Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,322
- 33,128
Ninarudia tena kwa imani ya Dini ya kiislam Dreadlock kwa Wanaume ni Haramu kwa wanawake ni halali. Ninafikiri nimekujibu swali lako. Na ukimuona Muislam anayo Dreadlock huyu Sio Muislam atakuwa ametoka ndani ya imani ya Dini ya Kiislam ndio hivyo kazi kwako kusuka au kunyowa.Ok MziziMkavu. Comment yako ya kwanza nilikuwa nakuelewa ila comment yako hii ndio bado sijaelewa.
Unaposema watu wa imani yangu wengi wenye dreadlocks hawafuati dini una maana gani? Kwenye imani yangu mimi dreadlocks ni alama ya Nadhiri kuwa natural na kuacha attachments za kibinadamu na mtu mwenye Locked hair anaheshima kubwa sana kwetu, inaashiria amejitoa katika tamaa za kimwili, ameweka nadhiri, ana wisdom, na ni mnazareti. Ndio maana tunaacha nywele zitu kama zilivyoumbwa. Mambo ya kuchana nywele ni idea za mwanadamu, ila mwanadamu wa kale aliacha nywele zake bila kuziharibu mpangilio wake. Ila kama wakati nywele zinaanza kujiweka kuwa locks zenyewe tunaruhusiwa kuzitenganisha ili iwe rahisi kuzimaintain na kiwa safi. Ila haitakiwi kutumia kemikali yoyote ile. Hii sio sheria ya imanj yangu tu, ni sheria ya Wayahudi mpaka leo hii Marabi wa kiyahudi huvaa hivyo, ni Sheria ya Ethiopian Orthodox, wasuni wa kiislam pia wapo wenye locks, Watakatifu wa kihindi na monks wa Tibet huamini hivyo. Sijaona imani inayokataa Natural-locks kwa sababu ni Natural thing, you cant ban nature.
Kuhusu mwanaume kuwa mwanamke, wapo wanaume wanaoanza locks saloon na kuzisokota saluni mara kwa mara, hao kwao ni mapambo. Kwa imani yangu hairuhusiwi, kwa sababu they use chemicals. Kumbuka kuna Natural locks na Artificial Locks ni tofauti.
Pia watu wa Imani yangu hawarihusiwi kinyoa ndevu sana maana taratibu za kunyoa ndevu zimeandikwa kwenye Torah. Almost the same with Islam.
I respect all religions na pia nafahamu kikamilifu kuwa NATURAL Dreadlocks zina heshima kubwa katika Imani karibia zote. Soma maelezo mwanzo mwa topic. Asante.