Elections 2010 Dr. Slaa Jangwani katika Picha

............. Karatu hana lolot jipya kaleta. Yaaani hana mpya yoyote....
Kwani JK wakati anaingia Ikulu 2005 aliacha kipya gani Chalinze? Eleza japo viwili tu.
Kukusaidia tu, JK amekuwa mbunge wa Bagamoyo (chalinze iliwepo) kwa miaka ishirini.
1. Aliacha shule moja ya serikali (Lugoba Sec ambayo yeye alisoma middle School)
2. Kituo cha afya kibovu, hakina gari, tabibu wala dawa
3. Shule za Msingi 11 kwenye jimbo lenye kata 6
4. Vijana wakipoteza mwelekeo, wengi wakikimbilia kuuza korosho barabarani na kutengeneza magenge ya wezi na majambazi
5.Barabara za vijijini zisizopitika iwe kiangazi au wakati wa Masika
6
7
8
Kulinganisha Miaka 15 ya Rais Slaa Karatu na miaka 20 ya JK Chalinze ni sawa na kulinganisha umakini na Usanii
 
Kazi si wanafanya mafisadi ndiyo wanaojazwa mapesa? au umesahau?

Rostam miaka michache iliyopita hakuwa bilionea sasa baada ya kufanya vizuri kazi zake ni bilionea wa kutupa. Mkapa, Mkono, Karamagi, Manji, Subhash, Mzindakaya, wale wa EPA na wengineo wote hawa miaka michache iliyopita hawakuwa mabilionea lakini sasa kutokana na kazi zao nzuri sana ndani ya chama twawala wamekuwa mabilionea katika muda mfupi sana na wavuja jasho wa Watanzania, wakulima na wafanyakazi wanalipwa kiduchu mazao yao bei wanalaliwa haya ukilinganisha na nchi jirani wanashindwa kujikwamua kuachana na umaskini eti kwa sababu wanaambiwa nchi ni maskini lakini wakati huo huo Viongozi wanaishi kwa kutanua tena kwa sana tu kuliko hata katika nchi tajiri duniani.

CCM si baba yako wala mama yako hata Mwalimu aliwahi kusema hivyo kwa kuona inaelekea kule ambako yeye hakuona kama ni kwa maslahi ya nchi bali kwa mafisadi wachache ndani ya CCM.

Amka uyaone maovu ya CCM ndani ya Tanzania ambayo yanadidimiza maendeleo ya nchi badala ya kuendelea kuwapigia debe mafisadi.


Haya mkuu. Subiri mtu aje achukue pesa za mafisadi awapeni. Sina ziada.
 
sasa kama ulijua siyo lugha yako kwanini uliidandia? ulidhani ukiandika kiingerza ndo utaonekana una hoja? shwain

Hapa tunaongelea Slaa. tukija kwenye kidhungu, utakaa kimya wewe na shwain wenzako, msiongee wiki nzima!. Weka hoja ya Slaa tu.
 
Alafu we mtu, nchi huwa haiendeshwi kihuni namna hiyo. Kwamba nikitaja leo kuwa Keil ni kibaka basi unatakiwa utiwe ndani! Nina wasi wasi kama ndiyo mnafikiria huyo jamaa yenu atakuwa hivyo basi mmepotea. Nchi ni system ambayo inafanya kazi kwa ndani na kwa kushirikiana na kimataifa. Mtu haweze kimbilia Uswizi ukaaanza sema yuko wapi mbona hammkamati? Unataka kuleta mambo ya Kagame na generali wake aliyeko South Africa? Sasa hivi itamtokea puani. Kwa kifupi bwana Keil, nchi inaendeshwa kwa mpangilia wa kisheria. Siyo kukurupuka tu asubuhi ,,,, oohhh, hii ni list ya mafisadi wakamateni! Utakuwa uhuni huo. Na kama mtu wenu anawaambia hivyo hapo ndiyo anazidi kuongezea alama za kutokuwa anafaa hata Ubunge!
Kweli wewe hamnazo!! Yaani nimejikuta nacheka bila kutaka. Hivi ni kifunguu gani cha sheria kinachosema mtu akiiba, unampa mda arudishe kile alichoiba, na akirudisha on time unamsamehe? Nina hamu kweli ya kuwa mwanasheria ili niyajue haya. Maana nakumbuka pale JK alipowapa miezi mitatu mafisadi wote wawe wamerudisha hela waliyoiba, na kama wasingerudisha angewapeleka mahakamani. Nafikiri Rostam atakuwa alirudisha ndiyo maana hakushitakiwa.

Pia nakumbuka pale JK aliposema anayo orodha ya wafanyabiashara wa madawa ya kulevya. Wasipojirekebisha atawachukulia hatua kali. Nakumbuka pia JK aliposema rushwa haizuiliki, kitochi ni lazima. Tafadhari KN niambie ni sheria gani iliyokuwa inafuatwa katika kutoa maamuzi haya? Hivi mtu kaiba bilions unampa muda wa kurudisha, halafu akirudisha amesamehewa. Wakati kibaka akichomoa simu ya elfu ishirini hata akikamatwa na kuirudisha, bado sheria inachukua mkondo wake? Halafu ni sheria gani inayomruhusu Rais kupanga matumizi ya pesa bila kupitishwa na bunge? Kwa mfano hela ya EPA aliamua kuiingiza kwenye kilimo, hata mgawanyo wake hatujui ulikuwa vipi, wala hakututajia kwamba zilirudishwa bei gani! Yaani ni burudani kwelikweli. Ni vile tu Tanzania ina bunge chovu. otherwise alikuwa apigiwe kura ya kutokuwa na imani naye.
 
Ila nimeshangaa kuona kuwa kuna watu ambao wako busy kujaribu kumponda Dr Slaa kwa hiyo wakiona thread yoyote wanaingia na kuandika Hate speech, lakini nataka kufanya observation: Law of Universe inasema the more you talk about someone the better, ndo unamwongezea nguvu, hata kama unamwongelea mabaya, kama wanavyosema wadhungu haterz are ur secret fans!! Hahahaha!
 
wewe keil, hujui unaongeaje na unaongea katika hanga hizi. Ni hiari yako, anyway. Lakini jamaa yenu slaa kwisha bin mufulisi. Karatu hana lolot jipya kaleta. Yaaani hana mpya yoyote. Ataaibika sana na kupoteza umaarufu wake wa bungeni hivi hivi. Chukua maneno yangu. Si kweli kwamba ccm ni mafisadi, ila kuna watu mafisadi ambao wanashughulikiwa squarely right now. Wanachama wa chadema ni mafisadi zaidi. Yeye mwenyewe slaa, mbowe na wenzake wakina komu just to mention a few. Nitawapa mafile yao soon. Subirini tuanze kampeni. Niwafungue macho yenu muone nyuchi (uchi) zao.

who cares who the hello are you,umeishiwa hoja you go into personals ,
ivi hata kama umetumwa huoni kuwa unaisaliti nchi yako shame on you
 
Na ushahidi ulidhihirisha kwamba wale wote waliotajwa Dr ni mafisadi, lakini tukirudi kwa Kikwete kuna ushahidi chungu nzima wa kuonyesha ubabaishaji wake hadi Watanzania kumpa jina la msanii.
Ndio ni Watanzania ila ungekuwa more specific kuwa ni wana CCM wenzake walimwita msanii kwenye ile thread yao!
 
Ila nimeshangaa kuona kuwa kuna watu ambao wako busy kujaribu kumponda Dr Slaa kwa hiyo wakiona thread yoyote wanaingia na kuandika Hate speech, lakini nataka kufanya observation: Law of Universe inasema the more you talk about someone the better, ndo unamwongezea nguvu, hata kama unamwongelea mabaya, kama wanavyosema wadhungu haterz are ur secret fans!! Hahahaha!
Ha ha ha haaaaa wao wanadhani haters wanapojazana humu kumsema vibaya Slaa ndiyo wanammaliza, hawajui kuwa mara nyingi publicity ya mtu haikuzwi na pro wake hukuzwa na wapinzani wake, kina MS, KN, Tumaini, Kiranga & co. kama hawalijui hilo basi kazi tupu.
 
Duh! I don't know of what happended right now! But I gave all the weaknesses of slaa, Mod have have removed them!. strange as it is! I previoulsy have an idea that JF is a platform where we dare talk openly. I never knew that it is a platfom where Chadema dare talk openly! And for the same reasons, I will never be back on this platform. However, at this juncture, I have no means to convince you that Slaa he is unfit for anything except for MP position. The mass of Tanzania know it all, and we know it all. Keep on dreaming and goodluck


I might have some indifferences with the trend and intricasies of Dr Slaa's candidancy lakini hili la kuwa mbabaishaji I say BIG NO. Dr Slaa is one among few credible candidates for leadership positions we have ever had. Find some other flaws lakini not hili la ubabaishaji. Na pia acha kutumia the so called the mass of Tanzanians kuhalalisha ur personal opinion kwani unajua wazi the state of our mass when it comes to the issue of knowing our leaders real competence and so their character.

omarilyas
 
Dar hamna kitu. wamemshtukia kuwa mbabaishaji tu
Tofauti ya hawa waliokuja hapa na wale wanakuja kwenye mikutano ya CCM ni moja. Wanaokuja kwenye mikutano ya CCM husombwa kwenye Maroli na kuvalishwa Fulana na kofia za bure pamoja na kupewa pilau za Amira!!

Pia Mikutano ya CCM hutangazwa sana na vyombo vya habari na kuhamasishwa kwa kutumia mfumo wa Dola. Hawa walikuja hapa wenyewe bila ya kusombwa wala kufuata maslahi yao binafsi.

Haijawahi kutokea kwa CHADEMA kujaza watu wengi kama hawa kwenye uwanja wa Jangwani!!
 
Wewe Keil, hujui unaongeaje na unaongea katika hanga hizi. Ni hiari yako, anyway. Lakini jamaa yenu Slaa kwisha bin mufulisi. Karatu hana lolot jipya kaleta. Yaaani hana mpya yoyote. Ataaibika sana na kupoteza umaarufu wake wa bungeni hivi hivi. Chukua maneno yangu. Si kweli kwamba CCM ni mafisadi, ila kuna watu mafisadi ambao wanashughulikiwa squarely right now. Wanachama wa Chadema ni mafisadi zaidi. Yeye mwenyewe Slaa, Mbowe na wenzake wakina Komu just to mention a few. Nitawapa mafile yao soon. Subirini tuanze kampeni. Niwafungue macho yenu muone nyuchi (uchi) zao.

Wewe kweli ni mtanzania? ama ni wale wale waliotumwa kuwakatisha watu tamaa. Leta hayo mafaili yako tuyaone, usisahau na mafailki ya EPA, Richmond, Geen Finance, Tangold, Meremeta, Kiwira na ufisadi wa halmashuri zote chini ya CCM.
 
Mie ningependa aerial fotos jamani! hiyo helicopter si wangepandisha mpiga picha mmoja kupiga umati! jamani fanyeni hivyo kuvuta hisia
 
Wewe kweli ni mtanzania? ama ni wale wale waliotumwa kuwakatisha watu tamaa. Leta hayo mafaili yako tuyaone, usisahau na mafailki ya EPA, Richmond, Geen Finance, Tangold, Meremeta, Kiwira na ufisadi wa halmashuri zote chini ya CCM.

Msihangaike kubishana na hii mitoto ya mafisadi! They will stop at nothing until they see us all worshiping them! Kwa mtu ambaye si mgonjwa akili hawezi hata siku moja kuendelea kutetea ujangili huu wa mcahana tunafanyiwa na serikali ya CCM hata kama ungekuwa mkereketwa wa chama, vinginevyo wewe ni FISADI AU MTOTO WA FISADI. Mjiandae kuihama hii nchi because we are coming for you!
 
Wewe Keil, hujui unaongeaje na unaongea katika hanga hizi. Ni hiari yako, anyway. Lakini jamaa yenu Slaa kwisha bin mufulisi. Karatu hana lolot jipya kaleta. Yaaani hana mpya yoyote. Ataaibika sana na kupoteza umaarufu wake wa bungeni hivi hivi. Chukua maneno yangu. Si kweli kwamba CCM ni mafisadi, ila kuna watu mafisadi ambao wanashughulikiwa squarely right now. Wanachama wa Chadema ni mafisadi zaidi. Yeye mwenyewe Slaa, Mbowe na wenzake wakina Komu just to mention a few. Nitawapa mafile yao soon. Subirini tuanze kampeni. Niwafungue macho yenu muone nyuchi (uchi) zao.

jamani muacheni huyu ni mgonjwa wa akili yaani UFISADI UMEMFUNGA AKILI ZAKE ZIMETREAD SASA
 
Back
Top Bottom