DSTV wamepandisha tena

DSTV wamepandisha tena

sio lazima wote mtumie dstv, hapa ni stiff competition
 
Mi ndo nshawaaga jana walichopokea toka kwangu ndo cha mwisho. Sifanyii kazi kulipa cable mimi. Huduma kwa wateja zenyewe ni kichefuchefu. Wamenifika kooni. Mnisaidie tu nifahamu kuhusu Azam na mie nihamie huko.


Kweli kabisa mdogo wangu. Nilijaribu kufuatilia Azam, bei zao ni kawaida sana. Decoder niliambiwa 93K na malipo ya mwezi ni kawaida. Niliona mengine kama 10K na kuendelea. Sikuona product yenye gharama inayofikia 50K.


DSTV wanahitaji kujipanga upya. Vinginevyo tutarudia enzi zile za kuangalia EPL bar au kwenye vibanda vya uswahilini!!
 
Guys hawa jamaa wananunua leseni kwa dolla..na sie twaona kila siku dola ikipanda..let's argue with facts and reasonings..kama kweli vifurushi vimepanda,they are right guys..


Kinachowazuia kuongea na wateja wao wakawaelewesha ni nini?

Unadhani kutuma tu sms kwamba kuanzia October tupandisha bei inatosha??

Bado wanatakiwa kurudi kwa wateja na kuwajulisha kinachoendelea.
 
  • Thanks
Reactions: bht
Ccm wamelala walisema hakuna.malipo kwa dola sasa kwani moaka iwe dola si inavyothaminishwa ndiyo.malipo.kwadola?eti shilingi imeshuka mbona mafuta hayapandi kila siku?
 
Ndio muda huu sasa wa kuchagua rais atakae simamia nchi, sio wa kutembelea nchi za watu na kutoa majibu mepesi, ya kuogelea na kuvunjilia mbali.
 
199000 was the limit,219 silipi aisee. ngoja nijidemote to compact plus
 
Tanzania kumbuka wameweka VAT mwaka huuu....
Na pia kumbuka dollar ni 2150
Kawaida ni dollar 82 kwa Tanzania ila sababu ya VAT na hiyo Dollar ndo maana inaongezeka hadi hukooo

Vat inakua appliex kwenye commodities na services hio bei niliokutajia hapo imejumuisha VAT kwa huko south africa sema hawa jamaa wanatumia kigezo hicho kulaghai watu VAT ilikua inatozwa tangu muda mrefu sema labda walikua hawajabanwa ila hio bei ya south africa ni pamoja na vat...wajinga ndo waliwao...hata south africa dola 1 ni rand 14 wakati ilikuaga rand 8...kwaio sio tija tanzania wananyonywa kuendekeza....vitu vya nje
 
Vat inakua appliex kwenye commodities na services hio bei niliokutajia hapo imejumuisha VAT kwa huko south africa sema hawa jamaa wanatumia kigezo hicho kulaghai watu VAT ilikua inatozwa tangu muda mrefu sema labda walikua hawajabanwa ila hio bei ya south africa ni pamoja na vat...wajinga ndo waliwao...hata south africa dola 1 ni rand 14 wakati ilikuaga rand 8...kwaio sio tija tanzania wananyonywa kuendekeza....vitu vya nje

Mkuuu nadhani unakosea bishana na mie..
Dstv wao malipo yao ni kwa dollar na kwa hapa Tanzania wanacharge dollar 82 kwa mwezi exclusive of vat......
Vat imeanza rasmi mwaka huu na ndo maana kina azam na startimes wamepandisha bei zao za vifurushi.
Ukipiga hesabu za dollar ambayo ni 2150
Unakuta ni 176300
Ukijumlisha VAT ya 18% 31734
Jumla yake ni 208034
Pia kumbuka kuwa Premier League wamepandisha dau la kuonesha mechi zao, yaani dau wanalolipwa timu limeongezeka msimu huu hivyo lazima dstv nao waongeze...

Mwisho kabisa sio lazima ule mbuzi kama hela yako ni ya dagaaaaaa
 
Mkuuu nadhani unakosea bishana na mie..
Dstv wao malipo yao ni kwa dollar na kwa hapa Tanzania wanacharge dollar 82 kwa mwezi exclusive of vat......
Vat imeanza rasmi mwaka huu na ndo maana kina azam na startimes wamepandisha bei zao za vifurushi.
Ukipiga hesabu za dollar ambayo ni 2150
Unakuta ni 176300
Ukijumlisha VAT ya 18% 31734
Jumla yake ni 208034
Pia kumbuka kuwa Premier League wamepandisha dau la kuonesha mechi zao, yaani dau wanalolipwa timu limeongezeka msimu huu hivyo lazima dstv nao waongeze...

Mwisho kabisa sio lazima ule mbuzi kama hela yako ni ya dagaaaaaa
Umeeleweka mkuu hapa ni swala la mfuko, basi tutakuwa tunaulizia matokeo ya premier.
 
Life's got classes. Japo TCRA wnatakiwa ku regulate haya mambo, lakini wengi wanabeba mizigo iliyowazidi uwezo.
 
Mi wameniletea meseji ya kulipia 147,000/- ! Mi naona tukuze biashara za wazawa tu. Maana, wote tukiitosa DSTV, Azam atadunduliza na atapata mtaji wa kulipia Ligi ya Uingereza mwakani na kutuonesha kwa bei ya hali ya mtu/ bei ya ndugu wananchi.
 
nimeachana na dstv rasmi mwezi wa pili sasa mwanzo nilikuwa nalipia kifurushi cha 56,000 wakapandisha 66,000 then 80,000 SAA hivi itakuwa 100,000 nadhani. ilikuwa dstv compact
 
Wametulisha uongo eti EPL inapendwa mno duniani na sie tukakubali, sasa wanatugeuza wapendavo kwa ujinga wetu. Tuamke kwani Azam na Startimes ndio suluhisho letu.
 
Kwa ninyi walevi mipira mbona kuna channel nyingi tu zinaonyesha mpira free kabisa
 
Back
Top Bottom