DSTV wana mfumo wa kizamani?

DSTV wana mfumo wa kizamani?

Mnondwe

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2015
Posts
4,012
Reaction score
3,683
Salamu,kwa miaka nimekuwa nikijiuliza maswali mengi kuhusu mfumo wa hawa jamaa wa kuwasha king'amuzi chao.
Kusoma chaneli kinachukua zaidi ya dakika kumi,ukiwa umeunganishwa na extra view ndiyo balaa kabisa.
Azam na startimes wao ukiwasha tu sekunde kumi unaanza kuona.
Je ni mfumo wa kikoloni au nini wajuzi.
 
Ushawahi ona kukiwa na wingu au mvua ikinyesha Dstv inakata mawasiliano kama zilivyo hizo Azam na hao Wachina?
 
kwa elimu yangu ndogo naamini kuwa; mfumo wa satellite wanaotumia dstv ni wakujihami kila dakika code zinbadilika kutoka makao makuu ili wle wachakachuaji washindwe kufanya yao. pia channels zao ni nyingi na zina jiupdate kila muda kwenye system mfano ule mfumo wa EPG kwenye software yao unafanya decorder ichelewe pia kuwaka
 
Ndio mvua ikinyesha Dstv inakata inaanza kuscratch scratch mwishoni inaanza kublink namba kwenye interfacew decorder
Nina almost miaka7 tangu nianze kutumia Dstv kiukweli sijakumbana na tatizo la kuscratch mvua ikinyesha.
 
Shida zaidi ukiondoa football,news na michezo mingine,vipindi vingine ni program za kizaman kwel kwel
 
Bado nalia na bei zao tu mambo mengine nawakubali sana sijawahi juta kuwa nao
 
Ushawahi ona kukiwa na wingu au mvua ikinyesha Dstv inakata mawasiliano kama zilivyo hizo Azam na hao Wachina?
Me natumia Hd dstv huku mvua ikimwaga nazima nawasha azam iko safi 100%
Inapendeza sana[emoji41]
 
Back
Top Bottom