Aina za maandamano

Mto Songwe

JF-Expert Member
Jul 17, 2023
6,015
12,281
Katika suala la maandamano kuna aina mbili maarufu za maandamano.

Moja maandamano ya amani haya pia unaweza kuyaita maandamano ya hisani au matembezi ya hisani .

Ni aina ya maandamano ambayo huhusisha njia za amani katika kukemea, kupongeza, kuunga mkono au kuonesha hisia kuhusu jambo fulani katika jamii.

Mfano wa maandamano haya ni matembezi ya hisani kama siku ya wanawake duniani, kuhimiza kuchangia damu n.k

Pili ni maandamano ya fujo, haya ni maandamano ambayo huusisha matumizi ya nguvu kubwa kwa kundi la watu katika kudai kile wanacho amini, hitaji, kutoa malalamiko au kuonesha hali ya kuto kufurahishwa kuhusu jambo fulani.

Msingi wa maandamano ya namna hii ni katika kushinikiza jambo fulani litekelezwe kutokana na matakwa ya waandamanaji.

Maandamano ya namna hii yametumika sana katika shughuli za kisiasa kuleta mabadiliko ya kiutawala, sheria, muongozo, mifumo n.k katika historia ya tawala mbalimbali hapa duniani.

Utofauti mkubwa uliopo baina ya aina hii ya maandamano ni sehemu za matumizi yake na lengo kusudiwa la waandamanaji.

Katika siasa matembezi ya hisani sio mahala pake sahihi.
 
Hayo maandamano ya fujo wangekuwa wanaenda kuyafanya bungeni au ikulu ningewaona wanaakili timamu.

Ila kuchoma mali za masikini wenzio na kuharibu miundombinu huo ni ujambazi.
 
Hayo maandamano ya fujo wangekuwa wanaenda kuyafanya bungeni au ikulu ningewaona wanaakili timamu.

Ila kuchoma mali za masikini wenzio na kuharibu miundombinu huo ni ujambazi.
Maandamano ya fujo mara nyingi huzalisha armed struggle baina ya watawala na watawaliwa
 
Katika suala la maandamano kuna aina mbili maarufu za maandamano.

Moja maandamano ya amani haya pia unaweza kuyaita maandamano ya hisani au matembezi ya hisani .

Ni aina ya maandamano ambayo huhusisha njia za amani katika kukemea, kupongeza, kuunga mkono au kuonesha hisia kuhusu jambo fulani katika jamii.

Mfano wa maandamano haya ni matembezi ya hisani kama siku ya wanawake duniani, kuhimiza kuchangia damu n.k

Pili ni maandamano ya fujo, haya ni maandamano ambayo huusisha matumizi ya nguvu kubwa kwa kundi la watu katika kudai kile wanacho amini, hitaji, kutoa malalamiko au kuonesha hali ya kuto kufurahishwa kuhusu jambo fulani.

Msingi wa maandamano ya namna hii ni katika kushinikiza jambo fulani litekelezwe kutokana na matakwa ya waandamanaji.

Maandamano ya namna hii yametumika sana katika shughuli za kisiasa kuleta mabadiliko ya kiutawala, sheria, muongozo, mifumo n.k katika historia ya tawala mbalimbali hapa duniani.

Utofauti mkubwa uliopo baina ya aina hii ya maandamano ni sehemu za matumizi yake na lengo kusudiwa la waandamanaji.

Katika siasa matembezi ya hisani sio mahala pake sahihi.
Mikusanyiko mkubwa wa wananchi hata wakiwa wamefumba midomo kwa bandeji unaongea sana kwa watawala. Kwa mfano maandamano ya amani ya Chadema kama yataendelea mikoa yote itakuwa mwiba mkali kwa Samia kwani CDM wanapata uungwaji mkono kila siku.
 
Mikusanyiko mkubwa wa wananchi hata wakiwa wamefumba midomo kwa bandeji unaongea sana kwa watawala. Kwa mfano maandamano ya amani ya Chadema kama yataendelea mikoa yote itakuwa mwiba mkali kwa Samia kwani CDM wanapata uungwaji mkono kila siku.
Mleta mada hajui kinachoendelea yeye anadhani mafanikio ni lazima utumie jaziba, Lowasa kwenye kamoeni zake 2015 jukwaani alikuwa anasema sera yetu ni ELIMU, ELIMU,ELIMU baada ya hapo mkutano unafungwa lkn alipata viongozi wengi wa kuchaguliwa kuliko wale walioenda na ngojera jukwaani.
 
Katika suala la maandamano kuna aina mbili maarufu za maandamano.

Moja maandamano ya amani haya pia unaweza kuyaita maandamano ya hisani au matembezi ya hisani .

Ni aina ya maandamano ambayo huhusisha njia za amani katika kukemea, kupongeza, kuunga mkono au kuonesha hisia kuhusu jambo fulani katika jamii.

Mfano wa maandamano haya ni matembezi ya hisani kama siku ya wanawake duniani, kuhimiza kuchangia damu n.k

Pili ni maandamano ya fujo, haya ni maandamano ambayo huusisha matumizi ya nguvu kubwa kwa kundi la watu katika kudai kile wanacho amini, hitaji, kutoa malalamiko au kuonesha hali ya kuto kufurahishwa kuhusu jambo fulani.

Msingi wa maandamano ya namna hii ni katika kushinikiza jambo fulani litekelezwe kutokana na matakwa ya waandamanaji.

Maandamano ya namna hii yametumika sana katika shughuli za kisiasa kuleta mabadiliko ya kiutawala, sheria, muongozo, mifumo n.k katika historia ya tawala mbalimbali hapa duniani.

Utofauti mkubwa uliopo baina ya aina hii ya maandamano ni sehemu za matumizi yake na lengo kusudiwa la waandamanaji.

Katika siasa matembezi ya hisani sio mahala pake sahihi.
Kila kitu kina hatua zake...
Moja huzaa mbili!
Huko unakokutaka tutafika tu!
 
Kila kitu kina hatua zake...
Moja huzaa mbili!
Huko unakokutaka tutafika tu!
Awamu hii waendelee na mikutano ya amani kupeleka ujumbe,wakitumia maandamano ya nguvu yataleta umwagaji damu kwa nchi zetu za kiafrika na kwa Tanzania hakuna mwananchi atakayeandamana siyo mkakati mzuri kwa sasa. wajenge utamaduni wa maandamano ya amani ila waongeze uhamasishaji wa makundi mengi zaidi kuandamana hadi mabadiliko yatokee.
 
Maandamano ya kisiasa yanatakiwa kuwa BRUTAL kweli kweli, hiki kinachofanyika ni kumjenga Rais na ni kupoteza muda tu
 
Mikusanyiko mkubwa wa wananchi hata wakiwa wamefumba midomo kwa bandeji unaongea sana kwa watawala. Kwa mfano maandamano ya amani ya Chadema kama yataendelea mikoa yote itakuwa mwiba mkali kwa Samia kwani CDM wanapata uungwaji mkono kila siku.
Inaweza ikawa hivyo lakini siku zote matembezi ya hisani huwa si rahisi mpaka kuleta impact hiyo kwa watawala
 
Mleta mada hajui kinachoendelea yeye anadhani mafanikio ni lazima utumie jaziba, Lowasa kwenye kamoeni zake 2015 jukwaani alikuwa anasema sera yetu ni ELIMU, ELIMU,ELIMU baada ya hapo mkutano unafungwa lkn alipata viongozi wengi wa kuchaguliwa kuliko wale walioenda na ngojera jukwaani.
Chadema hawakufanikiwa kuchua nchi hiyo 2015 licha ya hayo yote uliyosema.

Pia yale yalikuwa masuala ya uchaguzi zaidi tofauti na maandamano wenda kuna mahali unachanganya
 
Awamu hii waendelee na mikutano ya amani kupeleka ujumbe,wakitumia maandamano ya nguvu yataleta umwagaji damu kwa nchi zetu za kiafrika na kwa Tanzania hakuna mwananchi atakayeandamana siyo mkakati mzuri kwa sasa. wajenge utamaduni wa maandamano ya amani ila waongeze uhamasishaji wa makundi mengi zaidi kuandamana hadi mabadiliko yatokee.
Sio rahisi mabadiliko kutokea kwa matembezi ya hisani. Mara nyingi historia za mabadiliko duniani huletwa na aina ya pili ya maandamano sio hiyo aina ya kwanza.
 
Haya ya CHADEMA ni matembezi ya hisani,hayawezi kuleta impact yoyote aisee.. maandamano ya kisiasa yanatakiwa kuwa jino kwa jino kiasi kwamba mtawala hatulii kabisa.
 
Maandamano ya kisiasa yanatakiwa kuwa BRUTAL kweli kweli, hiki kinachofanyika ni kumjenga Rais na ni kupoteza muda tu
Inaweza kuwa ni mchakato kuelekea aina ya pili ya maandamano kama aina ya kwanza haitoleta matokeo tarajiwa tusubiri tuone
 
Walioandamana jana Arusha mvua ikiwa inanyesha wananyeshewa na mvua huku viongozi wao wakiwa kwenye magari tinted
Wakiandamana wakiwa ndani ya magari
Hapana viongozi wa maandamano nao walinyeshewa na hiyo mvua wenda wewe sio mfuatiliaji
 
Haya ya CHADEMA ni matembezi ya hisani,hayawezi kuleta impact yoyote aisee.. maandamano ya kisiasa yanatakiwa kuwa jino kwa jino kiasi kwamba mtawala hatulii kabisa.
Wenda ni mchakato kuelekea aina ya pili ya maandamano kama maandamano ya kwanza hayata fua dafu
 
Haya maandamano kwa kuanzia siyo ya kudharau. Yanajenga msingi wa baadaye, mimi ninajiuliza kwani demokrasia ya uhuru wa kuandamana na kudai haki lazima iwe ni kundamana kwa mapambano kupora kuvunja magari nk nielemishwe.Na yanaanzia wapi,kwa mfumo upi na kwa namna gani? ili yawe confrotational, utayalazimishaje iwapo polisi haijawazuia au kuyapinga na kupiga mabomu? maandamano ya amani yanakuwa hivyo tu iwapo polisi hawatashambulia. mkiachwa tu na polisi na waandamanaji wakafuata sheria za nchi aina ya pili ya maandano yenye vurugu hutayaona.
 
Back
Top Bottom