Dr Slaa na Zanzibar

Dr Slaa na Zanzibar

Ukitaka kugundua kuwa wazanzibari ndio waelewa zaidi pima toka ulipoanza uchaguzi wa kwanza mwaka 1995 utagundua kwamba wazanibari ni watu wenye uelwa mkubwa sana na hata hawajalala kama munavyodhania angalieni mapinduzi ya kisisa yalivyotokea zanzibar halafu pimeni na bara hasa bara sio pwani maana hata pwani watu wengi walishaanza kuvichagua vyama vya upinzani kama znz hii inaonesha wazanzibari ni kiio cha watanganyika kuyaendea mapinduzi ya kisiasa na kiuchumi.
Mkuu, kwa nia njema kabisa naomba unieleweshe umesema 'hata pwani watu wengi walishaanza kuchagua vyama vya upinzani kama zanzibar', ni pwani ya wapi hiyo??? Na ukisema kama zanzibar unamaanisha pemba au unguja?
Fafanua tafadhali pwani yenye kuchagua upinzani na unguja yenye kuchagua upinzani.
 
Muandishi umeona hapo red ? Mi naweza kusema zanzbar ni part ya jamuhuri ya muungano lakini sio wa tanzania,kwa sababu muungano wa nchi mbili ni ulikuwa unaitwa hivi jamuhuri wa muungano wa tanganyika na zanzibar.

Sasa kilichofanyika ni kwamba tanganyika imeitwa tanzania sawa na kuita zaire CONGO,so unaponiambia ni part ya jamuhuri ya tanzania inamaaa tumo ndani ya tanaganyika.

Ndio maana tumekibadilisha kile kipengele cha katiba kuwa zanzibar n nchi ina mipaka yake ,wengi ya watanganyia wakifahamu na part ya jamuhuri ya tanzania lakini so hivyooo.

kweli hapo kwenye nyekundu nilikosea nitarekebisha nashukuru kwa msaada wako zanzibar ni nchi kamili na mipaka yake ahsante naomba tuoendelee na mjadala
 
Mkuu, kwa nia njema kabisa naomba unieleweshe umesema 'hata pwani watu wengi walishaanza kuchagua vyama vya upinzani kama zanzibar', ni pwani ya wapi hiyo??? Na ukisema kama zanzibar unamaanisha pemba au unguja?
Fafanua tafadhali pwani yenye kuchagua upinzani na unguja yenye kuchagua upinzani.

Nikisema pwani namaanisha DAR (Mfano jimbo la temeke, kigamboni) wapinzani walianza zamani kupata haya majimbo na kule mtwara na lindi yote ni powani hio
 
Chadema ikiwa kitakuja zanzbar kuleta sera naamini kitaungwa mkono kwa rais wa jamuhuri ya muungano kupata kura, kwanini ? Kwa sababu kwanza ni chama kilichopata nguvu sana bara kuliko CUF,so utakuta hata tukimteuwa lipumba kuwa rais wa jamuhuri ya muungano ni nothin tu,kutokana bara bado hakina nguvu,mi ka mimi ningetoa kura yangu kwa slaa kwa rais kutokana na sera zao,na vile wananguvu sana bara ili tuweze kuitoa CCM.

Kwa upande wa wabunge ni vigumu kupata zanzibar kwani hawatotetea maslahi ya zanzbar kwa vile sio wazawa wa zanzibar na wenye machungu na zanzibar,lakini pia wataungwa mkono sana zanzibar kwa vile nia yetu ni moja ya kuitoa CCM madarakani kwani nusu karne sasa hivi CCM wameshindwa kuondoa tatizo la umeme na maji kuwa ndio tatizo sugu kwetu.

salaam kwa chadema

KWA VILE tuna muungano huu wa sehemu mbili,na zanzbar ingawa na uchache wetu lakini tunaweza kutikisa tanzania kwa uchache wetu,niwapa ushauri pia waje zanzibar kuleta sera zao lakini pia sera hizo ziwanufaishe wazanzibari wapate haki zao za msingi.

Ikiwa tutafanya maandamano ya kweli na kushirikiana na nyinyi tanganyika kwa makosa kama hayo ya kupinga wanayofanya CCM basi naamini sauti itasikika zaidi na lengo litapatikana.

chadema badili mfumo wenu,tambueni kuwa,tutakapo badilisha katiba tunataka kuwe na silimia hamsini zanzbar na hamsini tanganyika hatujali uchache wala wingi,sasa ikiwa utapa nguvu zanzibar ujue umeramba dumeee..

Na kama utakwepa zanzibar ujue utaishia sakafuni mbio zakoo.
 
Si rahisi kwa Chadema kufikiria kufanya kampeni au kuelekeza nguvu Zanzibar. Hiyo inatokana na mfumo wao walijiwekea na malengo yao yapo tofauti kabisa na Zanzibar.

Mfumo wao mkuu ni ukanda, Ukabila na Udini kitu ambacho kinawawia vigumu sana kufikiria Zanzibar.
HIZO NI KAULI ZA MA-KADA WA CCM. Nawewe ni mmoja wao?
 
Wazanzibari ndio waelewa zaidi? Waelewa wa nini? Kuolewa na CCM ndio uelewa? Laiti mngejua mlivyousaliti upinzani usileta porojo zako hapa.

ni waelewa zaidi wa siasa huoni walivyotulia sasa nyinyi ndio kwanza mnauwana, wazanzibar wamewatangulia waTanganyika, humo mnamopita leo nyinyi Watanganyika Wanzanzibar wapita zamani sana.
 
Zanzibar ni sehemu ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania (Yaani muunganiko wa nchi mbili ya Zanzaibar na Tanganyika) katika kupitia habari nyingi kutoka kwenye vyanzo mbali mbali vya habari nimegundua kwamba Dr Slaa pamoja na chama chake cha Chadema huwa siwasikii kuyaongelea sana masuala ya Zanziabar na hata hizo harakati zinazofanyika Tanganyika yaani upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano hazihusishi sana upende wa pili wa Muungano yaani Zanzibar je kwa mtazamo huo, Tunaweza kusema ya kwamba Chadema na uongozi wa Chadema hawana habari na Zanzibar. kwa nini Chadema wasipeleke nguvu zao Zanzibar maana naamini Zanzibar kama upande wa pili wa muungano chadema haijulikani kama vile CCM na CUF.(nao pia wanahitaji kusikia sera zao, kwa nini wanawatenga wanzanzibari)

Naomba kuwasilisha.

Ni kupoteza muda wa wananchi wa Mwanza au Bukoba kuongelea masuala ya Zenji. Wakiwa Zenji wataongelea ya huko.
 
Kwanini Wakuu mnapenda kutumia matusi na maneno ya kashfa badala ya kujadiliana kwa hoja.

Sielewi kwanini watu wakubwa na wasomi wakajifikisha hivi katika ustaarabu wa kujadiliana.

Mada nzuri lakini wengine kwa umri wetu tumesita kwa kuhofia kutukanwa na vijana wetu.

Hebu tujirekebisheni Wakuu, huu ni ukumbi wa Great Thinkers msisahau.
 
Habari wana Jamii..?
Nilikuwa nimetoka kidogo, nilikuwepo Disneyland Paris kwa mapumziko mafupi lakini nimerejea tena. Suala la muungano tulionao ni tete na hakuna mtanzania anauelewe isipokuwa tumewekewa viini macho na serikali iliyopo madarakani. Muundo sahihi ambao zamani kidogo Mtikila aliwasilisha hoja ni ya kuwa na serikali tatu, dhana ambayo inaungwa mkono na Chadema. Iwepo serikali ya Tanganyika, Zanzibar na Tanzania. Yapo mambo kama vile ulinzi, fedha, mambo ya nje, uhamiaji, Afya na mambo yote ya social security services ziende eneo la muungano. Mengine yaliyobaki yabakie Tanganyika na zanzibar. Awepo waziri mkuu wa Tanganyika, awepo rais mmoja wa Tanzania na awepo Chief minister wa serikali ya Zanzibar. Mnasemaje hapo?
Mabadiriko haya lazima yaanzie kwenye katiba bila hivyo tunakokwenda ni kubaya zaidi maana generation ya sasa ni kizazi chenye kutaka mabadiriko.
 
Si rahisi kwa Chadema kufikiria kufanya kampeni au kuelekeza nguvu Zanzibar. Hiyo inatokana na mfumo wao walijiwekea na malengo yao yapo tofauti kabisa na Zanzibar.

Mfumo wao mkuu ni ukanda, Ukabila na Udini kitu ambacho kinawawia vigumu sana kufikiria Zanzibar.

Hamad Rashid na hoja rojorojo!!
 
Yakhe tuna historia tofauti.Zanzibar mna dini moja na tamaduni moja hilo ni jambo zuri.Ila,kuna watwana(wamakonde,nyamwezi,shiraz)halafu kuna waarabu wa pemba(oman).CUF ni PEMBA PEOPLES PARTY ambayo haifuati sheria ya muingereza bali wanyamwezi ambao wana uhusiano wa damu sio wa kirafiki na watwana wa huko!CCM huko ni sawa na AFRO tu yakhe! imebidi mkubali tu kushindwa vibaraka wenu huku bara hawana la maana!
Kwa hiyo ndio hivyo yakhe mambo ya kojani huku bongo hayalipi,kajiungeni nawangazija au kwa blaza bashir!

Vizuri Yakhe ukaangalia na upande wa pili wa shilingi. Wa Bara au watanganyika mna makabila mengi sana zaidi ya tisiini lakini mna dini kuu mbili tu Yaani Ukristu na Uislamu.

Wakristu ndio waliosoma zaidi na kushika vyeo vya juu wengi na waislam wengi ni madereva na tarishi.
Kwa sasa waislam nao wamesoma na wanataka uongozi sasa ukivunjika muungano hali itakuwaje? nahisi kutakuwa kama kule Nigeria. Jonathan analindwa na wanamgambo wa kikristu
 
Habari wana Jamii..?
Nilikuwa nimetoka kidogo, nilikuwepo Disneyland Paris kwa mapumziko mafupi lakini nimerejea tena. Suala la muungano tulionao ni tete na hakuna mtanzania anauelewe isipokuwa tumewekewa viini macho na serikali iliyopo madarakani. Muundo sahihi ambao zamani kidogo Mtikila aliwasilisha hoja ni ya kuwa na serikali tatu, dhana ambayo inaungwa mkono na Chadema. Iwepo serikali ya Tanganyika, Zanzibar na Tanzania. Yapo mambo kama vile ulinzi, fedha, mambo ya nje, uhamiaji, Afya na mambo yote ya social security services ziende eneo la muungano. Mengine yaliyobaki yabakie Tanganyika na zanzibar. Awepo waziri mkuu wa Tanganyika, awepo rais mmoja wa Tanzania na awepo Chief minister wa serikali ya Zanzibar. Mnasemaje hapo?
Mabadiriko haya lazima yaanzie kwenye katiba bila hivyo tunakokwenda ni kubaya zaidi maana generation ya sasa ni kizazi chenye kutaka mabadiriko.

Cha masingi ni kuujadili huu muungano kwa kina kwa pande zote kisha mapendekezo yote yaliyokubaliwa na pande zote ndio yawekwe kwenye katiba. Kinyume cha hapo hakuna kitu Wazanzibari tutaonewa tu na huo mburuzano sorry muungano
 
Si rahisi kwa Chadema kufikiria kufanya kampeni au kuelekeza nguvu Zanzibar. Hiyo inatokana na mfumo wao walijiwekea na malengo yao yapo tofauti kabisa na Zanzibar.

Mfumo wao mkuu ni ukanda, Ukabila na Udini kitu ambacho kinawawia vigumu sana kufikiria Zanzibar.
Ahsante wewe umewajibu ipasavyo hawa Wagalatia wa CHADEMA kwao wao sio siasa wala mapambano ni Ukabila, Uzawa, Udini ndio unao wasumbua si unamuona Padre Slaa alivyo ni udini uliomjaa hata haya hana, hivi kuiacha Zanzibar kuisemea na kuitetea hata ziara hafanzi sio yeye wala Huyo Dj Mbowe wameiacha Zanzibar solemba sawa na Wasubiri waendelee na Kejeli zao za kijinga zilizo wajaa ambazo zimewafikisha hata UTU Kuusahau ya kuwa lau sio CUF iliovunja amri ya Mapuri 2001 ya kuvitaka vyama vya upinzani visubiri kufanya siasa hadi 2005 na CHADEMA na Vyama vyengine vikafyata ni CUF ILIOTOWA DAMU NA ROHO ZA WAFUASI WAKE NA KUIRUDISHA SIASA PAHALA PAKE, LEO CHADEMA WAMEKAA KAMA PUNDA KULIPA MALIPO KWA KUTOWA UPEPO
 
Back
Top Bottom