Dr. Slaa: Kukimbia bunge hakusaidii

Dr. Slaa: Kukimbia bunge hakusaidii

mkuu kwani nani amekataa kuwa kufagia ofcni kwa makene hapo ufipa kunalipa vizuri kuliko kazi yangu mm hapa lumumba? hongera sana mkuu msalimie boss wako makene but nipigie pande na mm nipate day waka hapo ufipa tuje tusaidiane kupga deki. HIYO OFISI NI KUBWA HUUMII MGONGO?
aaah!
 
Kwa kweli kama ni wwazalenmdo wajizulu wafuate mfano wa MWANAUMER wa uingereza sio kulia lia hapa./ Siasa wameifanya Ajira ndio maana!
Ngoja bunge liishe hivi karibuni.
Tutataka kujua majumuisho ya ujinga huu waliotuonyesha.
 
With due respect kwa Dr Slaa anamuonea Mbowe ambaye siku hizi ni zombie, non-entity. Mchokozi ni Mbatiya aliyeteuliwa ubunge na Kikwete sijui wamemtoa wapi, anaapiza kupambana na Magufuli huku akitoka mijasho. Nadhani wapinzani wamechanyikiwa.
UKAWA hawana wa kumlaumu kwa umbumbumbu unaoonekana kukithiri.
Ni katika Tanzania tu ndo tunsona wapinzani, kugomea uwanja wa majadiliano.
Mbaya zaidi hawaelewi kuwa HAWANA UBAVU wa kumtosa refa, Dr Tulia.
 
Dr Slaa amelonga kutoka huko Canada aliko.

Amesema kulikimbia bunge kwa mbinu za kulikwepa, ati kumpinga Dr Tulia Ackson kwa uonevu, hakusaidii upinzani katika malengo mapana.

Kulingana na gazeti la Raia Mwema toleo la June29~July2, 2016, Dr Slaa amesema msimamo huo ungekuwa na maana kama UKAWA ungekuwa na nguvu ya wingi bungeni.

Dr Slaa amesema alikuwa KUB katika bunge la Tisa na Kumi, na amekuwa bungeni toka bunge la Nane.

Amesema,
"Kambi rasmi ya upinzani daima tulitambua uchache wetu, na hivyo kwa kutambua hili, hatukuwahi kufanya maamuzi, kwa mfano ya kumsusia Spika, kwa kutambua kuwa hata kama hatumtaki, hatuna wingi wa kutosha kumkataa"

Dr Slaa amesema mbaya zaidi ni tamko la Mbowe ati kupambana na serikali, tamko alilolitoa Kahama, Shinyanga, hivi karibuni.

Matamshi hayo, Dr Slaa amesema si ya kisiasa kwa mwanasiasa makini.
Dr Slaa amesema tangazo la mapambano na serikali haliko katika shughuli za kawaida za kisiasa, kulingana na Sheria na 5/1992, na hivyo basi ukianza mapambano na dola mtu utegemee consequences.

MY TAKE
UKAWA huo ushauri wa bure toka kwa "kichwa" wa upinzani nchini.
Sasa hivi UKAWA hakuna uelekeo unaoeleweka, kazi kwenu.
Nenda kamwambie hata yeye kukimbia Nchi sio Suluhisho
 
Mkuu Ukawa wajiuzulu kabisa ubunge kuonyesha udhati wao kumpinga Dr Ackson.
Kwa sasa wanacheza makida makida, mchezo wa kitoto.

Sijawahi kuona mtu makini anayemwomba fundi aondoshe breki katika gari lake kwa vile zinachelewesha safari yake. Hiyo itakuwa haraka ya kuwahi kifo. Hiyo ndiyo dhana ya checks and balances ktk multi partism
 
Kwa kweli kama ni wwazalenmdo wajizulu wafuate mfano wa MWANAUMER wa uingereza sio kulia lia hapa./ Siasa wameifanya Ajira ndio maana!

Kujiuzulu ni kukubali kushindwa pambano!

Na nani kawaambia ukiwa mbunge basi mapambano yanaendeshwa ukiwa ndani ya jengo la bunge pekee?

Tuna siku 365 kwa mwaka ambazo kila mmoja anapaswa kuzitumia vilivyo kulingana na anachokifanya

Kwa wabunge kwa mwaka wana takribani mikutano kama minne hivi (ya kukutana Dodoma ndani ya jengo) yenye takribani siku zisizozidi 80 kwa ujumla wake

Sasa chukua 365 - 90 = 275. Maana yake nje ya mbunge, wabunge wana siku zaidi 270 ktk mwaka kufanya kazi zao za kibunge!!

Na nadhani tuache upotoshaji wa makusudi kwa wabunge wa UKAWA wamesusia vikao vya bunge.

Ukweli ni kuwa wana mgogoro na NS na wamekubaliana kutoshiriki kikao chochote atakachokuwa anakiongoza yeye mpaka pale mgogoro kati yao na yeye utakapokuwa umemalizika!!

Na taratibu zimefuatwa kikamilifu ili kufikia hitimisho la kuumaliza mgogoro huo. Kilichopo ni kuchezwa kwa mchezo tu wa kisiasa na nyinyi huku mlio nje mnaucheza tu pasipo kuelewa!!

Wabunge wa UKAWA waendelee na kazi yao, kama Dr Tulia hajakalia kiti watashiriki kikamilifu kwenye vikao vya bunge, kwenye kamati zote za bunge watashiriki kikamilifu. Na nje ya bunge wabunge wa UKAWA watafanya shughuli zao za kibunge kama kawaida

Hakuna kujiuzulu, mchezo unaendelea hadi aoneshe uongozi wake kikamilifu!!
 
Muda wa bungebla bajeti ndo unaypypma, hebu mtupatie majumuisho ya mafanikio ya mgomo wenu.

Kwa akili ndogo tu tena ya kawaida, CCM huwa wanapongeza kitu kinachofanywa na mpinzani, pale wanapoona kwamba kinawasaidia. ndio maana na wewe umeleta haya malalamiko ya Dr. Slaa - huo unaoitwa "ushauri". impact unayoiuliza mojawapo ni hiyo jitihada kubwa sana ya ninyi wapiga filimbi, kupigia kelele sana kwamba wanachofanya UKAWA hakina maana na haikifai. kingekuwa kweli hakifai, wala msingepiga kelele hivyo!

Jiulize, huyo Naibu Spika kukailia kiti kile mfululizo, kuna impact gani? maana kwa kawaida kuna Spika, Naibu Spika, wenyeviti, na wote huwa wanafanya kazi pamoja. sasa Spika hayupo - anatibiwa India, Wenyeviti wamepigwa ban, sasa hizo shughuli zingine ambazo anatakiwa kuzifanya Naibu spika kwa niaba ya Spika, na kwa niaba yake mwenyewe, ambazo sasa hivi hazifanyiki ili kupambana na UKAWA. Jiulize impact kwa afya yake, kufanya kazi hiyo mfululizo, na kuacha zingine zote. Jiulize psychological impact kwa kila siku unasusiwa, unaingia watu wanaondoka, hata kama amekula jiwe usoni, kuna vitu vinaungua ndani yake.

Taasisi nzima ya Bunge sasa inayumba, kutokana na jitihada kubwa za kudeal na UKAWA. na kama panic tactics, imekuja ban ya kuwazuia kuongea na wananchi waliowachagua, ambayo ni kinyume na katiba na sheria ya vyama vya siasa. kwa hiyo kuvunja huko sheria kwa serikali, ni mojawapo ya impact ya action ya UKAWA. na kwa kuwa serikali inavunja katiba na sheria halali, hiyo inaweka rekodi mbaya na kuiweka serikali katika wakati mgumu, na hii itajitokeza baadaye. kwa hiyo hizo kelele zenu ni dalili tosha kabisa kwamba mmekalia moto, matako hayatulii. toka lini mkawa na uchungu na mafanikio ya UKAWA???
 
Kwani wao walipelekwa bungeni na huyo tulia?sisi wapiga kura ndiyo tuliyo watuma bungeni na hivyo tupo nao na tuna wapongeza kwa wanacho endelea kufanya

Nyie wangapi?
 
Ni vema nyie mlio na akili nyingi mkafanya tathmini ya matokeo ya kukimbia bunge mpaka sasa imeisaidia vipi Ukawa.
Chamuhimu Ni to think straight sio swala la akili nyingi. Ukiwa na uwezo wa kutumia akili sooote tunatakiwa kupima jinsi tulivyopoteza kwa kutoshirikishwa woote kwenye bajeti. Kumbuka mengi yanayofanywa sasaivi ndiyo yaliyopigiwa kelele na wabunge walionje! Elimu bure,matumizi bora ya pesa za serikali,ukusanyaji kodi madhubuti,safari holela,kugawiana vyeo kwa vigogo nk.
wake up and think straight,avoid been derogatory!!
 
Kwa akili ndogo tu tena ya kawaida, CCM huwa wanapongeza kitu kinachofanywa na mpinzani, pale wanapoona kwamba kinawasaidia. ndio maana na wewe umeleta haya malalamiko ya Dr. Slaa - huo unaoitwa "ushauri". impact unayoiuliza mojawapo ni hiyo jitihada kubwa sana ya ninyi wapiga filimbi, kupigia kelele sana kwamba wanachofanya UKAWA hakina maana na haikifai. kingekuwa kweli hakifai, wala msingepiga kelele hivyo!

Jiulize, huyo Naibu Spika kukailia kiti kile mfululizo, kuna impact gani? maana kwa kawaida kuna Spika, Naibu Spika, wenyeviti, na wote huwa wanafanya kazi pamoja. sasa Spika hayupo - anatibiwa India, Wenyeviti wamepigwa ban, sasa hizo shughuli zingine ambazo anatakiwa kuzifanya Naibu spika kwa niaba ya Spika, na kwa niaba yake mwenyewe, ambazo sasa hivi hazifanyiki ili kupambana na UKAWA. Jiulize impact kwa afya yake, kufanya kazi hiyo mfululizo, na kuacha zingine zote. Jiulize psychological impact kwa kila siku unasusiwa, unaingia watu wanaondoka, hata kama amekula jiwe usoni, kuna vitu vinaungua ndani yake.

Taasisi nzima ya Bunge sasa inayumba, kutokana na jitihada kubwa za kudeal na UKAWA. na kama panic tactics, imekuja ban ya kuwazuia kuongea na wananchi waliowachagua, ambayo ni kinyume na katiba na sheria ya vyama vya siasa. kwa hiyo kuvunja huko sheria kwa serikali, ni mojawapo ya impact ya action ya UKAWA. na kwa kuwa serikali inavunja katiba na sheria halali, hiyo inaweka rekodi mbaya na kuiweka serikali katika wakati mgumu, na hii itajitokeza baadaye. kwa hiyo hizo kelele zenu ni dalili tosha kabisa kwamba mmekalia moto, matako hayatulii. toka lini mkawa na uchungu na mafanikio ya UKAWA???
Mkuu acha uongo, serikali ni lini ilimzuia Mbowe kuandamana jimboni kwake?
Anachukua mtatizo ya chama chadema na kufanya fujo Kahama!
Hizo mbinu ni mjinga tu hawezi kudadavua.
 
Kujiuzulu ni kukubali kushindwa pambano!

Na nani kawaambia ukiwa mbunge basi mapambano yanaendeshwa ukiwa ndani ya jengo la bunge pekee?

Tuna siku 365 kwa mwaka ambazo kila mmoja anapaswa kuzitumia vilivyo kulingana na anachokifanya

Kwa wabunge kwa mwaka wana takribani mikutano kama minne hivi (ya kukutana Dodoma ndani ya jengo) yenye takribani siku zisizozidi 80 kwa ujumla wake

Sasa chukua 365 - 90 = 275. Maana yake nje ya mbunge, wabunge wana siku zaidi 270 ktk mwaka kufanya kazi zao za kibunge!!

Na nadhani tuache upotoshaji wa makusudi kwa wabunge wa UKAWA wamesusia vikao vya bunge.

Ukweli ni kuwa wana mgogoro na NS na wamekubaliana kutoshiriki kikao chochote atakachokuwa anakiongoza yeye mpaka pale mgogoro kati yao na yeye utakapokuwa umemalizika!!

Na taratibu zimefuatwa kikamilifu ili kufikia hitimisho la kuumaliza mgogoro huo. Kilichopo ni kuchezwa kwa mchezo tu wa kisiasa na nyinyi huku mlio nje mnaucheza tu pasipo kuelewa!!

Wabunge wa UKAWA waendelee na kazi yao, kama Dr Tulia hajakalia kiti watashiriki kikamilifu kwenye vikao vya bunge, kwenye kamati zote za bunge watashiriki kikamilifu. Na nje ya bunge wabunge wa UKAWA watafanya shughuli zao za kibunge kama kawaida

Hakuna kujiuzulu, mchezo unaendelea hadi aoneshe uongozi wake kikamilifu!!
Wanatingisha kibiriti wakati kimejaa! Wanaleta utani kwa wananchi waliowachagua. Kama Wkeli ni wanaume wajiuzulu kwani wanatupotezea wakati tuachague wapinzani wengine wenye nia ya dhati ya kuwaletea wananchi wao maendeleo. Sisis hatuna muda wa kupoteza . Wasichojua UKAWA ni kuwa MUDA ni MALI pia! KWani wanadai kama posho hawapati lakini muda wetu je?????? yaani hii haikubaliki hata kidogo?!?!?! Tulia yuko pale kwa muju=ibu wa Sheria badala kupambana nae kwa hoja wao wanatoka nje. Hawakututendea haki hata kidogo. Eti Bado wana muda siku 365. Wanatuamabia nini kwa hiypo Mh. Tulia akiendesha Bunge kwa siku 365 hawataingia watangojea tena siku 365.No Hatutaki watu wa kutupoetezea muda!
 
Slaa akimuacha Josephine ndiyo nitaanza kumsikiliza. Kwa kuwa busara zake zitakuwa zimerudi
 
Dr Slaa amelonga kutoka huko Canada aliko.

Amesema kulikimbia bunge kwa mbinu za kulikwepa, ati kumpinga Dr Tulia Ackson kwa uonevu, hakusaidii upinzani katika malengo mapana.

Kulingana na gazeti la Raia Mwema toleo la June29~July2, 2016, Dr Slaa amesema msimamo huo ungekuwa na maana kama UKAWA ungekuwa na nguvu ya wingi bungeni.

Dr Slaa amesema alikuwa KUB katika bunge la Tisa na Kumi, na amekuwa bungeni toka bunge la Nane.

Amesema,
"Kambi rasmi ya upinzani daima tulitambua uchache wetu, na hivyo kwa kutambua hili, hatukuwahi kufanya maamuzi, kwa mfano ya kumsusia Spika, kwa kutambua kuwa hata kama hatumtaki, hatuna wingi wa kutosha kumkataa"

Dr Slaa amesema mbaya zaidi ni tamko la Mbowe ati kupambana na serikali, tamko alilolitoa Kahama, Shinyanga, hivi karibuni.

Matamshi hayo, Dr Slaa amesema si ya kisiasa kwa mwanasiasa makini.
Dr Slaa amesema tangazo la mapambano na serikali haliko katika shughuli za kawaida za kisiasa, kulingana na Sheria na 5/1992, na hivyo basi ukianza mapambano na dola mtu utegemee consequences.

MY TAKE
UKAWA huo ushauri wa bure toka kwa "kichwa" wa upinzani nchini.
Sasa hivi UKAWA hakuna uelekeo unaoeleweka, kazi kwenu.
Kwani Dr. ameshatoka honeymoon au kaachiwa na yule Baby?????????????????????na yeye yuko chama gani kwa sasa???????????
Maana kama CHADEMA hatutaki hata kumsikia Msaliti aungane na mwenzake na wenzake pia.
 
Wanatingisha kibiriti wakati kimejaa! Wanaleta utani kwa wananchi waliowachagua. Kama Wkeli ni wanaume wajiuzulu kwani wanatupotezea wakati tuachague wapinzani wengine wenye nia ya dhati ya kuwaletea wananchi wao maendeleo. Sisis hatuna muda wa kupoteza . Wasichojua UKAWA ni kuwa MUDA ni MALI pia! KWani wanadai kama posho hawapati lakini muda wetu je?????? yaani hii haikubaliki hata kidogo?!?!?! Tulia yuko pale kwa muju=ibu wa Sheria badala kupambana nae kwa hoja wao wanatoka nje. Hawakututendea haki hata kidogo. Eti Bado wana muda siku 365. Wanatuamabia nini kwa hiypo Mh. Tulia akiendesha Bunge kwa siku 365 hawataingia watangojea tena siku 365.No Hatutaki watu wa kutupoetezea muda!

Unajua ukizungumzacho kweli wewe?

Well, Tulia yuko pale kwa mujibu wa sheria.

Hawa usiowataka wewe wapo pale kwa mujibu wako kwani?...Watoe sasa!!

Jishughulishe kidogo kufahamu chanzo cha mgogoro wa wabunge hao na NS halafu uje tujadiliane

Vinginevyo naona kama tunabishana na mtu mwenye mahaba yasiyo na macho wala ufahamu asiyeona wala kuelewa chochote!!
 
Back
Top Bottom