Dr Slaa na njama ya kukwepa kodi

Dr Slaa na njama ya kukwepa kodi

Status
Not open for further replies.
Maskin Ritz yaani unaangaika kufunika yalyowatokea makada wenu wauza sembe kwa kufoji ishu na kutajataja jina la Dr. Slaa hivi CCM Dr wa ukweli mnamtaja mara ngapi?
 
Nadhani hakuna anayepinga ili jambo la kujenga hospitali watu wanachapinga ukwepaji kodi.

Hiyo kodi unayozungumzia ni bidhaa zipi na aina gani ya kodi? tunapozungumzia kodi kuna:
1. ushuru wa forodha
2. kodi ya ongezeko la thamani (VAT)
nk.

Katika sheria ya kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ya mwaka 1997, kuna mambo ambayo kwa kiingereza wanasema:
1. taxable supplies - which includes standard rate (18%), zero rated and special relief (which is either 100% or 45%)
2. Exempt supplies
3. Out of scope.

Ritz nakuomba umtafute mtu yoyote aliye mtaalamu wa masuala ya kodi akushauri na hatimaye utakapokuwa umeelewa ni aina gani ya kodi inayokwepwa basi utuletee hayo matokeo humu. Kwa jinsi ninavyoona kwa mbali ulicholeta hapa kinaweza kuwa utaratibu wako wa kawaida wa kuhangaika na maisha ya Dr. Slaa hata kwa gharama ya kusema uwongo.

Kama taasisi inayotaka kujenga Hospitali itaomba msamaha wa kodi basi itaomba kwa mujibu wa sheria kodi ya nchi hii. Na kama anakwepa basi taasisi hiyo na wahusika watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria ya nchi. Wewe ulichokileta bado hakijakamilika na hapo hapo unadai ukwepaji wa kodi. Hapo hapo unazungumzia uagizaji wa vifaa na vifaa vyenyewe hujabitaja ili tujue kama kweli vinalipiwa kodi na kodi hiyo ni ya aina gani.
 
Ritz umekurupuka mno kwa kubashiri kitu ambacho hakijatokea ukiongozwa na hisia zako. Jaribu kusoma posts za kina Pasco, Mkirua na malcom2 hapo juu kwa umakini ujitafakari upya.

Kama ni urafiki kati ya Dr Slaa na Askofu haihalalishi thread hii.
 
Last edited by a moderator:
Sijaona uthibitisho kwamba amekwepa kulipa kodi, au mleta mada anafanyakazi TRA, tuletee uthibitisho basi!!!!!!
 
Ritz huu uzi si ulishagautoa humu au umesahau, au leo umekosa cha kuandika kuhusu DR.Slaa? maana wewe na Hamida tumeshawazoea.
 
Upo sahihi mkuu umenena kweli. Hiyo ni njama ya waziwazi ya kukwepa kodi. Hivi wewe kwani unawaamini hawa viongozi wa chadema wanachokisema hadharani ndicho hali halisi

Hiyo njama unaiona kweli au kwa sababu ya buku za Lumumba unaunga mkono hoja.
 
Sijaona uthibitisho kwamba amekwepa kulipa kodi, au mleta mada anafanyakazi TRA, tuletee uthibitisho basi!!!!!!

Hahaaa.. Ritz amesema anaweka picha Dr. Slaa akikwepa kodi pamoja na wajapani na Askofu...Ukisikia kuingia choo cha kike ndiyo huku. Kila siku wanapost utumbo hapa leo tumemkamata sehemu mbaya na hachomoki hapa na propaganda zake za Lumumba.

Hata wenzio kina HAMY-D na Lizaboni wamestuka wameshaingia mitini.
 
Last edited by a moderator:
Ritz huu uzi si ulishagautoa humu au umesahau, au leo umekosa cha kuandika kuhusu DR.Slaa? maana wewe na Hamida tumeshawazoea.

Kumbe ndiyo kirefu cha HAMY-D???
 
Last edited by a moderator:
chama umeona jinsi nchi inavyoliwa;
na ukifuatilia hata hao wageni watakuwa aliingia kwa
mwavuli wa dini.

Hapa hajaingia ikulu siku akiingia hiyo misamaha ya kodi
itasambazwa kama njungu.
 
Last edited by a moderator:
inawezekana kabisa unachosema kikawa kweli,but take heed to words.watanzania wengi tunaiunga mkono cdm,sikwasababu ya uadilifu,na usafi wa viongozi wao no(nahapa simaanishi kuwa viongozi wacdm ni wachafu kama unavyotaka kutuaminish ila nayapa maneno yako bennefit of doubt.nikwa sababu ccm ni janga linalo tishia kusambaratisha nchi yetu wakati wowote.nakatika hili tunasema,nyinyi ccm ambao mmeishathibitika kuwa hamfai,lazima mpishe.ikija cdm nayo ikabronga tutaihukumu acodingly.sijui kama naeleweka!ccm lazima mpishe,mengine tutajadiliana baadae.
 
Wanaukumbi.

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema, Dr. Slaa anapenda sana kujinasibisha kwamba yeye ni mzalendo wa kupindukia, anayechukia vitendo vya ufisadi na anayeionea huruma nchi yetu.

Taarifa za uhakika kabisa zinathibitisha kwamba mwishoni wa mwezi Juni, mwaka 2013 Dr.Slaa na Mchumba wake walitembelewa na kundi la Wapani wapatao 20 nyumbani kwao Mbweni, Kinondoni ambapo wote kwa pamoja walikula cha jioni.

Dhumuni la ugeni huo wa Wajapani, ilikuwa ni kuthibitisha kama kweli Chadema kina mpango wa kujenga hospitali kubwa ya kisasa katika eneo la Mlalakuwa Dar es Salaam, Wajapani hao ndiyo walipangwa au kuteuliwa kujenga hospitali hiyo, wameakikishiwa pamoja na mambo mengine ya kimaslahi yao makampuni yao mengine, kwamba msimamizi wa hospitali hiyo ndiyo atakayekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015, kwa maana ya Dr. Slaa.

Mipango yote ya kujenga hospitali hiyo, inaratibiwa na Askofu mmoja anayemiliki Kanisa lake maeneo ya Kawe, Dar es Salaam, Askofu huyo amekuwa akifanya safari za Japani akiwa ameandamana na mchumba wa Dr. Slaa, Josephine, mpango unafanyanyika vifaa vyote vitakavyoingizwa kutoka Japani vipitie mikononi mwa Kanisa ili tu visitozwe kodi na serikali.

Ni Dr.Slaa huyu huyu, ambaye miaka michache iliyopita alitangaza orodha ya aibu ya mafisadi pale Mwembe yanga, leo hii anawakimbia Mamlaka ya Mapato nchini TRA.

Kukwepa kulipa kodi ni kosa kubwa sana kisheria. Huyu mzee hana tofauti na akina mama Rwakatale wanaotumia kanisa vibaya huku akiuza madawa ya kulevya. Haiwezekani kuigeuza nyumba ya ibada ni pango la kupitishia magendo yake. Huyu ndie rais mtarajiwa wa makamanda! Mungu atuepushie hatari kubwa hii inayokuja na kuchafua taifa letu. Nilikuwa nasikia kuwa huyu mzee na wahaini wengine ndio waliokuwa wanasafirisha 'MALIASILI' zetu kinyemela kuzipeleka ulaya hasa ITALY na baadae wanaenda na kupewa vijimisaada kwa mgongo wa kanisa. Sasa naamini hazikuwa allegations ila ni ukweli mtupu.
 
564850_451742318204638_1389975028_n.jpg
 
Afadhali umekiri dr slaa atakua rais 2015 umeanza kupona na kale ka ugonjwa wako
 
chama umeona jinsi nchi inavyoliwa;
na ukifuatilia hata hao wageni watakuwa aliingia kwa
mwavuli wa dini.

Hapa hajaingia ikulu siku akiingia hiyo misamaha ya kodi
itasambazwa kama njungu.

chama kafanyakazi nzuri sana. Lol!
 
Last edited by a moderator:
kwani vifaa vya hospital huwa vinalipiwa kodi?
Ritz embu jipange upya.
===hata ile biashara ya sembe hailipiwi kodi!
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom