Majungu mengine bwana, mimi ni mtu wa kutoka Iringa, kaka yangu anaishi Mbeya na alikua na tatizo kubwa sana la jicho la kushoto, alishughulikiwa kwa muda mfupi sana tu, kwanza ilikuwa tumpeleke Mwezi december baadhi ya rafiki zetu wa Dar wakatwambia (Nadhani walikuwa wana hisi, hawakuwa na uhakika) mwezi huu madaktari wengi wa kihindi wameenda kwao kwa mapumziko so tulirudi mwezi February ana alipata matibabu bila ubaguzi wowote, Mleta hoja siku nyingine uwe unakuja na ushahidi na sio kuja na Cooked data hapa.
Huko nyuma tuliwahi kuaminishwa kuwa Nyerere ndiye aliyefuta mahakama ya Kadhi nchini, ukweli huu uliendelea sana hata nami nikauamini but siku Kikwete anahutubia sherehe za Idd-el Fitri pale Dodoma nilimsikia akisema, "Nchi hi haijawahi kuwa na mahakama ya Kadhi, waliokuwepo ni maliwali ambao walihukumu bila kuzingatia dini ya mtu bali sehem husika, yaani kama kwetu Iringa walihukum kwa kuzingai uenyeji tu" Kuanzia wakati huo nimekua pro active kusikiliza malalamiko ya watu hasa wanapolenga kumchafua mtu au Chama hasa cha upinzani.