Elections 2010 Dr. Slaa umebeep, watanzania sasa wamepiga!

Kaka nakushukuru kwa taarifa hiyo, ni kweli uliyoongea n nayaombea kwa mwenyezi Mungu. Nashangaa watu wanaotaka kuona tunaendelea kuishi hivi kwa kunifaisha matumbo yao. Taratibu tutafika .....Mimi mwaka huu silali mpaka nipige kura piga ua labda nife ili waibe zoooote.
 
Kama amebeep anaweza asipigiwe simu. kuna watu ukiwabeep hawapigi.

True man, ila inategemea na aliebeep, ukiona missed call jina JK ofcoz kupiga itakua mgogoro maana unajua utasikia nyimbo zilezile ila kwa Jina kama Dr SLaa kupiga muhimu unajua utapata maneno ya mbolea.
 
Ni kweli mtaalam!watanzania sasa wamebadilika wanataka kuona mabadiliko katika uongozi .Yatakayowaletea watandania maendeleo katika nchi yao, iliyo mikononi mwa mafisadi!
 
CCM wanaweweseka sana mwaka huu, ila wataisoma namba october 31.
 
True man, ila inategemea na aliebeep, ukiona missed call jina JK ofcoz kupiga itakua mgogoro maana unajua utasikia nyimbo zilezile ila kwa Jina kama Dr SLaa kupiga muhimu unajua utapata maneno ya mbolea.

hii nimeipenda.
 
kabeep kapigiwa na vocha kawekewa, naona mnajidanganya, kikwete akubali kuichia ikulu???????? ha ha ha haaaaa!!!!!!!!!!
impossible, afiche wapi uso wake kwa dunia nzima wakati amejiaminisha kuwa anapendwa sana???
 
Big up dr. Slaa, kura yangu nimeshakupa tayari, ole wao ccm waiibe watanieleza vema
 
Ushauri wangu kwa Dr. Slaa, KAMA ALIWA’BEEP WATANZANIA, BASI WAMEAMUA KUMPIGIA, HAWABAHATISHI, AZIDISHE KAMPENI, NA AJIANDAE KUINGIA IKULU.

Hapo umenena Mkuu.....................
 
Ushauri wangu kwa Dr. Slaa, KAMA ALIWA’BEEP WATANZANIA, BASI WAMEAMUA KUMPIGIA, HAWABAHATISHI, AZIDISHE KAMPENI, NA AJIANDAE KUINGIA IKULU.

Nawakumbusha CCM na maneno ya Lula wa Ndali-Mwananzela kuwa “Mbinu ya vyombo vya dola kutumia nguvu kuzima mabadiliko zimeshaonyeshwa mara kadhaa kushindwa. Zimeshindwa Zimbambwe, zimeshindwa Ukraine, zimeshindwa Kenya, zitaendelea kushindwa kwani kila zama zina mashujaa wake na kila shujaa ana ujumbe wake”.

Kwanza nimekuvotia "senks" halafu naona watu wasome maneno yako ya busara tena na tena na tena. Yaani ame"beep" sisi tunampigia...ungejua utamu ulivyotiririka kwenye medulla oblangata yangu na kutokea kwenye cerebrum na cerebellum....mambo ya voluntary actions tayari Slaa kura yangu kanasa! We acha tu!!!!
 
Tatizo lilipo ni kuwa si wote waendao ktk mikutano ni wapiga kura,na tz ni zaidi ya watu mil 40 lakini wapiga kura ni mil 19,na %kubwa waliojiandikisha ni wwanavijiji(najua hilo kwani niliandikisha moro mjini) na kule vijijini kama malinyi ulanga wanajua kuwa Raisi bado ni nyerere na hata kura yao watampigia huyo nyerere najuwa wasomaji hamtaamini hili lakini kwa sisi tunaokaa vijijini ngoilanga mahenge tunajua hili,sasa sijui kama kuna mbinu zimetumika kuwabadilisha %kubwa ya wapiga kura walioko vijijini kuwa tunahitaji mabadiliko? tutaweza vuna wabunge wengi toka upinzani sina uhakika na urais.
TUNAWATAKIA CHAGUZI NJEMA,KWANI HATUNA FURSA YA KUPIGA KURA​
 
Aisee sijatoa SENKSI siku nyingi, lakini imebidi nigonge kile kitufe.

The Following 34 Users Say Thank You to zumbemkuu For This Useful Post:


... Sinkala (Today), ...
 
Mbio za sakafuni huishia ukingoni...Mtashangaa siku ya mwisho kwani ilikuwaje enzi zile za Mrema...wafuasi niwengi sana lakiniwapigakura ni wachache....CCM for 2010 read my words hakuna cha DR slaa wala cousin wake Dr Slaa.....Lets Go CCM Na tulenge JUU Thats out Motto@.

xoxo BM

Pigia CCM peke yako ni haki yako. Heshimu haki ya wengine tunaokueleza wazi kuwa tutampigia slaa. Wizi wa CCM umedhibitiwa na utadhibiwa
.
 
Pigia CCM peke yako ni haki yako. Heshimu haki ya wengine tunaokueleza wazi kuwa tutampigia slaa. Wizi wa CCM umedhibitiwa na utadhibiwa
.


mkuu hao mavuvuzela hawajui hatima yao Dr.Slaa akiingia ikulu coz wanategemea fadhila za kupewa ukuu wa wilaya na usimamizi wa miradi ya kifisadi.
 
Back
Top Bottom