Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 3,129
- 4,285
Dr. Slaa ana matatizo ya kisaikolojia...
Kwa hiyo, yale majimbo waliyoshinda ccm pale moshi tuseme kuwa wanaccm walipigiwa kura na wakwere kwa kuwa akina kinabo na Kweka wako chadema wote.
Tuambie Kwa nini mmewasahau watu wa mtwara, ndo mada ya uzi huu.
dr. Slaa ana matatizo ya kisaikolojia...
Kwanza karibu,
Mada ni vurugu za mtwara, hoja ni kwa nini watu wa mtwara wametelekezwa? Tatu, kwa nini mnaficha mikataba ya kuchimba gesi yao? Je, lini mtayaweka hadharani?
huyu mzee anahangaika tu amechoka kuchochea suala la kuchinja sasa kahamia kwingine,swali dogo hivi mzee slaa na jk nani aliyejitenga na mungu,kwa sababu mzee slaa aliasi dini na kufanya uovu mwingi ndani ya kanisa sasa uko wapi uadilifu wa slaa.
Rais Jakaya Kikwete anapaswa kuomba hekima kwa Mwenyezi Mungu kutokana na matukio yanayotokea sasa nchini.huyu mzee anahangaika tu amechoka kuchochea suala la kuchinja sasa kahamia kwingine,swali dogo hivi mzee slaa na jk nani aliyejitenga na mungu,kwa sababu mzee slaa aliasi dini na kufanya uovu mwingi ndani ya kanisa sasa uko wapi uadilifu wa slaa.
Hivi kwa nini mnataka kuleta machafuko? Kwa nini Dr Slaa anasema atahakikisha nchi haitawaliki?
Kwa hiyo nyie watu wakaskazini ndiyo mnawakumbuka watu wa Mtwara?
Jenerali Ulimwengu aliuliza hili swali pale Movenpic kama kuna aliyekuwa na idadi ya kura za urais kwa kila jimbo kila mtu kimya! Kweli labda ua unaweza kufichua makubwaHizo kura laki 2 za znbar nazo unahesabu? Kwa taarifa yako jk aliiba kura zaidi ya million moja. Mimi naamini siri itafichuka tu huko tuendako.
Parochial thinking and arguing at the dimension of your nose. Kwanza unalazimisha timing na tamko la nchi haitawaliki ili ukidhi matakwa yako ambayo nachelea kuyahita devilish. Kuenedelea kugangania kauli ya nchi haitawaliki ni kutaka kuficha udhaifu wa serikali unaoonekana mchana kweupe. Kauli hiyo ndiyo inafanya polisi wambambike mtu kichwa cha mtu, wapakie bhangi kwa gari la polisi/umma, washiriki kusindikiza bidhaa ya magendo ili kukwepa kodi, wapige watu wasio kuwa na hatia virungu na mabomu? Nguvu nyingi ya vyombo vya dola inatumika katika vitu vya ajabu badala ya kutumi elimu, ethics na skills kulinda usalama wa raia. Nimesahau utoshwaji wa twiga na meno ya ndovu. Hii yote ni kauli ya Dr.Slaa? Kama ni kweli basi nchi hii haipaswi kuwepo
Ni jambo la busara wananchi kuchoma ofisi na nyumba za watu ili kudai kunufaika na rasilimali za nchi yao; hapa kunahitajika elimu kwa serikali kutowazuia wananchi kuchoma nyumba na ofisi za watu. < MAKUBWA HAYA DAAAH>KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema Rais Jakaya Kikwete anapaswa kuomba hekima kwa Mwenyezi Mungu kutokana na matukio yanayotokea sasa nchini.
Alisema hali inayotokea sasa ni matokeo ya wananchi kupuuzwa na kutokusikilizwa katika suala zima la uwekezaji unaofanyika sehemu mbalimbali za nchi. Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana katika kijiji cha Giroda Babati vijijini, wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika ziara yake ya siku tisa ya ujenzi wa Chama mkoani Manyara.
Kabla ya kutoa kauli hiyo Dk. Slaa aliwaomba wananchi wasimame kwa muda wa dakika moja, kuomboleza vifo vilivyotokea mkoani Mtwara.
Aliongeza kuwa kuendelea kuwapuuza wananchi wa Mtwara ni kuendelea kucheza na jipu linalopaswa kutumbuliwa na kwamba njia sahihi ni kukaa na kuwasililiza wananchi katika uwekezaji na kufikia muafaka pasipo kutumia nguvu. Alisema wanachotaka wananchi wa Mtwara ni kujua namna watakavyonufaika kwa kile alichoeleza kuwa katika uwekezaji wowote wanufaikaji wa kwanza wanapaswa kuwa wananchi.
Alisisitiza kuwa katika hali ya Mtwara kulihitajika busara za kawaida za kutatua msingi wa tatizo badala ya wananchi kupigwa mabomu, risasi na kisha kukamatwa.
Ni jambo la aibu kuwapiga mabomu wananchi wanaodai kunufaika na rasilimali za nchi yao hapa kunahitajika elimu ya kuwafahamisha haki zao ni zipi na siyo mabomu.,alisema Dr Slaa.
Source:Tanzania Daima.
Mbona unataka kuwapangia watu vitu vya kuongea hii ni forum acha watu wafunguke.
Jenerali Ulimwengu aliuliza hili swali pale Movenpic kama kuna aliyekuwa na idadi ya kula za urais kwa kila jimbo kila mtu kimya! Kweli labda ua unaweza kufichua makubwa
WEWE unahitaji msaada wa mambo 5 tu ili uwe huru nayo ni;
1.fikira pevu,
2.msimamo thabiti juu ya mambo ya kijamii yenye maslahi chanya kwa wazalendo.
3.upeo wa hekima na adabu,
4.kukataa roho y akukataliwa,
5.Kujifunza kwa bidii misingi ya haki,utu na demokrasia ya kweli.
TAFAKARI CHUKUWA HATUA.
sina dini ila namwamini mungu mmoja wangapi mnaenda kanisani na misitini halafu waovu wakubwa.
Kwa hiyo watu wasiokuwa watumishi wa kanisa au misikiti wamejitenga na mungu? ushauri wa Dr ndio suluhisho la kidiplomasia na si risasii..listen them! Kuwe na transparency kwenye mikataba watu waelewe faida zake...simple! USHIRIKISHAJI UMMA-Maendeleo kwa kila mtu!
au umesahau Mtwar wengi ni CUF na slogan yao inasema HAKI SAWA KWA KILA MTU!!
WEWE unahitaji msaada wa mambo 5 tu ili uwe huru nayo ni;
1.fikira pevu,
2.msimamo thabiti juu ya mambo ya kijamii yenye maslahi chanya kwa wazalendo.
3.upeo wa hekima na adabu,
4.kukataa roho y akukataliwa,
5.Kujifunza kwa bidii misingi ya haki,utu na demokrasia ya kweli.
TAFAKARI CHUKUWA HATUA.
Hivi kwa nini mnataka kuleta machafuko? Kwa nini Dr Slaa anasema atahakikisha nchi haitawaliki?
Kwa hiyo nyie watu wakaskazini ndiyo mnawakumbuka watu wa Mtwara?
Nakushauri huo msaada wako wapelekee Bavicha.