Dr Tulia Ackson Miaka yote aikuwa wapi?

Dr Tulia Ackson Miaka yote aikuwa wapi?

Wakuu natanguliza salamu ,

Naomba kuweka wazi kabisa kwamba mimi ni mwenyeji wa Mkoa wa Mbeya , Wilaya ya Kyela , kijiji cha Kajunjumele ,utamaduni wa Kyela na Rungwe unashabihiiana kwa kiasi kikubwa sana , wakazi wengi wa Wilaya hii ni Wanyakyusa , japo kuna makabila mengine.

Tunazo ngoma za asili ambazo kwa uchache ni Mang'oma , Ipenenga , Samba nk , na tumecheza ngoma hizi kwa miaka mingi bila msaada wa hela ama chochote kutoka kwa yeyote , kama kuna aliyetoa chochote basi alitoa kama vile PDG Ndama Mutoto wa ng'ombe anavyowapa wanamuziki wa FM ACADEMIA .

Sasa cha kushangaza mwaka huu amezuka mfadhili wa ngoma za asili aitwaye Tulia Ackson , Huyu tetesi zinadokeza kwamba lengo lake si kufadhili ngoma za asili , maana alikuwepo miaka yote na alikuwa na uwezo kama huu wa leo , lakini hakufanya hivi , taarifa zinaonyesha kwamba amelenga kurubuni wakazi wa Rungwe ili achaguliwe mbunge uchaguzi ujao .

Mbinu hii ya kizamani haikubaliki , na naomba kuchukua nafasi hii kuwaasa wana Rungwe kumuogopa huyu mama kama ukoma .

Dr Tulia aliyeingia bungeni na kubebwa kwa mbeleko ya chuma hadi kwenye unaibu spika , amekuwa mstari wa mbele kudhalilisha na kunyanyasa wabunge wa upinzani , amezima mijadala mingi yenye tija ili kuokoa chama chake , huyu hawezi kuwa msaada wa Akina Mama wauza ndizi na maziwa wa ushirika au Kiwira , hafai hata kuwa Mwenyekiti wa kijiji cha Makandana , hafai .

Dr Ngunangwa aliwahi kuwauliza waliokuwa wanajipitisha kwenye jimbo lake huko Njombe na kutoa zawadi za baiskeli nk , kwamba WALIKWINA ? yaani kwa kiswahili , MIAKA YOTE WALIKUWA WAPI ?

Nakala ya uzi huu imfikie JOHN MWAMBIGIJA .
Malafysle hizo siasa za kizamani sana.

Akina Dr Mwakyusa walifanya nini Rungwe ? CCM hii iliyoshindwa kwa miaka 60 usitegemee ifanye lolote , nenda Kyela ukaone jinsi msomi Mwakyembe anavyoiteketeza , Mango Tree imekwenda hivi hivi tunaona !
Mwabigija ndo tutegemee nini!
 
mkimpa ubunge huyu dada, nitawadharau sana wanyakyusa.
huyu nakwambia hawezi kushinda jimbo lolote katika mkoa wa Mbeya hata akiroga.

watu wa Mbeya wanamdeku tu anavyocheza "kiboleni" chake!

labda ajaribu mikoa ya jirani huko wapi sijui Songwe, Rukwa, Katavi huko!!
 
Haya mambo yalikuwepo toka siku nyingi tena mashindano hasa .Nakumbuka tulikuwa wadogo tunayaona haya.Naona wewe akili zako zote umejaa siasa kuna watu wanaona mbali zaidi ya siasa , vile vile kufufua ngoma za asili ambazo siku nyingi zilishaanza kusahaulika anatakiwa kupongezwa badala ya kushutumiwa .Badilikeni jamani.


Soma alama za nyakati mkuu.....huyu aliyeandika haya hapo juu ni Mh. Sugu....alisaidiwa na kina Mbiwe kuandika hizi porojo.
 
Wanyakyusa (wote tu wa Kyela na Tukuyu/Rungwe) ni miongoni mwa makabila ya kwanza kwanza kuijua elimu; ukweli nitawadharau sana huyu mkimpitisha kwenye nafsi ya ubunge, ningependa huyu asipewe nafasi hata kwenye ngazi ya chama tu hapo hapo kwao kwanza ili ashike adabu. Mijadara ya maana yote anaitupa kule, anataka watu wawe wanajadiri nini!? Sorry, nae ana PhD
 
Haya mambo yalikuwepo toka siku nyingi tena mashindano hasa .Nakumbuka tulikuwa wadogo tunayaona haya.Naona wewe akili zako zote umejaa siasa kuna watu wanaona mbali zaidi ya siasa , vile vile kufufua ngoma za asili ambazo siku nyingi zilishaanza kusahaulika anatakiwa kupongezwa badala ya kushutumiwa .Badilikeni jamani.
Kuna sehemu hata moja mleta UZI kasema hizi ngoma ni mpya!?
 
Mkuu Erythrocyte, umenikumbusha mbunge wetu wa G 55 Ndembelwa Ngunangwa yupo wapi huyu mshua alikuwa machachari sana?
 
Ngoma nyingi huko kwa wanyaki zimehusishwa na mambo ya uganga na mambo ya kishirikina. Kwa hiyo huyu msomi Acks amechagua kutegemea misukule? Nilipata kusikia ni mcha Mungu sana!
Kwa dhana hii uliyonayo kichwa ni uchaw pia hvyo nawe ni mshirikina
 
Wakuu natanguliza salamu ,

Naomba kuweka wazi kabisa kwamba mimi ni mwenyeji wa Mkoa wa Mbeya , Wilaya ya Kyela , kijiji cha Kajunjumele ,utamaduni wa Kyela na Rungwe unashabihiiana kwa kiasi kikubwa sana , wakazi wengi wa Wilaya hii ni Wanyakyusa , japo kuna makabila mengine.

Tunazo ngoma za asili ambazo kwa uchache ni Mang'oma , Ipenenga , Samba nk , na tumecheza ngoma hizi kwa miaka mingi bila msaada wa hela ama chochote kutoka kwa yeyote , kama kuna aliyetoa chochote basi alitoa kama vile PDG Ndama Mutoto wa ng'ombe anavyowapa wanamuziki wa FM ACADEMIA .

Sasa cha kushangaza mwaka huu amezuka mfadhili wa ngoma za asili aitwaye Tulia Ackson , Huyu tetesi zinadokeza kwamba lengo lake si kufadhili ngoma za asili , maana alikuwepo miaka yote na alikuwa na uwezo kama huu wa leo , lakini hakufanya hivi , taarifa zinaonyesha kwamba amelenga kurubuni wakazi wa Rungwe ili achaguliwe mbunge uchaguzi ujao .

Mbinu hii ya kizamani haikubaliki , na naomba kuchukua nafasi hii kuwaasa wana Rungwe kumuogopa huyu mama kama ukoma .

Dr Tulia aliyeingia bungeni na kubebwa kwa mbeleko ya chuma hadi kwenye unaibu spika , amekuwa mstari wa mbele kudhalilisha na kunyanyasa wabunge wa upinzani , amezima mijadala mingi yenye tija ili kuokoa chama chake , huyu hawezi kuwa msaada wa Akina Mama wauza ndizi na maziwa wa ushirika au Kiwira , hafai hata kuwa Mwenyekiti wa kijiji cha Makandana , hafai .

Dr Ngunangwa aliwahi kuwauliza waliokuwa wanajipitisha kwenye jimbo lake huko Njombe na kutoa zawadi za baiskeli nk , kwamba WALIKWINA ? yaani kwa kiswahili , MIAKA YOTE WALIKUWA WAPI ?

Nakala ya uzi huu imfikie JOHN MWAMBIGIJA .
Katika utamaduni wa wanyakyusa ngoma huwa haziandaliwi na wanawake, mwanamke hushiriki kucheza tu baadhi ya ngoma, ila ngoma za mama huyu zilikuwa za kibiashara zsidi.
 
Hukumbuki alivyokuwa anawasonga makundi mbalimbali yaje kwake eti yakimshauri agombee URAIS. Kila siku ALIKUWA akipokea maandamano. Mara wanafunzi udom waendesha bodaboda nk
hahaha,ilikuwa..kwelii?/
 
Wakuu natanguliza salamu ,

Naomba kuweka wazi kabisa kwamba mimi ni mwenyeji wa Mkoa wa Mbeya , Wilaya ya Kyela , kijiji cha Kajunjumele ,utamaduni wa Kyela na Rungwe unashabihiiana kwa kiasi kikubwa sana , wakazi wengi wa Wilaya hii ni Wanyakyusa , japo kuna makabila mengine.

Tunazo ngoma za asili ambazo kwa uchache ni Mang'oma , Ipenenga , Samba nk , na tumecheza ngoma hizi kwa miaka mingi bila msaada wa hela ama chochote kutoka kwa yeyote , kama kuna aliyetoa chochote basi alitoa kama vile PDG Ndama Mutoto wa ng'ombe anavyowapa wanamuziki wa FM ACADEMIA .

Sasa cha kushangaza mwaka huu amezuka mfadhili wa ngoma za asili aitwaye Tulia Ackson , Huyu tetesi zinadokeza kwamba lengo lake si kufadhili ngoma za asili , maana alikuwepo miaka yote na alikuwa na uwezo kama huu wa leo , lakini hakufanya hivi , taarifa zinaonyesha kwamba amelenga kurubuni wakazi wa Rungwe ili achaguliwe mbunge uchaguzi ujao .

Mbinu hii ya kizamani haikubaliki , na naomba kuchukua nafasi hii kuwaasa wana Rungwe kumuogopa huyu mama kama ukoma .

Dr Tulia aliyeingia bungeni na kubebwa kwa mbeleko ya chuma hadi kwenye unaibu spika , amekuwa mstari wa mbele kudhalilisha na kunyanyasa wabunge wa upinzani , amezima mijadala mingi yenye tija ili kuokoa chama chake , huyu hawezi kuwa msaada wa Akina Mama wauza ndizi na maziwa wa ushirika au Kiwira , hafai hata kuwa Mwenyekiti wa kijiji cha Makandana , hafai .

Dr Ngunangwa aliwahi kuwauliza waliokuwa wanajipitisha kwenye jimbo lake huko Njombe na kutoa zawadi za baiskeli nk , kwamba WALIKWINA ? yaani kwa kiswahili , MIAKA YOTE WALIKUWA WAPI ?

Nakala ya uzi huu imfikie JOHN MWAMBIGIJA .
Msiotaka viti vya kisiasa mmefanyaje kuinua utamaduni wa wanyakyusa?Pungusya mdomo na ubufi mbomba imbombo jiboneke. Tuache uzabina zabina. Huko Kajujumele umefanya nini wewe?
 
Msiotaka viti vya kisiasa mmefanyaje kuinua utamaduni wa wanyakyusa?Pungusya mdomo na ubufi mbomba imbombo jiboneke. Tuache uzabina zabina. Huko Kajujumele umefanya nini wewe?
Karibu Kajunjumele mkuu , sasa hivi ni mavuno tu
 
Wanyakyusa (wote tu wa Kyela na Tukuyu/Rungwe) ni miongoni mwa makabila ya kwanza kwanza kuijua elimu; ukweli nitawadharau sana huyu mkimpitisha kwenye nafsi ya ubunge, ningependa huyu asipewe nafasi hata kwenye ngazi ya chama tu hapo hapo kwao kwanza ili ashike adabu. Mijadara ya maana yote anaitupa kule, anataka watu wawe wanajadiri nini!? Sorry, nae ana pHD
PhD
 
Endelea kutega sikio hapa hapa jf
Akina Dr Mwakyusa walifanya nini Rungwe ? CCM hii iliyoshindwa kwa miaka 60 usitegemee ifanye lolote , nenda Kyela ukaone jinsi msomi Mwakyembe anavyoiteketeza , Mango Tree imekwenda hivi hivi tunaona !
maendeleo ya wanakyela yataletwa na nyie wanakyela wenyewe mkisaidiana na mbunge wenu, sio kila kitu afanye mbunge peke yake, HESHIMA kwa viongozi wenu na wakitaifa kwa ujumla ndio jambo la muhimu kabisa, kazi kwa bidii ndio msingi imara wa maendeleo , si mbowe wala luwassa atakaeleta maendeleo kwenu ni nyie wenyewe kwa bidii na uelewa ulio bora kabisa.
 
Nskubaliana ksbisa na msoni haya.
Wanyakyusa TUAMKE.
Panya anayejamata panya ndio wa kumtuza.
Huyo Mwambigija na hata Sauli ni magharasha.
Kwa Rungwe mbali na kwamba siwakubali CCM. Ila Tulia atawafaa sana watu wa Rungwe. Mbunge ni mtu anayewakilisha watu kwenye kuisimamia Serikali kwenye nchi ambazo ni Republic au kwenye mfumo wetu wa kijinga mbunge ni mtu anayeweza kulobby na kueleweka/kusikilizwa. Tulia anafaa sana kuwa mwakilishi wa Rungwe kuliko Sauli na Mwambigija. Ila Mwambieni huku Mbeya mjini tutaweka unyakyusa pembeni tupo na Sugu.
 
Back
Top Bottom