo kusema kwamba angeweka kila kitu hadharani kilimchanganya mno.
“Kwa hiyo tufanye nini Kimwinyi?” aliuliza rais.
“Sijajua! Hii hali inanichanganya sana. Nani anamwambia huyu mtu mambo haya?” aliuliza Kimwinyi.
“Hilo ndilo la msingi kujiuliza. Ila aliponipigia simu, kulikuwa na namba aliyotumia, nadhani tukiitumia hii, tutafanikiwa kumpata,” alisema mwanaume huyo.
“Unayo?”
“Ndiyo!”
“Hebu tuanze kuifuatilia.”
Hilo ndilo lililofanyika, siku iliyofuata Kimwinyi akaondoka kwenda makao makuu ya Mtandao wa Simu wa Tritel ambapo baada ya kufika huko akawapa namba ile iliyotumika kumpigia huku dhumuni lake likiwa ni kujua mahali namba hiyo ilipokuwa mara ya mwisho ilipokuwa ikitumika.
“Hii ndiyo namba yenyewe?” aliuliza dada aliyekaa kwenye meza iliyokuwa na kompyuta.
“Ndiyo!”
Akaanza kuifanyia kazi, akaiangalia kwenye kompyuta yake, muda wote alikuwa kimya, aliikodolea macho kompyuta yake huku Kimwinyi akiwa mbele yake akimwangalia tu.
Msichana yule alihangaika kwa dakika kumi nzima, hakufanikiwa, akaichukua laini ile na kumpatia Kimwinyi ambaye alikuwa na hamu ya kusikia mahali ilipokuwa.
“Hiyo namba bado haijaanza kutumika,” alisema msichana huyo.
“Haijaanza kutumika?”
“Ndiyo! Yaani kwa kifupi bado hatujatengeneza namba ya namna hiyo,” alisema msichana huyo huku akimwangalia Kimwinyi.
“Yaani sijakuelewa. Umesemaje?”
“Tuna namba ambazo tunazitengeneza. Namba zinazoanzia 8 bado hazijaanza kutengenezwa, zipo zinazoanzia na 6 ambazo ndizo tulizofikia,” alisema msichana huyo.
“Kwa hiyo hii namba haipo?”
“Ndiyo!”
“Sasa aliyenipigia mbona ndiyo kaitumia hii?” aliuliza.
“Hebu niione!”
Kimwinyi akampatia simu yake msichana yule ambaye aliiangalia ile namba, kweli ilitumika. Yeye mwenyewe hakujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, kwa nini namba ile itumike na wakati haikuwa imetengenezwa kwa matumizi.
Kila mtu aliyeulizwa humo, hakujua, vijana wa IT nao walishangaa. Mpaka Kimwinyi akaondoka baada ya kutumia saa mbili makao makuu hapo hakuwa amepata jibu la maswali yake juu ya namba ile.
“Kwa hiyo haipo?”
“Ndiyo mkuu!”
Wakati wao wakijiuliza kuhusu namba, upande wa pili Watanzania walikuwa wakijiuliza kuhusu mauaji ya Mzee Filipo, hawakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mpaka muda huo. Walitaka kusikia taarifa kutoka ikulu juu ya kile kilichokuwa kikiendelea nchini.
“Kumbe Mzee Filipo aliuawa?” aliuliza jamaa mmoja.
“Mmh! Wewe umepata wapi taarifa?”
“Ingia Instagram uone kwenye akaunti ya Mabadiliko ya Kweli ilivyoadikwa,” alijibu jamaa aliyeulizwa swali.
Jamaa huyo alipoingia, kila alichoambiwa ndicho alichokiona, hakuamini macho yake, si yeye tu bali kila mtu aliyeingia na kusoma katika akaunti ile hakuamini kama Mzee Filipo alikuwa ameuawa.
Kulikuwa na maswali ambayo yaliambatana na picha ile iliyowekwa, maswali hayo ndiyo yaliyozua gumzo kubwa hasa la jamaa ambaye alisema kwamba alikuwa mwanakijiji wa kijiji kilichotokea ajali na wakati hakuwa akijulikana na mtu yeyote hapo.
Jinsi maswali yale yaliyoulizwa yalivyokuwa, kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba Mzee Filipo alikuwa ameuawa na kisha ajali ile kutengenezwa ili ionekane kwamba alipata ajali mbaya na kufa.
Vichwani mwa watu wengi walikuwa na hamu ya kujua ni mtu gani alikuwa amehusika katika mauaji hayo. Waliambiwa kwenye akaunti ile kwamba hatimaye mtu aliyehusika angewekwa hadharani lakini pia waliambiwa kwamba kulikuwa na kikao cha watu sita kilichowekwa, kilikuwa kikao muhimu cha kummaliza mtu aliyekuwa na akaunti hiyo, hawakumfahamu, walikuwa wakicheza mchazo wa kubahatisha tu.
“Mimi ninataka kuwajua hao watu waliokuwa kwenye hicho kikao. Ni nani na nani sasa?” aliuliza msichana mmoja aliyekuwa akisoma posti katika akaunti hiyo.
Hilo ndilo lilikuwa hitaji la watu wengi, kila mmoja alitaka kuona majina ya watu waliokuwa kwenye kikao hicho na pia walitaka kujua watu wawili waliokuwa wamepanga mpango wa kumuua Mzee Filipo, tatizo lilikuwa nini na wakati kila mtu ndani ya chama alikuwa akimpenda mzee huyo?
Wakati watu wakihitaji majibu ya maswali yote waliyokuwa wakijiuliza, Rais Bokasa alikuwa na hofu tele, kwa kile kilichokuwa kikiendelea kilimchanganya kichwa chake.
Alitaka kuwaua watu wanne ambao aliamini kwamba kwa namna moja au nyingine mmoja kati ya ndiye aliyekuwa akihusika katika kumiliki akaunti hiyo lakini kitu cha ajabu kabisa, hata alipokaa na Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Bwana Kimwinyi watu walijua kile kilichokuwa kimezungumziwa, mipango yao mpaka jinsi mauaji hayo yalivyotakiwa kufanyika.
“Sasa huyu atakuwa nani? Au Kimwinyi mwenyewe? Kama tulipanga mipango wawili tu, mimi na yeye halafu kesho huyu mtu wa mtandao anajua, nani kamwambia kama si yeye? Nina wasiwasi naye, atakuwa anahusika huyu,” alijiuliza Rais Kimwinyi huku akionekana kuchanganyikiwa.
Kama walikuwa wawili tu, wakapanga dili na baadaye kubumbulika, akawa na uhakika kwamba Kimwinyi alikuwa akihusika na akaunti ile na kama si yeye basi alikuwa akimpa mtu huyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea, ili aendelee kuwa salama ilikuwa ni lazima amuue huyo Kimwinyi kwani tayari alikuwa na wasiwasi naye kupita kawaida.
Katika harakati za kumuua Kimwinyi hakutaka kumshirikisha mtu yeyote yule, alitaka kila kitu kiwe siri kubwa na kusiwe na mtu yeyote ambaye alitakiwa kufahamu kilichokuwa kikiendelea.
“Ni lazima nimtume aende Nigeria, akifika huko niwasiliane na Boko Haram wamuue,” aliwaza Rais Bokasa, mbinu hiyo ndiyo aliyotaka kuitumia, ilikuwa ni lazima amuue mwanaume huyo ambaye aliamini ndiye aliyemsaidia mtu mwenye akaunti ile Instagram kupata taarifa ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
***
Rais Bokasa hakutaka kukubali, alihisi kabisa kwamba Kimwinyi ndiye alikuwa adui yake namba moja, hakutaka kuona mwanaume huyo akiendelea kuvuta pumzi ya dunia hii, kile alichokitaka ni kumuua kisiri kwa kuamini kwamba baada ya kufanya mauaji hayo basi angekuwa salama kabisa.
Usiku mzima alikuwa na mawazo tele, aliwasiliana na mkuu wa kundi la Boko Haram lililokuwa Afrika Magharibi hasa nchini Nigeria, akamwambia kwamba alikuwa na kazi ambayo ilitakiwa kufanyika haraka sana, kulikuwa na mtu ambaye alitakiwa kuuawa.
Hilo hakukuwa na tatizo kwa Boko Haram, kwa kuwa kundi hilo lilihitaji sana pesa kwa ajili ya kujiendeleza, kazi ambayo waliambiwa kwamba waifanye haikuwa na tatizo lolote lile, wakapanga tarehe, akawatumia picha na kuwapa ratiba kamili ambayo Kimwinyi alikuwa akiondoka Tanzania na kufika nchini Nigeria.
Rais Bokasa akampigia simu Kimwinyi na kumpa taarifa kwamba alitakiwa kuelekea nchini humo kwa ajili ya kuzungumza na baadhi ya viongozi wa huko kuhusu kuidhibiti akaunti mtandaoni ambayo ilikuwa ikisumbua, alimwambia kwamba hakukuwa na mtu aliyekuwa akimwamini katika serikali yake zaidi ya huyo Kimwinyi maneno ambayo yalimfurahisha pasipo kujua kulikuwa na mpango kabambe wa kummaliza hata kabla hajafika hotelini.
“Nashukuru sana kwa kuniamini!” alisema Kimwinyi.
“Haina shida. Wewe nenda Nigeria kisiri na kila kitu tutazungumza ukifika huko,” alisema rais.
“Sawa.”
Wakati wakizungumza hayo mchana siku ya Ijumaa, kwa nchini Japan tayari ilikuwa ni asubuhi ya Siku ya Jumamosi asubuhi. Godwin alikuwa darasani akijisomea, mara akaona kompyuta yake ikimwambia kwamba kulikuwa na mawasiliano yalikuwa yakifanyika kutoka katika namba ya Rais Bokasa aliyokuwa ameidukua.
Haraka sana akachukua ‘hearphone’ zake, akazichomeka na kuanza kusikiliza mawasiliano yao. Simu ilikuwa imetoka kwa rais huyo na kwenda kwa Mkurugenzi wa Usalama wa taifa, Kimwinyi, aliyasikiliza mazungumzo yote na kitu kilichomjia kwa haraka mno kichwani mwake kilikuwa ni mauaji tu.
Alijua kwamba rais huyo alikuwa akijitahidi kufanya kila kitu kuona akaunti ya Mabadiliko ya Kweli inafutika, na kwa sababu alikuwa amemtuma Kimwinyi kumuua Mzee Filipo, basi alitaka kuificha siri hiyo hivyo kumuua Kimwinyi.
Saa moja baada ya kuyasikia mazungumzo hayo, Godwin akaingia kwenye akaunti yake na kuweka picha ya Tanzania kisha kuandika R.I.P na chini kuweka maneno machache yaliyosomeka ‘Kuna mtu anakwenda kufa, hatokufa Tanzania, atakufa mbali kabisa ila ni mchezo ambao umechezwa na mtu fulani. Unataka kujua ni nani? Endelea kusubiri tu!’.
Alipomaliza, akaiposti. Kila mtu aliyeiona posti hiyo alishtuka, walimwamini mtu aliyekuwa akiitumia akaunti hiyo, waliamini kwamba kulikuwa na mtu alikuwa akienda kufa na watu wengi wakauliza alikuwa nani lakini hakukuwa na aliyekuwa na majibu ya maswali yao.
Kimwinyi hakuwa akijua lolote lile, alipoambiwa hivyo, ndani ya saa moja akapanda ndege na kuanza kuondoka nchini Tanzania huku akiambiwa kwamba hapo uwanja wa ndege angepokelewa na mkurugenzi wa Usalama wa Taifa wa huko, The National Intelligence Agency (NIA), Bwana Andrew Okafor.
Njia nzima alikuwa na mawazo tele, kama alivyokuwa amechanganyikiwa rais naye alichanganyikiwa hivyohivyo. Muda mwingi alikuwa akiongea peke yake, kichwa chake hakikuwa sawa hata kidogo.
Safari hiyo ilichukua saa kadhaa ndipo ndege ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Murtala Muhammed uliokuwa jijini Lagos. Haraka sana baada ya ndege kusimama, abiria wakaanza kuteremka akiwemo yeye mwenyewe.
Mzigo wake ulipochunguzwa na kuuchukua akaanza kutoka ndani ya jengo hilo ambapo nje akakutana na mwanaume mmoja ambaye alikuwa akimwangalia sana, kwa muonekano wake tu ulionyesha ni ofisa wa usalama wa taifa kitu kilichomfanya kumsogelea.
“My name is Jonas Ogwadugu! I was told to come and pick you up,” (naitwa Jonas Ogwadugu! Niliambiwa nije kukuchukua) alisema mwanaume huyo huku akiwa na tabasamu pana.
“Ooh! Thank you! My name is Kimwinyi! How do you find me?” (Ooh! Asante! Naitwa Kimwinyi! Umenipataje?) aliuliza huku naye akitoa tabasamu.
“I got your picture,” (nina picha yako)
Akamchukua na kuelekea naye katika gari moja la kifahari. Kwa jinsi mapokezi yalivyokuwa, muonekano wa gari ulionyesha kabisa mtu huyo alikuwa ni kutoka katika usalama wa taifa wa Nigeria. Gari likawashwa na dereva wa gari hilo na kuondoka mahali hapo.
Njiani walikuwa wakizungumza mambo mengi, Jonas alionekana kuwa mchangamfu kupita kawaida. Kila wakati uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana na alipokuwa akiongea alionekana kama mtu aliyekuwa na akili kubwa mno.
Alimwambia Kimwinyi jinsi walivyokuwa wakifanya kazi, walikuwa na kikosi hatari sana ambacho kilipambana juu chini kuhakikisha nchi inalindwa kwa ngumu kubwa kuliko kitu chochote kile.
Hakumficha, alimwambia jinsi walivyoguswa kwa kuambiwa kwamba kulikuwa na akaunti ambayo ilikuwa ikiwasumbua. Wao, Nigeria walipita huko zamani, kulikuwa na wataalamu wa kompyuta mitaani, wote baadaye wakaajiliwa serikalini, hakukuwa na mtu aliyekuwa na uwezo mkubwa ambaye alikuwa nje ya serikali ila pamoja na hayo, wangemwambia ni jinsi gani wataweza kuizuia akaunti hiyo.
“Nitafurahi sana! Hakika imetusumbua sana,” alisema Kimwinyi huku akijisikia amani kabisa kana kwamba alipokelewa kupelekwa harusini.
Safari iliendelea, kile alichokitarajia kwamba hotelini alipotakiwa kwenda palikuwa karibuni kilikuwa tofauti na mategemeo yake, gari liliendeshwa kwa mwendo wa kawaida, wakaanza kutoka katika Jiji la Lagos na kuanza kwenda katika Jiji la Ibadan.
Alishangaa, alitamani kuuliza lakini akahisi kama kuingilia jukumu la watu hao hivyo kukaa kimya. Gari lilikwenda mpaka likaacha barabara ya lami na kuanza kuingia kwenye barabara ya vumbi, walikwenda kwa dakika zaidi ya ishirini, gari likasimama nje ya jumba moja kuukuu na kuambiwa kuteremka.
“Tumefika?” aliuliza lakini Okafor hakujibu chochote kile, akateremka kutoka garini.
Hata kabla Kimwinyi hajajua nini kilikuwa kikiendelea mahali hapo, wanaume sita waliokuwa na bunduki aina ya AK47 wakatokea mahali hapo, alishtuka, hakujua kitu chochote kile, akaamliwa kuteremka kutoka garini huku mikono yake ikiwa kichwani, akafanya hivyo huku akitetemeka mno.
“Nimefanya nini jamani?” aliuliza huku akitetemeka.
“Utamuuliza rais wako!”
“Rais wangu? Bokasa ndiye aliyewat...” aliuliza lakini hata kabla hajamalizia swali lake, akapigwa na kitako cha bunduki, akapoteza fahamu, wakamchukua na kuondoka naye.
****
Godwin alikuwa akiandaa ripoti yake ndefu, alitaka kuwaambia Watanzania kila kitu kilichokuwa kikiendelea, tangu mwanzo wa kikao chao mpaka hapo walipofikia, hakutaka kuficha kitu chochote kile, katika ripoti ile aliweka bayana hata ile mipango ambayo ilitakiwa kufanywa baada ya Kimwinyi kuuawa.
Ilikuwa ripoti ndefu na yenye kusisimua sana, aliamini kila Mtanzania ambaye angekwenda kuisoma ilikuwa ni lazima kumchukua rais huyo ambaye alijitahidi kuwaangamiza watu ili mambo yake machafu yasiendelee kutolewa.
Alimini kwamba kwa watu milioni ishirini ambao waliifolo akaunti yake wangeweza kubadilisha kila kitu, aliamini kwamba wengi waliokuwa wamemfolo walikuwa watu wake, waliunga kile alichokuwa akikifanya.
“Ila kweli rais ana mpango wa kumuua Kimwinyi au? Nisije kuonekana muongo!” alijiuliza Godwin, kila wakati macho yake yalikuwa kwenye mitandao mbalimbali nchini Nigeria kuona kama kweli Kimwinyi alikuwa ameuawa kama alivyohisi au la.
Saa ziliendelea kukatika, bado macho na masikio yake yalikuwa yakisikilizia kile kilichokuwa kikiendelea nchini Nigeria. Ilipofika majira ya saa kumi jioni siku ya Jumapili, taarifa aliyokuwa akiisubiri kwa hamu kubwa ikatangazwa.
Mtanzania mmoja alikutwa akiwa ameuawa na mwili wake kutupwa msituni. Japokuwa ilionekana kuwa habari mbaya lakini kwa Godwin ilimfanya kutabasamu sana. Hapohapo akaichukua na kuiweka katika mtandao wake na kuwakumbusha watu kwamba jana yake usiku kwa majira ya Afrika aliandika kwamba kungekuwa na mauaji ambayo yangekwenda kutokea nje ya Tanzania na hatimaye yalikuwa yametokea.
Kila mtu alishangaa, hawakujua ni kwa namna gani mtu huyo aliweza kupata mambo yote hayo. Ni kweli mkurugenzi wa usalama wa taifa alikuwa ameuawa nchini Nigeria ambapo taarifa zilisema kwamba alitekwa na Boko Haram kimakosa kwa kufikiri kwamba alikuwa Mganda, Oseah Mambo waliyekuwa wakimtafuta kwa kipindi kirefu.
“Huu ni mpango na si kwamba walimchanganya! Walijua kwamba walikuwa wakienda kumuua mkurugenzi wa usalama wa taifa, hivyo mnaposikia kwamba walimteka na kumuua kimakosa ni uongo, nitakuwekeeni ripoti kamili ya mambo yote haya” aliandika Godwin katika akaunti yake.
Watanzania wengi wakahisi kama akaunti hiyo ilikuwa ikiendeshwa na malaika kwani mtu huyo alikuwa alikuwa akijua mambo mengi sana, hata kama kulikuwa na mpango mliokuwa mkiufanya chumbani, kesho yake alikuwa akijua kila kitu.
Wengi wakamsifu lakini pia wakatamani kuiona ripoti hiyo ambayo ingezungumzia mambo mengi mno. Mitaani, kila mtu alikuwa akizungumza lake lakini wengi wakabaki na ukweli kwamba Kimwinyi aliyeuawa na Boko Haram ulikuwa ni mpango na si kutekwa kimakosa.
“Nitarudi Tanzania wiki hiihii ndani ya siku tatu! Nikija, nitahakikisha nawapeni mambo mengi zaidi,” aliandika Godwin ambapo watu wengi wakakomenti kwa kumkaribisha kwani hawakuona kama kungekuwa na mtu mwingine wa kuikomboa Tanzania zaidi yake.
“Karibu sana mkombozi wetu,” alikomenti jamaa mmoja. Godwin akajiandaa kurudi nchini Tanzania.
***
Mara baada ya taarifa za kifo cha Kimwinyi kusambazwa katika mitandao mbalimbali, Rais Bokasa akapigiwa simu na rais wa Nigeria na kuambiwa kilichokuwa kimetokea. kwanza akajifanya kushtuka kwa kutokuamini kile kilichokuwa kimetokea. Aliulizwa kama alimruhusu mtu huyo kuelekea nchini Nigeria lakini akakataa katakataka.
Alitaka kujisafisha, alijua fika kwamba kungekuwa na taarifa nyingi ambazo zingeandikwa kuhusu mauaji hayo, alitaka kuyazima mapema hata kabla mitandao ya kijamii haijaweka wazi hisia zao kwa kuhisi kwamba mtu huyo alikuwa ameuawa kimakusudi.
Hakutaka kuchelewa, hapohapo akachukua simu yake na kumpigia mkurugenzi wa televisheni ya taifa ambaye alimwambia kwamba alihitaji waandishi wa habari kwani kulikuwa na mambo aliyotaka kuzungumza.
Hilo halikuwa tatizo, baada ya dakika kadhaa, waandishi hao wakawa ikulu ambapo wakaanza kurusha matangazo moja kwa moja. Hakutaka kujificha, aliwaambia watu hao namna Kimwinyi alivyoondoka, alijifanya kuwasiliana na mawaziri wengine kutaka kujua sababu ya Kimwinyi kuelekea nchini Nigeria lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyekuwa na majibu.
“Nilishangaa kupigiwa simu na rais wa Nigeria na kuambiwa kuwa Kimwinyi alitekwa. Alikwenda Nigeria kufanya nini? Nani alimruhusu? Haya ni maswali ambayo nimekosa maj...” alisema lakini hata kabla hajamaliza sentensi yake, akaanza kulia.
Huo ndiyo ulikuwa ujanja wa kwanza kabisa alioufanya. Hakutaka kugundulika, alihisi kitendo cha kutoa machozi mbele ya waandishi wa habari kingemfanya kila mtu kuamini kile alichokisema, hilo ndilo lilivyokuwa kwani baadhi ya wananchi waliokuwa wakimwangalia katika televisheni hiyo waliamini kwamba hakuwa amefanya jambo hilo.
“Mpaka rais analia! Ameguswa sana jamani halafu kuna mpuuzi mmoja kwenye mtandao kajiunga na kibando chake cha wiki anamchafua rais wetu kwamba kahusika na mauaji hayo. Hivi kweli aliyehusika anaweza kulia?” alihoji jamaa mmoja aliyekuwa akiuza duka.
“Kwani kulia tatizo bwana?” aliuliza jamaa mwingine.
“Unadhani chozi la mwanaume linatoka hivihivi!”
“Mbona wengi wanalia bwana! Tena si kulia, wengine wamefiwa na bado wanacheka msibani,” alisema jamaa mwingine.
Ili kuonyesha kwamba alikuwa ameguswa na msiba huo, Rais Bokasa alikuwa bega kwa bega na familia ya Kimwinyi, alikuwa akijitolea kwa kila hali ili isionekane kama yeye ndiye aliyehusika katika mauaji hayo.
Kulikuwa na misiba mingi iliyokuwa imetokea lakini kwa msiba huo, rais huyo alijitoa kwa nguvu zote kiasi kwamba akaanza kuwalaghai Watanzania kwamba hakuwa amehusika katika mauaji hayo. Wakati akiwa msibani, akasikia simu yake ikiita, haraka sana akaichukua kutoka mfukoni na kuipeleka sikioni.
“Kuna nini?” aliuliza.
“Kumbe yule mtu wa ile akaunti hayupo Tanzania! Nimeona posti yake, amesema kwamba atakuja Tanzania ndani ya siku mbili tatu,” alisema mwanaume huyo.
“Hakikisheni mnaweka usalama wa kutosha katika uwanja wa ndege na mipakani, hakikisheni mnampata huyu mtu,” alisema Rais.
“Sawa.”
Akakata simu. Kichwa chake kilichanganyikiwa zaidi, alitamani kuondoka msibani hapo, hakukuwa na kitu alichokitaka kama kumfahamu mtu aliyekuwa nyuma ya akaunti ile iliyokuwa ikimuumiza kichwa chake. Hakutaka kukaa sana msibani, akaondoka na kuelekea ikulu.
Njiani, alikuwa na mawazo tele, aliongea peke yake, hakuonekana kuwa na raha hata mara moja na mpaka anafika ikulu alihisi kabisa kichwa chake kuwa kziito mno, hivyo akajilaza.
Aliamka majira ya saa tatu usiku, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuchukua simu yake na kumpigia mwanaume aliyempigia kabla na kumpa taarifa kwamba mtu aliyekuwa akitumia akaunti ile angefika nchini Tanzania ndani ya siku mbili tatu, alitaka kujua waliishia wap, alitaka kufahamu kila kitu.
“Mmefikia wapi?”
“Ulinzi umewekwa kila kona mkuu! Kila Mtanzania anayefika ni lazima kuchunguzwa sana!” alijibu mwanaume wa upande wa pili.
“Basi sawa. Ngoja niwaambie kitu kimoja. Mkiwakagua hakikisheni mnawaambia waingie kwenye akaunti zao za Instagram, wasijitoe, hakikisheni mnaangalia akaunti inayotumika ni ipi. Sawa?” alisema na kuuliza.
“Sawa mkuu!”
Hicho ndicho walichokifanya. Polisi na wanausalama wa taifa wakaambiwa kile kilichotakiwa kufanywa. Kila mtu aliyekuwa akiingia nchini Tanzania kupitia mipakani au uwanja wa ndege ilikuwa ni lazima kuchunguzwa yeye kama yeye na pia kuambiwa kufungua akaunti yake ya Instagram kwa ajili ya kuangalia kama wangekuwa watumiaji wa akaunti ya Mabadiliko ya Kweli.
Ilikuwa kazi kubwa lakini ilikuwa ni lazima kufanyika. Kila mtu alikuwa akishangaa, hawakujua sababu ya polisi na wanausalama kufanya kitu kama hicho.
Wakati hali hiyo ikiendelea, Godwin hakuwa akijua lolote lile. Alipanga kurudi nchini Tanzania kwani alisoma na kupata PhD yake katika masuala ya kompyuta. Hakutaka kubaki nchini Japana, akashukuru kwa Mzee Takesh na kurudi nchini Tanzania.
Njiani alikuwa akifikiria kile alichotakiwa kufanya, hakukubali kuona Tanzania ikiendeshwa na rais mmoja kwa miaka mingi, alitaka kubadilisha kila kitu, kama Bokasa aliiongoza Tanzania kwa miaka mingi kwa kuwa tu alibadilisha baadhi ya vipengele kwenye katiba, sasa ulikuwa muda wake kung’oka.
“Habari yako!” alisikia sauti ya msichana mmoja ikimsalimia.
“Salama! Za kwako!”
“Njema tu! Na wewe umetoka Dubai?” aliuliza msichana huyo kwa sauti nyembamba, alionekana kuwa mchangamfu mno.
“Hapana! Nimetoka Uholanzi!”
“Ulikuwa masomoni?”
“Yeah! Jiji Amsterdam!”
“Ooh! Naitwa Manka Msuya!” alisema msichana huo huku akimpa mkono.
“Naitwa Godwin Jr!”
Japokuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana lakini kila mmoja alionekana kuwa mchangamfu sana. Walikuwa katika kiti kimoja huku ndege ikiendelea kukata mawingu kuelekea nchini Tanzania. Walizungumza mengi, msichana huyo alionekana kuwa mkweli kwa kila kitu alichokuwa akikizungumza lakini kwa Godwin, hakukuwa hata na kitu kimoja cha kweli alichomwambia Manka.
Baada ya saa kadhaa, ndege ikatua katika Uwanja wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi nchini Kenya. Hawakuteremka, walibaki ndani ya ndege ambapo baada ya muda fulani ikapaa tena na kuelekea nchini Tanzania.
Wote walichoka lakini hakukuwa na mtu aliyekuwa ladhi kulala kwani kwa jinsi stori zilivyonoga, hakukuwa na yeyote aliyekuwa tayari kumuacha mwenzake na yeye kulala.
Baada ya saa chache wakaingia jijini Dar es Salaam ambapo ndege ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Huku wakiwa pamoja kama mke na mume, wakateremka na kuelekea nje ya ndege ambapo wao na abiria wengine wakaunganisha mpaka katika jengo la uwanja huo.
“Mnatakiwa muende kule,” alisema dada mmoja huku akiwaangalia wawili hao.
“Kufanya nini?”
“Ni maagizo ambayo tumeachiwa! Hatujui kufanya nini!” alijibu dada huyo.
“Ni sisi tu?”
“Hapana! Hata wengine pia!”
“Sasa mbona Wazungu wanasepa zao?”
“Ni kwa ajili ya Watanzania tu,” alijibu msichana.
Si Godwin wala Manka aliyejua kilichokuwa kikiendelea kule, walishangaa lakini hawakuwa na jinsi kwani wenzao ambao walikwenda upande ule hawakuwa wakilalamika kwa lolote lile.
Kule, kulikuwa na watu wa usalama wa taifa waliovalia suti zao, walikuwa na wajibu wa kumchukua mtu yeyote na kumpeleka katika vyumba ambavyo walivitenga kwa ajili ya kufanyia kazi yao.
“Kuna nini?” aliuliza Manka.
“Hata mimi sijui! Hebu twende tukawasikilizie. “
“Ila naogopa mwenzio!”
“Hahaha! Kwani umeua Manka! Twende tukawasikilize,” alisema Godwin.
Walipowafikia usalama wa taifa, wakawachukua na kuwaambia kuingia ndani ya chumba kimoja. Godwin akaambiwa asubiri, Manka akachukuliwa na kuingizwa humo. Alikuwa akitetemeka, hakuwa amefanya kosa lolote lile lakini alijiona kama mhalifu.
Alipoingia, akaanza kuhojiwa baadhi ya maswali na kuambiwa kutoa simu yake. Hakubisha, akaitoa na kuambiwa aingie katika akaunti zake za Facebook na Instagram, hilo halikuwa tatizo, akafanya kama alivyoambiwa.
Ofisa mmoja wa usalama wa taifa akachukua simu ile na kuanza kuangalia alichotaka kuangalia. Alichukua dakika tano, alipomaliza, akamrudishia na kumtaka mtu mwingine aingie.
Godwin akaingia, akaambiwa akae kwenye kiti, akakaa na kuanza kuangalia na wanaume hao walioonekana kuwa makini kwa kila kilichokuwa kikitokea ndani ya chumba hicho.
Wakamuuliza maswali kadhaa, Godwin hakuonekana kutetemeka, alijibu kwa usahihi kila swali aliloulizwa, baada ya kila kitu akaambiwa atoe simu yake na kuwakabidhi.
“Ya kazi gani?” aliuliza Godwin.
“Kuna kitu tunataka kuangalia!”
“Kitu gani?”
“Wewe tupe simu yako,” alisema ofisa usalama.
“Hapana! Siwezi kuwapa kirahisi namna hiyo!” alisema Godwin huku akiachia tabasamu kana kwamba kile alichokuwa akikizungumza kilikuwa na utani.
Huo ndiyo ulikuwa msimamo wake, alikataa katakata kuwapa simu yake. Kila mmoja aliyekuwa ndani ya chumba kile akahisi kwamba inawezekana Godwin alikuwa mtu waliyekuwa wakimtafuta.
Walimlazimisha, walipoona amekataa, wakaichukua kinguvu. Wala hakubisha. Walipoichukua, kazi kubwa ilikuwa ni kuifungua simu hiyo. Ilikuwa imefungwa, hakukuwa na mtu aliyejua namba za siri zaidi yake.
“Tupe namba zako za siri!”
“Nitawapa vipi na wakati mmeichukua kinguvu! Itumieni basi,” alisema Godwin, hapohapo akakunja nne, kuonyesha kwamba hakuwa na hofu yoyote ile.
Wakaanza kumpa vitisho ndani ya chumba kile ili aogope. Alihisi kabisa kulikuwa na kitu wanausalama hao walitaka kuangalia na kama akili yake ilikuwa imemwambia kwani akaunti ya Mabadiliko ya Kweli iliyokuwa Instagram haikuwa imetolewa hivyo kama watu wale wangeingia katika mtandao huo, wangekutana na akaunti hiyo.
“Toa namba za siri!” alisema mwanaume mmoja.
“Kutoa siwezi! Kama mna uwezo, futeni kila kitu,” alisema Godwin huku akionekana kumaanisha, mwanausalama yule aliyekuwa akimuhoji na mwenzake wakajiangalia viunoni mwao kuona kama kulikuwa na bastola, zilikuwepo, na pingu nazo, zilikuwepo.
“Tunakupa nafasi ya mwisho! Fungua simu yako!”
“Simu ni yangu, nilinunua kwa pesa yangu, hamkunichangia kwa chochote, iweje niwafungulie? Kufungua siwezi! Mkikasirika, vimbeni mpasuke,” alisema Godwin maneno yaliyowafanya maofisa wale kuvimba kwa hasira.

Je, nini kitaendelea?

Sina wasi wasi na Godwin najua atachomoka kwenye hilo...


Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom