Elishaosati
Member
- Oct 31, 2010
- 8
- 5
Habari wadau, kwa taarifa za uhakika Dr.Steven Ulimboka anarudi nchini kesho, Madaktari wote na wadau wote mnaombwa kufika uwanja wa ndege saa sita na nusu mchana kwa ajili ya kumpokea jemedari, mtaarifu daktari mwingine!
Aliyekuwa M/kiti wa Jumuiya ya madaktari MAT anarudi leo siku ya Jumapili saa saba mchana kutoka Africa kusini alipokuwa akiendelea na matibabu, baada ya kutekwa na kuteswa vibaya na watu wanaosemekana kuwa hawajulikani. Akizungumza na wanahabari Katibu wa Jumuiya hiyo anasema kuwa leo kuanzia saa tano mchana madaktari wote pamoja na wanafamilia na wapenda haki wote tutakuwa viwanja vya ndege vya kimataifa vya mwl. Nyerere kwa ajili ya kumpokea kamanda wetu Dr. Steven Ulimboka.
Source Clouds radio