Dr. W. Slaa anaondoka CHADEMA

Dr. W. Slaa anaondoka CHADEMA

Nimezungumza na Dr. Slaa jioni anasema huo ni uzushi. Hajajiuzulu wala walatoki Chadema. Mkewe alipokea simu na kugomba
 
Nimeangalia post zako za nyuma hujawai kuwa mfuasi wa Dr wala Ukawa.
Ufuasi haupo tu kwenye comment mkuu..... upo katika nyanja nyingi ikiwa ni fikra, mawazo, msimamo nk. Pia, katika siasa masaa 24 ni mengi sana kutokea mabadiliko hivyo hata hii inaweza kuwa ni comment yangu ya kwanza kuonesha mabadiliko.
 
Kwa hali ilivyo CHADEMA sasa hivi chama ni bora kuliko mtu yeyote na hakuna maarufu kuliko CHADEMA hivyo hata taarifa hii ikiwa kweli CHADEMA itabaki kama ilivyo sasa, hii ni sawa na ilivyo sasa MAN UNITED kumuuza Vanpas na kumnunua Ronaldo
 
..siwezi kuamini hadi iwe hivyo..ila kama ndivyo...basi nitaamini kuwa dr.Slaa si strategist mzuri....maana kama ataondoka ataua sana nguvu ya UKAWA...na lazima itajulikana kuwa nae alijali zaidi madaraka....na ata provekuwa Mbowe ni zaidi yake ki mikakati...maana Mbowe ameweza kukubali hali halisi kufatana na mazingira yaliyopo...na hata kuamua kugombea ubunge jimboni mwake....Kinachowazuia hawa kina Dr. Slaa kufanya hivyo ni nini???....

...Lazima Dr. Slaa atambue kuwa odds za yeye kushinda uchaguzi mkuu kama angepitishwa UKAWA ingekuwa ndogo sana..maana kwanza alishindwa mwaka 2010...kinacho mfanya afikiri angeshinda this time around dhidi ya magufuli ni nini???..Lazima awe strategist anaefanya maamuzi kwa kufatana na wakati..

...Nilianza kupoteza msimamo wangu dhidi ya Dr. Slaa tangu alipokuwa anaandamwa na ma kesi ya kifamilia....pale alimwacha mke wake wa zamani mama Rose Kamili na kumchukua mke wa mtu mama mshumbusi....Kwa hiyo lazima nae kabla hajafanya maamuzi ya kuondoka chadema atambue kuwa hakuna binadamu aliye perfect...na kwamba siasa hubadilika kutokana na mazingira (kama wanavyosema dynamics za kisiasa)....Mbona wenzak huko chadema wamekubali hali halisi???....napata mashaka na maamuzi yake (kama itakua hivyo)kuyafanya kwa kumsikiliza mamamshumbusi....Hatumtaki rais afanyae maamuzi kwa kumsiliza mkewe....Hata Lowassa aliombwa sana na mkewe asihame ccm lakini alifanya maamuzi magumu.....Maamuzi yaliyowafungua watanzania ma milioni toka vifungo vya kifikra....

Tuweke akiba....tukumbuke mapito.....tusubiri uhakika wa taarifa hizi.....
 
Duh hii kali, usiku!! Anatoroka nchini au!?
CHADEMA wamewatenda vibaya CCM wamebaki kupiga ramli tu.
Hiyo inaitwa 'Snake in the Monkey Shadow' unasogezewa mkono, una concetrate halafu unapojaribu kuusogelea ili kuugonga, unajikuta umekula bonge la kwenzi kutoka mkono mwingine.
 
Kuna watu wamekaa kusumbua akili za watanzania Jana tumeambiwa kigunge naye kamsima Lowasa Leo wengine hao
 
Asante sana strategists wa Chadema kwa hii movie, kwa leo niishie hapo.
 
Manyerere Jackton ujicommit hapa kwa kuchagua adhabu endapo haitatokea.Naprefer upewe Ban hata ya mwezi mzima sio mbaya
 
Ndugu zangu msiwe watu wa kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa,nyie ni watu wa kukibali tu kila lisemwalo. Mtafanyiwa maamzi magumu nyie wenyewe
 
Chagua adhabu ya kueleweka kama unajiamini ata life ban
 
Back
Top Bottom