Dr. Slaa kumjibu askofu Gwajima

Dr. Slaa kumjibu askofu Gwajima

Status
Not open for further replies.

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
25,990
Reaction score
25,384
Kuna tetesi kuwa huenda Dr Slaa akaibuka wiki ijayo kumjibu askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima. Dr Slaa anamtuhumu mtumishi huyo wa Mungu kumleta Laigwanan Lowassa ndani ya UKAWA hivyo kumnyima fursa ya kugombea urais kupitia muungano huo wa vyama vya siasa.

Majibu ya Dr Slaa yanakuja baada ya kimya cha muda mrefu tangu askofu Gwajima alipoanika hadharani ukweli kuhusu Dr Slaa kustaafu siasa. Inadaiwa kwamba Dr Slaa amechukua muda mrefu kwa kuwa kwanza alikuwa akitafuta bomu kali la kuja kulipua.

Kwa sasa Dr Slaa yupo nchini Marekani akipumzika na mchumba wake Josephine Mushumbushi.

Awali askofu Gwajima alitahadhalisha kwamba atalipua bomu kali sana endapo Dr Slaa atajitokeza hadharani kumjibu. Haifahamiki mwanasiasa huyo mstaafu amejiandaa kiasi gani kupangua hoja za Gwajima ambazo zina ushahidi wa kutosha. Ni suala la kusubiri na kuona jinsi alivyojiandaa kujibu hoja.

MAONI YANGU
Naomba watanzania wenzangu tutulize mawazo yetu kwenye kampeni; tusiyumbishwe kamwe.

:yield:
 
Dr.slaa alianza kutuhumu naakajibiwa na Askofu Gwajima.Kwasasa, labda angekuja na jambo jingine tofauti na lile aliloongea Serena hotel,
 
Hebu tupishe bwana na vibabu vyako vilivyochakaa kwa mihogo, watu tuko bize kumpunga shetani aondoke atuachie nchi yetu tule maziwa na asali kutoka Monduli.

Ah no..., ngoja...mchumba? Father Cassava ana mchumba?
 
Dr. Slaa asiwe tu kapewa shinikizo na mkewe. Atumie akili yake maana inaonekana kama ameiazimisha siku zinavyokwenda.
 
Dr Slaa Akijibu Bishop Atamuumbua Mchana Kweupe
 
Gwajima alimtahadharisha Kama akija tena ataeleza pesa alizopewa na sisiemu,Lini na bank gani ziliingia.
 
  • Thanks
Reactions: aye
MI'm baya sana jamaa wamefrizi hela zote kwny akaunti yake anaishi km matonya us anachangiwa hadi dola tatu tatu aibu aiiibuuuu
 
Aje tu alipe fedha za siisiieem alizokula. Aliwaahidi kummaliza Legwanani kumbe akamwongezea sifa. Sasa yupo kwenye chati ya juu kabisa mpaka Lumumba wanalia mbwataaa.
Nasikia kaandaliwa chopa kuzunguka nchi hii ya malofa kuwaeleza jinsi raha ilivyo kule Marekani. Kishasahau mihogo hali tena. Kama usaliti ni mtamu kiasi hiki, basi alijitahidi kuliko kungojea za kutukanwa kila uchwao.
Cha muhimu, asjisumbue kupambana na Legwanani kwani yule ndio chaguo letu. Alivyo ndivyo tulimkuta na ndivyo tutampeleka Ikulu
 
Kama anataka kutunza ka heshima alikobakisha atulie, ila kama anataka aimalizie aje abwabwaje atakuwa anazomewa hadi na watoto njiani.

Kwa wale wenye kumbukumbu Quinine alimpigania sana Slaa uchaguzi uliopita ila alichofanya hakikubaliki.
 
Last edited by a moderator:
Kama anataka kutunza ka heshima alikobakisha atulie, ila kama anataka aimalizie aje abwabwaje atakuwa anazomewa hadi na watoto
usimzibe mdomo mkuu hiyo siyo demokrasia...hata kama wewe hutakubaliana nae kuna watu bado tunaamini falsafa zake licha ya kutuita majina yanayowapendeza nyie
 
Slaa alinde heshima ndogo iliyobaki, anaweza akaizamisha akawa kama kina mwigulu.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom