Muuliza swali kama alihitaji kujua, aelimishwe siyo kumpotosha na Siasa za uchochoroni. Kama hoja ya swali ilikuwa ni kwa kuteuliwa kwake, Rais ana mamlaka ya kumteua "mtanzania" yeyote yule kushika nyadhifa yoyote ile, ambayo anadhani angeikidhi. Watanzania wote kwa ujumla wetu, tunawajibika kwa yote ktk nchi yetu.
Kama msingi wa hoja ni kwa kuipongeza serikali kiutendaji, Siasa za upinzani si kupinga kila kitu hata kama kinaendana na unayoyaamini. Member wa republic anaweza akajiunga na wale wa Democratic ktk voting, kwa US.
Kwahiyo inawezekana si kada wa Ccm ila ameyakubali yanayotendeka na Ccm, kama alivyosema mwenyewe, sio kosa. Kukubali uteuzi, ni uzalendo wake kwa nchi yake. Vikitokea vita vya kijeshi watz bila kujali itikadi ya kivyama tutaungana, tuko kwenye vita vya kiuchumi na kuliletea maendeleo taifa, itikadi tuviweke kando.
Kama msingi