Dr.W.P.Slaa ndani ya EATV

Dr.W.P.Slaa ndani ya EATV

Atwambie amejipangaje na chama chake ikiwa watachukua hatamu hasa katika kupunguza mfumiko wa bei, watafanya nini juu ya wote walioihujumu nchi hii na wakatufanya tuwepo tulipo sasa.
 
Ni leo jumatano kuanzia 5-7pm LIVE ndani ya kipindi cha HotMix..

Ni nini ungependa kusikia toka kwake ama ufafanuzi upi naa wa jambo lipi ungependa kusikia akiongelea?

Mkuu naomba nisaidie kunifikishia maswali haya kwa Dr Slaa. M4C imeonyesha mafanikio makubwa sana kwa baadhi ya maeneo iliyopita.je kuna mpango wowote wa kufanya oporesheni ya M4C maeneo ya Zanzibar? Maeneo mengi nchini viongozi wa CDM wamewekwa vipindi vya oporesheni sangara Wilaya,Kata na Vijiji.Je hamuoni kuwa kuna haja ya kuwa na viongozi imara waliochaguliwa kikatiba na si kuteuliwa?
 
Mkuu naomba nisaidie kunifikishia maswali haya kwa Dr Slaa. M4C imeonyesha mafanikio makubwa sana kwa baadhi ya maeneo iliyopita.je kuna mpango wowote wa kufanya oporesheni ya M4C maeneo ya Zanzibar? Maeneo mengi nchini viongozi wa CDM wamewekwa vipindi vya oporesheni sangara Wilaya,Kata na Vijiji.Je hamuoni kuwa kuna haja ya kuwa na viongozi imara waliochaguliwa kikatiba na si kuteuliwa?

kama sijakusoma soma!!? hebu niweke sawa mkuu
 
mimi ningependa atuambie wazi wazi kwamba ni ipi itikadi ya chadema? Chadema ikiingia madarakani tanzania itaendelea kupokea misaada toka nje au la?

wewe gamba unataka kujua itikadi ikusaidie nn vua kwanza gamba ndio unaweza kuelewa itikadi za chadema!
 
1) Anamshauri nini JK ili aweze kupunguza mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola ya kimarekani?

2) Ziara za ufunguzi wa matawi nje ya nchi zinafadhiliwa na nani?

3) Ni lini viongozi wa CHADEMA watatangaza mali zao kwa umma wa wa Tanzania?

4) Ni kiasi gani analipwa na CHADEMA kwa mwezi akijumuisha na marupu rupu? Mbali na shughuli za kisiasa, ana shughuli yoyote nyigine ya kiuchumi anayoshiriki?
swali la 4 sijaelewa nafikiri hata yeye hataelewa - mshahara wa nani?
 
Swali kwa docta.,...kwanini aliamua kuvunja ndoa yake na kuamua kumchukua mke wa mtu yaani christina na kuishi naye hali ni mke wa mtu.
wote mnaofaidika na mfumo kandamizi -- wizi wa mali za umma, kujilimbikizia mali as if hamtakufa, u will always be in negative side.

Sisi maskini tusio na kitu tunaoishi kama ndege; leo afadhali na jana tunawaambia tutawaondoa marakakani 2015 - kuleni mkipuliza your days are numbered - hatukubali kuishi Tanzania kama wakimbizi - hizi mali ni zetu sote -- go on DR. Slaa.
 
Ni leo jumatano kuanzia 5-7pm LIVE ndani ya kipindi cha HotMix..

Ni nini ungependa kusikia toka kwake ama ufafanuzi upi naa wa jambo lipi ungependa kusikia akiongelea?

Mda huo wengine tupo ofisini, je tunaweza kupata link ya kuangalia online?
 
swali la kwanza kuna haja yakuwa na mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa wakati kuna mkurugenzi wa wilaya. swali la pili lini chadema wataanza kuwa na wajumbe wanyumba kumi kwa sababu tunaona ccm wameweza kwakuwa wajumbe wa nyumba kumi ndio wanajenga chama hasa wamama sasa chadema wanampango gani kuimalisha chama kupitia wajumbe wanyumba 10.
 
Manataka kujua hilo sakata la yeye kumiliki kadi ya ccm. Na jee! Nikweli huwa anailipia kila mwezi?
 
swali la kwanza kuna haja yakuwa na mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa wakati kuna mkurugenzi wa wilaya. swali la pili lini chadema wataanza kuwa na wajumbe wanyumba kumi kwa sababu tunaona ccm wameweza kwakuwa wajumbe wa nyumba kumi ndio wanajenga chama hasa wamama sasa chadema wanampango gani kuimalisha chama kupitia wajumbe wanyumba 10.
 
Ni maswali mawili ya msingi kwa Dr Slaa.

1. Bavicha karibia wote wameishanunuliwa kwa kuendekeza njaa nani ataisaidia chama kushinda nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu 2012.

2. Kwa nini unakuwa mwepesi wa kukusanya kadi za CCM kwenye mikutano yako huku wewe mwenyewe binafsi kadi yako ya CCM umeificha mchagoni na kuilipia ada kila mwezi.
nepi anayo ya ccj yeye ameificha masaburini au wapi?
 
Ninaomba Dr atueleze.
1) Anaonaje wazo kuwa wanachama wa CDM ambao kwa hekima zao wasingependa kuharibu kadi zao za CCM, ikianzishwa maktaba pale makao makuu ya chama zikahifadhiwa hapo itafaa?
2) Je, CHADEMA inapata msaada wowote wa scholarships kwa ajili ya wanachama wake kupata elimu vyuo vikuu vilivyopo nchi za nje ama hapa Tanzania? Kama zipo utaratibu gani hutumika?
 
Back
Top Bottom