nilikuwa na mpenzi tuliedum nae takriban mwaka mmoja na nusu tukashindana tabia. kikubwa ni kwamba nimekuwa nikimfuma live kitandani na wanawake tofaut,kila nikimfuma anaomba msamaha tena huku machozi yanamtoka, tunaenda kupima ukimwi then namsamehe;nimemfuma mara nne na wanawake tofauti tofauti nikamwambia its enough. tukaachana. tatizo linakuja pale anaponisumbua mara kwa mar kwenye sim kwamba hawezi kuishi bila mimi. ananitumia text za mapenzi ukizingatia mim ninampenz mwingine.ameshanigombanisha na wapenzi wawili kila mara akijua mwanaume niliye nae anamfanyia fujo na matusi kem kem. nimemuweka black list, imeshindikana. nimebadilisha namba mara 3,anaitafuta namba yangu anaendeleza fujo zake,kibaya zaidi anatabia za uasherati kiasi cha kuzini na wanaume wenzake,jamani nimeshachoka na huu usumbufu naomben ushauri jaman.