Dua ya Muhammad Ali Kinshasa 1974

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,925
30,273
DUA YA MUHAMMAD ALI KINSHASA 1974
Kwenye kitabu cha maisha yake, "The Greatest My Own Story," Ali anaeleza vipi mzee mmoja kutoka Cuba mchuaji wake misuli alivyokuwa anamnanga kuhusu yeye kujiita, "The Greatest."

Akimwambia kama kweli wewe ni Greatest mpige Foreman siyo ajisifu kwa kumpiga Sonny Liston aliyekuwa kachoka anasubiri mtu atokee ampige.

"Foreman ni simba ndani ya tundu na nyama yake anakula. Ingia ndani ya tundu lake mpore hiyo nyama kama kweli wewe ni Greatest.

Ukiliweza hilo ulimwengu mzima utakutambua kweli wewe ni Greatest. "
Ali alimleta kambini kwake mtu mmoja anaitwa Bossman.

Huyu alipatakuwa "sparring partner," wa Foreman. Katika kitabu kampa sura nzima: "Bossman Comes."

Alisubiriwa kwa hamu kubwa.

Alipowasili Ali na timu yake akiwepo kocha wake Angelo Dundee na Drew Bundini na handlers wakenda faragha.

Ali akamuuliza Bossman amueleze kwa ukweli wa nafsi yake. "Bossman niambie kweli ikiwa leo nitapigana na Foreman nani atapigwa?"

"Utapigwa wewe."
"Toka, toka ondoka hapa msaliti mkubwa wewe."

Bundini kaghadhibika.
Ali akamtuliza Bundini.

"Nimemuuliza swali kwa ukweli na Bossman kajibu kwa ukweli wa nafsi yake.

"Sasa Bossman nataka unifundishe kila kitu unachokijua vipi Foreman anavyopigana."

Kuna mengi sana katika sura hii siwezi kueleza yote. Lakini Ali anasema silaha yake kubwa iliyomwangusha Foreman ni stamina.

Ali alijitayarisha kwa kupigana raundi 30 akiwatumia sparring partner watatu.

Katikati ya pambano mtangazaji alimuuliza Joe Frazier anaonaje pambano linavyokwenda?

Frazier alijibu, "Foreman hatofika mbali kwani naziona dalili za kuchoka."
Waingereza wanasema, "The rest is history."

337847571_229751879461212_8495968594707754348_n.jpg
 
Baada ya kumaliza historia ya wazee wa kariakoo sasa umehamia za usa,tupe story ya martin luther king?
 
Baada ya kumaliza historia ya wazee wa kariakoo sasa umehamia za usa,tupe story ya martin luther king?

Kuna kijana kaweka hotuba ya mwisho ya Martin Luther King hapa Majlis, '' I Have Been to the Mountain Top.''

Hili limenikumbusha mbali sana na kunirudisha nyakati hizo naomba sote tutembee katika barabara ile ya kumbukumbu niliyokanyaga mimi hata kama wewe hukuwapo siku hizo:

Martin Luther King alikuwa mpigania haki za watu weusi Marekani.

Kumbukumbu hizi zinanirudisha mimi miaka 50 nyuma nikiwa kijana mdogo na umri wa miaka 18 na mwanafunzi wa St. Joseph’s Convent, Dar es Salaam.

Shule yetu ilikuwa katikati ya mji karibu na Bahari ya Hindi Bridge Street.

Kutoka shule ilipokuwapo na nyumbani kwetu Libya Street ilikuwa inanichukua kama dakika 20 au zaidi kidogo kufika shule.

Miaka ile ya 1960 Wamarekani walikuwa na ushawishi mkubwa sana kwa sisi vijana na safari ya Mwalimu Nyerere Amerika mwaka wa 1963 wakati wa John Kennedy akiwa rais wa Marekani ilizidisha pia uhusiano mwema katika ya Marekani na Tanganyika.

Miaka hii ya 1960 Waingereza wakiita, ‘’Roaring 60s’’ kwetu vijana katika ‘’teens.’’ hasa wa Dar es Salaam hakika ilikuwa miaka ya wazimu khasa na tukiiga kila kitu cha Kimarekani, kuanzia mavazi hadi muziki wake.

Hizi zilikuwa enzi za ‘’Soul Music,’’ Muziki maalum na makhsusi kwa watu weusi wa Marekani na nje yake.

Si rahisi kwa leo kueleza wazimu uliotukumba wakati tukisikiliza nyimbo za James Brown, Wilson Picket, Ray Charles, Stevie Wonder, Ottis Redding kuwataja wachache katika miziki ya vijana, yaani ‘’Pop.’’

Lakini ilikuwa pia enzi za miziki ya jazz ya wapigaji kama Duke Ellington na waimbaji bingwa kama Nat King Cole, Frank Sinatra, Louis Armstrong, ambayo ilikuwa ikipendwa na wenye umri wa kati na hapa sitaki kuwagusa wanamuziki kutoka Uingereza.

Magazeti tuliyokuwa tukipenda kusoma yalikuwa Newsweek, Time na Ebony gazeti la watu weusi Marekani.

Wengi wetu nami nikiwa katika kundi hilo tulikuwa na ndoto kuwa iko siku tutakwenda Marekani kusoma katika moja ya vyuo vikuu vya huko na wako ambao ndoto zao zikaja kuwa kweli na tuko pia ndoto zikabakia ndoto.

Wamarekani walikuwa na kituo chao cha utamaduni mji ambacho ndani mlikuwa na maktaba na ‘’theatre,’’ sehemu wakionyesha filamu.

Kwa kuwa na vitu hivi Wamarekani walituteka na mimi nilinasa katika dema lile kwani nilikuwa mwanachama wa maktaba ile na nilipofikia makamu ya kuwa naandika katika magazeti ya Uingereza kama Africa Events na New African Mkurugenzi wa United States Information Service alinipa uanachama wa Library of Congress, Washington nikiweza kuazima kitabu au jarida kutoka huko na nikaletewa Dar es Salaam.

Sasa tuje kwa Martin Luther King na mimi.

Mwalimu wangu wa Kiingereza alikuwa mama mmoja wa Kingereza jina lake Mrs. Grant.

Mume wake alikuwa anaitwa Grant na wote walikuja Tanzania katika mpango wa British Council wa kusomesha Kiingereza.

Bwana Grant alikuwa alikuwa akisomesha Chuo Cha Ualimu Chang’ombe.

Mrs. Grant sijui kwa vipi lakini alikuwa mwalimu aliyenipenda labda kwa kuwa nilikuwa na mapenzi makubwa na somo lake lililokuwa linaitwa, ‘’Reading Labaratory,’’ tukifunzwa kusoma kwa haraka, yaani kwa ‘’speed,’’ akiweka, ‘’time clock,’’ kupima unasoma maneno mangapi kwa dakika ngapi kisha kuna maswali unajibu kuonyesha kuwa umeelewa ulichosoma.

Kulikuwa na mashindano ya Elocution Kiingereza na Kiswahili kwa shule zote za Dar es Salam na shule yetu kila mwaka ikishinda katika English Elocution na kuna mwaka tuliwahi kushinda kwa pamoja English na Swahili Elocution.

Nakumbuka mwaka mmoja Swahili Elocution alishinda Athumani Uzigo ambae baadae alikuja kuwa mtangazaji RTD.

Mrs. Grant akaniambia kuwa mwaka ule nitafute passage yeyote niihifadhi kichwani niingie katika mashindano ya English Elocution.

Mwaka wa 1963 ndiyo mwaka ambao Martin Luther King alitoa hotuba yake maarufu, ‘’I have a Dream,’’ Lincoln Memorial, Washington DC.

Nilikuwa nimehifadhi mengi kutoka michezo ya William Shakespeare kama ‘’Julius Caesar,’’ ‘’Merchant of Venice,’’ ambayo wala nisingeihitaji kujifunza kwani tayari nilikuwa nimeshahifadhi na ningeweza kusoma wakati wowote hata nikiamshwa usiku wa manane.

Lakini haya yalikuwa mashindano na nilitaka niingie katika mashindano na mtu mashuhuri kama Martin Luther King siyo na Cassius katika ‘’Julius Caesar,’’ au Shylock katika ‘’Merchant of Venice,’’

Niliamua kumsoma Martin Luther King na hotuba yake ‘’I Have a Dream.’’

Nikitoka nyumbani asubuhi nakwenda shule njia nzima naisoma kimya kimya hotuba hiyo na tulikuwa wanafunzi wengi tunawania nafasi hiyo na kila mtu kachukua chake anachotaka kusoma na sote tutasoma mbele ya mwalimu wetu na mbele ya wanafunzi wenzetu na yule aliye bora ndiye atakaewakilisha shule latika mashindano yale.

Nilishindwa kwa hiyo sikuweza kuiwakilisha St. Joseph’s Convent katika English Elocution.

Kwa nini nilishindwa?

Wenzangu walikuwa wanasema Kiingereza kwa ‘’accent,’’ nzuri ya Kiingereza.

Mimi Mswahili wa Kariakoo ‘’accent,’’ yangu ndiyo iliyonifanya nishindwe.

Picha hiyo hapo chini nimesimama Lincoln Memorial Washington, DC mahali ambako Dr. Martin Luther King alisimama wakati anatoa hotuba yake mashuhuri, ''I Have a Dream.''


55752396_427344678012916_5220900264344551424_n.jpg

Lincoln Memorial Washington DC
54727311_427348544679196_895206059344396288_n.jpg

Library of Congress, Washington DC​
 
Kuna kijana kaweka hotuba ya mwisho ya Martin Luther King hapa Majlis, '' I Have Been to the Mountain Top.''

Hili limenikumbusha mbali sana na kunirudisha nyakati hizo naomba sote tutembee katika barabara ile ya kumbukumbu niliyokanyaga mimi hata kama wewe hukuwapo siku hizo:

Martin Luther King alikuwa mpigania haki za watu weusi Marekani.

Kumbukumbu hizi zinanirudisha mimi miaka 50 nyuma nikiwa kijana mdogo na umri wa miaka 18 na mwanafunzi wa St. Joseph’s Convent, Dar es Salaam.

Shule yetu ilikuwa katikati ya mji karibu na Bahari ya Hindi Bridge Street.

Kutoka shule ilipokuwapo na nyumbani kwetu Libya Street ilikuwa inanichukua kama dakika 20 au zaidi kidogo kufika shule.

Miaka ile ya 1960 Wamarekani walikuwa na ushawishi mkubwa sana kwa sisi vijana na safari ya Mwalimu Nyerere Amerika mwaka wa 1963 wakati wa John Kennedy akiwa rais wa Marekani ilizidisha pia uhusiano mwema katika ya Marekani na Tanganyika.

Miaka hii ya 1960 Waingereza wakiita, ‘’Roaring 60s’’ kwetu vijana katika ‘’teens.’’ hasa wa Dar es Salaam hakika ilikuwa miaka ya wazimu khasa na tukiiga kila kitu cha Kimarekani, kuanzia mavazi hadi muziki wake.

Hizi zilikuwa enzi za ‘’Soul Music,’’ Muziki maalum na makhsusi kwa watu weusi wa Marekani na nje yake.

Si rahisi kwa leo kueleza wazimu uliotukumba wakati tukisikiliza nyimbo za James Brown, Wilson Picket, Ray Charles, Stevie Wonder, Ottis Redding kuwataja wachache katika miziki ya vijana, yaani ‘’Pop.’’

Lakini ilikuwa pia enzi za miziki ya jazz ya wapigaji kama Duke Ellington na waimbaji bingwa kama Nat King Cole, Frank Sinatra, Louis Armstrong, ambayo ilikuwa ikipendwa na wenye umri wa kati na hapa sitaki kuwagusa wanamuziki kutoka Uingereza.

Magazeti tuliyokuwa tukipenda kusoma yalikuwa Newsweek, Time na Ebony gazeti la watu weusi Marekani.

Wengi wetu nami nikiwa katika kundi hilo tulikuwa na ndoto kuwa iko siku tutakwenda Marekani kusoma katika moja ya vyuo vikuu vya huko na wako ambao ndoto zao zikaja kuwa kweli na tuko pia ndoto zikabakia ndoto.

Wamarekani walikuwa na kituo chao cha utamaduni mji ambacho ndani mlikuwa na maktaba na ‘’theatre,’’ sehemu wakionyesha filamu.

Kwa kuwa na vitu hivi Wamarekani walituteka na mimi nilinasa katika dema lile kwani nilikuwa mwanachama wa maktaba ile na nilipofikia makamu ya kuwa naandika katika magazeti ya Uingereza kama Africa Events na New African Mkurugenzi wa United States Information Service alinipa uanachama wa Library of Congress, Washington nikiweza kuazima kitabu au jarida kutoka huko na nikaletewa Dar es Salaam.

Sasa tuje kwa Martin Luther King na mimi.

Mwalimu wangu wa Kiingereza alikuwa mama mmoja wa Kingereza jina lake Mrs. Grant.

Mume wake alikuwa anaitwa Grant na wote walikuja Tanzania katika mpango wa British Council wa kusomesha Kiingereza.

Bwana Grant alikuwa alikuwa akisomesha Chuo Cha Ualimu Chang’ombe.

Mrs. Grant sijui kwa vipi lakini alikuwa mwalimu aliyenipenda labda kwa kuwa nilikuwa na mapenzi makubwa na somo lake lililokuwa linaitwa, ‘’Reading Labaratory,’’ tukifunzwa kusoma kwa haraka, yaani kwa ‘’speed,’’ akiweka, ‘’time clock,’’ kupima unasoma maneno mangapi kwa dakika ngapi kisha kuna maswali unajibu kuonyesha kuwa umeelewa ulichosoma.

Kulikuwa na mashindano ya Elocution Kiingereza na Kiswahili kwa shule zote za Dar es Salam na shule yetu kila mwaka ikishinda katika English Elocution na kuna mwaka tuliwahi kushinda kwa pamoja English na Swahili Elocution.

Nakumbuka mwaka mmoja Swahili Elocution alishinda Athumani Uzigo ambae baadae alikuja kuwa mtangazaji RTD.

Mrs. Grant akaniambia kuwa mwaka ule nitafute passage yeyote niihifadhi kichwani niingie katika mashindano ya English Elocution.

Mwaka wa 1963 ndiyo mwaka ambao Martin Luther King alitoa hotuba yake maarufu, ‘’I have a Dream,’’ Lincoln Memorial, Washington DC.

Nilikuwa nimehifadhi mengi kutoka michezo ya William Shakespeare kama ‘’Julius Caesar,’’ ‘’Merchant of Venice,’’ ambayo wala nisingeihitaji kujifunza kwani tayari nilikuwa nimeshahifadhi na ningeweza kusoma wakati wowote hata nikiamshwa usiku wa manane.

Lakini haya yalikuwa mashindano na nilitaka niingie katika mashindano na mtu mashuhuri kama Martin Luther King siyo na Cassius katika ‘’Julius Caesar,’’ au Shylock katika ‘’Merchant of Venice,’’

Niliamua kumsoma Martin Luther King na hotuba yake ‘’I Have a Dream.’’

Nikitoka nyumbani asubuhi nakwenda shule njia nzima naisoma kimya kimya hotuba hiyo na tulikuwa wanafunzi wengi tunawania nafasi hiyo na kila mtu kachukua chake anachotaka kusoma na sote tutasoma mbele ya mwalimu wetu na mbele ya wanafunzi wenzetu na yule aliye bora ndiye atakaewakilisha shule latika mashindano yale.

Nilishindwa kwa hiyo sikuweza kuiwakilisha St. Joseph’s Convent katika English Elocution.

Kwa nini nilishindwa?

Wenzangu walikuwa wanasema Kiingereza kwa ‘’accent,’’ nzuri ya Kiingereza.

Mimi Mswahili wa Kariakoo ‘’accent,’’ yangu ndiyo iliyonifanya nishindwe.

Picha hiyo hapo chini nimesimama Lincoln Memorial Washington, DC mahali ambako Dr. Martin Luther King alisimama wakati anatoa hotuba yake mashuhuri, ''I Have a Dream.''


55752396_427344678012916_5220900264344551424_n.jpg

Lincoln Memorial Washington DC
54727311_427348544679196_895206059344396288_n.jpg

Library of Congress, Washington DC​
Mkuu@Mohamed Said nimekusoma vizuri sana hapo juu kwenye hilo bandiko lako,unaonekana kwenye lugha ya kingereza upo "Above average" kudos...
 
Tran...
Wapi kaka nababaisha tu.
Ahsante.

Mzee Said naomba Sana uitafute history ya James Brown alivyokuja Tanzania...naambiwa aliimba bure kabisa MnaziMmoja...na wasanii mbali mbali pia...naamini wapo watu unawajua kama huyo uliesoma nae akaenda fanya kazi RTD ambao hawatakosa hiko kipande cha history
 
Mzee Said naomba Sana uitafute history ya James Brown alivyokuja Tanzania...naambiwa aliimba bure kabisa MnaziMmoja...na wasanii mbali mbali pia...naamini wapo watu unawajua kama huyo uliesoma nae akaenda fanya kazi RTD ambao hawatakosa hiko kipande cha history
The Boss,
James Brown aliishia uwanja wa ndege alikuwa anapita njia.
 
Back
Top Bottom